![]() |
| Kwa kawaida tumezoea kusikia kuwa vijana wakipigana kuhusu wanawake huku tukidhani kuwa wivu wa mapenzi unawatesa vijana peke yao kumbe si kweli mpaka wazee nao wanateswa sana na wivu, Hiki ndicho kilicho tokea katikati ya jiji ambapo wazee wawili walinasa na kamera yetu wakitaka kupigana kisa denti wa shule aliyekuwa akiwachanganya wote wawili bila wao kujijua utata ulikuja pale wazee hao marafiki mmoja wao alipopigiwa simu na msichana huyo baada ya kumaliza kuongea ndipo mzee wa jirani alipouliza huyo nani mwenzake akajibu huyu mpenzi wangu zai hapo ndipo ugomvi ulipoanza na wazee hao kutaka kupigana kisa mwaafunzi wa kidato cha tatu. |
Thursday, March 21, 2013
PENZI LA MWANAFUNZI LAZUA BALAA LASABABISHA VIZEE KUPIGANA HADHARANI
Wanafunzi washinda danguroni Dar
Dar
es Salaam. Baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Kata
ya Majani ya Chai iliyopo Kipawa jijini Dar es Salaam, wametajwa
kujiingiza katika kashfa ya ngono, kuvuta na kuuza bangi katika moja ya
nyumba zinazozunguka shule hiyo.
Hilo ni tukio lingine jipya, kwani mwishoni mwa mwaka jana, kuliibuka matukio ya ajabu kwa wanafunzi wa Shule ya Msingi, Ruaruke, Rufiji mkoani Pwani ambao walielezwa kujihusisha na uvutaji bangi hata kukonyeza na kubaka walimu wao.
Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Majani ya Chai, Yasinta Assey akionyesha baadhi ya nguo na viatu vya wanafunzi vilivyokutwa katika eneo linalodaiwa kuwa danguro linalotumiwa na wanafunzi wa shule hiyo, jana. Picha na Pamela Chilongola
Mkuu wa Sekondari hiyo, Jasinta Assey alikiri na kusema kwamba vitendo vya uvutaji bangi na biashara ya ukahaba kwa wanafunzi wake, vinachangiwa na askari wa Kituo kidogo cha Stakishari ambao alidai wanachukua rushwa kwa wauzaji wa bangi na nyumba bubu za wageni. Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Mkuu wa Shule hiyo, Jasinta Assey alisema ni kawaida ya polisi hao kwenda kwenye nyumba hizo kunakofanyika biashara hizo na kuchukua rushwa badala ya kutatua tatizo.
Alisema ongezeko la utoro katika shule hiyo ni tatizo kubwa na wanafunzi wa kidato cha nne wanaosoma masomo ya sanaa ndiyo wanaoongoza kwa kuvuta bangi na kwenda kufanya ngono katika nyumba zilizo jirani na eneo la shule hiyo.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa
Ilala, Marietha Minangi alisema hajapata taarifa za hali hiyo.
“Ngoja nimtume Mkuu wa Kituo cha Polisi Stakishari afuatilie kwa karibu,” alisema Minangi na kuongeza: “Lakini ngoja nikwambie, hili suala nakumbuka liliwahi kuripotiwa 2011 wakati nikiwa mkuu wa kituo hicho; nililishughulikia na tulibaini kuwa hakuna mwanafunzi ambaye alikuwa anaenda kwenye nyumba hizo kuvuta bangi wala kufanya ngono.
“Ngoja nimtume Mkuu wa Kituo cha Polisi Stakishari afuatilie kwa karibu,” alisema Minangi na kuongeza: “Lakini ngoja nikwambie, hili suala nakumbuka liliwahi kuripotiwa 2011 wakati nikiwa mkuu wa kituo hicho; nililishughulikia na tulibaini kuwa hakuna mwanafunzi ambaye alikuwa anaenda kwenye nyumba hizo kuvuta bangi wala kufanya ngono.
“Kilichotokea
kwa wakati huo ni kwamba, tuliwachukua baadhi ya wanafunzi ili
watupeleke mahali walipokuwa wakifanyia vitendo hivyo kutokana na
maelezo na vielelezo vyao, lakini hatukubaini hizo sehemu.
“Inawezekana basi haya mambo yameibuka upya baada ya kuona kuna mkuu wa kituo mwingine mpya,” alisema Kamanda Minangi.
Kutokana na matendo hayo, wanafunzi wengi walifanya vibaya mtihani wa kumaliza kidato cha nne mwaka jana.
“Walifeli sana mwaka jana hawa, walimu wapo, tunawapa nyenzo lakini hawataki, ninaiomba Serikali kuingilia kati suala hili kwani ni la muda mrefu na ni faida ya vijana hawa,” alisema.
Shule ya Majani ya Chai ilishika nafasi ya 61 kimkoa kati ya shule 226 wakati ngazi ya taifa, ilishika nafasi ya 543 kati ya shule 3,392.
Wanafunzi 274 walijisajili kufanya mtihani wa kidato cha nne mwaka jana na kati yao 130 walipata sifuri, wakati waliopata daraja la nne ni 85, waliopata Daraja la Tatu ni 18 wakati waliopata daraja la pili ni watano. Hakukuwa na daraja la kwanza na wanafunzi 36 hawakufanya mtihani.
“Baada ya kuona utoro umekithiri shuleni hapo, nilikwenda kutoa taarifa kituo kidogo cha Polisi Stakishari, lakini hawakuonyesha ushirikiano matokeo yake wanakwenda kwa wenyeji hao na kuchukua rushwa.
“Hili inaonekana kama ni dili la hawa askari, kwani wapo walionifuata na kunieleza niache kufuatilia, lakini mimi niliwaambia nitafuatilia tu na ilifikia hatua nikatishiwa maisha.
“Baada ya kuona nazidi kutishiwa maisha, niliogopa, nikaacha...na hivi ninavyoongea na wewe, najua tu watanifuata kwani nimeshaambiwa nikipita peke yangu eneo wanakofanyia biashara zao watanifanyia kitu kibaya,” alisema Assey.Mwalimu huyo alisema kwamba, wanafunzi wa kidato cha nne wanaosoma masomo ya sanaa wapo 54, lakini wakati mwingine utakuta wanafunzi watano tu darasani na waliobakia wanakwenda kuvuta bangi na kufanya vitendo vya ngono.
Assey alisema kuwa iliwahi kutokea wasamaria wema waliwapelekea baadhi ya nguo na viatu vya wanafunzi wa shule hiyo vilivyokutwa eneo wanakofanya biashara hiyo ya haramu.
“Hili darasa linaongoza kwa utovu wa nidhamu na limeshindikana...Nilikuwa nawategemea sana polisi, lakini hawaonyeshi ushirikiano wowote ule...Unaona hizi nguo za wanafunzi zililetwa na mama mmoja baada ya kuzikuta kwenye danguro ‘bubu’,” alisema Assey huku akionyesha sare hizo za shule.
SHILOLE, BABY MADAHA WAFUATA NYAYO ZA WEMA

