
MGOMBEA urais kwa tiketi ya Chadema anayeungwa mkono na vyama vingine
vitatu vya upinzani vinavyounda umoja unaofahamika kwa jina la Ukawa,
Edward Lowassa jana alichukua fomu za kuwania rasmi nafasi hiyo kutoka
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC).
Lowassa, Waziri Mkuu wa zamani aliyejiunga Chadema hivi karibuni
baada ya kushindwa katika mchakato wa kumpata mgombea urais kwa tiketi
ya CCM, sasa ameungana na wagombea wengine kujitokeza NEC kuchukua fomu
za kuwania urais.
Ametanguliwa na mgombea wa CCM, Dk John Magufuli ambaye pia ni Waziri
wa Ujenzi na Mwenyekiti wa UPDP, Fahmi Dovutwa. Wengine ni Mchungaji
Christopher Mtikila wa DP, Mac-Millan Lyimo wa TLP, Hashim Rungwe wa
CHAUMMA, Chifu Lutasola Yemba wa ADC na Dk Godfrey Malisa wa CCK. Asante kwa kutembelea blog hii, endelea kuwa nasi, like page yetu ya facebook bofya neno Jambo Tz.