Monday, May 20, 2013

BUNGE LAAHIRISHWA BAADA YA KAULI NZITO TOKA UPINZANI


Bunge limeahirishwa baada ya kambi upinzani kudai kwamba serikali inatoa kucha, macho, meno na kuwaua waandishi wa habari. Hayo yalikuwepo ktk hotuba ya kambi ya upinzani iliyosomwa na msemaji wa wizara hiyo mheshimiwa Sugu. Kwa mujibu wa asasi ya kimataifa (jina limenitoka) inafuatilia haki na usalama wa waandishi wa habari, Tanzania iko ktk nchi kumi hatari kwa maisha ya waandishi wa habari ktk ripoti yake ya 2012.

Kama serikali haihusiki, kwa nini serikali isiunde tume ya kimahakama kama ilivyoombwa na chadema ili tujue ukweli? Ama waunde tume ya mahakama au wakubali tu kwamba wao ndo wanaohusika.

JK: MNAOTAKA URAIS 2015 ANZENI KUPITAPITA.


MWENYEKITI WA CCM DK JAKAYA KIKWETE.
MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Jakaya Kikwete amefungua milango kwa kuwataka baadhi ya watu ndani ya chama hicho wanaowania urais mwaka 2015 kuendelea na mchakato huo.
Rais Kikwete amewatahadharisha watu hao kuendesha kampeni zao kwa ustaarabu pasipo kuibua chuki wala kujenga makundi ambayo alisema ni hatari kwa kuwa yanaweza kukipasua chama.
Rais Kikwete aliyasema hayo katika mkutano ndani wa wabunge wa chama hicho uliofanyika jana katika ukumbi wa CCM (white house) mkoani hapa.
Mkutano huo ambao ulianza saa 3.00 asubuhi ulilenga kujadili masuala mbalimbali ya taifa ikiwamo utekelezaki wa ilani ya uchaguzi ya chama hicho katika majimbo na ahadi mbalimbali za viongozi wa taifa.
Chanzo chetu cha habari kutoka ndani ya ukumbi huo kilieleza kuwa Rais Kikwete aliwataka wanachama wenye nia ya kugombea urais kuwa na tahadhari na watu aliowaita vishoka wa siasa.
Kwa mujibu wa chanzo hicho, Rais Kikwete alisema watu wa aina hiyo wana tabia ya kula huku na huku kwa kujiingiza katika kambi zaidi ya moja.

Polisi Wakamatwa na Bangi Gunia 18 Wakisafirisha na Gari ya Mkuu wa Polisi

Siku chache baada ya Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam kuwakamata askari 16 wakituhumiwa kujihusisha na biashara ya magendo, askari wengine wawili wa jeshi hilo wamekamatwa mkoani Kilimanjaro wakiwa na shehena kubwa ya bangi wakiisafrisha kwenda nchini Kenya.
Askari hao walikamatwa Mei 19 mwaka huu saa nne usiku eneo la Kilemapofu, Wilaya ya Moshi Vijijini wakiwa na magunia 18 ya bangi ambayo walikuwa wameyapakia kwenye gari la Mkuu wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) mkoani Arusha aina ya Toyota Land Cruiser lenye namba PT 2025.

Akithibitisha kukamatwa kwa askari hao, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Robert Boaz alisema askari hao walikuwa wakipeleka bangi hiyo Wilaya ya Rombo kwa mfanyabiashra mmoja ambaye hakutaka kumtaja jina lake.
Kamanda Boaz aliwataja askari waliokamatwa na wanashikiliwa kwenye kituo kikuu cha polisi katika mji mdogo wa Himo kuwa ni F.1734 Koplo Edward (dereva) wa kikosi cha kutuliza ghasia (FFU) mkoani Arusha na G.2434 Konstebo George wa kituo cha polisi Ngarenanyuki Wilaya ya Arumeru.

Alibainisha kuwa kukamatwa kwa askari hao kunatokana na operesheni ya kukabiliana na dawa za kulevya inayofanywa na polisi katika mikoa ya Arusha na Kilimanjaro.

ANGALIA PICHA ZA DIAMOND, NAY WA MITEGO WAFANYA KUFURU DAR LIVE......!!!

Diamond Platnumz akiwapa hi mashabiki.
Ney wa Mitego akiwarusha wapenzi wa burudani.
Nyomi iliyoitikia shoo hiyo.

MAWAZIRI WATATU WA JK KUNG'OLEWA.

Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi  Dk Shukuru Kawambwa.
 Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Dk. Mathayo David Mathayo 
Dk. Mathayo David Mathayo, Mifugo na Maendeleo ya Uvuvi.https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjFUbOhVVOJm2f6bdqpXvu56CscHBIeGzm4K-xRWmBDHm6ydKFrQ776hSwU2kVohVht2rPOL3pxvEcg1JcJ4GiUaUfdpTgRk4_xRxonDr-2eFGrBNoBPZ8DOI2hkZ-ctvPdadyvd-RSiXg/s1600/Dk.+Fenella+Mukangara,+Waziri+wa+Habari,+Vijana,+Utamaduni+na+Michezo.JPG 
Dk. Fenella Mukangara, Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo

UPEPO mbaya ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) unazidi kuvuma, safari hii wabunge wake wakimtaka Rais Jakaya Kikwete kuwafukuza kazi mawaziri watatu.

Mawaziri wanaotakiwa kung’olewa ni Dk. Shukuru Kawambwa (Elimu na Mafunzo ya Ufundi), Dk. Mathayo David Mathayo (Mifugo na Maendeleo ya Uvuvi) na Dk. Fenella Mukangara (Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo).
Kama Rais Kikwete atakubali kuwaondoa madarakani mawaziri hao, hii itakuwa mara ya pili kwake kufanya hivyo. Mara ya kwanza ilikuwa Mei mwaka jana.

Mwaka jana Rais Kikwete aliamua kuwaengua madarakani baadhi ya mawaziri waliokuwa wakiandamwa kwa tuhuma mbalimbali, ikiwemo uwajibikaji mbovu.

Miongoni mwa walioenguliwa mwaka jana ni Dk. Haji Mponda aliyekuwa Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Mustafa Mkulo (Waziri wa Fedha), William Ngel
eja (Nishati na Madini na Ezekiel Maige (Maliasili na Utalii).

HUYU NDIE BINTI ALIYETOROKEA UINGEREZA AKIKWEPA KUTOMASWA NA MFALME MSWATI


Msichana mdogo ameomba hifadhi ya ukimbizi nchini Uingereza baada ya kukataa kwa dharau harakati za ndoa za wake wengi za Mfalme Mswati III wa Swaziland na kugoma kujiunga kwenye nyumba harimu ya wake 13.

Tintswalo Ngobeni, mwenye umri wa miaka 22, alitimkia Uingereza kutoka taifa hilo la kusini mwa Afrika akiwa na umri wa chini ya miaka 18 baada ya kuvuta hisia za mfalme huyo milionea, mtawala maarufu mkandamizaji kwa maisha yake ya anasa.

Ikiwa ni sehemu ya mila za Swazi, Mfalme Mswati III, mwenye umri wa miaka 45, anaruhusiwa kuchagua mke mpya kila mwaka.

Tintswalo, ambaye sasa anaishi mjini Birmingham, alikuwa na umri wa miaka 15 tu wakati Mfalme huyo alipofanya harakati zake baada kumuona kwenye jumba la kifalme la mke wake wa nne, LaNgangaza. Binti huyo alisema 'alitishika' pale alipogundua dhamira zake za ndoa.


Aliongeza: "Alianza kunipigia simu kwenye shule ya bweni. Aliniuliza kama ningetaka kuwa sehemu ya familia ya kifalme. Ilinibidi kukaa kimya kuhusu mashaka yangu lakini nilifahamu sikutaka kuolewa naye na kujitolea maisha yangu kwa mfalme huyo.


"Wake zake wamewekwa kwenye majumba yao, wakizingirwa na walinzi, na hakika hawawezi kwenda kokote isipokuwa tu mfalme akisema hivyo. Kitu pekee wanachofanya ni kwenda Marekani mara moja kwa mwaka, wakati mfalme huyo anapowapatia posho kwa ajili ya manunuzi."

Tintswalo alikuwa amelazimishwa kuachana na maisha ya starehe kwenye shule moja ya bweni huku shangazi yake, ambaye alikuwa mlezi wake mkuu, akisuka mipango ya kutorokea Uingereza kuungana na mama yake, ambaye alihamia mjini Birmingham miaka mitano kabla, akimtoroka mume wake mnyanyasaji.


"Sikuwa na jinsi," alisema. "Hakuna aliyewahi kumwangusha mfalme huyo au kuthubutu kumdharau, hivyo nikatoweka tu."

MAGAZETI YA LEO JUMATATU TAREHE 20.05.2013

DSC 0027 30a55

DSC 0030 bf0b6

DSC 0029 ec2e3

MWANGALIE SHILOLE AKIKATA MAUNO MBELE YA MIDUME AKIWA NDANI YA GARI...!!!


 

ANGALIA VIDEO YENYEWE HAPO CHINI...

