Monday, October 07, 2013

TUNDU LISSU AMJIBU JK

siku-tundu-lisu-alipokutana-na-jk-ikulu-jijini-dar-es-salaam_f685e.jpg
Mnadhimu wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Tundu Lissu amesema hotuba ya kila mwezi ya Rais Jakaya Kikwete aliyoitoa siku tatu zilizopita, imejaa maneno mengi ya kuambiwa hasa kuhusu mchakato wa Katiba Mpya, ikiwa ni pamoja na uteuzi alioufanya wa wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba.
Akizungumza na waandishi wa habari jana katika ofisi za makao makuu wa Chadema, Lissu alisema kauli zilizotolewa na Rais za kumshutumu yeye (Lissu) kuzungumza uongo bungeni, kuhusu uteuzi wa wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba zilikuwa zakuambiwa, hazina ukweli wowote.
"Pengine rais Kikwete angesoma hotuba yangu niliyoitoa bungeni asingezungumza vile kuhusu mimi."


Katika hotuba yake, Rais Kikwete alimshutumu Lissu kwa kusema kwamba katika uteuzi wa wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba kuwa Rais hakuheshimu mawazo ya Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) na Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT).

Rais Kikwete alisema kauli hiyo ya Lissu ni uzushi, uongo na uzandiki wa hali ya juu huku akisisitiza kuwa Lissu alitoa kauli hiyo ili kupotosha ukweli na pengine isaidie kujenga hoja yake ya kutaka Rais asiteue wajumbe 166 wa Bunge Maalum la Katiba.

Saturday, October 05, 2013

WALINZI WA MLIMANI CITY WANASWA WAKIPOKEA RUSHWA LIVE LIVE

Harufu ya rushwa! Safu ya ulinzi katika maduka ya biashara ya Mlimani City, Dar kwenye geti la kuingilia na lile la kutokea, inadaiwa kutawaliwa na rushwa ambapo walinzi wamenaswa ‘laivu’ wakipokea ‘mlungula’.
Kwa mujibu wa walalamikaji, walinzi hao wanadaiwa kujiwekea utaratibu usiyo rasmi chini ya kampuni ya ulinzi wa eneo hilo iliyotajwa kwa jina la Omega Nitro Risk Solutions ya jijini Dar ambapo ‘vijana’ wake wanatuhumiwa kutoza watu faini ya shilingi elfu kumi kwa gari ambalo mhusika wake amepoteza kadi ya kuingia na kutoka. 
 
Madai hayo yalikwenda mbele zaidi ikielezwa kuwa kumekuwa hakuna utaratibu mahususi kwenye ishu hiyo kwani baadhi ya walinzi kila mmoja hujiamulia kuchukua fedha bila mhusika kupewa risiti ya malipo. “Kuna tatizo kwenye safu ya ulinzi, huwa tunatozwa faini shilingi elfu kumi ukipoteza kadi,” alisema mmoja wa walalamikaji hao.

MUSWADA BINAFSI KUFUTA SHERIA YA MAGAZETI YA 1976

Zitto-Kabwe_839e8.jpg
Na Zitto Kabwe
Napenda kuujulisha umma kwamba leo Ijumaa tarehe 4 Oktoba, 2013 nimewasilisha kwa Katibu wa Bunge muswada binafsi Bungeni kufuta Sheria ya Magazeti ya mwaka 1976.
Changamoto iliyopo ni Sheria mbadala ya vyombo vya habari baada ya Sheria ya sasa kufutwa. Hata hivyo wadau wa habari kama Baraza la Habari Tanzania wameshafanyia kazi suala hili kwa muda mrefu sana na wana mawazo kuhusu sheria mbadala. 
Nimejulishwa kuwa muswada wa sheria mpya ya habari tayari upo. Kwa hiyo katika mchakato wa kujadili muswada binafsi wa kufuta sheria ya magazeti ya mwaka 1976 mabadiliko yanaweza kufanywa ili kutunga sheria mpya. Hatua ya kwanza ni kuifuta sheria hii kandamizi ambayo kiukweli tumechukua muda mrefu sana na baada ya madhara makubwa kufikia hatua ya muswada wa kuifuta.
Nimeamua kutumia njia za kawaida za kuwasilisha muswada na kuepuka njia ya dharura ili kujenga mazingira ya wadau wa habari kushiriki vya kutosha katika mabadiliko yanayotakiwa.

