Thursday, September 12, 2013

NDOA YA MZEE MAJUTO NA KABINTI KA MIAKA 20 YAVUNJIKA....!!


MWANAMKE anayedaiwa kufunga ndoa ya siri na mchekeshaji mahiri Bongo, Amri Athuman maarufu kama Mzee Majuto au King Majuto, Rahma Abdallah (20), ameibuka na kudai kutelekezwa na mumewe huyo.

Ndoa hiyo ambayo ilifungwa kwa siri jijini Dar Julai 28, mwaka huu na kudumu siku 44, inaonekana imevunjika rasmi baada ya Mzee Majuto kutoa talaka kupitia kwa msanii wa filamu aitwaye Rehema Omary.
 
Akizungumza na mwandishi wetu, Septemba 9, mwaka huu, Rahma alidai kuwa alikutana na Mzee Majuto jijini Tanga na kuanzisha uhusiano wa kimapenzi kwa miezi sita kabla ya kufunga ndoa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani uliopita.

“Tulifahamiana Tanga, mimi ni mwenyeji wa huko kama ilivyo kwa Mzee Majuto, wakati tukiwa kwenye uhusiano, ulipofika Mwezi wa Ramadhani akaona bora tufunge ndoa ili tusiendelee kutenda dhambi, akaniambia dhamira yake hiyo nami sikukataa,” alisema Rahma.

MAGAZETI YA LEO ALHAMISI SEPTEMBA 12, 2013

DSC 0016 8abf5
DSC 0017 c9f85

POLISI MKOANI DODOMA YASHINDWA KUMFIKISHA SUGU MAHAKAMANI


JESHI la Polisi mkoani Dodoma limeshindwa kumpandisha kizimbani Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi (CHADEMA), kwa madai kuwa upelelezi bado haujakamilika. Mbilinyi, maarufu kama ‘Sugu’ alifunguliwa jalada na jeshi hilo Ijumaa iliyopita, akidaiwa kumjeruhi jichoni askari wa Bunge, Koplo Nikwisa Nkisu.
Akizungumza na waandishi wa habari jana mjini hapa, Wakili wake, Tundu Lissu, alisema kuwa hawakufikishwa mahakamani kama walivyotegemea kutokana na kuelezwa kuwa upelelzi haujakamilika.
Lissu ambaye ni Mbunge wa Singida Mashariki, alisema kuwa baada ya mteja wake kuripoti kituoni aliambiwa kwamba upelelezi huo ukikamilika wataitwa ili kupewa maelezo ya hatua gani inafuata.
Alisema kitendo hicho cha polisi kuwaita bila kukamilisha upelelezi wao ni kuwapotezea muda.
“Nashangaa ni kwanini tunaitwa, tuliambiwa tufike hapa, lakini tulipokuja hapa hakuna jambo lolote la maana tuliloambiwa, badala yake wanasema tuendelee na shughuli zetu upelelezi haujakamilika na baada ya wiki mbili watatuambia kinachoendelea.

JWTZ WAMPA KICHAPO CHA MBWA MWIZI HAKIMU HUKO KARAGWE KWA KUMDHANIA KUWA NI MNYARWANDA

Matendo Manono (kushoto)
Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Matendo Manono ambaye ni Hakimu Mkazi katika Mahakama ya Wilaya ya Karagwe mkoani Kagera amelalamikia kitendo cha kupigwa na kujeruhiwa vibaya na Askari wa Tanzania, katika zoezi la kuwaswaga wahamiaji haramu wa kinyarwanda wanao ishi nchini Tanzania.
 
 Soma maelezo ya hakimu huyo hapo chini...

" i have a serious contempt of this country...while they know for sure that this country has no National ID stil they want us to show Citizenship ID...
 
Imagine this was travelling to western part of TZ (Karagwe) today i have been arrested by the damned Immigration, police officers and JW people that am a prohibited immigrant simply because am tall with big (long,edged?)nose ..

i have been seriously humiliated and beaten simply because i resemble Rwandese something which is neither sin nor unlawful under The Immigration Act or The Citizenship Act....
I don't know if those people of Human Rights know what is happening in Kagera...total violation of human rights "

KLABU YA SOKA YA SUNDERLAND YA UINGEREZA KUWEKEZA KATIKA SEKTA YA UTALII PAMOJA NA KUINUA MCHEZO WA MPIRA WA MIGUU NCHINI

