Sunday, June 09, 2013

AKAMATWA KWA KUIBA STULI YA MWENGE WA UHURU...!!!

 

JIJI la Arusha limeendelea kujijengea sifa ya kuwa moja ya maeneo yenye vituko, kufuatia kijana mmoja mkazi wa eneo la Phillips, kata ya Sekei jijini humo, Hamad Rashid (32) kukamatwa leo akiiba kiti (stuli) kinachotumika kuwekea mwenge wa Uhuru wakati mwenge ukiwa katika mbio zake mkoani Arusha.
Tukio la kuiba na kisha kukamatwa limetokea jana saa 11 jioni katika eneo la Sanawari Mataa eneo lililopangwa kwaajili ya mkesha wa mwenge huo baada ya kukamilisha mbio zake na kazi ya kuweka mawe ya msingi na uzinduzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo.

Kamanda wa polisi mkoa wa  Arusha Liberatus Sabas ameithibitishia Nkoromo Blog kutokea tukio hilo na kwamba mtuhumiwa huyo alikamatwa na polisi waliokuwa wakiulinda mwenge pamoja na kiti hicho.

SALAMA JABIR ATAMANI KUOLEWA NA A.Y.....!!!

  

Mtangazaji mahili wa show za TV/Radio aliyeisimamisha wima show mpya na kali inayorushwa kupitia channel 5 ‘Mkasi’ namzungumzia Salama Jabir ametupia ‘neno’ kupitia kipindi hicho kuwa huenda siku moja akaolewa na AY!

Kama uliiangalia show ya Mkasi jumatatu ama marudio yake leo (jumamosi) ambapo crew nzima ya kipindi cha mkasi chini ya C.E.O na Producer wa show Ambwene Yesaya ‘AY’ walikuwa wakieleza changamoto na mambo mbalimbali waliyokutana nayo wakati wanaanza kufanya kipindi hicho, mwishoni Salama ambae alikuwa akimuelezea AY kuwa ni msanii ambae anajivunia kufanya nae kazi kutokana na jinsi alivyomchapakazi na mtu wa kuaminika alimaliza kwa kusema “huenda ipo siku moja tutaona..!”.

Wote tunajua Salama  alivyo mtu wa utani sana, kitu kinachoongeza burudani ya ziada katika show zake, alitamka hivyo na kumgeukia AY akimuuliza, na AY mwenyewe akajikuta anacheka na kukubali.
Pengine ulikuwa ni utani tu, lakini hakuna aijuae kesho ukizingatia wote wako single!

"MNAOWANIA URAIS MSIKUBALI KUPOKEA PESA ZA HUYU MFANYABIASHARA FISADI AMBAYE NI KINARA WA MADAWA YA KULEVYA".... REGINALD MENGI


Mwenyekiti wa makampuni ya IPP Reginald Mengi ametoa ya moyoni kwa wote wenye mpango wa kugombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania miaka miwili ijayo.

Bwana Mengi ameyatoa maombi yake ya moyoni na kuyaweka hadharani kupitia akaunti yake ya twitter June 7, na hiki ndicho alichokiandika.

“Nawaombea Mungu wanaotaka Urais wasipokee mshiko wa mfanyabiashara fisadi mkubwa ambaye pia ni kinara wa madawa ya kulevya.”

Swali ni mfanyabiashara gani, hilo linaweza kuwa ni jiwe gizani kama yupo kweli aliyetajwa litakuwa limemfikia. 
Na  kama  kuna  msomaji  wetu  anayemjua, ANARUHUSIWA  KUMTAJA  kwenye  COMMENTS  hapo  chini

WASHINDI WA TUZO ZA MUZIKI ZA KILI ( KILIMANJARO ) 2013


KALA JEREMIAH, OMMY DIMPOZ  WATISHA KWA KUZOA TUZO TATU 

* CHALZ BABA,  , OMMY DIMPOZ  WAZOA TUZO MBILI MBILI

NEY WA MITEGO ABEBA TUZO NDANI YA SIKU YAKE YA KUZALIWA

*OMMY DIMPOZ AMSHUKURU ZITTO KABWE KWA KUFANIKISHA UTENGENEZAJI WA VIDEO YAKE YA BAADAE

* ZEMBELA ATISHA KWA USHEHERESHAJI

* SALEHE ABDALLAH YAZIPU NA KILIMANJARO BAND WABEBA TUZO ZA HESHIMA
* LADY JAY DEE ABEBA TUZO YA MSANII BORA WA KIKE


MBUNGE WA MTWARA MJINI AKAMATWA NA POLISI KWA TUHUMA ZA KUCHOCHEA VURUGU ZA MTWARA

Jeshi la Polisi mkoani Mtwara limemkamata mbunge wa Mtwara Mjini (CCM), Hasnain Murji likimtuhumu kuchochea vurugu za kupinga mradi wa bomba la gesi kutoka mkoani humo kwenda jijini Dar es Salaam.