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI OKTOBA 05, 2013

DSC 0038 be9ab
DSC 0039 6c203

RATIBA YA LIGI KUU YA UINGEREZA LEO JUMAMOSI

Premier-Leage2_7f8b6.jpg
14:45 Manchester City na  Everton
17:00 Cardiff City na Newcastle United
17:00 Fulham na Stoke City
17:00 Hull City na Aston Villa
17:00 Liverpool na Crystal Palace
19:30 Sunderland na Manchester United

Friday, October 04, 2013

HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE, KWA WANANCHI, TAREHE 4 OKTOBA, 2013

JKNEWCABINET_7ce8b.jpg
HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA JAKAYA MRISHO KIKWETE, KWA WANANCHI, TAREHE 4 OKTOBA, 2013

Ndugu Wananchi;

Namshukuru Mwenyezi Mungu, mwingi wa rehma, kwa kutujaalia uzima na kutuwezesha kumaliza mwezi Septemba salama na kuwasiliana kwa kutumia utaratibu wetu huu mzuri. Naomba radhi kuzungumza nanyi siku ya leo kwa sababu nilikuwa safari na nilirejea jioni ya tarehe 30 Septemba, 2013. Awali nilifikiria nisiseme, nisubiri mwisho wa mwezi wa Oktoba. Lakini, baada ya kupata taarifa ya yaliyojiri, nimeshauriwa na nimekubali angalau niyasemee baadhi ya mambo huenda itasaidia. Niwieni radhi nisipoyasemea baadhi ya mambo siyo kwa kuyapuuza, bali kwa kuepuka hotuba kuwa ndefu mno. Nitayatafutia mahali pengine pa kuyasemea.

Uhusiano na Rwanda

Ndugu Wananchi;
Katika hotuba yangu ya mwisho wa mwezi wa Julai, nilizungumzia hali ya uhusiano wetu na Rwanda kutokuwa mzuri na tatizo la ujambazi na wahamiaji haramu katika Mikoa ya Kigoma, Geita na Kagera. Nafurahi kusema kuwa kwa yote mawili kuna maendeleo ya kutia moyo.

WAFUASI WA MORSI WAKABILIANA NA POLISI MISRI

131003231510_egypt_muslim_brotherhood_mb_304x171_ap_nocredit_e5ae6.jpg
Vikosi vya usalama nchini Misri vimeimarisha ulinzi katika sehemu kadhaa mjini Cairo baada ya vurugu kuzuka kutokana na makabiliano kati ya wafuasi wa Mohammed Morsi na vikosi vya usalama katika mji huo na ule wa Alexandria.
Mwandishi wa BBC mjini Cairo Quentin Sommerville anasema kuwa milipuko na milio mikuwa ya risasi imesikika katika sehemu za katikati mwa mji mkuu.
Sehemu ambazo zimezingirwa ni kama vile ambako wafuasi wa rais aliepindiliwa Mohammed Morsi waliwahi kupiga kambi baada ya Morsi kuondolewa kwa nguvu mamlakani na vikosi vya usalama mwezi Agosti katika operesheni iliyosababisha mamia kadhaa kupoteza maisha.
Pia usalama umeimarishwa karibu na medani ya Tahrir ambako waandamanaji waliokuwa wanapinga Morsi walikusanyika katika maandamano ya kumtaka ajiuzulu kabla ya majeshi kumtoa madarani miezi mitatu iliopita.
Vyombo vya habari vimeripoti kutokea ghasia zaidi katika mkoa wa Kaskazini wa Sharqiya, Mashariki mwa Giza, pamoja na Kaskazini mwa mji wa bandarini wa Alexandria.
Mamia ya watu wameuwa tangu jeshi kumuondoa mamlakani Morsi mwezi Julai.
Maelfu ya wanachama wa vuguvugu la Muslim Brotherhood pia wamezuiliwa katika miezi miwili iliopita.
Baadhi ya maafisa wakuu wa chama hicho akiwemo bwana Morsi na generali Mohammed Badie, wanazuiliwa kwa madai ya kuchochea ghasia na mauaji.
Vuguvugu hilo limelalamika na kusema kuwa maafisa wanazifanya juhudi zao dhidi yaokuonekana kama vita dhidi ya ugaidi

KABURI LA ALIYEFUFUKA LAFUKULIWA

DSCF1980 800x600 5ffda
Valence Robert, Geita
KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida kaburi ambalo alizikwa mtoto Shabani Maulidi (15), ambaye anadaiwa kufariki dunia miaka mitatu iliyopita na kuonekana akiwa hai hivi karibuni, jana lilifukuliwa na viungo vya mwili wake kukutwa ndani.
Kazi hiyo iliyofanyika chini ya ulinzi mkali wa polisi pamoja na Mtafiti wa Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali Mkoa wa Mwanza, Lucas Ndungulu, ilizua taharuki kwa umati wa watu waliokuwa eneo hilo, baada ya nyumba ya jirani lilipo kaburi hilo, Masanja Marwa, kubomoka ghafla wakati ufukuaji huo ukiendelea, huku mwanamke mmoja ambaye hakufahamika jina lake mara moja naye akianguka na kuzirai. 

