Thursday, May 09, 2013

NAFASI ZA AJIRA ZA KADA ZA AFYA KWA MWAKA 2012/2013

Coat of arms of Tanzania
Katibu Mkuu Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, alitangaza nafasi za ajira kwa Wataalam wa Kada za Afya kwa mwaka 2012/2013 ambapo tarehe ya mwisho ya kuwasilisha maombi hayo ilikuwa tarehe 10 Mei, 2013. Kwa tangazo hili Wananchi wanajulishwa kuwa muda wa kuwasilisha maombi hayo umeongezwa hadi tarehe 20 Mei, 2013.  Aidha inasisitizwa kuwa hata wahitimu wa mwaka 2012 wanapaswa kutuma maombi yao kwa sababu hakutakuwa na utaratibu wa wahitimu kupangiwa vituo vya kazi moja kwa moja.Maombi hayo yaendelee kuwasilishwa kwa njia ya Posta kwa kutumia anuani iliyopo chini ya tangazohili. 

Tunaomba radhi kwa usumbufu wowote utakaojitokeza.

KAIMU KATIBU MKUU,

WIZARA YA AFYA NA USTAWI WA JAMII,

S.L.P. 9083,

DAR ES SALAAM.

MBUNGE GODBLESS LEMA NA MKUU WA MKOA WA ARUSHA MULONGO USO KWA USO LEO ........... WAONE WALIVYOCHUNIANA


p1 6ed46


photo

Naibu waziri wa maliasili na utalii Lazaro Nyalandu Katikati akiwa na mbunge wa Arusha mjini Godbless Lema kushoto na Mkuu wa mkoa wa Arusha Maggesa Mulongo wakati wakikabidhi misaada ya kibinadamu kwa wahanga wa bomu kwenye hospitali ya St.Elizabeth jijini Arusha Leo Asubuhi

HakiElimu YAKATAA KUFUTA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE.

Hayo yalielezwa jana jijini Dar es Salaam na muungano wa asasi tano za kiraia uliowakilishwa na Mkurugenzi Mtendaji wa HakiElimu, Elizabeth Missokia.

Asasi zilizotoa tamko la pamoja huku zikipendekeza njia sahihi ya serikali kuwekeza katika elimu ni pamoja na Hakielimu yenyewe, Policy forum, Sikika, TenMet na TGNP.
Kwa niaba ya mitandao hiyo mkurugenzi huyo alisema hakukuwa na haja ya kufuta matokeo hayo na kufanya maboresho kwa kuwa sababu zilizosababisha kufeli kwa wanafunzi zinajulikana na si kama serikali inavyodai kwa sasa.

Missokia alisema kabla ya serikali kutoa uamuzi huo ilitakiwa kuweka wazi mapendekezo ya Tume ya Waziri Mkuu iliyoundwa kuchunguza matokeo hayo ili wadau wa elimu wapate fursa ya kuona sababu zilizochangia kushuka kwa ufaulu katika mitihani hiyo.

“Kwa kufuta matokeo hayo bila wadau kujua sababu na kutoa mchango wao inawaaminisha Watanzania kwamba sababu nyingine hata kama zipo ziliathiri kwa kiwango kidogo matokeo hayo na suala la upangaji wa madaraja kuonekana ni sababu kubwa zaidi kuliko nyingine,” alisema Missokia.

RATIBA YA KOMBE LA SHIRIKISHO AFRIKA HII HAPA.


KLABU ya Tout Puissant Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), ambayo inajivunia washambuliaji wawili wa Kitanzania, Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu itamenyana na Liga Maculmana ya Msumbiji kuwania tiketi ya kucheza hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika. Hiyo inafuatia upangwaji wa droo ya hatua ya 16 Bora ya michuano hiyo, inayodhaminiwa na Orange mjini Cairo, Misri leo. Katika droo hiyo, AS FAR Rabat ya Morocco iliyoitoa Azam FC katika Kombe la Shirikisho imepangwa kukutana na wapinzani wao, FUS Rabat. Katibu Mkuu wa CAF, Hicham El Amrani aliongoza droo hiyo kwa pamoja na wawakilishi wa baadhi ya klabu zinazoshiriki michuano hiyo.



