Tuesday, October 08, 2013

SIKILIZA NA DOWNLOAD WIMBO MPYA WA DIAMOND "KAMA NIKIFA KESHO"



MAZISHI YA BABA MZAZI WA MSANII WA KIZAZI KIPYA 20 PERCENT YAFANYIKA KATIKA KIJIJI CHA KIMANZICHANA


Abas Kinzasa kwa jina la usanii anaitwa 20 Percent akiwa kwenye majonzi baada ya kufiwa na Baba yake mzazi Mzee Kinzasa aliyefariki juzi siku ya Jumapili na kuzikwa siku ya Jumatatu kwenye kijiji cha Kimanzichana kilichopo Wilaya ya Mkuranga Mkoani Pwani.
Hapa ndipo alikozikwa Mzee Kinzasa baba mzazi wa 20 Percent aliyefariki siku ya jumapili na kuzikwa siku ya jumatatu kwenye kijiji cha Kimanzichana kilichopo Wilaya ya Mkuranga

Msanii 20 Percent na ndugu zake wakiweka udongo kwenye kaburi la marehemu baba yake mzazi mzee Kinzasa

MAGAZETI YA LEO JUMANNE OKTOBA 08, 2013

DSC 0014 9ef01
DSC 0015 4e1af

UCHAGUZI UTAFANYIKA OKTOBA 27- TENGA


Leodgar-Tenga1 5ecb7
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Leodegar Tenga amewahakikishia Watanzania kuwa uchaguzi wa kupata Kamati mpya ya Utendaji ya shirikisho utafanyika Oktoba 27 mwaka huu kama ilivyopangwa.
"Wazungu wanasema ije mvua au jua, uchaguzi utafanyika. Isipokuwa tunachotaka kuhakikisha ni kuwa unakuwa uchaguzi huru na wa haki," amesema Rais Tenga wakati akizungumza na waandishi wa habari kwenye ofisi za TFF leo mchana (Oktoba 7 mwaka huu).
Amesema mchakato unakwenda vizuri kilichobaki ni revision (mapitio) na rufani, masuala ambayo yako mbele ya Kamati ya Rufani ya Maadili na Kamati ya Rufani ya Uchaguzi.
Rais Tenga amesema lengo la hatua hizo si kuzuia watu wasigombee kwani ni lazima mambo ya msingi ikiwemo sifa za wagombea yaangaliwe, lakini kwenye haki ni lazima kuhakikisha inatendeka hata kama ni kwa mtu mmoja.
Mchakato wa uchaguzi ulivutia waombaji 58 ambapo watatu wamekata rufani Kamati ya Rufani ya Uchaguzi kupinga kuondolewa na Kamati ya Uchaguzi wakati wengine wanane masuala yao yamepelekwa Kamati ya Rufani ya Maadili kwa njia ya mapitio (revision) ili kupata mwongozo wa utekelezaji.

HATARI....!!! VIJANA WAKAMATWA MSITUNI MTWARA NA CD ZENYE MAFUNZO YA AL-QAEDA, AL-SHABAAB

zzzzzkamanda_mtwara_ca9c9.jpg
Na Abdallah Bakari, Mtwara
POLISI mkoani Mtwara inawashikilia watu 11 kwa tuhuma za kupata mafunzo ya kijeshi msituni kwa kutumia CDs za al-Shabaab.
Tukio hilo la aina yake limetokea katika mlima Makolionga wilaya ya Nanyumbu mkoani hapa ambapo pia CDs zenye mafunzo mbalimbali ya kijeshi 25 zimekamatwa.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mtwara, Zelothe Stephen ameuambia "mtandao wa Kusini Leo" kuwa watuhumiwa hao
walikamatwa wiki moja iliyopita baada ya jeshi lake kupata taarifa kutoka kwa wasamaria wema: "CD hizo zilikuwa zinatoa mafunzo ya Al-Shabaab ya kuchinja watu, Mauaji wa Osama Bin Laden, Zindukeni Zanzibar, Kuandaa Majeshi, Mauaji wa Idd Amin na Mogadishu Sniper," alisema Stephen.


Monday, October 07, 2013

WASTARA APEWA MGUU WA BANDIA BURE NCHINI KENYA...!!!

STAA wa filamu za Kibongo, Wastara Juma Jumamosi iliyopita alikwea pipa kuelekea nchini Kenya ambako ana ziara ya siku nne kikazi na akiwa humo alipata fursa ya kupewa mguu wa bandia bure na wenyeji wake huku pia akiahidiwa kufanyiwa ‘check-up’ ya mwili mzima.
 
