Sunday, October 25, 2015

UCHAGUZI WAHAIRISHWA KWA KUKOSA KARATASI ZA UDIWANI


Wakati zoezi la upigaji kura likiendelea nchi nzima wakazi wa kata ya Matongo, jimbo la Bariadi, mkoani Simiyu wameshindwa kupiga kura kwa nafasi ya udiwani kwa kile kinachodaiwa uhaba wa karatasi za kupigia kura.

Akiongea na waandishi wa habari Msimamizi wa uchaguzi katika jimbo hilo Abdallah Malela amesema kukosekana kwa karatasi ndicho chanzo cha uchaguzi kwa ngazi ya udiwani kusitishwa katika eneo hilo.

Alisema kuwa kata hiyo ina jumla ya wapiga kura 7500, na vituo 17 lakini karatasi ambazo zimetoka Tume ya ucHaguzi zilikuwa 3400 tu, huku zaidi ya wapigakura 4100 wakikosa karatasi hizo za kupigia kura.


“Baada ya kuona hali hiyo niliwasiliana na viongozi wa tume kutoa taarifa ambao waliamua kuhairisha zoezi kwa nafasi ya udiwani tu, mpaka tena itakapotangazwa na tume,” alsiema Malela.

Kwa upande wa rais na mbunge, zoezi liliendelea kama kawaida kwa kuwa karatasi hizo zililetwa za kutosha.

Kwa upande wa Jimbo la Itilima Mkoani hapa Msimamizi wa uchaguzi Alphonce Aloyce alisema zoezi lilienda salama licha ya mihuri kukwama ingawa tatizo hilo lilipatiwa ufumbuzi mapema.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...