Klabu nane zilizotolewa katika Ligi ya Mabingwa, St George, CA Bizerte, TP Mazembe, Enugu Rangers, JSM Bejaia, FUS Rabat, Stade Malien na Entente Setif zimeingia kwenye mbio za kuwania kurithi taji la AC Leopards ya Kongo, mabingwa wa Kombe la Shirikisho na mechi za kwanza zitachezwa kati ya Mei 17, 18 na 19 mwaka huu wakati marudiano yatakuwa kati ya Mei 31 , Juni 1 na 2. Mazembe ambao ni mabingwa mara nne Afrika, walitolewa na Orlando Pirates ya Afrika Kusini katika Raundi ya Tatu ya Ligi ya Mabingwa kwa jumla ya mabao 3-2, wakifungwa 3-1 Afrika Kusini na kushinda 1-0 nyumbani.

DROO KAMILI YA 16 BORA KOMBE LA SHIRIKISHO:
Stade Malien (Mali) vs Lydia (Burundi)
Enugu Rangers ( Nigeria) vs C.S.S (Tunisia)
FUS Rabat ( Morocco) vs ASFAR (Morocco)
CAB (Tunisia) vs Ismailia (Misri)
E.S Setif ( Algeria) vs US Bitam (Gabon)
JSM Bejaia ( Algeria) vs E.S.S (Tunisia)
TP Mazembe (DRC) vs Liga Maculmana (Msumbiji)
St George (Ethiopia) vs ENPPI (Misri)  

JK aaga kikosi cha kwenda DRC

Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama ya Tanzania, Rais Jakaya Kikwete amewaaga wapiganaji wa Tanzania wanaokwenda DR Congo kulinda amani kwa kuwadhibiti waasi wa vikundi mbalimbali kikiwamo cha M23 walioko Mashariki wa nchi hiyo.

Amiri Jeshi Mkuu Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi bendera kiongozi wa batalioni ya  wanajeshi wa JWTZ wanaokwenda kujiunga na  jeshi la Umoja wa Mataifa la kulinda amani Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo,  katika sherehe za kuwaaga zilizofanyika Msangani, Kibaha, Mkoa wa Pwani jana.Picha na Ikulu 

Kikwete alimkabidhi bendera kiongozi wa batalioni ya wapiganaji wa JWTZ wanaokwenda kujiunga na Jeshi la Umoja wa Mataifa la kulinda amani nchini humo katika hafla iliyofanyika Msangani, Kibaha, Mkoa wa Pwani jana. Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Shamsi Vuai Nahodha na Mkuu wa Majeshi Jenerali Davis Mwamunyange ni miongoni mwa mashuhuda katika hafla hiyo.
“Ninawatakia kila la kheri kwenye mapambano,” Amiri Jeshi Mkuu alimwambia kiongozi wa Batalioni ya Wanajeshi wa JWTZ wanaokwenda nchini humo. Tanzania inaungana na Afrika Kusini na Malawi kufanya kuwapo kwa kikosi cha askari 3,100 huku Tanzania ikipeleka askari 850 kwa ajili ya kazi hiyo.
Vikosi vya awali vya Tanzania vimekwishatangulia nchini humo vikiongozwa na Jenerali James Mwakibolwa anayeongoza Brigedi hiyo chini ya UN, na tayari amewasili kwenye Mji wa Goma, ambao ndio Mji Mkuu wa Jimbo la Kivu ya Kaskazini unaokaliwa na waasi wa M23 tangu Aprili 2012.
Kwa mujibu wa Mtandao wa Monusco, vikosi vingine vya wapiganaji wa Tanzania na Afrika Kusini vitawasili wiki ijayo wakati Wanajeshi wa Malawi haijafahamika tarehe ya wao kuwasili.
Msemaji wa wapiganaji wa M23, Kanali, Vianney Kazarama alikaririwa akisema: “Tuko tayari kwa mapambano, wapiganaji wako kambini Rumangabo, wakifanya mazoezi makali ya kushambulia, kujilinda na mbinu za kukabiliana na adui pamoja na kucheza kung fu.

