Friday, May 10, 2013

KOCHA WA EVERTON DAVID MOYES ATANGAZWA KURITHI MIKOBA YA SIR ALEX FERGUSON MAN U



Kocha wa Klbau ya Everton, David Moyes, leo mchana ametangazwa rasmi kurithi mikoba ya Sir Alex Ferguson, aliyetangaza kujiuzulu jana, ambapo sasa kocha huyo atakua na kibarua cha mkataba wa miaka 6, ya kuinoa timu hiyo ya Mashetani wekundu.

Moyes, amesaini kataba wa miaka sita leo mchana na kutangazwa rasmi kukabidhiwa mikoba hiyo, ya Ferguson, aliyeitumikia Klabu hiyo kwa kipindi cha miaka 27 na kuipa mataji 20.

Akizungumza wakati wa mahojiano na waandishi wa habari baada ya kusaini mkataba huo, Moyes, alisema kuwa anatarajia kujiunga na wekundu hao mara tu utakapomalizika rasmi msimu huu wa Ligi ya England.

Wakati hayo yakijiri, Kuna habari zilizochini ya Kapeti hadi sasa kuwa huenda, katika msimu ujao wa Ligi Kuu ya England, Timu hito ya Man U, ikamkosa mshambuliaji wake, Wyne Rooney anayetarajia kutimka katika Kikosi hicho na badala yake sasa anayetarajia kujiunga kwa mara ya pili na kikosi hicho ni aliyekuwa mshambuliaji wa timu hiyo, ambaye kwa sasa anakipiga na Klabu ya Real Madri, Christiano Ronaldo.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...