Wastara Juma.
Akizungumza na Ijumaa Wikienda, Wastara alisema kuwa anajisikia furaha kupewa ofa hiyo kutoka kwa wadau wa tasnia ya filamu pande za Kenya ambao wamekuwa wakivutiwa na kazi zake.
“Nimepewa ofa ya mguu bandia wa bure ambao utanisaidia, pia nitafanyiwa uchunguzi wa mwili mzima pamoja na mambo mengine. Nina furaha kwa heshima hiyo niliyopewa na wadau hao na kwa msaada wao huo, Mungu atawalipa,” alisema Wastara.
Enzi za uchumba wake na marehemu Juma Kilowoko ‘Sajuki’ walipata ajali iliyosababisha Wastara kukatwa mguu ambapo aliwekewa wa bandia. hivyo mguu huo aliopewa ni wa pili ili kama atahitaji abalishe ule wa zamani.

KAULI YA SERIKALI JUU YA MGOMO WA WASAFIRISHAJI

Picha_1_1fb96.jpg
Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli akisisitiza jambo kuhusu mgomo uliopangwa kufanywa na wadau wa usafirishaji nchini wakati akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) leo jijini Dar Es Salaam
Picha_33_60d3c.jpg
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar Es Salaam Kamishna Suleiman Kova akieleza jinsi Jeshi la Polisi lilivyojipanga kulinda usalama ili watumiaji wa barabara wasiweze kupata usumbufu huku akisisitiza kuwa kabla ya Jeshi la polisi kuchukua hatua za kisheria ni vema vyombo vinavyosimamia usafirishaji vikachukua hatuaKushoto ni Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli
Picha_4_5579d.jpg
Baadhi ya Maafisa wa Wizara ya Ujenzi na Waandishi wa Habari wakifuatilia kwa makini maelezo toka kwa Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli.
Picha Zote na Eliphace Marwa (MAELEZO)

MAGAZETI YA LEO JUMATATU OKTOBA 07, 2013

DSC 0013 193f0
DSC 0014 7b671

MTUHUMIWA'MUHIMU'WA MAUAJI YA BILIONEA AKAMATWA AKIDAIWA KUTOROKA

erastomsuya_5e7a1.jpg
Jeshi la Polisi nchini limefanikiwa kumtia mbaroni mtuhumiwa muhimu wa mauaji ya mfanyabiashara bilionea wa Arusha Erasto Msuya wakati akijaribu kutoroka kwenda Burundi.
Habari za uhakika zilizopatikana jana, zilisema mtuhumiwa huyo (jina tunalo), alikamatwa juzi asubuhi mkoani Kigoma akiwa katika harakati za kutoroka kuelekea nchi jirani ya Burundi.
Mtuhumiwa huyo ndiye anadaiwa kumshawishi marehemu kwenda kukutana na wauaji wake eneo la Mijohoroni wilayani Hai Agosti 7, mwaka huu na alikwenda pamoja na marehemu hadi eneo la tukio.
Habari zinadai mara baada ya marehemu kuuawa kwa kumiminiwa risasi zaidi ya 20, mtuhumiwa huyo alitoroka kutoka eneo la tukio akitumia moja kati ya pikipiki mbili zilizotumika katika mauaji hayo.

TUNDU LISSU AMJIBU JK

siku-tundu-lisu-alipokutana-na-jk-ikulu-jijini-dar-es-salaam_f685e.jpg
Mnadhimu wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Tundu Lissu amesema hotuba ya kila mwezi ya Rais Jakaya Kikwete aliyoitoa siku tatu zilizopita, imejaa maneno mengi ya kuambiwa hasa kuhusu mchakato wa Katiba Mpya, ikiwa ni pamoja na uteuzi alioufanya wa wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba.
Akizungumza na waandishi wa habari jana katika ofisi za makao makuu wa Chadema, Lissu alisema kauli zilizotolewa na Rais za kumshutumu yeye (Lissu) kuzungumza uongo bungeni, kuhusu uteuzi wa wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba zilikuwa zakuambiwa, hazina ukweli wowote.
"Pengine rais Kikwete angesoma hotuba yangu niliyoitoa bungeni asingezungumza vile kuhusu mimi."


Katika hotuba yake, Rais Kikwete alimshutumu Lissu kwa kusema kwamba katika uteuzi wa wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba kuwa Rais hakuheshimu mawazo ya Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) na Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT).

Rais Kikwete alisema kauli hiyo ya Lissu ni uzushi, uongo na uzandiki wa hali ya juu huku akisisitiza kuwa Lissu alitoa kauli hiyo ili kupotosha ukweli na pengine isaidie kujenga hoja yake ya kutaka Rais asiteue wajumbe 166 wa Bunge Maalum la Katiba.