Mkurugenzi wa Biashara wa klabu ya Sunderland.Bw Gary Hutchinson(wapili kushoto)akiongea na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam kuhusu hatua ya mazungumzo waliyofikia na kujenga kituo cha michezo katika Manispaa ya Ilala ambayo itakuwa chimbuko la kuinua mchezo wa mpira wa miguu(wakwanza kulia)Mkurugenzi wa Michezo Nchini bw.leonard tadeo(wapili kulia)Mkurugenzi wa Mwendeshaji wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) Dk. Aloyce Nzuki(wakwanza kushoto)Mwakilishi wa klabu ya Sunderland Tanzania,Bw Edmund Hazzad.
Mkurugenzi wa Mwendeshaji wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) Dk. Aloyce Nzuki.akifafanua kuhusu sekta ya Utalii inafanikiwa na kuinua uchumi wa nchi kupitia michezo Nchini.
Mkurugenzi wa Biashara wa klabu ya Sunderland.Bw Gary Hutchinson,(kushoto)akimkabidhi mkurugenzi wa wizara ya michezo bw.leonard Tadeo.jezi ambao imesainiwa sahihi na wachezaji wa sunderland.

Wednesday, September 11, 2013

KILICHOMUUA MSANII HUYU KINASIKITISHA.....!!!


TASNIA ya filamu Bongo imepata pigo lingine baada ya mwishoni mwa wiki iliyopita kuondokewa na msanii aliyekuwa akichipukia kwa kasi aliyefahamika kwa jina la Zuhura Maftah ‘Malisa’.
Malisa alifariki dunia katika Hospitali ya Hindu Mandal jijini Dar baada ya kusumbuliwa na uvimbe kichwani kwa takriban miezi mitatu.
Wakizungumza na gazeti hili mara baada ya kifo hicho, baadhi ya wasanii wa filamu walielezea masikitiko yao na kusema hakika wamemkosa msanii ambaye siku za baadaye angekuwa moto wa kuotea mbali.
“Kifo chake kimetusikitisha sana, Malisa alikuwa mmoja wa wasanii ambao walikuwa wakija kwa kasi, amefariki dunia wakati ndiyo kwanza nyota yake ilikuwa imeanza kung’ara lakini kazi ya Mungu siku zote haina makosa, akapumzike kwa amani,” alisema mmoja wasanii aliyeomba hifadhi ya jina lake.
Msanii mwingine wa filamu ambaye huenda kifo hicho kimemgusa kuliko wengine ni Yvonne Cheryl ‘Monalisa’ ambaye inadaiwa muda mfupi kabla ya Malisa kufariki waliongea na kumwambia anaendelea vizuri.
Mmoja wa watu waliokuwa wakimhudumia Malisa hospitalini hapo aliyefahamika kwa jina la Vanitha alisema: “Siku ya kifo chake aliniambia nimpigie simu Mona aongee naye kwani hajamuona siku hiyo, ilikuwa saa 12 jioni baada ya kumaliza kumuogesha.
“Waliongea na kumwambia anaendelea vizuri. Baada ya Malisa kumaliza kuongea na Mona niliondoka lakini nilipofika Surender Bridge nikapata taarifa kuwa amefariki dunia,” alisema Vanitha.

NDUNGAI NA MBOWE WALIVUNJA KANUNI ZA BUNGE MAKUSUDI KWA MASLAHI YA VYAMA VYAO


Kumekuwa na mjadala mkali kuhusu iwapo Naibu Spika, Job Ndugai alikiuka Kanuni za Bunge katika kushughulikia vurugu zilizotokea Bungeni Alhamisi iliyopita kwa kuamuru kutolewa nje kwa Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe. 

Ndugai ambaye alikuwa kiongozi wa shughuli za Bunge siku hiyo, aliwaamuru askari kumtoa nje Mbowe baada ya kukaidi amri yake ya kutaka kuketi chini aliposimama kutaka kupewa nafasi ya kuzungumza, hali iliyozua tafrani bungeni. 

Pamoja na mambo mengine Ndugai amekuwa akituhumiwa kwamba anaminya uhuru wa wabunge wa upinzani kutokana na mapenzi aliyonayo kwa chama chake, CCM.
 
Kwa upande mwingine, kumekuwa na lawama kwamba Mbowe alikosea kukaidi amri ya Naibu Spika kwa kuwa kanuni zinamtaka mbunge yeyote (hata akiwa waziri), kuketi pale kiongozi wa Bunge (Spika, Naibu au Mwenyekiti) anaposimama, hivyo kusababisha mtafaruku.

NAPE: CHADEMA WAMEPEWA MABILIONI TOKA NJE KUVURUGA MCHAKATO WA KATIBA.


ZNape_7c07c.png
Adai ndio chanzo cha kupigana bungeni Asema ndizo walizotumia kuzunguka na helkopta nchini. Aeleza yaliyotokea bungeni sio bahati mbaya, Chadema waliyapanga Ashukuru bunge kuendelea kuonyeshwa"live" ili wananchi waone ujinga wao.
 Awatuhumu kuweka masilahi yao mbele badala ya nchi. Asisitiza CCM kuendelea kuheshimu uamuzi wa wananchi juu ya katiba. Aonyesha madai ya Chadema kitakwimu yasivyojali wakulima na wafanyakazi.



