Friday, January 03, 2014

"SARAFU YA TSH. 50,000 HAITATUMIKA KATIKA MANUNUZI" PROF. NDULU

Gavana wa BoT, Profesa Benno Ndulu

BENKI Kuu ya Tanzania (BoT) imetoa sarafu maalumu ya kumbukumbu ya miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar yenye thamani ya sh 50,000.

Gavana wa BoT, Profesa Benno Ndulu, alisema jana kuwa sarafu hiyo iliyotengenezwa kwa madini ya fedha kwa asilimia 92.50, imetolewa kwa ajili ya kumbukumbu tu na haitaingizwa katika mzunguko wala kutumika kwa kulipia malipo ya aina yoyote.


Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

WACHINA WENGINE WAKAMATWA NA MENO YA TEMBO 81 BANDARINI DAR ES SALAAM

 
TAARIFA KWA UMMA

Mamlaka ya Bandari Tanzania kwa kushirikiana na Wizara ya Maliasili na Utalii pamoja na vyombo vingine vya Dola, tarehe 2 Januari 2014 majira ya saa tatu asubuhi kwenye Bandari ya Dar es Salaam, imekamata meno 81 ya tembo yenye uzito wa kilo 303 sawa na tembo 41. Aidha, magamba 120 ya kakakuona na mazao ya bahari nayo yamekamtwa. 

Hii ni baada ya Askari wa Bandari kutilia shaka mizigo iliyokuwa kwenye gari ikiingizwa bandarini. Meno ya tembo yaliyokamatwa bado ni mapya ikiwa na maana tembo hao wameuawa katika kipindi kizichozidi mwezi mmoja uliopita.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

DK.SHEIN AFUNGUA MAONESHO YA MIAKA 50 YA MAPINDUZI

 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akipata maelezo kutoka Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Hassan Khatib, (kulia) alipotembelea banda la Ofisi ya faragha Ikulu, wakati wa Maonesho ya Miaka 50 ya Mapinduzi Zanzibar, yaliyofanyika jana viwanja vya Beit el Ras, katika shamra shamra za sherehe za Mapinduzi
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

WARIOBA: SERIKALI TATU SI MZIGO

MWENYEKITI wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba nchini, Jaji Mstaafu Joseph Sinde Warioba, ametetea muundo wa serikali tatu kuwa hauna gharama, tofauti na inavyotafsiriwa na wengi. Mbali na kutetea gharama za uendeshaji wa serikali tatu, Jaji Warioba pia amewashukia wanaodhani mapendekezo ya muundo wa serikali tatu ni yake binafsi, kutokana na msimamo wa siku nyingi wa kiongozi huyo.
 
 Akizungumza na Jukwaa la Wahariri nchini (TEF), Jaji Warioba alisema muundo wa serikali tatu umepunguza gharama za uendeshaji. Kwa mujibu wa Jaji Warioba, chini ya muundo huo hata Bunge linatarajiwa kuwa na wabunge 75 tu, hatua ambayo itapunguza gharama. Mwenyekiti huyo alisema kuwa gharama za uendeshaji wa Serikali ya Muungano zitakuwa katika Wizara ya Ulinzi na Usalama pamoja na Mambo ya Nje huku katika maeneo yaliyobaki gharama zake zitakuwa zimepungua zaidi. 
“Hivi kwa nini hili la muundo wa muungano tunajadili gharama wakati kila mwaka tunapoongeza mikoa, wilaya, tarafa, majimbo na vijiji gharama zinaongezeka wala hakuna anayezungumzia wala kuhoji? Hivyo hivyo kwa kuwa na serikali tatu, hakuna gharama, tena kimsingi tumepunguza gharama za migogoro ya mara kwa mara ya kushughulikia kero za Muungano,” alisema Jaji Warioba.

MAGAZETI YA LEO IJUMAA JANUARI 03, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS



.
.