Wednesday, May 08, 2013

AUNTY LULU...... "NIMEAMUA KUACHA BIASHARA YA KUJIUZA.....NATAKA KUWA MJASIRIAMALI"



Siku chache baada ya msanii wa filamu Bongo, Lulu Semagongo ‘Aunty Lulu’ kunaswa kwenye mtego wa kujiuza, sasa ameamua kubadilisha mfumo wa maisha aliyokuwa akiishi zamani na kuwa na mwingine mpya.

Katika ‘exclusive interview’ na paparazi wetu jijini Dar, juzikati, Aunty Lulu alifunguka kuwa kwa sasa ameamua kubadilika kwani kama ni starehe amefanya sana pamoja na uchafu mwingi ila kutokana na mtego wa kujiuza kumnasa na ushauri aliopewa na familia yake, amebadilika na sasa amegeukia kwenye ujasiriamali.
Alisema kuwa anawashukuru waandishi wa habari wa magazeti ya Global Publishers kwani wamebadilisha maisha yake, kama siyo wao angefikia hatua mbaya lakini kwa sasa ametulia na anafanya mambo ya maendeleo tofauti na zamani ambapo alikuwa hajielewi anafanya nini.

“Yaani kutokana na mtego wa kujiuza nimeamua kubadilika kwa sababu jamii ilinichukulia tofauti sana hivyo nikaamua kufanyia kazi ushauri wa familia yangu niliokuwa nikipewa kila siku lakini nikawa naukataa.
Kwa sasa nafanya ujasiriamali na ninafurahia maisha haya kuliko yale niliyokuwa nikiishi zamani.
Aunty Lulu kwa sasa anamiliki duka la vipodozi na ni wakala wa kutoa na kuweka fedha kwa kupitia mitandao ya simu za mkononi maeneo ya Kinondoni Kanisani, Dar ambapo ndipo anashinda kwa sasa na kwa mujibu wake  ameachana kabisa na kujiachia kwenye sehemu za starehe na kufanya mambo yasiyotakiwa katika jamii.

SIR ALEX FERGASON KUSTAFU MWISHO WA MSIMU HUU


Taarifa rasmi zinasema Kocha wa timu ya Manchester United Sir Alex Fergason Ameamua kustafu Mwisho wa Msimu, Tayari bodi ya timu hiyo imepokea taarifa toka kwa kocha huyo tayari kwa majadiliano ya kumtafuta mrithi wa kocha huyo aliyewapa mafanikio makubwa timu ya Manchester united kwa kipindi cha muda mrefu aliyokaa katika timu hiyo..

Kocha huyo mwenye umri wa miaka 71 ataondoka mwisho wa msimu huu na mechi yake ya mwisho ataiongoza Manchester United Dhidi ya West Bromwich Albion tarehe 19 Mei .
Akiwa kocha wa Manchester united Sir Alex Fergason Ameipa timu hiyo jumla ya makombe 38 toka ameanza kuifundisha timu hiyo mwaka 1986.