WAREMBO wawili wanaotesa katika soko la muziki na filamu Bongo, Baby Joseph Madaha na Zuwena Mohamed ‘Shilole’ wameamua kufuata nyayo za Wema Sepetu kwa kunyoa nywele na kuonekana katika muonekano mpya.
Akizungumza na paparazi wetu, Shilole ambaye amenyoa nywele staili ya kiduku alisema ameamua kufanya bhiv yo ili kuwa na muonekano wa tofauti kwani watu wameshamzoea kila siku kumuona na mawigi na rasta.
Kwa upande wa Baby Madaha alisema ameamua kubadilisha mfumo wa maisha kuanzia nywele hadi mavazi kwani huu ni mwaka mpya hivyo kutoka na staili mpya.
Hivi karibuni Wema alikuwa wa kwanza kutangaza kuwa na muonekano tofauti kwa kutupia picha zake mtandaoni zilizomuonesha akiwa amenyoa.
CCM, Chadema Dar wamgeuzia kibao JK
Ni
nadra kutokea lakini wafuasi wa vyama vya siasa vya CCM na Chadema,
wameungana kumweleza Rais Jakaya Kikwete kuhusu kero ya maji eneo la
Kimara-Golani, Dar es Salaam.
Rais Kikwete alikutana na hali hiyo wakati akifungua Daraja
la Kimara jana, tukio hilo liliwakusanya watu wengi hasa wanachama wa
CCM na Chadema waliokuwa wamevalia sare za vyama vyao.
Wafuasi wa Chadema waliongozwa na Mbunge wa Ubungo, John
Mnyika ambao walikuwa wakipeperusha bendera za chama chao na kuimba
nyimbo mbalimbali huku wakidai maji. Hata hivyo, kutokana na hali hiyo,
wafuasi wa CCM waliungana na wenzao wa Chadema, kupiga kelele juu ya
suala hilo kiasi cha kugusa hisia za Rais Kikwete.
Akizungumza baada ya uzinduzi wa daraja hilo, Rais Kikwete
aliahidi kuitisha kikao Jumatatu ijayo kitakachomhusisha Profesa
Maghembe na maofisa wa wizara yake, wabunge wa Dar es Salaam, Mkuu wa
Mkoa, wakuu wa wilaya ili kuweka mikatati ya pamoja kutafuta ufumbuzi wa
suala hilo.
“Ninaomba Machi 25... tukutane ili tuweke mikakati ya pamoja
kutafuta ufumbuzi wa suala hili,” alisema Rais Kikwete.
Akiwa Hospitali ya Mwananyamala, Rais Kikwete alizindua
maabara ya kisasa kwa ajili ya uchunguzi na akazungumzia suala la dawa
za kulevya kwa kusema atahakikisha mapambano yanaendelea kwani dawa hizo
zinaua nguvu kazi ya taifa ambayo ni vijana.
KISA KINENE KESI YA LWAKATARE
MBOWE ASEMA HUO NI
MTIRIRIKO WA MABAVU YA DOLA
MAHAKAMA ya
Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, jana ilimfutia kesi ya makosa ya
ugaidi Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chama cha Demokrasia na
Maendeleo (CHADEMA), Wilfred Lwakatare na Ludovick Joseph, kisha
kuwakamata tena na kuwafungulia kesi mpya yenye mashitaka yaleyale.
Awali
ilielezwa kuwa Mkurugenzi wa Mashitaka ( DPP), Dk. Eliezer Feleshi,
aliwasilisha hati ya kuwafutia kesi washitakiwa kwa sababu hana haja ya
kuendelea nayo.
Hata hivyo
baada ya kuachiwa, Lwakatare na mwenzake walikamatwa tena na kufikishwa
mahakamani hapo kisha kufunguliwa kesi mpya namba 6/2013 ambayo
imepangiwa kwa Hakimu mpya, Aloyce Katemana.
Katika kesi
ya awali namba 37/2013 iliyofunguliwa na Jamhuri dhidi ya Lwakatare na
wenzake Machi 18, mwaka huu, jana ilikuwa imekuja kwa ajili ya Hakimu
Mkazi, Emilius Mchauru, kuitolea uamuzi wa ama kuwapatia dhamana
washitakiwa hao au la.
Lakini
Hakimu Mchauru alijikuta akishindwa kutoa uamuzi wake kwa
sababu mawakili viongozi wa serikali, Ponsian Lukosi, Prudence
Rweyongeza na Peter Mahugo, waliwasilisha hati hiyo ya DPP chini ya
kifungu cha 91(1) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai ya mwaka
2002.
“Kwa kuwa kesi hii Na. 37/2013 ilifunguliwa na
upande wa Jamhuri Machi 18, mwaka huu, na leo kesi hii ilikuja kwa ajili
ya mahakama kutolea uamuzi wa maombi ya washitakiwa kupatiwa dhamana au
la, pamoja na maombi mengine…mahakama hii inasema haitaweza kutoa
uamuzi wake kwa sababu DPP amewasilisha hati ya kutotaka kuendelea
kuwashitaki, hivyo mahakama hii inawafutia kesi washitakiwa wote,”
alisema Hakimu Mchauru.
Baada ya
Hakimu Mchauru kuwafutia kesi, askari kanzu waliwakamata tena
washitakiwa hao na kuwaweka chini ya ulinzi na ilipofika saa 4:20
asubuhi, waliingizwa tena katika ukumbi namba mbili wa mahakama hiyo
mbele ya Hakimu Mkazi mwingine, Aloyce Katemana.
SERIKALI YAAPA KUFA NA MATANGAZO YA DIGITAL
Mkurugenzi
wa Idara Habari MAELEZO, Asah Mwambene.
Serikali
imesema haiwezi kusitisha matangazo ya Digiatl na kurudi kwenye
analojia, akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana,
Mkurugenzi wa Idara HABARI MAELEZO, Asah Mwambene alisema seriakli
haitaraji kurudi kwenye analojia kama baadhi ya watu wanavyotaka .
aliongeza
kwa kusema mpaka kufikia hapa mchakato ulipita na maandalizi yalifanyika
ya kutosha kabla ya kuingia kwenye matangazo ya Digital.
Waziri Mkuu Pinda alipohuduria sherehe za kusimikwa rasmi Papa Francis 1 mjini Roma.
Waziri
Mkuu, Mizengo Pinda na Mkewe Tunu wakifanya mahojiano na mtangazaji wa
Radio Vatican, Padri Richard Mjigwa (katikati) kweye moja kati ya
studio za Raido hiyo Mjini Roma walikohudhuria sherehe za kusimikwa
Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani, Papa Francis 1 Machi 20, 2013.
(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).
Picha
juu na chini Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na Mkewe Tunu wakiongozwa na
Padri Alquine Nyirenda wa Makao Makuu ya Shirika la Watawa wa
Benedikti, Roma kutoka kwenye Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro la Roma
