Thursday, May 05, 2016

VYUO VIKUU BORA DUNIA

Orodha mpya ya vyuo vikuu bora zaidi duniani ya Times Higher Education, kwa kuangazia sifa za chuo kikuu husika, imetolewa, huku vyuo vikuu kutoka bara Asia vikiimarika sana. Mwaka huu, kuna vyuo vikuu 17 kutoka Asia vilivyomo kwenye orodha ya vyuo 100 bora, likiwa ongezeko kutoka vyuo 10 mwaka jana.

Kwa mara ya kwanza, kuna chuo kikuu kutoka Uchina katika 20 bora, Chuo Kikuu cha Tsinghua University kutoka Beijing ambacho kimo nambari 18. Vyuo vikuu vya Marekani bado vinatawala orodha hiyo, chuo kikuu cha Harvard kikiwa ndicho kinachoongoza. Vifuatavyo ni vyuo vikuu bora 100.

1 . Harvard University

Marekani

2 . Massachusetts Institute of Technology

Marekani

3. Stanford University

Marekani


4. University of Cambridge

Uingereza

WAPENZI WA JINSIA MOJA WAPINGA UKAGUZI WA 'TUPU ZA NYUMA'

wapenzi wa jinsia moja
 
Wanaume wawili wanaosema kuwa maafisa wa polisi wa Kenya waliwalazimisha kufanyiwa ukaguzi wa tupu ya nyuma ili kubaini kwamba walishiriki katika ngono ya mapenzi ya jinsia moja wameanzisha kesi mahakamani wakitaka ukaguzi huo kuwa ukiukaji wa katiba.

Wanasema kuwa walilazimishwa kufanyiwa ukaguzi wa magonjwa ya virusi vya ukimwi na Hepatitis kufuatia kukamatwa kwao mnamo mwezi Februari 2015 baada ya kushukiwa kwamba wanashiriki katika ngono ya mapenzi ya jinsia moja.

Vitendo vya wapenzi wa jinsia moja kushiriki ngono ni kinyume na sheria nchini Kenya na adhabu ya makosa hayo ni miaka 14 jela. Mahakama ya Mombasa imewapatia mawakili wa serikali wiki moja kutoa jibu. Chini ya sheria ya kimataifa, ukaguzi wa lazima katika tupu ya nyuma ni kitendo cha kikatili,unyama na ni sawa na mateso kulingana na kundi la haki za kibinaadamu Human Wrights Watch

KATUMBI ATANGAZA KUWANIA URAIS CONGO

 Mwanasiasa mashuhuri nchini Jamhuri ya Demokrasi ya Congo Moise Katumbi amethibitisha kuwa atagombea urais kwenye uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwezi Novemba.

Mfanyabiashara huyo na gavana wa zamani wa jimbo la Katanga alitoa tangazo hilo kupitia kwa mitandao ya kijamii. Muungano wa vyama kadha vya upinzani uliamua kumuidhinisha Bw Katumbi kuwa mgombea mwezi Machi.
Bw Katumbi, akitangaza kuwania kwake, amepuuzilia mbali madai kwamba alipokuwa waziri wa hati alitumia mamluki kutoka nje akisema habari hizo ni za uongo. Kwa mujibu wa katiba ya nchi hiyo Rais Joseph Kabila anatakiwa kuondoka madarakani mwaka huu lakini wapinzani wake wana hofu kuwa huenda ana mipango ya kusalia madarakani.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...