Katibu wa NEC ya CCM itikadi na Uenezi amesema kinachowasumbua Chadema mpaka wanafanya yote waliyoyafanya hasa ngumi na vurugu bungeni ni namna watakavyoeleza kwa waliowapa pesa za kuvuruga mchakato wa katiba nchini kwani wanatakiwa kupeleka mrejesho jinsi walivyofanikiwa na jinsi walivyotumia mabilioni hayo.

Nape ameyasema hayo kwenye mkutano mkubwa wa hadhara mjini Kahama kwenye ziara ya karibu siku ishirini kanda ya ziwa kwa mikoa mitatu yaani Shinyanga,Simiyu na Mara ya Katibu Mkuu wa CCM Taifa Ndg. Abralhaman Kinana.

MAGAZETI YA LEO JUMATANO SEPTEMBA 11, 2013

DSC 0525 d5eb2
DSC 0526 0ce62

MASHITAKA MATATU ALIYOSOMEWA MAKAMU WA RAIS WA KENYA MBELE YA MAHAKAMA YA ICC


William Ruto amekana mashtaka yote yanayomkabili kwenye Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC).

Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Mahakama hiyo, Fatou Bensouda anayesimamia kesi hiyo, alisema watuhumiwa wawili waliofikishwa mahakamani hapo jana, Ruto na mtangazaji wa Redio, Joshua arap Sang wanakabiliwa na mashtaka matatu kila mmoja, ambayo ni kuwalazimisha watu kukimbia makazi yao, mauaji na kuchochea ghasia.


Kesi hiyo imeanza kusikilizwa siku chache baada ya Bunge la Kenya kupiga kura kutaka nchi hiyo ijitoe uanachama wa ICC, wakieleza kwamba imekuwa haina tija na inatumiwa kuwakandamiza Waafrika.


Ruto ambaye alionekana kujiamini alifika kwenye jengo la Mahakama akiwa ameambatana na baadhi ya wabunge waliosafiri kutoka Kenya hadi The Hague kwa ajili ya kumuunga mkono.

MFANYABIASHARA MAARUFU ALEX MASSAWE AFIKISHWA MAHAKAMANI HUKO DUBAI


Mfanyabiashara maarufu nchini, Alex Massawe amefikishwa mahakamani Dubai, Falme za Kiarabu (UAE), kwa tuhuma za mauaji baada ya Serikali ya Tanzania kupitia Shirika la Polisi la Kimataifa (Interpol), kuiomba Serikali ya nchi hiyo kumkamata.

Massawe anayetarajiwa kuletwa nchini wakati wowote kuanzia sasa, alikuwa anatafutwa na Polisi wa Tanzania kwa muda mrefu na alikamatwa Dubai, mapema Julai na maofisa wa usalama wa UAE baada ya alama zake za vidole kuonyesha kuwa alikuwamo kwenye orodha ya watu waliokuwa wanasakwa na Interpol.

Baada ya kukamatwa, Mkuu wa Interpol, Tawi la Tanzania, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP), Gustav Babile alisema Massawe alikamatwa kati ya Juni 20 na 25, mwaka huu kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dubai akitokea Afrika Kusini.

Massawe ambaye anafanya biashara zake katika Miji ya Arusha, Dar es Salaam na Moshi, inadaiwa kwamba akiwa Dubai, alikutwa na pasi tatu bandia za kusafiria zilizokuwa na majina tofauti wakati alama zake za vidole zilionyesha anaitwa Alex Massawe. “Ombi la kuleta mhalifu nchini kutoka nje ya nchi (extradition request), lina hatua ndefu.
Unajua kuna mlolongo wa taratibu za kutekeleza. Kwanza lazima Polisi wa Tanzania watoe tangazo kwa Interpol kuhusu kumsaka mtu huyo ili aletwe,” alisema Babile.

Tuesday, September 10, 2013

"NAJUTA KUMJUA LORD EYEZ MAISHANI MWANGU".... RAY C


INAWEZEKANA umekuwa ukisikia vitu vingi kuhusu lejendari wa Bongo Fleva, Rehema Chalamila ‘Ray C’ lakini hukupata chansi ya kumsikia mwenyewe akifunguka mwanzo mwisho juu ya kisanga kilichompata alipojikuta kwenye janga la matumizi ya dawa za kulevya.

Ijumaa Wikienda limefanya naye mahojiano (exclusive interview) ambapo amekidhi kiu yako ya kujua chochote kinachomhusu. UNGANA NAYE…
KWA MTU ASIYEKUJUA, UMETOKEA WAPI?
“Nimezaliwa Mei 15, 1982 mkoani Iringa. Kabla ya kuingia kwenye muziki nilifanya kazi ya utangazaji. Watu wengi walinijua wakati nikiwa Radio Clouds FM. Albamu yangu ya kwanza ni Mapenzi Yangu niliyoitoa mwaka 2003. Kilichofuata ni kujipatia mashabiki wengi sana ndani na nje ya nchi. Baadaye niliachia Albamu ya pili ya Na Wewe Milele ya mwaka 2004. 

