Thursday, September 05, 2013

ANGALIA PICHA ZA RAIS KIKWETE WALIPOKUTANA NA KAGAME HUKO KAMPALA LEO...!!!


Rais Jakaya Kikwete leo amefanya mazungumzo na Rais Paul Kagame wa Rwanda katika mkutano wa saba wa kimataifa wa nchi za maziwa makuu, unaofanyika Kampala, Uganda.
Haijafahamika mara moja walichozungumza, hizi ni picha za mkutano wao.
9676681299_b3707d20a5_c
9676687273_13e1849eb2_b
9679917620_3f83a214d0_b
Marais hao wamekutana wakati ambapo uhusiano kati ya nchi hizo mbili unaendelea kuzorota.

DULLY SYKES AMFANANISHA DIAMOND NA KANUMBA...!!! NI BAADA YA VIDEO MPYA YA DIAMOND KUTOKA

Baada ya kuachia video yake mpya iliyofanywa kwa gharama ya  takribani milioni arobaini na tano za kitanzania, mwanamuziki wa muziki wa kizazi kipya Diamond Platnumz amefananishwa na marehemu Steven kanumba kwa jinsi anavyothubutu kufanya mambo makubwa kukuza Sanaa na kipaji chake tofauti na wasanii wengine wenye majina makubwa nchini.

  Hayo yameongelewa na Msanii dully sykes katika mahojiano yake na mtandao wa Bongo5 hii leo... Katika interview hiyo Dully amemuelezea marehemu kanumba kama ni mtu aliyethubutu kutumia nguvu, hali na mali, kwa ajili tuu ta kukuza jina lake kitu ambacho ni nadra sana kwa wasanii hasa wa Tanzania.
“Kanumba alikuwa ana uwezo wa hata kuchukua nauli yake ya kwenda sehemu kama Ghana kwenye tamasha la movie lakini ilimradi kujitengenezea status yake. Kwahiyo Diamond ni mtu ambaye tayari ameshajitolea kwaajili ya kuutetea muziki wetu.” Alisema Dully sykes

KIZAAZAA CHATOKEA TENA BUNGENI.....WABUNGE WA CHADEMA WATOKA NJE YA BUNGE BAADA YA MBOWE KUAMRIWA KUTOKA NJE...!!!

Wabunge wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) wametoka nje muda huu baada ya Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni ambaye pia ni Mbunge wa Hai, Mhe. Freeman Mbowe kuamriwa atolewe nje na Naibu Spika wa Bunge Job Ndugai. 


Mbowe alisimama ili achangie lakini aliamriwa na Job Ndugai kukaa chini jambo ambalo hakuliafiki na kuendelea kusimama. Baada ya tukio hilo, Ndugai aliwaamuru askari wa bunge kumtoa nje Kiongozi huyo wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni na ndipo mzozo ulipotokea.

Hali hiyo ilitokea wakati wa Majadiliano ya Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Mabadiliko ya Katiba wa mwaka 2013. Mbowe aligoma kutolewa nje ya bunge baada ya askari kufika alipokuwa amekaa kwa lengo la kumtoa nje, ndipo ilipotokea sintofahamu na mzozo mkubwa ndani ya bunge hali iliyopelekea wabunge wote wa Chadema kutoka nje.

Hali kama hii pia ilitokea jana wakati muswada wa marekebisho ya pili ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, Sura ya 83 ukisomwa na kupelekea wabunge wa vyama vya Chadema, CUF na NCCR-Mageuzi kutoka nje wakishinikiza muswada huo usisomwe hadi maoni ya wadau kutoka Zanzibar yapatikane.

MAGAZETI LEO ALHAMISI SEPTEMBA 05, 2013

DSC 0020 2b75e
DSC 0021 88774

ATAFUNWA USO NA MWAJIRI WAKE NYUMBANI


IMG 4471 6ee8f
KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida mkazi wa Kijiji cha Nyabibuye Kakongo katika Wilaya ya Kibondo mkoani Kigoma, Susuluka (16) anadaiwa kujeruhiwa vibaya usoni na bosi wake, Imani Paulo (36) kwa kung'atwa ng'atwa usoni na kisha kunyofolewa macho, pua na meno kubaki nje, kama ambavyo anaonekana pichani ukurasa wa mbele.