KINANA AJIBU TUHUMA ZA MCHUNGAJI MSIGWA


Dodoma. Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana amesema anaamini chanzo cha kuchafuliwa kwake na wapinzani ni wadhifa wake.
Akizungumza na mwandishi wetu Dodoma jana, Kinana alisema anaamini kuwa kama asingekuwa na wadhifa huo, asingesakamwa kwa tuhuma alizoziita za uzushi.
Aprili 29, mwaka huu, Msemaji wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni kwa Wizara ya Maliasili na Utalii, ambaye pia ni Mbunge wa Iringa Mjini (Chadema), Mchungaji Peter Msigwa alimtuhumu Kinana kujihusisha na biashara haramu ya meno ya tembo na kudai kuwa meli iliyokuwa chini ya uwakala wa Kampuni Sharaf Shipping inayomilikiwa na Kinana ilikamatwa huko Vietnam na nyara hizo za Serikali.

“Hivi vitu havinisumbui. Hapa tatizo ni kuwa Katibu Mkuu wa CCM. ‘I am a senior officer’ (Ofisa Mwandamizi) sasa katika chama changu kama ningekuwa nimekaa nyumbani nafanya biashara zangu yasingetokea haya.
“Nataka kuwaambia tu, waelewe kuwa hawawezi kunitoa katika ajenda yangu ya msingi. Hii ni sawa na mwanajeshi anayekwenda kupigana vita na adui halafu akawa na vikundi vidogo vinakushambulia kutoka kila upande kukutoa katika lengo la msingi... ni lazima mtu ukomae na ili ufanikiwe,” alisema Kinana.

KADINAL PENGO ASISITIZA TENA KUWA ALIYERUSHA BOMU SI MUISLAMU.......KIKWETE AWATAKA WATU WAENDELEE KUSALI

Kadinali Pengo

“Jana (juzi), niliongelea kwamba suala zima la tukio la Arusha halihusiani na imani yoyote ya kidini. Tamko hilo nilitamka kutokana na taarifa nilizofikishiwa na watu ambao sikuweza kuwa na shaka kwamba wanaoniambia ni kweli na sidhani kama ningekuwa na sababu ya kusema wamefika kwa kunidanganya kwa hiyo tamko litakuwa limesimama juu ya msimamo huo,” alisema Kadinali Pengo na kuongeza:

“Lengo la msingi kabisa, langu na la kanisa ni kwamba tukio lolote lile liwe kwa nia mbaya au nzuri kwa upande wetu isiwe ni sababu ya kuanza mapambano na kuwa chimbuko la ukosefu wa amani katika nchi yetu,” alisema Pengo.

MUSWADA WA KUZUIA MAANDAMANO NCHINI WAANDALIWA


Katika hali ya kushtusha Waziri wa mambo ya ndani Emmanuel Nchimbi aliliambia bunge jana  jioni  kwamba serikali  imeridhia kuleta mswada bungeni ili itungwe sheria ya kuzuia maandamano kote nchini.

Waziri Nchimbi alisema kuwa  hiyo ndiyo njia pekee ya kuondoa uvunjifu wa amani nchini unaofanywa na watu wasiolitakia mema Taifa....

Alisema mswada huo utaletwa wakati wowote kuanzia sasa akimaanisha tayari umeshakamilika.Nchimbi alikuwa akishangiliwa sana na wabunge wa CCM wakati alipokuwa akitamka maneno hayo. 

Huenda  azimio hili litakuwa ni pigo kubwa kwa demokrasia katika ukanda huu wa Afrika Mashariki. 

Ikumbukwe ni hapo juzi  tu Chadema kilidai kunasa mpango wa siri wa serikali  wa kuzuia maandamano na mikutano ya hadhara ili kudhibiti wapinzani kuiimarisha CCM.

HILI NDO NENO LA P-FUNK MAJANI KWA LADY JAYDEE KUHUSU BIFU LA JIDE NA CLOUDS

Producer mwenye historia kubwa na ya kipekee katika muziki wa Bongo Fleva P-Funk Majani ameonesha kumuunga mkono Lady JayDee na kwamba anadhani ni muda sasa wengine wakafuata nyayo zake, yeye mwenyewe majani amemhakikishia Jide kuwa yuko nae “Count Me in”.
Ameongeza kuwa endapo wasanii na watayarishaji wa muziki wakiungana hakuna kitakachowazua isipokuwa Mungu.