Nilipata mialiko mingi nje ya nchi zote Afrika Mashariki, China, Uingereza na kwingineko. Kilichofuata ni singo kibao na tuzo hadi nilipopata matatizo mwaka jana. Unazikumbuka Mama Ntilie, Mahaba ya Dhati, Touch Me, Na Wewe Milele, Wanifuatia Nini na Nihurumie? Huyo ndiye Ray C mwenyewe.

JALADA LA SUGU LATUA KWA DPP


JALADA la Kesi inayomkabili Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi (CHADEMA), limefikishwa katika Ofisi ya Mwanasheria wa Serikali. Mbilinyi maarufu kwa jina la ‘Sugu’(pichani), anadaiwa kumjeruhi askari wa Bunge katika vurugu zilizotokea Bungeni mwishoni mwa wiki iliyopita. Kwa mujibu wa Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Susan Kaganda alisema polisi wameshapeleka jalada la mbunge huyo katika Ofisi ya Mwanasheria wa Serikali na kwamba upelelezi unaendelea.

“Tayari jalada la kesi yake lipo katika Ofisi ya Mwanasheria wa Serikali na upelelezi unaendelea,” alisema.

Kwa mujibu wa vyanzo kutoka Jeshi hilo, Sugu alikwenda Polisi kujisalimisha siku ya kuahirishwa Bunge na kwamba aliambiwa arudi tena kuripoti Jumatano (kesho). “Kama akiripoti Jumatano, ndiyo itajulikana na kama jalada lake litakuwa limeshafikishwa mahakamani au bado,” kilieleza chanzo hicho.

Habari za uhakika kutoka katika Mahakama ya Mkoa wa Dodoma hadi jana mchana, hakukuwa na jalada lolote lililokuwa limefika mahakamani linalomuhusu Sugu. “Kwa leo (jana), majalada yaliyopokelewa hadi sasa ni mawili tu na yote yanahusu ‘Trafiki kesi’ kilieleza chanzo hicho.


Kusakwa kwa mbunge huyo kulitokana na vurugu zilizotokea katika ukumbi wa Bunge ambao uligeuka ulingo wa masumbwi, baada ya wabunge wa kambi ya upinzani kupigana hadharani na askari wa Bunge.

Wabunge hao walichapana ndani na nje ya ukumbi, hali iliyosababisha tafrani kubwa, huku maofisa usalama na askari polisi kutoka kituo kikuu mjini Dodoma, wakilazimika kuitwa kwenda kuongeza nguvu ili kukabiliana na hali hiyo.

WEMA SEPETU AWATOA MATE MANJEMBA KWA USTADI WA KUKATA KIUNO...!!!

MADAM, Wema Sepetu ameonesha upande wa pili wa maisha yake baada ya kunaswa akikata mauno mwanzo mwisho.  
Kwa mujibu wa mtandao mmoja wa Kibongo, Madam alifi ka na kampani yake katika Ukumbi wa Thai Village, Masaki jijini Dar hivi karibuni na ndipo ‘mashetani’ yalipompanda baada ya kusikia sebene lililokuwa likiporomoshwa na Bendi ya Skylight.
Wema akiwa na kampani yake wakionekana kukolea kwa kilevi, waliinuka na kuanza kushindana kucheza huku Wema akijiweka ziro distance na mmoja wa wanamuziki wa bendi hiyo na kuanza kumkatikia.

NDUNGAI ATAJA SABABU ZAKE ZILIZOFANYWA AMTIMUE FREEMAN MBOWE BUNGENI


NAIBU Spika, Job Ndugai ametetea uamuzi wake wa kuagiza kutolewa ndani ya ukumbi wa Bunge, Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe akisema alikuwa sahihi.

Mabishano hayo ambayo yalisababisha kuibuka kwa vurugu bungeni yalitokea mwishoni mwa wiki, muda mfupi baada ya kipindi cha maswali na majibu, ambapo kiongozi huyo wa Bunge aliruhusu mjadala kuhusu Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba uendelee.

Kutokana na hali hiyo, Mbowe alisimama kutaka kutoa ufafanuzi juu ya mjadala huo, lakini Ndugai alimzima na kumtaka kukaa chini, jambo ambalo halikumfurahisha Mbowe na kumfanya agomee agizo lake.

Akizungumza na MTANZANIA jana kwa njia ya simu, Ndugai alitumia muda mwingi kutetea uamuzi wake na kukosoa hoja za watu wanaompinga juu ya uamuzi wake huo.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...