walikohudhuria sherehe za kumsimikwa kiongozi wa Kanisa Katoliki
Duniani, Papa Francis 1 kwenye viwanja vya Kanisa hiloMachi 19,2013.
Waziri
Mkuu, Mizengo Pinda na mkewe Tunu (wapili kulia) wakipata maelezo
kuhusu historia ya Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro la Roma kutoka kwa
Padri Alquine Nyirenda wa Makao Makuu ya Shirika la Watawa wa wa
Benedikti, Roma walikohudhuria sherehe za kusimikwa Kiongozi wa Kanisa
Katoliki Duniani, Papa Francis, Machi 202013. (Picha na Ofisi ya Waziri
Mkuu).
Waziri
Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la
Umoja wa Mataifa la Chakula (FAO), Jose Graziano da Silva wakati
alipotembelea Makao Makuu ya Shirika hilo Mjini Roma, Machi 20, 2013.
Waziri
Mkuu, Mizengo Pinda akikaribishwa na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la
Chakula , FAO, Bw. Jose Graziano da Silva kutia saini katika kitabu cha
wageni mshuhuri wakati alipotembelea Ofisi za FAO mjini Rome Machi 20,
2013.
Waziri
Mkuu, Mizengo Pinda akisindikizwa na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la
Chakula la Umoja wa Mataifa, FAO Bw. Jose Graziano da Silva baada ya
mazungumzo yao wakati alipotembelea makao makuu ya FAO mjini Roma,
Machi 20, 2013. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).
Maafisa 7 Waandamizi katika Wizara ya Ujenzi na Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) watimuliwa kwa Ubadhilifu na Utendaji mbovu
Waziri
wa Ujenzi Dkt. John Magufuli.
Wizara
ya Ujenzi na Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) imewafukuza kazi na
kusitisha mikataba ya Wafanyakazi Waandamizi saba wa Wizara na Wakala wa
Majengo Tanzania (TBA) kwa tuhuma za ubadhilifu na utendaji kazi mbovu.
Hatua hiyo ni sehemu ya dhamira ya Wizara ya Ujenzi ya kusafisha Wakala
zake na kuongeza ufanisi.
Katika
nyakati tofauti Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi amekuwa akipokea tuhuma za
vitendo vya ubadhilifu miongoni mwa watendaji waandamizi katika Wakala
zinazotoa huduma chini ya wizara hii. Kufuatia tuhuma hizo Mdhibiti na
Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) alifanya ukaguzi maalum katika
ofisi za TBA Mkoa wa Dar es salaam na Katibu Mkuu wa wizara Balozi
Herbert E. Mrango na Mtendaji Mkuu wa TBA Arch. Elius Mwakalinga
waliunda Kamati za kupitia taarifa za CAG na taarifa nyingine. Kamati
hizo zimeweza kubaini kuwepo kwa ukiukwaji mkubwa wa taratibu za fedha,
manunuzi na uendeshaji.
Maafisa
waliofukuzwa kazi ni pamoja na Bw. Charles Gabriel Lyatuu ambaye
alikuwa ni Meneja wa TBA mkoa wa Dar es Salaam; Bw. Ladislaus I. Kapongo
aliyekuwa Mhasibu Msaidizi (TBA mkoa wa Dar es Salaam) na Bi. Agness F.
Chambo aliyekuwa Mhasibu Msaidizi (TBA mkoa wa Dar es Salaam). Aidha,
kwa Mkurugenzi wa Biashara na Fedha Bibi Yona Orida na Injinia Charles
Makungu ambaye alikuwa ni Mkurugenzi wa Miliki wameondolewa katika
nafasi za uongozi walizokuwa nazo TBA.
Hatua
zaidi zilizochukukuliwa ni kuwashusha vyeo Meneja wa Mkoa wa Pwani Bibi
Esteria M. Nyamhanga na Bw. Samwel C. Samike ambaye alikuwa ni Meneja
wa TBA mkoa wa Mbeya.
Hatua
hizi zimechukuliwa kunatokana na watendaji hao kuhusishwa na tuhuma za
ubadhidilifu ambazo zimebainika kufanyika katika taasisi hiyo. Maeneo
ambayo yamebainika kuwa na ukiukwaji mkubwa ni pamoja na kufanya malipo
kwa kutumia mikataba isiyosainiwa na pande zote, kufanyika malipo
kinyume na taratibu za manunuzi na hata malipo kufanyika kwa fedha
taslim kinyume na taratibu.
Aidha,
eneo la manunuzi ya viwanja kwa ajili ya ujenzi wa majengo ya TBA pia
yameonyesha kuwa na vitendo vya ubadhilifu na ukiukwaji wa taratibu.
Vipo viwanja vilivyobainika kununuliwa nje ya taratibu, baadhi ya
nyaraka kuonyesha ukubwa tofauti na ule uliolipiwa, kununua maeneo
yasiyofaa kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za Serikali, kuongeza bei na
kufanyika kwa malipo kabla ya mikataba kusainiwa.
Hatua
zilizochukuliwa ni muendelezo wa juhudi za Wizara za kuhakikisha kuwa
maeneo yote yanayoashiria kuwa na utendaji ulio nje ya maadili
yanafuatiliwa na kuchukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria na taratibu za
utumishi wa umma.
Aidha,
ili kuboresha ufanisi katika Wakala hivi karibuni waliteuliwa Mameneja
wapya 15 wa TEMESA katika mikoa mbali mbali hapa nchini ikiwa ni pamoja
na kuwahamisha vituo mameneja wengine. Kwa upande mwingine, ajira za
Watendaji katika vituo vyote vya mizani tayari zimetangazwa na kwa sasa
kazi ya kupitia maombi yaliyowasilishwa inakamilishwa ili kuhakikisha
kuwa watendaji wasio waaminifu hawapati nafasi katika maeneo hayo ambayo
yamekuwa yakilalamikiwa kwa vitendo vya ubadhirifu.
Wizara
itaendelea kuchukua hatua za aina hii pale ukiukwaji wa sheria na
taratibu za utumishi wa umma utakapobainika.
Taarifa
hii imetolewa na;
M.S.
Ntemo
MSEMAJI
WA WIZARA YA UJENZI
Wednesday, March 20, 2013
NGASSA, SHILOLE WAZUA TIMBWILI CLUB
HUKU ikidaiwa kwamba ni wapenzi, mastaa wawili wa
fani tofauti, mcheza filamu na mwanamuziki, Zuwena Mohammed ‘Shilole’
na msakata kabumbu wa klabu ya Simba, Mrisho Ngassa, Jumatano iliyopita
walizua timbwili katika klabu ya usiku ya SunSiro iliyopo Ubungo
jijini Dar.