Kwa sasa mtoto huyo ambaye alionekana hai, amelazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Geita kwa uangalizi wa kitaalamu.
Akizungumza na waandishi wa habari eneo la tukio, Ndungulu alisema kuwa wameamua kufukua kaburi hilo ili kupata sehemu ya viungo vya mwili kwa ajili ya vipimo.
"Lengo la kufukua kaburi hili ni kutaka tupate kiungo chochote cha mwili wa marehemu ili tufanye utafiti wa kitaalamu ili tujue kama ni kweli huyu anayedaiwa kuwa ni mtoto wao ndiye," alisema.

130 WAFA MAJI WAKIJARIBU KWENDA ULAYA

wafa_maji_de7d8.jpg
Maafisa katika kisiwa kikubwa cha Sicily katika bahari ya Meditarenia wanasema kuwa wamepata maiti 130 baada ya mashua iliyokuwa imewabeba takriban wahamiaji 500 wa kiafrika kushika moto na kuzama katika kisiwa cha Lampedusa.
Boti hiyo ilikuwa safarini kuelekea Ulaya lakini ikazama katika kisiwa cha Lampedusa katika pwani ya Utaliana
Takriban miili 103 imepatikana baharini na mingine zaidi kupatikana ndani ya boti iliyozama.
Inaarifiwa abiria walijirusha baharini wakati moto ulipozuka ndani ya boti
Zaidi ya wahamiaji 150 wameokolewa.
Wengi wa wahamiaji hao walikuwa raia wa Eritrea na Somalia,kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa.
Shughuli kubwa ya uokozi ingali inaendelea kuwatafuta manusura kwani inahofiwa mamia zaidi huenda wamefariki kutokana na ajali hiyo.
Meya wa mji huo anasema kuwa walionusurika wako hatika hali ya mshutuko na walimwambia kuwa moto mdogo uliwashwa baada ya meli kukwama na lengo lilikuwa kuitisha msaada.
Lakini alisema kuwa moto ulisambaa kupita kiasi na ikawa vigumu kuudhibiti.
Kisiwa cha Lampedusa kiko kati ya Tunisia na Sicily na kimekuwa kiingilio kikuu cha wahamiaji kuingia barani Ulaya.

Thursday, October 03, 2013

MAJAMBAZI YATEKA BASI LA ABIRIA NA KUPORA SIMU NA FEDHA.....!!!

Abiria hamsini na moja waliokuwa wakisafiri na basi la Taqwa kutoka  Bujumbura kuelekea Dar-es-Salaam wametekwa katika kijiji cha Milade wilayani Mkalama na kuporwa mali , simu na fedha zaidi ya shilingi milioni mia mbili hamsini.
Akieleza kamanda wa polisi mkoani Singida bwana Godfrey Kamwela  amesema watekaji hao waliwaamrisha abiria kushuka chini ya basi baada ya kuvunja vyoo na kuanza kuwasachi na kufanikiwa kupora simu, fedha za  kitanzania shilingi milioni tano ,dola za kimaerekani dola laki moja elfu sitini na  faranga zenye thamani ya elfu ishirini kufuatia tukio hilo kamanda Kamwela amewaomba wananchi na makampuni ya simu kushirikiana na jeshi la polisi ili kuweza kuwa kamata watu ambao wamefanya tukio hilo.

Kwa upande wake dereva la basi hilo bwana Ahamed Seif amesema gafla aliona majani barabarani na alipoangalia vizuri aliona kuna mawe makubwa  mawili  yakiwa barabarani na kushindwa  kuyakwepa ,baada ya kugonga mawe hayo magurudumu yote mawili ya mbele yalipasuka na gari  ikaserereka umbali wa mita mia moja.

MWANAMKE AFARIKI DUNIA MARA BAADA YA KUNYWA DAWA ZA KIMASAI KAMA TIBA HUKO MOSHI.

DAWA za kienyeji za Kimasai zinadaiwa kusababisha kifo kwa mkazi wa Moshi Vijijini, Restituta Alen baada ya kuzinunua kutoka kwa mfanyabiashara na kunywa.Mfanyabiashara wa dawa hizo, Lanyani Lukumay anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kusababisha kifo cha mwanamke huyo. Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kilimanjaro, Robert Boaz alisema tukio hilo lilitokea Septemba 30 saa 9.30 alasiri eneo la Marangu wilayani Moshi Vijijini.

