Saturday, April 20, 2013

ROSE NDAUKA AWATEGA MADENTI WA DSJ, HIKI NDO ALICHOKIFANYA

STAA mwenye mvuto wa kipekee kwenye ‘industry’ ya filamu Bongo, Rose Ndauka hivi karibuni alitinga kivazi kifupi ambacho kiliwachengua madenti wa Chuo cha Uandishi wa Habari Dar es Salaam (DSJ) ambao walibaki kumkodolea macho mwanzo mwisho.
Mpango mzima ulitokea Aprili 13, mwaka huu katika Ufukwe wa Belinda, jijini Dar wakati mwanadafada huyo alipokuwa amealikwa katika sherehe za kuwakaribisha wanafunzi wapya wa chuo hicho.

Kutokana na kivazi hicho alichokivaa na mvuto alionao staa huyo, baadhi ya madenti wakware walionekana wakipoteza usikivu wa hotuba ya mgeni rasmi na kubaki kumtazama.
“Mh! Rose ni mzuri jamani uongo dhambi, nilikuwa nikimuona katika runinga leo nimemuona live daaah!” alisikika denti mmoja aliyeomba hifadhi ya jina lake.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...