Tukio hilo ambalo tunaweza kulifananisha na dunia kuelekea kufika mwisho, limegusa hisia za watu wengi hasa wakazi wa Kibondo, huku wengine wakitokwa na machozi kutokana na kuguswa na ukatili ambao amefanyiwa kijana huyo.Tunaweza kufikiria kuwa tukio hilo ni sinema, lakini Mkuu wa Wilaya ya Kibondo, Venance Mwamotto, ameliambia Majira kuwa tukio hilo limetokea miezi miwili iliyopita.


Akizungumza na Majira katika mahojiano maalumu, Mwamotto, alisema kuwa kabla ya kijana huyo kujeruhiwa na bosi wake, alimtuma dukani ili akamnunulie soda.Aliliambia Majira kuwa baada ya kufika nyumbani alimkuta bosi wake akiwa amemkaba koo mbwa na kutokana na maumivu aliyokuwa akiyapata mbwa huyo, alianza kuhema akitoa ulimi nje.


DC Mwamotto alisema kuwa mtuhumiwa huyo ghafla alianza kuung'ata ulimi wa mbwa na kisha kumeza vipande jambo lililosababisha mbwa huyo kupiga kelele kutokana na maumivu.Aliongeza kuwa aliendelea kula vipande vya ulimi huo wa mbwa hadi alipoumaliza.

WABUNGE CHADEMA, CUF NA NCCR MAGEUZI WATOKA NJE....!!!

mbowe_chadema_08064.jpg
Wabunge wa Kambi ya Upinzani Bungeni jana jioni walitoka ndani ya Ukumbi wa Bunge, baada ya kupuuzwa kwa mwongozo wao wa kutaka kuahirishwa kujadiliwa kwa Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, hadi hapo Zanzibar itakaposhirikishwa.Wabunge waliotoka bungeni jana yapata saa 12.15 ni kutoka vyama vya Chadema, CUF na NCCR- Mageuzi huku Mbunge wa Vunjo na Mwenyekiti wa Taifa wa Tanzania Labour Party (TLP, Augustine Mrema akiendelea kubaki ukumbini.

Kitendo cha wabunge hao wa upinzani kilionekana kuwakera baadhi ya wabunge wa CCM, ambao walisikika wakiwakejeli kwa kupiga meza huku wakisema: "Kwendeni zenu, tumewazoea."
Wakati wabunge hao wakiondoka, Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai, alikuwa akiwasisitiza wabunge wanaobakia wawe watulivu, maana kuna usalama wa kutosha ndani ya ukumbi huo.
"Mnaotoka nimewaona wote na mnanijua," alisikika Naibu Spika Ndugai akiwatahadharisha wabunge wa upinzani waliosusa mjadala huo.
Wabunge wa CCM waliendeleza vituko ambapo baada ya wapinzani kutoka, wabunge Juma Nkamia (Kondoa Kusini), Hilary Aeshi ( Sumbawanga Mjini) na Murtaza Mangungu (Kilwa Kaskazini) walikwenda kukaa katika viti vya kambi ya upinzani.

Kabla ya kutoka kwa wabunge hao wabunge wawili kutoka CUF waliomba mwongozo wa Spika, wakitaka muswada huo kuondolewa ili kuwapa nafasi Wanzanzibar kutoa maoni yao.
Mbunge wa Mkanyageni, Habib Mohamed Mnyaa (CUF) aliomba mwongozo akitaka muswada huo uondolewe, hadi hapo Wazanzibar watakaposikilizwa.

Alisema kuwa kwa maoni ya Kamati ya Katiba, Sheria na Utawala wamesikiliza maoni ya wadau wengi, lakini Zanzibar hawakwenda kuwasikiliza wadau wa eneo hilo.

MUSEVENI AWAKUTANISHA RAIS KIKWETE NA KAGAME

museven_d895a.jpg
Rais wa Uganda, Yoweri Museveni ameitisha mkutano wa dharura wa marais wa nchi za Maziwa Makuu (ICGLR), kujadili hali ya usalama Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.Rais Jakaya Kikwete ni miongoni mwa waalikwa kwenye mkutano huo ambao pia unatarajiwa kuhudhuriwa na Rais wa Rwanda, Paul Kagame.


Wakati hali ya usalama Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ikidhoofika, katika siku za karibuni, uhusiano wa Tanzania na Rwanda umekuwa wa shaka hasa baada ya Rais Kikwete kuishauri Serikali ya Rwanda kukaa na wapinzani ili kumaliza mzozo uliolikumba eneo la Maziwa Makuu.