Hizi ni Tweet za P-Funk Majani za May 4:

@JideJaydee I think its really high time others follow in ur Footsteps!! Count Me in!

HIKI NDICHO ALICHOSEMA JACKLINE WOLPER BAADA YA MAGAZETI KUANDIKA KUWA AMETUPIWA ZAGA ZAKE NJE YA NYUMBA ALIYOKUWA AKIISHI


JESHI LA TANZANIA LIMESHATUA CONGO..... WAASI WA M23 WAANZA KUHAHA KWA KUJIKOSHA KWA WANANCHI


Kwa mujibu wa mwandishi aliye na waasi  wa  m23, Diana Katabarwa kwenye Blog yake  anamnukuu kiongozi wa kisiasa wa M23  Mr. Bisimwa akiwambia wakazi wa North Kivu kuwa majeshi ya Tanzania na South Africa nimajeshi dhalimu yaliyo jaa rushwa na hayawezi kuibadili Congo.... 

Bisimwa anadai  kwamba  majeshi  ya  Tanzania  yamekuja kuiba mali na kumsaidia KABILA awatawale   hali  itakayosababisha   jeshi lake la FDLR na waasi wa MAI MAI wapewa nafasi ya kuwa pora mali zao na kuwabaka wake zao na watoto....

Mbali  na  hayo,  bwana Busimwa anadai kinyume na taarifa zilivyo , kikosi cha jeshi la Tanzania kikiwa na askari 450 kimesha ingia mashariki ya CONGO kwenye mji wa UVIRA SOUTH KIVU huku Kamanda wao (TPDF) akiwa mjini Goma.  

Kikosi cha jeshi la SOUTH AFRICA kiko mita 20 kutoka waasi walipo kwenye mji wa MUNGI nje kidogo ya GOMA.  

Pia aliwaeleza wananchi hao kuwa kuna makomandoo 30 wa jeshi la Ufaransa ambao wako mjini GOMA na  wamefikia Linda Hotel... 


BUSIMWA alidai wafaransa ndio walisimamia mauaji ya kimbari ya Rwanda ,kwa hiyo kuwepo kwao ni ishara mbaya kwa wakazi wa mashariki ya CONGO ambao wengi ni watusi

HUYU NDIO MUIGIZAJI ANGA'NGANIA WATOTO WA MICHAEL JACKSON, HUU NDO USHAHIDI ALIOTOA




MUIGIZAJI nyota kutoka nchini Uingereza, Mark Lester amesema anaendelea na taratibu za kuthibitisha kuwa watoto wa Michael Jackson ni wake.
Nyota huyo amesema anaendelea na taratibu za kupima vinasaba (DNA) ili kuthibitisha kwamba Prince, Prince II, na Paris pia ni watoto wake.Hayo yalibainishwa katika gazeti la Mirror nchini Uingereza.
“Siwezi kufanya vipimo vya vinasaba kama sijapata kibali kutoka kwa watoto pindi watakapokuwa kiumri na si muda mrefu wataamua mimi kufanya hivyo, nami nitafanya," alisema Nyota huyo.

Lester, ambaye aling'ara katika wimbo wa Oliver alikuwa rafiki wa muda mrefu wa Michael Jackson kwa zaidi ya miaka 30 iliyopita.

Pia nyota huyo alisema, mwanadada Paris amefanana kwa kila kitu na binti yake, Olivia.

Tangu Lester aanze kutoa malalamiko yake hayo kwa mujibu wa Mirror, alisema familia ya Jackson imekata mawasiliano yote na yeye.

Kwa mujibu wa Mirror, Lester halizuiliwa kuwaona watoto tangu kifo cha Michael Jackson mwaka 2009.

MAGAZETI YA LEO JUMATANO APRIL 8, 2013

1 c281d

2 108fd

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...