Zuwena
Mohammed ‘Shilole’.
Kwa mujibu wa chanzo chetu, Ngassa alifika katika klabu hiyo saa saba za usiku kushuhudia Bendi ya Mashujaa iliyokuwa ikitumbuiza akifuatana na watu wawili, mmoja mwanaume na mwingine mwanamke.
Inadaiwa kuwa Shilole alipoingia ukumbini humo na kuonana na Ngassa aliyekuwa na kampani yake, alipandwa na hasira na kuanza kujibishana naye.
Chanzo kinatiririka kuwa kabla Shilole hajaingia ukumbini humo, alimuomba kijana anayeuza pipi aitwaye Abdallah Rashid amuoshee gari lake kwani lilikuwa limechafuka bila ya kukubaliana naye bei.
Baada ya Shilole kutoka kwa hasira kutokana na kujibishana na Ngassa, moja kwa moja aliingia kwenye gari lake na kutaka kuondoka bila ya kumlipa kijana aliyemuoshea gari lake.
“Kwani unanidai shilingi ngapi?” Shilole alimuuliza kijana aliyesema kwamba anadai shilingi elfu tano.
“Baada ya Shilole kutajiwa kiasi hicho, alikataa kulipa kwa kuwa ni kikubwa na kumfanya kijana huyo kuwa mbogo na kuanza kurushiana maneno na staa huyo,” kilisema chanzo chetu.
Chanzo hicho kikaendelea kutoboa kuwa wakati kijana huyo akipigizana kelele na Shilole, Ngassa alitokea na kumvaa huku akimuuliza kwa nini anagombana na wanawake na kuanza kurushiana naye maneno, kiasi cha kutaka kuzipiga lakini wakatulizwa na wasamaria wema.
“Ngassa alikunjwa na jamaa ambaye alikuwa amekasirika kutokana na kudhulumiwa haki yake,” kilisema chanzo chetu.
Hata hivyo, baada ya ugomvi huo, Shilole na Ngassa kila mmoja aliingia kwenye gari lake na kutokomea bila kumlipa aliyeosha gari.
Baadhi ya mashuhuda walisema kuwa Ngassa na Shilole walikuwa na ugomvi uliohusiana na masuala ya kimapenzi.
“Hata yule mwanamke aliyekuwa na Ngassa alisema kwamba Shilole anahangaika kumfuata Ngassa wakati mcheza soka huyo hamtaki,” kilisema chanzo chetu.