Saturday, October 05, 2013

WALINZI WA MLIMANI CITY WANASWA WAKIPOKEA RUSHWA LIVE LIVE

Harufu ya rushwa! Safu ya ulinzi katika maduka ya biashara ya Mlimani City, Dar kwenye geti la kuingilia na lile la kutokea, inadaiwa kutawaliwa na rushwa ambapo walinzi wamenaswa ‘laivu’ wakipokea ‘mlungula’.
Kwa mujibu wa walalamikaji, walinzi hao wanadaiwa kujiwekea utaratibu usiyo rasmi chini ya kampuni ya ulinzi wa eneo hilo iliyotajwa kwa jina la Omega Nitro Risk Solutions ya jijini Dar ambapo ‘vijana’ wake wanatuhumiwa kutoza watu faini ya shilingi elfu kumi kwa gari ambalo mhusika wake amepoteza kadi ya kuingia na kutoka. 
 
Madai hayo yalikwenda mbele zaidi ikielezwa kuwa kumekuwa hakuna utaratibu mahususi kwenye ishu hiyo kwani baadhi ya walinzi kila mmoja hujiamulia kuchukua fedha bila mhusika kupewa risiti ya malipo. “Kuna tatizo kwenye safu ya ulinzi, huwa tunatozwa faini shilingi elfu kumi ukipoteza kadi,” alisema mmoja wa walalamikaji hao.

MUSWADA BINAFSI KUFUTA SHERIA YA MAGAZETI YA 1976

Zitto-Kabwe_839e8.jpg
Na Zitto Kabwe
Napenda kuujulisha umma kwamba leo Ijumaa tarehe 4 Oktoba, 2013 nimewasilisha kwa Katibu wa Bunge muswada binafsi Bungeni kufuta Sheria ya Magazeti ya mwaka 1976.
Changamoto iliyopo ni Sheria mbadala ya vyombo vya habari baada ya Sheria ya sasa kufutwa. Hata hivyo wadau wa habari kama Baraza la Habari Tanzania wameshafanyia kazi suala hili kwa muda mrefu sana na wana mawazo kuhusu sheria mbadala. 
Nimejulishwa kuwa muswada wa sheria mpya ya habari tayari upo. Kwa hiyo katika mchakato wa kujadili muswada binafsi wa kufuta sheria ya magazeti ya mwaka 1976 mabadiliko yanaweza kufanywa ili kutunga sheria mpya. Hatua ya kwanza ni kuifuta sheria hii kandamizi ambayo kiukweli tumechukua muda mrefu sana na baada ya madhara makubwa kufikia hatua ya muswada wa kuifuta.
Nimeamua kutumia njia za kawaida za kuwasilisha muswada na kuepuka njia ya dharura ili kujenga mazingira ya wadau wa habari kushiriki vya kutosha katika mabadiliko yanayotakiwa.

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI OKTOBA 05, 2013

DSC 0038 be9ab
DSC 0039 6c203

RATIBA YA LIGI KUU YA UINGEREZA LEO JUMAMOSI

Premier-Leage2_7f8b6.jpg
14:45 Manchester City na  Everton
17:00 Cardiff City na Newcastle United
17:00 Fulham na Stoke City
17:00 Hull City na Aston Villa
17:00 Liverpool na Crystal Palace
19:30 Sunderland na Manchester United

Friday, October 04, 2013

HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE, KWA WANANCHI, TAREHE 4 OKTOBA, 2013

JKNEWCABINET_7ce8b.jpg
HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA JAKAYA MRISHO KIKWETE, KWA WANANCHI, TAREHE 4 OKTOBA, 2013

Ndugu Wananchi;

Namshukuru Mwenyezi Mungu, mwingi wa rehma, kwa kutujaalia uzima na kutuwezesha kumaliza mwezi Septemba salama na kuwasiliana kwa kutumia utaratibu wetu huu mzuri. Naomba radhi kuzungumza nanyi siku ya leo kwa sababu nilikuwa safari na nilirejea jioni ya tarehe 30 Septemba, 2013. Awali nilifikiria nisiseme, nisubiri mwisho wa mwezi wa Oktoba. Lakini, baada ya kupata taarifa ya yaliyojiri, nimeshauriwa na nimekubali angalau niyasemee baadhi ya mambo huenda itasaidia. Niwieni radhi nisipoyasemea baadhi ya mambo siyo kwa kuyapuuza, bali kwa kuepuka hotuba kuwa ndefu mno. Nitayatafutia mahali pengine pa kuyasemea.

Uhusiano na Rwanda

Ndugu Wananchi;
Katika hotuba yangu ya mwisho wa mwezi wa Julai, nilizungumzia hali ya uhusiano wetu na Rwanda kutokuwa mzuri na tatizo la ujambazi na wahamiaji haramu katika Mikoa ya Kigoma, Geita na Kagera. Nafurahi kusema kuwa kwa yote mawili kuna maendeleo ya kutia moyo.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...