Habari zilizopatikana na kuthibitishwa na Msemaji wa Jeshi la polisi nchini, Advera Senso zinaeleza kuwa Murji alikamatwa jana jioni nyumbani kwake maeneo ya Shangani mjini Mtwara.

Kukamatwa kwa mbunge huyo kunakuja ikiwa zimepita siku tano tangu viongozi wanne wa vyama vya upinzani mkoani Mtwara, kufikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Mtwara, Juni 4, mwaka huu wakikabiliwa na mashtaka matatu ikiwamo kula njama, kufanya uchochezi na kuamsha hisia mbaya kwa wakazi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Washtakiwa hao ni Katani Ahmed Katani (33) na Saidi Kulaga (45) wa CUF, Hassan Uledi (35) wa NCCR Mageuzi na Hamza Licheta (51) wa TLP, wote wakazi wa Mtwara.

Taarifa zaidi zilieleza kuwa baada ya polisi kumkamata mbunge huyo, walifanya upekuzi katika nyumba yake kwa saa kadhaa na baada ya kujiridhisha walikwenda kupekua na ofisi yake.


“Amekamatwa kwenye saa 11:00 jioni, hata hati ya kukamatwa kwake imeeleza kuwa anatuhumiwa kuchochea vurugu za kupinga gesi inayopatikana mkoani Mtwara kwenda Dar es Salaam,” alisema Katibu wa Mbunge huyo, Meckland Millanzi.

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI JUNI 9, 2013

2 b911e

3 21fb8

Saturday, June 08, 2013

WENGI WANACHANGANYA MAMBO, ILA HUU NDIO UHUSIKA WA BIG BROTHER NA FREEMASON

WATU WANASEMA MANENO UUMBA, INAWEZA KUA KWELI AU SI KWELI. JIONI HII WAKATI NIKIZUNGUKA ZUNGUKA NIMEKUTANA NA PICHA HAPO JUU IKIICHAMBUA LOGO MPYA YA BIG BROTHE. KAMA UNAVYOONA HAPO JUU KATIKA PICHA UTAONA KUA LOGO HIYO INAHUSISHWA NA MAMBO YA FREEMASON. UKIANZA NA HILO JICHO PAMOJA NA VITU VINGINE.

 SO KAZI KWAKO KUCHAMBUA PUMBA ZIPI NA MCHELE UPI.

HII NDO NYUMBA YA MASANJA MKANDAMIZAJI ALIYO JENGA KIJIJINI KWAO

Aliyekuwa na Ngwair "M 2 The P" Aongea na Kusema Haya...!!!

 'M 2 the P' ambaye awali naye aliripotiwa kuwa amefariki kabla ya taarifa hizo kukanushwa, alisema jana kuwa hadi sasa hajui nini kiliwatokea.
Msanii huyo alisema kwamba hakumbuki kilichotokea hadi wakazidiwa na kukimbizwa hospitali wakiwa hawajitambui.

Alisema pia bado anajisikia anaumwa hadi sasa licha ya kuruhusiwa kutoka katika hospitali ya St. Hellen Joseph ya Afrika Kusini alikokuwa amelazwa.
chanzo:Nipashe
Msanii 'M 2 the P' ambaye alikuwa na marehemu Albert Mangweha nchini Afrika Kusini wakati rapa huyo anafariki na yeye pia kuzidiwa hadi kulazwa katika chumba cha wagonjwa mahututi, alihudhuria mazishi mjini Morogoro juzi.

MAGARI MATANO YALIYOWAHI KUTUMIWA NA HAYATI BABA WA TAIFA ENZI ZA UHAI WAKE

Leo tupo katika utalii wa ndani kwa kutazama baadhi ya  magari aliyotumia Baba wa Taifa na Rais wa kwanza wa Tanzania Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere wakati wa harakati za Uhuru na baada ya Uhuru mpaka alipofariki Oktoba 14,1999. Maelezo ya makala haya ni kwa mujibu wa nyaraka zilizopo Makumbusho ya Taifa, Dar es Salaam hasa kuhusiana na magari na miaka ya magari yalipotumika. Fuatana nasi.
1.AUSTIN MORRIS A-40

AUSTIN MORRIS A-40

 Gari aina ya  Austin Morris A-40 lilitengenezwa nchini Uingereza kati ya mwaka 1940 – 1950. Ni gari la kwanza kutumiwa na Baba wa Taifa na Rais wa kwanza Tanzania hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI JUNI 8, 2013 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.
.
.
.