Aidha, Ngassa alikanusha madai ya kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Shilole kwa kusema kuwa hawezi kutembea na msanii wa filamu.
Naye Shilole alipopigiwa simu alisema kuwa timbwili lilizuka kati yake na mtu aliyeosha gari lake bila ya ridhaa yake.
“Miye nimeenda pale kimpango wangu wala sikumfuata Ngassa ingawaje kweli nilimuona lakini wala sikuongea naye,” alisema staa wa muziki na filamu.
Kwa mujibu wa chanzo chetu, Ngassa alifika katika klabu hiyo saa saba za usiku kushuhudia Bendi ya Mashujaa iliyokuwa ikitumbuiza akifuatana na watu wawili, mmoja mwanaume na mwingine mwanamke.
Inadaiwa kuwa Shilole alipoingia ukumbini humo na kuonana na Ngassa aliyekuwa na kampani yake, alipandwa na hasira na kuanza kujibishana naye.
Chanzo kinatiririka kuwa kabla Shilole hajaingia ukumbini humo, alimuomba kijana anayeuza pipi aitwaye Abdallah Rashid amuoshee gari lake kwani lilikuwa limechafuka bila ya kukubaliana naye bei.
Baada ya Shilole kutoka kwa hasira kutokana na kujibishana na Ngassa, moja kwa moja aliingia kwenye gari lake na kutaka kuondoka bila ya kumlipa kijana aliyemuoshea gari lake.
“Kwani unanidai shilingi ngapi?” Shilole alimuuliza kijana aliyesema kwamba anadai shilingi elfu tano.
“Baada ya Shilole kutajiwa kiasi hicho, alikataa kulipa kwa kuwa ni kikubwa na kumfanya kijana huyo kuwa mbogo na kuanza kurushiana maneno na staa huyo,” kilisema chanzo chetu.
Chanzo hicho kikaendelea kutoboa kuwa wakati kijana huyo akipigizana kelele na Shilole, Ngassa alitokea na kumvaa huku akimuuliza kwa nini anagombana na wanawake na kuanza kurushiana naye maneno, kiasi cha kutaka kuzipiga lakini wakatulizwa na wasamaria wema.
“Ngassa alikunjwa na jamaa ambaye alikuwa amekasirika kutokana na kudhulumiwa haki yake,” kilisema chanzo chetu.
Hata hivyo, baada ya ugomvi huo, Shilole na Ngassa kila mmoja aliingia kwenye gari lake na kutokomea bila kumlipa aliyeosha gari.
Baadhi ya mashuhuda walisema kuwa Ngassa na Shilole walikuwa na ugomvi uliohusiana na masuala ya kimapenzi.
“Hata yule mwanamke aliyekuwa na Ngassa alisema kwamba Shilole anahangaika kumfuata Ngassa wakati mcheza soka huyo hamtaki,” kilisema chanzo chetu.