Rais Kikwete alitoa ushauri huo wakati akiwa katika sherehe za maadhimisho ya miaka 50 ya Umoja wa Afrika (AU), zilizofanyika mjini Addis Ababa, Ethiopia. Mkutano wa leo utafanyika kwenye Ukumbi wa Commonwealth Resort, Munyonyo katikati ya Jiji la Kampala.  Tembelea http://jambotz8.blogspot.com/ kila siku.

Kwa mujibu wa taarifa Rais Museveni ameitisha mkutano huo hasa kuzungumzia hatua ya Umoja wa Mataifa kupambana na Kundi la Waasi wa M23.

Mbali na viongozi hao wa Tanzania na Rwanda, viongozi wengine wanaotarajiwa kuhudhuria mkutano huo wanatoka Angola, Burundi, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Jamhuri ya Kongo, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Kenya, Sudan, na Zambia.

SAKATA LA AGNESS MASOGANGE, AINGIZWA KWENYE CHUMBA CHA MATESO SAA 24. ... AWATAJA WALIOMTUMA

http://4.bp.blogspot.com/-LIqEEeOg9jY/UYOuPv4TsvI/AAAAAAAAfUY/LO4pQ528Ack/s1600/masogange.jpg

IMEVUJA! Staa muuza nyago kwenye video za wasanii wa muziki wa kizazi kipya na filamu za Kibongo, Agnes Gerald ‘Masogange’ na shosti wake, Mellisa Edward kabla ya
kupandishwa kizimbani kwa msala wa dawa za kulevya ‘unga’ Afrika Kusini waliingizwa kwenye chumba cha mateso kwa saa 24 ili kutaja waliowatuma.

Habari kutoka kwa chanzo chetu kilichopo jijini Johannesburg nchini humo zilidai kuwa baada ya kukamatwa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Oliver Tambo, walipelekwa polisi ambapo walichukuliwa maelezo.

Ilielezwa kuwa mwanzoni waligoma kueleza mzigo huo wa kilo 150 wa unga ulikuwa wa nani hivyo ikabidi polisi wa upelelezi watafute njia nyingine ya kuwalainisha kwa kuwabembeleza kuwa wakieleza ukweli wataachiwa.

MATESO SAA 24
Chanzo hicho kilisema kuwa baada ya mbinu hiyo kushindikana ndipo wawili hao wakaingizwa kwenye chumba maalum cha mateso ikiaminika kuwa watasema aliyewatuma.

MFANYABIASHARA ANUNUA NDEGE YA BOING 747 JUMBO NA KUIGEUZA NYUMBA YA KULALA WAGENI....!!!



Ndani ya ndege hii "nyumba ya kulala wageni" kuna vyumba 27, unapata utandawazi, vumba vina luninga, imesha aanza kuchukuwa wageni wa kulala na ipo karibu na uwanja wa ndege wa  Arlanda airport karibu na mji wa Stockholm, Sweden
The grounded Boeing 747 is now a fixed hostel at Arlanda airport, near Stockholm, where gusts can even pay to stay in the cockpit suite


Hii ni sehemu iliyokuwa ya rubani wa ndege hiyo unaweza kulala hapa kuanzia  £170 kwa usiku mmoja


The rooms are all kitted out with flatscreen TVs, WiFi and en-suites



Wednesday, September 04, 2013

WAZAZI WATELEKEZA WATOTO HOTELINI KWA MIEZI MITATU, WADAIWA MILIONI 3

Na Steven Kanyeph - SHINYANGA 
Wazazi ambao hawajulikani makazi yao maalumu wameitelekeza familia ya watoto wao wanne katika hoteli ya Ibanza iliyopo mjini Shinyanga kwa takribani miezi 3 ambapo mpaka sasa wanadaiwa kiasi cha shilingi milioni tatu. 

Mhasibu wa Hoteli hiyo bwana Julius Kiungu amemtaja bi Christina Peter ambaye ni mzazi wa watoto hao kuwa alifika katika hoteli ya Ibanza Mei, 15 mwaka huu akiwa na watoto wa wanne kwa lengo la kupumzika. Bi Chritina ambaye ni mzazi wa watoto hao alieendelea kuwepo katika hoteli hiyo kwa takribani wiki mbili lakini baada ya hapo aliondoka bila taarifa na kuwatelekeza watoto wake katika hoteli hiyo. Tembelea http://jambotz8.blogspot.com/ kila siku.

