Monday, August 04, 2014

MAGAZETI YA LEO JUMATATU AGOSTI 04, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.

.

.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAHASIMU WA SUDANI KUSINI WAKUTANA TENA

Kuna hofu na tisho la njaa Sudan Kusini
Mazungumzo ya amani kati ya serikali ya Sudan Kusini na waasi yameanza tena katika nchi jirani ya Ethiopia. Mazungumzo hayo, yalikuwa yameahirishwa kwa wiki kadhaa. Vita vimeendelea nchini Sudan Kusini licha ya makubaliano ya kusitisha vita kufikiwa kati ya pande husika.

Zaidi ya watu milioni moja unusu, wameachwa bila makazi kutokana na vita hivyo. Umoja wa Mataifa na mataifa mengine ya Magharibi yameonya kua Sudan Kusini inakabiliwa na tisho la kukumbwa na njaa.
Maafisa wa baraza la usalama la Umoja huo, wanatarajiwa kuzuru nchi hio wiki ijayo.

Katika mazungumzo hayo, serikali na waasi wanatarajiwa kuzungumzia swala la kubuni serikali ya mpito pamoja na muundo wake. Makataa ya makubaliano hayo ni chini ya wiki moja na huenda muda huo usifikiwe. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

KESI YA WANABLOG YAAHIRISHWA

Kesi ya wanablogu kumi waliokuwa wanakabiliwa na mashitaka ya ugaidi imeahairishwa hadi Agosti 20.
Kesi hiyo ilianza leo miezi mitatu baada ya tisa kati yao kukamatwa na polisi.
Mmoja wa wanablogu hao alishtakiwa bila kuwepo mahakamani.
Wanakabiliwa na mashitaka ya ugaidi chini ya sheria iliyoshutumiwa ya kupinga ugaidi.
Kesi hii imevutia hisia kubwa nje na ndani ya Ethiopia, hiyo basi hakukuwa na tofauti kubwa ilipoanza hivi leo.
Mahakama hiyo ilijazwa na raia wa Ethiopia, wanahabari hali kadhalika maafisa wa kidiplomasia. Wote walioshitakiwa walifika mahakamani. Mawakili walikuwa wamepinga kwa mapema mashitaka hayo wakisema kuwa hayakuwa na msingi.
Hata hivyo mahakama ilikataa kuwaachilia kwa dhamana wanablogu hao jinsi walivyokuwa wakitaka mawakili wao. Wote kumi wameshitakiwa kwa kubuni kikundi haramu vile vile kushirikiana na makundi ya upinzani yaliyopigwa marufuku ng’ambo na nchini.
Waendesha mashtaka walisema kuwa washtakiwa hao walipokea ufadhili na mafunzo ya kutengeneza vilipuzi.
Kitendo hicho cha kuwakamata wanablogu kimesababisha serikali ya Ethiopia kushutumiwa kimataifa na kutaja kuwa inatumia sheria dhidi ya ugaidi kukandamiza upinzani na uhuru wa vyombo vya habari nchini humo.
Katika mahojiano ya hivi majuzi na BBC waziri mkuu wa Ethiopia alikanusha madai ya kuwakandamiza wanahabari lakini akasema kuwa serikali haitawavumilia wanablogu na wanaharakati wanaonekana kushirikiana na makundi ya kigaidi nchini humo. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Tuesday, July 29, 2014

KAMA ULIKUWA HUJUI, HUYU NDIE ASKOFU BILLIONEA TANZANIA ... ANALINDWA KAMA RAIS.....!!!

ASKOFU na Nabii George David ‘Geordavie’ wa Kanisa la Geordavie Ministry ‘Ngurumo ya Upako’ lililoko jijini Arusha na Kawe, Dar hivi karibuni alifanya mkutano mkubwa na kutikisa nchini  kwa kuwa na magari ya kifahari na ndege aina ya helikopta ‘chopa’ iliyokuwa ikirandaranda juu ya anga kulinda usalama wake.

Katika mkutano huo uliofanyika Karatu mkoani Manyara, mwandishi wetu alishuhudia msafara wa Geordavie ambaye hutoa huduma ya uponyaji kwa njia za miujiza, ukiwavutia watu wengi kwa kuwa ulikuwa na ulinzi mkali ambao haujawahi kutokea. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

SAKATA LA KUTUPWA KWA VIUNGO VYA BINADAMU, IMTU WAPANDA KIZIMBANI


Wafanyakazi  wa Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Tiba na Teknolojia (IMTU) cha Dar es Salaam wakiwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kinondoni jana.

Sakata la kutupwa kwa viungo vya binadamu bila kufuata utaratibu jana liligeuka sinema wakati maofisa wanne wa Chuo Kikuu cha Tiba na Teknolojia (IMTU), walipofikishwa mahakamani Dar es Salaam.
Maofisa hao ambao ni maprofesa na wahadhiri wa chuo hicho walifikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni wakikabiliwa na mashtaka mawili likiwamo la kushindwa kufukia viroba 83 vya miili ya binadamu.
Baada ya mashtaka hayo kusomwa na taratibu za dhamana kukamilika huku mmoja wao akishindwa kutimiza masharti, watuhumiwa hao walirejeshwa kizimbani na kufutiwa mashtaka hayo kwa amri ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DDP) aliyewasilisha hati ya kutokuwa na nia ya kuendelea na mashtaka hayo.
Hata hivyo, furaha waliyoipata washtakiwa hao, Venkat Subbaiah (57), Appm Shankar Rao (64), Prabhakar  Rai (69) na Dinesh Kumar (27) ilikuwa ya muda tu, kwani polisi waliokuwapo mahakamani hapo waliwakamata tena na kuondoka nao.
Hati ya mashtaka
Akiwasomea mashtaka, Mwendesha Mashtaka Mwandamizi wa Polisi, Magoma Mtani alidai kuwa washtakiwa hao Julai 2014 katika eneo la Mpigi Majohe, walishindwa kufukia viroba 83 vya miili ya binadamu waliyoitumia kufundishia wanafunzi wa udaktari kinyume na Kifungu cha 128 cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu, Sura ya 16 ya mwaka 2002. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMANNE JULAI 29, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.

.

.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

JAMBO TZ INAWATAKIA WATU WOTE EID MUBARAK


Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

DR. BIRALI AWAONGOZA WATANZANIA SWALA YA IDD

20140729_074656_73ac8.jpg
20140729_074807_771af.jpg
Makamo wa rais Dr. Birali amewaongoza wananchi wa Jiji la Dar es salaam katika swala ya Idd iliyoswaliwa kitaifa katika viwanja vya Mnazi mmoja leo asubuhi. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Na Mjengwa Blog

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...