Shilole.
Paparazi
wetu alipompigia simu Ngassa kumuuliza kuhusiana na timbwili hilo,
alikiri kutokea na kusema kuwa alikuwa akimsaidia Shilole.Aidha, Ngassa alikanusha madai ya kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Shilole kwa kusema kuwa hawezi kutembea na msanii wa filamu.
Naye Shilole alipopigiwa simu alisema kuwa timbwili lilizuka kati yake na mtu aliyeosha gari lake bila ya ridhaa yake.
“Miye nimeenda pale kimpango wangu wala sikumfuata Ngassa ingawaje kweli nilimuona lakini wala sikuongea naye,” alisema staa wa muziki na filamu.
CHANZO; GLOBAL PUBLISHERZ
HATIMAYE SERIKALI NA TFF ZAFIKIA MUAFAKA KUHUSU UCHAGUZI MKUU
Serikali imekubali
mchakato wa uchaguzi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
uendelee kwa sharti la kuhakikisha haki inatendeka kwa wagombea
waliofika mbele ya Kamati ya Rufani ya Uchaguzi.
Akizungumza na
Waandishi wa Habari leo mchana, Rais wa TFF, Leodegar Tenga amesema
uamuzi huo umefikiwa kwenye kikao kati ya uongozi wa Wizara ya Habari,
Vijana, Utamaduni na Michezo chini ya Waziri Dk. Fenella Mukangara, TFF
na Baraza la Michezo la Taifa (BMT).
Amesema baada ya
maafikiano hayo, TFF italiandikia barua Shirikisho la Kimataifa la
Mpira wa Miguu (FIFA) ambalo ndilo lililosimamisha mchakato huo ili
litume ujumbe wake kwa ajili ya kusikiliza malalamiko ya wagombea
walioenguliwa.
Rais Tenga ambaye ameishukuru Serikali kwa kuruhusu
mchakato huo uendelee, pia ameahidi kuwa uchaguzi wa TFF utafanyika
kabla ya Mei 25 mwaka huu kama walivyokubaliana na Serikali, na kuwa
haki si tu itatendeka bali ionekane imetendeka.
“Serikali
imetuelekeza uchaguzi ufanyike kabla ya Mei 25. Tumewaambia kwetu huko
ni mbali. FIFA wakija hata kesho wakituambia endeleeni sisi tuko tayari.
Hesabu zetu ziko tayari, makabrasha yote yako tayari yanasubiri
mkutano tu. Labda itakuwa kutoa muda tu kwa wajumbe walioko mbali
waweze kujiandaa, maana wajumbe huwezi kuwaita ghafla,” amesema.
Amesisitiza kuwa TFF
ilishapanga tarehe ya uchaguzi, lakini ukasimamishwa na FIFA baada ya
baadhi ya walioenguliwa kulalamika huko. Hivyo maneno kuwa TFF hawataki
uchaguzi kwa sababu wanataka kuendelea kubaki madarakani haya maana
hata kidogo.
Hivyo amewataka wagombea wote waliofika kwenye
Kamati ya Rufani ya Uchaguzi na wakaendelea kujiandaa vizuri, kwani
FIFA watakapofika watawasikiliza wao na vyombo vilivyowaengua.
Pia amesema TFF ina
heshimu Serikali na itaendelea kufanya hivyo, lakini vilevile lazima
iheshimu FIFA sababu iko kwenye mpira wa miguu, na FIFA ndiyo
wasimamizi wa mchezo huo duniani.
Amewakumbusha
wanachama wa TFF, hasa wajumbe wa Mkutano Mkuu kufahamu kuwa TFF ina
katiba, lakini ni lazima pia wafahamu kwanini kuna FIFA.
Rais Tenga
amewahadharisha watu wanaopitapita mikoani kuomba saini za wajumbe ili
kuita Mkutano Mkuu wa dharura wakati wanajua mkutano ulishaitishwa,
lakini ukasimamishwa na FIFA. Jambo hilo kikatiba ni kosa.
MSANII MATUMAINI ANAOMBA ASAIDIWE....KWA SIKU ANAMEZA VIDONGE 39
Mchekeshaji na muigizaji wa Tanzania
Tumaini Martin ‘Matumaini’ amevunja ukimya kuelezea maendeleo ya afya
yake akidai kusumbuliwa na maumivu makali ya miguu kwasasa.
Akiongea na
BK Cop leo Matumaini amesema kuwa anaendelea kutumia dozi ingawa hali
ya afya yake bado si shwari kutokana na kugulia maumivu makali ya
Msanii huyo ameeleza kuwa kwa siku moja
huwa anameza vidonge zaidi ya 39 lakini hapati lishe nzuri kwababu ya
kutokuwa na pesa na kujinunulia chakula.
Aidha
amedai kuwa wakati alipokuwa msumbiji alipata misaada ya kifedha kutoka
kwa wasanii mbalimbali lakini hasaidiwi tena tangu alipofika Tanzania.
‘Niliomba
msaada kwenye magazeti ambapo niliacha namba zangu za tigo pesa lakini
meseji nyingi nazopokea ni za pole; hata hivyo kuna watu wanadai
wametuma kwa namba ya Michael Sangu (Mkt Chama cha waigizaji) ambayo
alitoa gazetini lakini mimi sikuwahi kuonana tena na Michael tangu
aliponililipia matibabu wakati natoka hospitali’. Alisema Matumaini
Mnamo
Februari 9 mwaka huu Matumaini aliruhusiwa kutoka hospitali ya Amana
jijini Dar es salaam alipokuwa amelazwa kwa siku tatu tatizo kubwa
likiwa ni miguu na alitakiwa kurudi tena hospitali baada ya kumaliza
dozi aliyoandikiwa na daktari.
Awali
Matumaini alikwenda kuishi nchini msumbiji na kuripotiwa kusumbuliwa na
maradhi, lakini alishindwa kutibiwa akiwa huko ambako Naibu Waziri wa
Habari vijana na utamaduni na michezo Bw Amos Makalla akishirikiana na
baadhi ya wasanii alichukua jukumu la kutoa nauli ya kumrudisha nchini.
SOURCE::MPEKUZI::
WASANII WAMELAZIMIKA KUTOA PENZI KWA WATOTO WADOGO KWA SABABU WANAUME WAMEADIMIKA..." BABY MADAHA
MSANII wa
nyimbo za muziki wa bongo fleva anayefahamika kwa jina la Baby Madaha
amewashukia baadhi ya wasanii wa kike nchini wanaojihusisha na maswala
ya ngono na wanaume wenye umri mdogo maarufu kwa jina la 'Kijibwa' kuwa
ni hali ya kukata tamaa na ushamba ndio unaochangia kufanya kitendo hiko
Akizungumza
jijini Dar es Salaam Msanii huyo alisema kuwa anashangazwa na baadhi ya
wasanii hususani wa kike kujihusisha na maswala ya ngono na wavulana
wenye umri mdogo huku wakitumia jina la 'kijibwa' kwa ajili ya kukidhi
matakwa yao ya kingono
Alieleza
kuwa hali ya kukata tamaa ndio chanzo kinachopelekea baadhi ya wasanii
hao kujihusisha na maswala ya ngono na vijana wadogo huku wakijipa moyo
kuwa wanatafuta faraja wakiwa na vijana hao
"Unajua hao
wasichana wanaonekana kukata tamaa kwa kukosa mwanaume wanaolingana
kiumri ndio maana ajimchukua mtoto mdogo na kumuhudumia kila kitu na
ndipo hapo jina la 'kijibwa' linapotumika kwa kumfananisha mvulana huyo
na mbwa unayemuudumia kila kitu huku kazi yake kubwa inakuwa ni kumlinda
tu " aliongezea kuwa
"Kwa sababu
mvulana huyo anapewa kila kitu ikiwemo kununuliwa hadi nguo yeye
anakuwa na kazi moja tu hivyo hapo hamna mapenzi zaidi ya utumwa na
kumsababisha mvulana huyo kukosa uhuru wa kuwa na maamuzi ya mambo yake
binafsi" alisema Madaha
Kutokana na
hicho kitendo Madaha alikiita ni ushamba kwa kuwa na mahusiano ambayo
hayana msingi wowote ule na si kwa ajili ya mtazamo wa maisha hivyo
mahusiano hayo hayaendana na mazingira ya nchi na kusababisha
kudharaulika kwenye jamii inayomzunguka
Alitoa wito
kwa wasichana hao wanaojihusisha na maswala hayo kuwa wanachotakiwa ni
kujiamini na kujipanga upya kwa ajili ya kupambana na maisha na
kutoyaogopa maisha hivyo wanachotakiwa ni kujipanga upya.
MSANII WA BONGO MOVIE MATATANI KWA UJAMBAZI
Lungi Mwaulanga.
STAA wa filamu za Kibongo, Lungi Mwaulanga
hivi karibuni aliswekwa lupango katika Kituo cha Polisi Oysterbay jijini
Dar baada ya kuzushiwa kesi ya ujambazi na mpangaji mwenzake (jina
tunalo).
Akizungumza na waandishi wetu, Lungi
aliyesota mahabusu kwa siku mbili alisema hivi karibuni usiku wa manane
aligongewa mlango nyumbani kwake na watu asiowafahamu, alipotoka
alikutana na askari waliomchukua na kumwambia kwamba anatuhumiwa kwa
ujambazi.
Hata hivyo, Lungi alisema kuwa baada ya kuwauliza
askari ni wapi dada huyo amevunjiwa au kitu gani alichoibiwa, askari
walimbadilishia kesi na kumwambia kuwa amemtukana. Mpaka sasa, Lungi
yuko nje kwa dhamana
CHANZO"GUMZOLA
JIJI BLOG
WASANII WA MOVIE NA MUZIKI WAUNGANA NA MASHABIKI KUMTETEA DIAMOND
Msanii Diamond plutnum
Msanii mkali na ambaye anaongoza kwa kuandikwa sana katika vyombo vya habari Diamond platnum ameanza kupata furaha mara baada ya mashabiki kuanza kumtetea na kuonyesha kukerwa na habari zinazoendelea kuvuma kila kukicha katika magazeti,redio na hata katika tv na blog mbali mbali kuwa yeye ni fremason na nyingine zikisema anategemea waganga.

