Rapper Chidi Benz leo kwa mdomo wake mwenyewe amekiri kuwa alikuwa
akitumia madawa ya kulevya kwa miaka mingi. Chidi amefunguka leo kwenye
kipindi cha XXL cha Clouds FM.Alisema japo hakwenda Nairobi kwaajili ya rehab, mazingira
yalimlazimu kutafuta tiba ili aondokane na madhara ya madawa hayo.
Alieleza kuwa alipofika jijini Nairobi alikuwa akitakiwa kufanya show
nyingi na mwandaaji alimuuliza kama kuna kitu atahitaji ili awezE
kufanya show vizuri.
“Nikamwambia Yeah kuna vitu ntavihitaji,” alisema Chidi. “Nikamwambia ‘mimi bana kuna vitu ninavyovitumia nikikaa 20 minutes bila hivyo vitu ni noma nachanganyikiwa na akili tena sina, kwahiyo sijui tutafanyaje’.
Akaniambia ‘mimi ntapataje hivyo vitu Chidi na Nairobi ni gharama sana. Nikamwambia ‘mimi pia nina wazo jingine kuna mtu alinitonya kwamba kuna kitu kinaweza kikafanyika na pesa Fulani, pesa nyingi kama milioni 15, 16 hivi za kibongo.
Akaniambia kikifanyika hicho maanake vinavyofolewa kabisa hivyo vitu vilivyokuwa vinanifanya niwe hivyo. Akaniambia ‘hiyo naijua lakini ni process, ndio maana dunia nzima haifanyi’. Nikamwambia ‘mimi nafanya kwasababu nilishakutwa na vitu vingi mimi ntafanya.”


















Mussa Hassan Mgosi.