SHOW YA SNURA YAACHA WANAUME MIDOMO WAZI, KWELI MAJANGA


 

Naamini kwapicha hizi uwezi kosa show yake jumapili hii NEW MAISHA CLUB atazindua video yake ya majanga kuwa mjanja kuwa wa kwanza kuiona, atasindikizwa na WEMA SEPETU atakata utepe wa video ya majanga,MIRROR,SAMIR,ALI NIPISHE,TIMBULO,BAUCHA,MENINAH, na MADEE kiingilio 10,000 tu hii show sio yakukosa kabisa.
 

MWIGIZAJI WA KIKE WA BOLLYWOOD “JIAH KHAN” AJIUA IKSA MAPENZI


Muigizaji maurufu ambae ni mmoja kati ya wanadada warembo nchini India anaejulikana kama “Jiah Khan” amekutwa amekufa juzi kwa kujiua baada ya kujua Boyfriend wake ana mwanamke mwingine….

Mama yake na Khan amesema kua alirudi na kukuta mwili wa mtoto wake akiwa ameshakufa huku Police wakiwa bado wanachunguza chanzo cha kifo cha mrembo huyo ila baadhi ya majirani walizungumza na Mtandao wa BBC na kusema kua wanachujua mwanadada Khan alikua na mkwaruzano na BF wake…..

Jiah Khan amefariki wakiwa na Miaka 25 na alijipatia umaarufu mkubwa Inchin india baada ya kuigiza na mkongwe wa tasnia ya movie anaijulikana kama Amitah Bachchan na pia aliweza kuigiza na Aamir Khan na Akshay Kumar kwa wale mnaofatilia Bollywood Movies hakika mnawatambua hawa.

mwili wa Jiah Khan ulipelekwa Hospital kwa uchunguzi zaidi…..


Khan alizaliwa New York na akakulia London kabla ya kwenda Mumbai India na kujiingiza kwenye mambo ya sanaa ya uigizaji wa filamu…

Filamu yake ya Mwisho kuigiza inaitwa Housefull ambayo ilitoka mwaka 2010..

TAZAMA VIDEO YA MAZISHI YAKE HAPA

Popout

SPIKA wa Bunge, Anne Makinda amekiri kuwepo kwa vitendo ngono UDOM.

SPIKA wa Bunge, Anne Makinda amekiri kuwepo kwa vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia na rushwa ya ngono kwa wanafunzi wa kike katika Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) na hivyo kukataa mwongozo wa mbunge akisema hali iko hivyo.


Makinda alitoa kauli hiyo jana mjini hapa wakati Bunge likiwachagua wawakilishi wake katika mabaraza ya vyuo na SADC-PF, ambapo Naibu Waziri wa Jamii, Jinsia na Watoto, Ummy Mwalimu aliuliza swali hilo la uwepo wa vitendo vya rushwa ya ngono.


Mwalimu alimuuliza mmoja wa wagombea, Murtaza Mangungu (CCM) kuwa UDOM imekithiri kwa vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia kwa wanafunzi wa kike kuombwa rushwa ya ngono na baadhi ya wahadhiri wasio waadilifu.

Naibu waziri huyo alitaka kujua, Mangungu ataondoshaje kero hiyo kwa wanafunzi wa kike chuoni hapo, endapo atachaguliwa kuwa mjumbe wa baraza.

Katika majibu yake, Mangungu alisema kuwa atashirikiana na wenzake kuhakikisha wanaondosha kero hiyo kwa wanafunzi wanaofanyiwa vitendo hivyo.

HOUSE GIRL AJINYONGA KISA PENZI LA CHRISTOPHER...!!






Mfanyakazi wa ndani aliyejiua kisa mapenzi aitwaye Devotha Sanga leo ameagwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar es Salaam. 
Marehemu Devotha alijinyonga Juni 4 mwaka huu akiwa nyumbani kwa bosi wake eneo la Kitunda jijini Dar kwa wivu wa mapenzi. 
Devotha alikuwa katika penzi na kijana mmoja aliyejulikana kwa jina moja la Christopher anayedaiwa kuwa na wapenzi wengi kiasi cha kusababisha marehemu kuchukua uamuzi huo. 
Baada ya kuagwa mwili wa Devotha umesafirishwa kuelekea Njombe kwa mazishi.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...