Kwa mujibu wa Kamanda, Lukumay alimuuzia dawa za miti shamba mteja wake kisha kuzinywa na alifariki muda mfupi baadaye.
Hata hivyo haikufahamika ugonjwa uliokuwa ukimsumbua.
Lukumay anauza dawa za asili ya Kimasai, ambazo ni baadhi ya mitishamba na vitu vingine, inadaiwa siku ya tukio alimpa dawa mteja wake huyo ambaye uchunguzi wa awali unaonesha alifariki baadaye, tunamhoji kujua chanzo cha kifo,”alisema.
Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospitali ya Mkoa ya Mawenzi. Polisi inafuatilia kufahamu iwapo dawa za mtuhumiwa huyo zinatambuliwa na mamlaka zilizopo na kama anatambulika kuendesha biashara anaifanya kienyeji.
Pamoja na tukio hilo la kifo, pia polisi imetoa taarifa juu ya mtoto mchanga wa kike anayekadiriwa kuwa na umri wa kati ya miezi sita na saba aliyekutwa amekufa akiwa katika dampo lililopo Kata ya Njoro, Manispaa ya Moshi. Polisi imeomba wananchi kushirikiana na polisi kubaini wahusika wa tukio hilo

MASHINE ZA TRA ZAZUA BALAA.... MBEYA WAGOMA KUZINUNUA, VURUGU ZAZUKA

9161303_orig_67cda.jpg

Mabomu ya machozi yalipigwa ili kuzuia wafanyabiashara wasilete vurugu

7024725_orig_b85b7.jpg

Maduka yakiwa yamefungwa

2503579_orig_f146a.jpg

Wafanyabiashara hao walichoma matairi ili kuwazuia polisi wasiweze kuwafikia

MAGAZETI YA LEO ALHAMISI OKTOBA 03, 2013

DSC 0011 c3260
DSC 0012 8e34e

LIGI YA MABINGWA WA ULAYA

ulaya_88499.jpg
CSKA Moskva 3 - 2 Viktoria Plzeň
Shakhtar Donetsk 1 - 1 Manchester United
Bayer Leverkusen 2 - 1 Real Sociedad
Juventus 2 - 2 Galatasaray
Real Madrid 4 - 0 København
PSG 3 - 0 Benfica
Anderlecht 0 - 3 Olympiakos Piraeus
Manchester City 1 - 3 Bayern München

KAULI YA CHADEMA KUHUSU KUFUNGIWA KWA MAGAZETI.

chadema-logo-i2 6aded
CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO Idara ya Habari ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), tangu ilivyopokea kwa masikitiko na mshituko mkubwa taarifa za Serikali ya CCM, kufungia magazeti ya Mwananchi na Mtanzania, imeendelea kufuatilia kwa ukaribu hatua zinazochukuliwa na kauli mbalimbali zinazotolewa na pande zote mbili, serikali na wadau wa uhuru wa habari na vyombo vya habari. 
Ni wazi bila shaka yoyote kuwa kwa mara nyingine tena, serikali hii, imeendelea kutumia sheria mbaya, kutumia madaraka vibaya kufanya uamuzi mbaya, kila inapokosa hoja na uwezo wa kukabiliana na sauti mbadala au maoni kinzani.
Suala hili limekuwa dhahiri zaidi baada ya Serikali kuamua hata kuanza kuingilia uhuru wa habari na maoni kwenye mitandao ya kompyuta (on line) na pia kutishia kulifungia Gazeti la Rai, linalotolewa na Kampuni ya New Habari (2006) Limited, kwa sababu limeanza kuchapiswa kila siku.
Wakati wamiliki wa gazeti hilo wametoa ushahidi unaotokana na nyaraka za serikali hiyo hiyo iliyotoa idhini kwa chombo hicho kuchapishwa kila siku, Serikali yenyewe kwa upande wake imetoa utetezi wa ajabu juu ya tishio lake hilo ikijitetea kuwa kibali hicho kilitolewa kwa Kampuni ya Habari Corporation iliyouza hisa zake kwa Kampuni ya New Habari (2006) Limited.
Katika hili serikali inajichanganya. Hii ni dalili ya wazi kwamba uamuzi wake huo ni mwendelezo wa maamuzi ya kibabe, yasiyofanywa kwa masilahi ya Watanzania, ndiyo maana yanaanza kuipatia tabu jinsi ya kujibu na kujenga hoja za kutetea uovu wake.
CHADEMA, inapinga na itaendelea kupinga kwa kauli na vitendo, hatua hii ya serikali yenye lengo ovu dhidi ya umma wa Watanzania.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...