Moja Show zake Uwanja wa Taifa
Kwa wiki kadhaa sasa tumefanya utafiti na kugundua jinsi msanii huyo anavyokubalika katika jamii na hata kwa wasanii wenzake.Nadhani utakumbuka msanii Prof jay aliwahi kuandika akimtetea msanii huyu na kusema tuache majungu na kama dogo kakosea inafaa aitwe na arekebishwe na si kumponda na kumshusha kisanii kwa skendo,

Hapa akipiga Kinanda Huku Anaimba
Hivi karibuni pia baadhi ya wasanii katika page na twita zao wameonekana kuponda jinsi watu wanavyoibuka kwa kusema wao ndio waganga wanaomfanya msanii huyu kukua kisanii,wengine wakimsema mganga huyo kuwa kama anataka kumshusha Diamond basi ajipandishe yeye aimbe au awasaidie ndugu zake waimbe ili wapate pesa kama diamond na wasaidie.Wadau hao wamefika mbali na kulaani maneno ya watu kumzushia msanii huyo kuwa yeye ni fremason ...Kiukweli kwa sasa hapa nchin tanzania kumeibuka tabia ambayo hata haileweki imetokea nchi gani hadi kufika hapa kwani msanii akifanikiwa kidogo tu basi ujue atahusishwa na fremanson,nadhan mtakubaliana na mm kuwa hata kwa marehem kanumba walisema ni fremason wakaja kwa ray,jackline wolper na sasa kwa Diamond sasa swali la kujiuliza ni kwamba kuna mtu hata mmoja ambaye alikutana naye huko kwa hao jamaa akathibitisha juu ya uhalali wawasanii wetu kuwa huko?ukiwauliza utasiki sijakutana nae lakini huoni amepata mafanikio ya haraka lazima atakuwa fremason yule jaman hebu tubadilike tuswe watu wakumuabudu shetan kila saa alisema mama brayan
Kiukweli inakatisha tamaa na tutabaki hivi hivi hatutakuwa na wasanii wazuri wala wachezaji wazuri kwa sababu hatujui kuthamini vya kwetu alisema bwana mikidadi wa masaki huku bwana Ally Jo akisema anashangazwa sana na staili ya hapa bongo Nadhani hii inatokana na watu kuijua fremason juzi juzi ndio maana kila mtu akipata pesa kidogo tu za kununua nyanya basi ni fremason hebu tuelimike jaman tuache ubabaishaji tupende na kuthamini wasanii wetu
Baada ya yote hayo mwandishi wetu aimvutia wayaJack Wolper na kumuliza anajisikiaje kuhusishwa na imani ya fremason.Binafsi sipendi kuhusishwa na jambo ambalo sijalifanya wala sina ndoto nalo na siwezi kulifanya hebu jiulize super star mimi na fremason wapi na wapi kwa pesa gani nilizo nazo hadi niwe fremason hebu watu wasitake kujulikana kwa kutunga habari za uwongo,Utasikia eti diamond naye ni fremason jaman kwa hiyo prado au?basi hao fremason wana kazi.Alisema jack huku akionyesha dhahiri kukerwa na watu hao wanaotunga habari za uwongo

Msanii vicent Kigosi (Ray)
Kwa upande wa Ray alisema yeye hana la kusema kwani kama ni maneno kashayazoea hivyo hawezi kumzuia mtu kusema maana ni binadamu na wamezaliwa wanasema kwa hiyo hawampi tabu.Unajua kaka hawa ni binadamu huwezi kuwazuia cha msingi ni kufanya kazi sana ili uendeleze maisha yako ila ukiwasikiliza utaharibikiwa ndugu yangu,mimi nimezoea ila na mshauri mdogo wangu Diamond akomae afunge masikio kwa yale anayoona hayana faida na afungue masikio kwa yale yenye faida na yeye Alisema Ray Kwa upande wa Diamond alisema kuwa bado anaimani kubwa sana na mashabiki wake kuwa hawatamuangusha kwa kuwa amekula kiapo kuwatumikia na kamwe hatafanya kinyume na hilo....Kaka sina mengi ila nachoweza kusema mashabiki wangu wasivunjike moyo haya ni mapito tu na yataisha so cha msingi wajue Diamond wao ni yule yule wa kamumbie mbagala ni yule yule wa kesho so nawapenda sana hizo ni stori tu kama movie na mungu atawanyoosha kwani yeye ndiye anayenijua zaidi yao kikubwa sintatetereka kwa maneno yao nimeandaa nyimbo za kutosha kwa ajili ya watu wangu u know sasa hayo maneno hayatani felisha kwakuwa namtegemea mungu.Alisema Diamond

Moja ya Show zake
Kwasasa Diamond ni msanii anayeongoza kwakufanya shoo nyingi sana ndani na nnje ya nchi huku wengine wakimtaja kama msanii mwenye mafanikio zaidi,kwa upande wake dimond amesema anashukuru mungu kwa kupiga hatua na anategemea kuingiza gari mpya na lenye thamani kubwa sana ukiachilia mbali Prado analomiliki hivi sasa,Pia msanii huyo ameweka wazi kuwa anamalizia mjengo wake ambao umebakia hatua ndogo sana kukamilika na soon atahamia huko na familia yake kwa sasa msanii huyo ana miliki Toyota prado na Alteza aliyomnunulia mama yake.

Mashabiki wa diamond

Mashabiki wa Diamond Waliofurika kupata show
The super stars tz inapongeza sana Diamond na kumtaka kukaza buti na asife moyo kwani bado anasafari ndefu sana ya muziki wakehivyo asilewe sifa wala asiumizwe na yanayotokea kwani hata fid Q alisema usuperstar mzigo wa mwiba ukiubeba utaumia.
Msanii mkali na ambaye anaongoza kwa kuandikwa sana katika vyombo vya habari Diamond platnum ameanza kupata furaha mara baada ya mashabiki kuanza kumtetea na kuonyesha kukerwa na habari zinazoendelea kuvuma kila kukicha katika magazeti,redio na hata katika tv na blog mbali mbali kuwa yeye ni fremason na nyingine zikisema anategemea waganga.

Moja Show zake Uwanja wa Taifa
Kwa wiki kadhaa sasa tumefanya utafiti na kugundua jinsi msanii huyo anavyokubalika katika jamii na hata kwa wasanii wenzake.Nadhani utakumbuka msanii Prof jay aliwahi kuandika akimtetea msanii huyu na kusema tuache majungu na kama dogo kakosea inafaa aitwe na arekebishwe na si kumponda na kumshusha kisanii kwa skendo,