Sunday, May 19, 2013

HII NDIO MOVIE YA AJABU ILIYOFANYWA NA WASANII WA NIGERIA



Bofya hapa kuangalia movie hiyo au hapa

SIMBA NA YANGA ZAINGIZA MILIONI 500

Mwamuzi Martine Saanya wa mechi ya watani wa jadi Yanga na Simba, akiwa chini baada ya kugongana kwa bahati mbaya na mchezaji Kavumbagu wa Yanga wakati wa alipokwenda kuamulia ugomvi.
Na Boniface Wambura, 
IMEWEKWA MEI 19, 2013 SAA 6:20 MCHANA

MECHI ya watani wa jadi Simba na Yanga la Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, iliyochezwa jana (Mei 18 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kumalizika kwa mabingwa wapya Yanga kushinda mabao 2-0 imeingiza sh. 500,390,000.

Mechi hiyo namba 180 ambayo ilikuwa kati ya saba la kuhitimisha ligi hiyo msimu wa 2012/2013 ilishuhudiwa na watazamaji 57,406 waliokata tiketi kwa viingilio vya sh. 5,000, sh. 7,000, sh. 10,000, sh. 15,000, sh. 20,000 na sh. 30,000.

Kila klabu imepata mgawo wa sh. 123,970,927.45 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 76,330,677.97.
Kiingilio cha sh. 5,000 ndicho kilichovutia watazamaji wengi ambapo waliokata tiketi hizo walikuwa 19,039 na kuingiza sh. 95,195,000 wakati kile cha sh. 7,000 kiliingiza watazamaji 17,647 na kupatikana sh. 123,515,000.

Mgawo mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 63,036,064.81, tiketi sh. 3,818,890, gharama za mechi sh. 37,821,638.88, Kamati ya Ligi sh. 37,821,638.88, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 18,910,819.44 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 14,708,415.12.

"WANAOCHOCHEA VURUGU ZA KIDINI NI WATU WALIOTUMWA NA MATAIFA YA NJE"..... RAIS KIKWETE


Rais Jakaya Kikwete amebainisha kuwa vurugu za kidini na kisiasa zinazotokea nchini, zina uhusiano na watu wa nchi za nje.
div style="line-height: 16.796875px; margin: 0px; text-align: center;"> Kikwete alitoa kauli hiyo jana kwenye ibada maalumu ya kuwekwa wakfu kwa Askofu Mkuu wa Sitta wa Kanisa Anglikana Tanzania, Dk Jacob Chimeledya.
Rais Kikwete alikuwa mgeni rasmi kwenye ibada hiyo iliyofanyika kwenye Kanisa Kuu la Roho Mtakatifu.
“Wanaohamasisha vurugu hizo ni watu wenye uhusiano ya karibu na watu wa nje ambao mambo yakiharibika nchini watakuwa wa kwanza kupanda ndege, ilhali wakiendelea kutoa matamko ya uchochezi wakiwa nje ya nchi wakati wengine wakiendelea kuumia,” alisema Kikwete.
Ibada hiyo ilifanyika chini ya ulinzi wa polisi na askari wa usalama, na ilihudhuriwa na Askofu Mkuu wa Anglikana duniani, Justin Welby.
Rais Kikwete alisema amekuwa akichukizwa na vurugu za kidini zinazofanywa na baadhi ya watu wasioitakia mema Tanzania, huku wakijua kuwa amani ikitoweka ni gharama kubwa kuipata.

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI TAREHE 19.05.2013

DSC 0001 147d5
DSC 0004 f935c

JACQUILINE WOLPER ATAJWA KWENYE LIST YA WASANII AMBAO NI FREEMASONS...!!

Inawezekana kila kitu kina wakati wake, kuna muda watu walikuwa wakisikia neno ‘Freemason’ ama ‘Illuminate’ kama inavyojulikana nchini Kenya wengi walikuwa wanaiona ni habari kubwa, lakini kwa sasa hivi inaweza kuchukuliwa kama sio big deal.

