Friday, December 09, 2016
Tuesday, November 01, 2016
WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE KUANZA MITIHANI LEO, WAZIRI AONYA UDANGANYIFU
Wanafunzi wa kidato cha nne wakimsikiliza naibu waziri Ofisi ya Rais Tamisemi Selemani Jafo mara baada ya kukagua maandalizi ya mtihani wa kidato cha nne unaofanyika Leo.
Naibu waziri ofisi ya Rais Tamisemi Selemani Jafo akiagana na wanafunzi wa shule ya sekondari Msalato mara baada ya kuzungumza nao.
Naibu
waziri Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi),
Selemani Jafo, amefanya ziara kwenye shule mbalimbali mjini Dodoma
kuangalia maandalizi kwa ajili ya mtihani wa kidato cha nne unaoanza Leo
nchini.
Katika
ziara yake kwenye Shule ya sekondari Jamhuri, Kiwanja cha ndege na
Msalato, Jafo amewaonya walimu na wanafunzi hao nchini kuepukana na
vitendo vya udanganyifu.
Akizungumza
na walimu na wanafunzi katika shule hizo, Jafo amesema katika mtihani
huo hawatarajii kuwepo na udanganyifu kwa kuwa wamejifunza kupitia
mtihani wa darasa la saba ambapo kumekuwepo na tabia ya walimu kujificha
chooni ili kuwasaidia wanafunzi.
Amesema shule zitakazofanya fanya hivyo zitakuwa zimepoteza thamani yake. Tangaza biashara yako hapa. Pia like page yetu ya facebook Jambo Tz. tu-follow
instagram @jambotz.
WANAWAKE WANAOFANYA NGONO BILA KINGA WANAUWEZEKANO MKUBWA WA KUPATA SARATANI YA MLANGO WA KIZAZI
Naibu waziri wa Afya
Maendeleo ya jamii wazee jinsia na Watoto Dkt. Hamis Kigwangala akiwa anazungumza na
waandishi wa habari wanawake kuhusu tatizo la Saratani ya shingo ya Kizazi,
katika Ukumbi wa Olasiti Lodge Jijini Arusha, aliyepo kushoto kwake ni
Dkt. Mathew Kasumuni kutoka hospital ya Mountmeru iliyopo jijini Arusha.
Waandishi wa habari
wanawake wakiwa katika picha ya pamoja na Naibu waziri wa Afya Maendeleo ya
jamii wazee jinsia na Watoto Dkt. Hamis Kigwangala, Aliyepo kushoto kwake ni
Dkt. Mwanahamis Ghembe kutoka Mountmeru Hospital.
Naibu
waziri wa Afya Hamisi Kigwangala amesema kuwa wanawake wanaoshiriki tendo la
ndoa bila kinga wapo hatarini kupata virusi vinavyoitwa HPV
vinavyosababisha Saratani ya mlango wa kizazi.
Kigwangala
amesema wanawake wanaofanya ngono bila kinga wanaweza kupata saratani ya mlango
wa kizazi, ambapo husababishwa kwa kufanya ngono bila kinga,huambukizwa
kwa kujaamiana. Tangaza biashara yako hapa. Pia like page yetu ya facebook Jambo Tz. tu-follow
instagram @jambotz.
Subscribe to:
Posts (Atom)