Hapa akipiga Kinanda Huku Anaimba
Hivi karibuni pia baadhi ya wasanii katika page na twita zao wameonekana kuponda jinsi watu wanavyoibuka kwa kusema wao ndio waganga wanaomfanya msanii huyu kukua kisanii,wengine wakimsema mganga huyo kuwa kama anataka kumshusha Diamond basi ajipandishe yeye aimbe au awasaidie ndugu zake waimbe ili wapate pesa kama diamond na wasaidie.Wadau hao wamefika mbali na kulaani maneno ya watu kumzushia msanii huyo kuwa yeye ni fremason ...Kiukweli kwa sasa hapa nchin tanzania kumeibuka tabia ambayo hata haileweki imetokea nchi gani hadi kufika hapa kwani msanii akifanikiwa kidogo tu basi ujue atahusishwa na fremanson,nadhan mtakubaliana na mm kuwa hata kwa marehem kanumba walisema ni fremason wakaja kwa ray,jackline wolper na sasa kwa Diamond sasa swali la kujiuliza ni kwamba kuna mtu hata mmoja ambaye alikutana naye huko kwa hao jamaa akathibitisha juu ya uhalali wawasanii wetu kuwa huko?ukiwauliza utasiki sijakutana nae lakini huoni amepata mafanikio ya haraka lazima atakuwa fremason yule jaman hebu tubadilike tuswe watu wakumuabudu shetan kila saa alisema mama brayan
Kiukweli inakatisha tamaa na tutabaki hivi hivi hatutakuwa na wasanii wazuri wala wachezaji wazuri kwa sababu hatujui kuthamini vya kwetu alisema bwana mikidadi wa masaki huku bwana Ally Jo akisema anashangazwa sana na staili ya hapa bongo Nadhani hii inatokana na watu kuijua fremason juzi juzi ndio maana kila mtu akipata pesa kidogo tu za kununua nyanya basi ni fremason hebu tuelimike jaman tuache ubabaishaji tupende na kuthamini wasanii wetu
Baada ya yote hayo mwandishi wetu aimvutia wayaJack Wolper na kumuliza anajisikiaje kuhusishwa na imani ya fremason.Binafsi sipendi kuhusishwa na jambo ambalo sijalifanya wala sina ndoto nalo na siwezi kulifanya hebu jiulize super star mimi na fremason wapi na wapi kwa pesa gani nilizo nazo hadi niwe fremason hebu watu wasitake kujulikana kwa kutunga habari za uwongo,Utasikia eti diamond naye ni fremason jaman kwa hiyo prado au?basi hao fremason wana kazi.Alisema jack huku akionyesha dhahiri kukerwa na watu hao wanaotunga habari za uwongo

Msanii vicent Kigosi (Ray)
Kwa upande wa Ray alisema yeye hana la kusema kwani kama ni maneno kashayazoea hivyo hawezi kumzuia mtu kusema maana ni binadamu na wamezaliwa wanasema kwa hiyo hawampi tabu.Unajua kaka hawa ni binadamu huwezi kuwazuia cha msingi ni kufanya kazi sana ili uendeleze maisha yako ila ukiwasikiliza utaharibikiwa ndugu yangu,mimi nimezoea ila na mshauri mdogo wangu Diamond akomae afunge masikio kwa yale anayoona hayana faida na afungue masikio kwa yale yenye faida na yeye Alisema Ray Kwa upande wa Diamond alisema kuwa bado anaimani kubwa sana na mashabiki wake kuwa hawatamuangusha kwa kuwa amekula kiapo kuwatumikia na kamwe hatafanya kinyume na hilo....Kaka sina mengi ila nachoweza kusema mashabiki wangu wasivunjike moyo haya ni mapito tu na yataisha so cha msingi wajue Diamond wao ni yule yule wa kamumbie mbagala ni yule yule wa kesho so nawapenda sana hizo ni stori tu kama movie na mungu atawanyoosha kwani yeye ndiye anayenijua zaidi yao kikubwa sintatetereka kwa maneno yao nimeandaa nyimbo za kutosha kwa ajili ya watu wangu u know sasa hayo maneno hayatani felisha kwakuwa namtegemea mungu.Alisema Diamond

Moja ya Show zake
Kwasasa Diamond ni msanii anayeongoza kwakufanya shoo nyingi sana ndani na nnje ya nchi huku wengine wakimtaja kama msanii mwenye mafanikio zaidi,kwa upande wake dimond amesema anashukuru mungu kwa kupiga hatua na anategemea kuingiza gari mpya na lenye thamani kubwa sana ukiachilia mbali Prado analomiliki hivi sasa,Pia msanii huyo ameweka wazi kuwa anamalizia mjengo wake ambao umebakia hatua ndogo sana kukamilika na soon atahamia huko na familia yake kwa sasa msanii huyo ana miliki Toyota prado na Alteza aliyomnunulia mama yake.

Mashabiki wa diamond

Mashabiki wa Diamond Waliofurika kupata show
The super stars tz inapongeza sana Diamond na kumtaka kukaza buti na asife moyo kwani bado anasafari ndefu sana ya muziki wakehivyo asilewe sifa wala asiumizwe na yanayotokea kwani hata fid Q alisema usuperstar mzigo wa mwiba ukiubeba utaumia.
Read more
Kikosi cha Morocco kutua nchini Ijumaa tayari kuikabili ‘Taifa Stars’ jijini Dar kwa mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia
Timu ya Taifa ya Morocco (Lions of the
Atlas) inatarajiwa kuwasili nchini kesho kutwa Ijumaa kwa ndege ya
Emirates tayari kwa mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia dhidi ya Tanzania
(Taifa Stars) itakayochezwa Jumapil9 na waandishi wa habari 12 utawasili Uwanja wa Ndege wa
Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) saa 8.55 mchana na utafikia hoteli ya
Kilimanjaro Hyatt Regency.
Siku hiyo Morocco inatarajia kufanya
mazoezi jioni kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karumei katika Uwanja wa Taifa, Dar es
Salaam.
Msafara wa timu hiyo yenye watu 58 wakiwemo
maofisa
na Jumamosi itafanya
mazoezi yake ya mwisho kwenye Uwanja wa Taifa kwa ajili ya mechi hiyo
itakayochezwa saa 9 kamili alasiri.
Wachezaji walioko kwenye kikosi hicho chini
ya Kocha Rachid Taoussi ni Nadir Lamyaghri, Anas Zniti, Yassine Bounou,
Younnes Bellakhadar, Abdellatif Noussair, Abderrahim Achchakir, Zoheir
Feddal, Younnes Hammal, Zakarya Bergdich na Abdeljalil Jbira.
Issam El Adou, Kamel Chafni, Salaheddine
Saidi, Mohamed Ali Bamaamar, Abdelaziz Barrada, Salaheddine Aqqal,
Abdessamad El Moubarky, Nordin Amrabat, Chahir Belghazouani, Abdelilah
Hafidi, Youssef Kaddioui, Brahim El Bahri, Hamza Abourazzouk na Youssef
El Arabi.
Wakati huo huo, tiketi kwa ajili ya mechi
hiyo zitaanza kuuzwa keshokutwa katika vituo vya Shule ya Sekondari
Benjamin Mkapa, Sokoni Kariakoo, mgahawa wa Steers ulioko mtaa wa
Ohio/Samora, Oilcom Ubungo, Kituo cha Mafuta Buguruni, Uwanja wa Taifa
na Dar Live Mbagala.
Milango siku ya mechi kwa ajili ya
watazamaji itafunguliwa saa 6 kamili mchana
Subscribe to:
Comments (Atom)




