Sababu ni ile ile kuwa wengi wanaoendelea kwa haraka ama kuwa juu katika kile wanachokifanya basi utasikia huyo ni member wa Freemason, kwa upande wa Marekani wanasema ‘he/she just sold her/his soul to the devil’.  Japo kwa upande wa Marekani wapo wanaokiri kufanya hivyo kweli, ila kwa Africa Mashariki hakuna msanii aliyewahi kukiri.
Lakini yote hayo ni kama yanakanganya na kuonekana kama hayana mantiki hasa pale ambapo vithibitisho vya kinachoongelewa huwa havileti mantiki ya moja kwa moja. Pengine watu wanatafuta pesa kwa bidii na kumuomba Mungu lakini kwa kuwa kwenye mstari wa juu wanajikuta wanahisiwa kuwa member wa secret society (Freemason). Oh..au labda ndo vile kwa upande mwingine lisemalo lipo na kama halipo laja !
Tunathubutu kuziita blaa blaa kwa upande mwingine, lakini tukiweka kwenye mabano kuwa inaweza kuwa na ukweli, who knows!
Mtandao wa malimwengu wa nchini Kenya huenda ukawa na mfano mzuri wa kile nilichokitaja hapo juu, mtandao huo kupitia mwandishi wake imetaja majina ya wasanii wa Tanzania na Kenya wanaosemekana kuwa ni wafuasi wa Freemason, lakini kizuri zaidi ni kwamba mtandao huo umejaribu kuonesha vithibitisho na kushindwa kupata jibu la moja kwa moja kwa nini wasanii hawa wamekumbwa na hili. Inabaki hivyo hivyo kuwa tetesi tu.
Hawa ni wasanii waliotajwa na maelezo yanayowahusu:
TANZANIA:
1.Naseeb Abdul Jumaa (Diamond Platinum)
Picha aliyopiga mwaka jana akiwa na mzungu anaeaminika kuwa ni moja kati ya viongozi wa Freemason wakiwa wameweka pozi na kuonesha ishara inayooaminika kuwa ni ya Freemason, na kwamba alipoulizwa yeye alisema hakufahamu kama alikuwa anaelekezwa kupiga picha kwa pozi la ki-freemason. Kwa mujibu wa mwandishi anaona inaweza kuwa kweli kwa sababu anaonekana kuenjoy!

HAYA NDIO MAJIBU YA HALIMA MDEE KUHUSU STORY ZA YEYE AKUJIHUSISHA NA MAPENZI YA JINSIA MOJA



Kupitia season mpya ya Clouds Fm, ndani ya so so fresh na fetty, Mh Halima Mdee jana amefunguka juu ya swali aliloulizwa kuhusu story zilizosambaa kuwa anashiriki mapenzi ya jinsia moja.
aah unajua huwezi kuzuia watu kusema, na mimi huwa sihangaiki na watu wanasema nini, lakini ukitaka kumjua Halima unaweza ukamchunguza kirahisi sana, kwa kumuangalia alipotoka, historia yake na mahusiano yake, ambayo mengine ni wazi sana watu walikuwa wanayajua, 
watu wanapenda ku speculate pale ambapo wanaona kitu ambacho hawati kuona, sasa hilo swala lilishaandikwa sana, nadhani walioandika baadae wakaja kuomba radhi kwasababu waligundua wameandika kitu kisicho sahihi, probably kutokana na sauti yangu you know, probably kutokana na tembea yangu, kwasababu mimi nimekulia kwenye familia ya wanaume watupu umeona eeh, mimi nimekuwa ni mpambanaji tokea utotoni, kwasababu nimezungukwa na jeshi la kibabe, thats who iam, lakini mtu anaetaka kumjua Halima na ana uhuru tu, hata akitaka niwatajie list ya watu wangu i can do that, lakini sidhani kama is their damn business, cause ma life is personal, na wakitaka kuchunguza wachunguze kwa mpango wao na watapata taarifa, kwa uhuru tu, na wanaweza wakatoa tangazo kwamba jamani watu waliowahi kuwa na uhusiano na huyu if any wajitokeze, watajitokeza kama wapo upande huo, watajitokeza kwasababu sasa hivi si dunia huru bana

Ufaransa yakubali ndoa ya jinsia moja



Rais wa Ufaransa, Francois Hollande, ametia saini sheria yenye utatanishi, inayohalalisha ndoa kati ya watu wa jinsia moja.
Ufaransa sasa imekuwa nchi ya 14 duniani kuruhusu ndoa kama hizo.
Makundi ya watu wanaofanya mapenzi ya jinsia moja nchini Ufaransa yamefurahi kuwa hatimaye sheria hiyo imepitishwa.
Wanasema kuna marafiki kadha wanaosubiri kufunga ndoa na maelfu ya watoto wanaolelewa na watu wa jinsia moja 
ambao sasa watapata hifadhi kisheria.
Wanaopinga sheria hiyo wamehamaki.
Wanaona kuwa Rais Hollande ameshughulika mno na ndoa kati ya jinsia moja kwa sababu ameshindwa katika maswala muhimu zaidi - kama swala la uchumi wa nchi.
Maandamano mengine ya kupinga ndoa kati ya jinsia moja yanapangwa kufanywa tarehe 26 May. 
Yanaweza kuwa makubwa na ya fujo kama yaliyopita.
Sababu ni upinzani dhidi ya ndoa za jinsia moja umechanganyika na malalamiko mengine ya mrengo wa kulia dhidi ya serikali.
Na hali nchini sasa ni tete.
Lakini kwa kweli vita vimemalizika.
Watu wa jinsia moja sasa wataanza kufunga ndoa nchini Ufaransa.
Baadhi ya wanasiasa wa mrengo wa kulia wataahidi kuwa watabatilisha sheria hiyo wakipata madaraka, lakini historia inaonesha kuwa kufuta mabadiliko kama haya katika jamii ni shida sana.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...