Mmoja wa watoto hao aliyejitambulisha kwa jina la Teddy Masumbuko mwenye umri wa miaka 20 amesema kuwa anashangazwa na kitendo cha mama yao kuondoka bila kutoa taarifa huku akimuacha na wadogo zake watatu wenye umri mdogo. Msemaji wa hoteli hiyo bwana Julius Kiungu anawaomba ndugu, jamaa na marafiki wa familia hiyo wafike ili kuwachukuwa watoto hao kwa ulinzi na usalama wa watoto hao.

MWANAMKE AKAMATWA NA DAWA ZA KULEVYA UWANJA WA NDEGE JNIA LEO MCHANA JIJINI DAR ES SALAAM TANZANIA

Jitihada za kurejesha heshima kwa viwanja vya ndege nchini zilizoanzishwa na waziri wa uchukuzu Dk. Harisson Mwakyembe zinaonekana kuzaa matunda baada ya mwanadada kutoka nchini Nigeria Anthonia Ojo (25) kukamatwa na kete 99 za madawa ya kulevya Dar es Salaam leo.

Zifuatazo ni picha mbalimbali za tukio zima la kunaswa kwa mtuhumiwa huyo ambapo anashikiliwa na polisi kwa uchunguzi zaidi wakati kete hizo zimepelekwa kwa ofisi ya Mkemia Mkuu kwa uchunguzi zaidi. 

ANTHONIA OJO AKIWASILI KITUO CHA POLISI CHA JNIA BAADA KUKAMATWA.
ANTHONIA OJO AKIELEKEA KWENYE GARI BAADA YA KUKAMATWA

MAGAZETI YA LEO JUMATANO SEPTEMBA 04, 2013

DSC 0018 857f5
DSC 0019 bd620

WAJUA KWANINI UNAHITAJI KULALA?

kulala_39d75.jpg
Wanasayansi wanaamini kuwa wamepata sababu moja mpya ya kwa nini tunahitaji usingizi.
Wanasema kuwa kulala kunasaidia katika kujenga celi mpya za ubongo.

Usingizi unasaidia kuzalisha upya celi za ubongo ambazo nazo hujenga kemikali inayojulikana kama Myelin ambayo ni muhimu katika kulinda ubongo wetu kwa ambavyo unafanya kazi.


Matokeo ya utafiti huu ambayo yalijitokeza katika panya wa mahabara, huenda yakachochea maelezo zaidi kuhusu umuhimu wa usingizi katika kukabarabati celi za ubongo na kukuza celi mpya pamoja na kuulinda kutokana na magonjwa.

Daktari Chiara Cirelli na wenzake kutoka chuo kikuu cha Wisconsin waligundua kuwa Panya hao walipokuwa wanalala, ndipo kemilaki hiyo ilikuwa inatengezwa kwa wingi na celi za mwili.

Tuesday, September 03, 2013

WIMBO MPYA WA DIAMOND - NUMBER ONE


MWANAMKE ANASWA NA SARE ZA JWTZ....!!!


JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, limemkamata Saida Mohamed (30), mkazi wa Mwasonga Kigamboni, akiwa na sare za Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ). 
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana, Kamishna wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleimani Kova, alisema mtuhumiwa huyo alikamatwa Agosti 31, mwaka huu, katika eneo la Mwasonga, Kigamboni.

Alisema Saida alikamatwa na suruali saba, mashati saba ya kombati, kofia 10, shati mbili nyepesi, fulana mbili na kofia moja aina ya bareti, vyote vikiwa mali ya JWTZ.

Alisema mtuhumiwa huyo, alikuwa na begi moja la kuwekea nguo za jeshi, cheo kimoja cha Koplo na mikanda miwili ya kijeshi.

Alisema uchunguzi unaendelea juu ya mwanamke huyo ili kubaini sababu za kumiliki sare za jeshi, kabla ya kufikishwa mahakamani.

Katika tukio jingine, polisi wamemkamata Husein Mkondoa (25), mkazi wa Gongolamboto Mzambarauni, akiwa anaendesha pikipiki huku akiwa amevaa nguo za kiraia na kofia ngumu ya kijani yenye nembo ya Polisi.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...