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

Thursday, January 02, 2014

MWANAJESHI AUA VIJANA WAWILI KWA BASTOLA

Mwanajeshi wa Jeshi la Wananchi Tanzania(JWTZ), ambaye jina lake limehifadhiwa anashikiliwa na Jeshi la Polisi baada ya kuwaua kwa kuwapiga risasi vijana wawili na kisha kuwajeruhi vibaya wengine wawili walipokuwa katika shamrashamra za kuukaribisha mwaka mpya. Tukio hilo lilitokea majira ya saa sita na robo usiku wa kuamkia jana, katika eneo la Pugu Kinyamwezi, Ilala jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na Mwandishi wa habari jana Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Ilala, Marietha Minangi (pichani) alisema tukio hilo lilitokea baada kundi la vijana waliokuwa wakisherehekea mwaka mpya kuzingira gari la mwanajeshi huyo aliyekuwa akielekea nyumbani kwake Pugu Kinyamwezi, akitokea katikati ya Jiji kwa shughuli zake.
Alisema mwanajeshi huyo alikuwa na gari aina ya Toyota Rava 4 na baada ya kufika katika eneo hilo alizingirwa na kundi la vijana hao waliokuwa wakisherehekea mwaka mpya na ndipo aliamua kutoa bastola yake na kufyatua risasi ambapo iliwapata vijana hao na kufa papo hapo na kujeruhi wengine.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

RAY C AFUNGUKA KUHUSU JACK CLIF... ASEMA WACHA AFE TU TENA ANYONGWE KABISA...!!!


Kutokana na maswahibu makubwa yaliyompata Ray C juu ya madawa ya kulevya, ameshindwa kujizuia kutokusema ya moyoni mwake juu ya mwanadada Jack Cliff aliyekamatwa na madawa ya kulevya nchini China. Kafunguka maneno mengi sana na alionyesha ni jinsi gani alivyokuwa hamuonei huruma mwanadada Jack mpaka kuamua kutamka bora anyongwe tu. 

Soma alichokisema hapa
 
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO ALHAMIS JANUARI 02, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

MSIMAMO WA LIGI KUU YA UINGEREZA ULIVYO SASA MARA BAADA YA MECHI ZA JANA

 
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

LOWASAA ATANGAZA KUANZA RASMI SAFARI YA NDOTO ZAKE...!!!

lowassa 9c1c5
Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa ametangaza kuanza rasmi kwa safari aliyoiita ya matumaini ya ndoto zake, ambayo amesema itatimiza ndoto za Watanzania za kupata elimu bure, maji safi na maendeleo ya uhakika.
Akizungumza katika ibada ya shukrani na kuupokea mwaka mpya, katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT),Usharika ya Monduli Mjini, Lowassa bila ya kutaja safari hiyo ni ipi, aliwashukuru watu wote kutoka maeneo mbalimbali nchini, ambao walimsindikiza katika ibada hiyo.
Lowassa alisema anaamini watu hao waliofika, wana uhakika wa ushindi katika safari hiyo kwa kumtegemea Mungu.
"Nimefarijika sana leo kuwaona hapa marafiki zangu wengi. Ninapowatazama hadi machozi yananitoka na kwa uwezo wa Mungu tutashinda kwani nyote mnajua nia na ndoto yangu,'' alisema Lowassa na kupokelewa na sauti za shangwe kanisani.
 
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz 

HII NDIO HISTORIA NZITO NA FUPI YA MAREHEMU DK. MGIMWA...!!!

 Historia fupi ya Waziri wa Fedha wa Tanzania, Dr. William Mgimwa aliyefariki dunia nchini Afrika Kusini alipokuwa amelazwa kwa matibabu.
Kuzaliwa: Januari 20, 1950 Kalenga Iringa.
Elimu:
1961 -1965 Shule ya Msingi Wasa
1966 - 1967 Shule ya Msingi Tosa
1968 - 1969 Tosamaganga Sekondari

1970-1971 Seminari ya Mafinga
1975 - 1984 Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM) - Postgraduate in Finance
1989 - 1991 IDM Mzumbe (MBA - Finance)

Ajira
1981 - 2000 - NBC Ltd (Mhasibu, Mhadhiri, Mkurugenzi, Mkurugenzi Mkuu)
2000 - 2010 - Chuo cha Benki Kuu ya Tanzania Mwanza (Mkuu wa Chuo)
2010 - 2013 - Mbunge, Kalenga (CCM)

Waziri wa Fedha,Dkt. William Mgimwa (pichani) alifariki Dunia Januari 1, 2014 katika Hospitali ya Mediclinic Kloff,alikokuwa amelazwa kwa matibabu.

Wednesday, January 01, 2014

KHERI YA MWAKA MPYA 2014...!!!

Jambo Tz Blog inapenda kuwatakia Watu wote husani wadau wa blog hii popote pale walipo HERI YA MWAKA MPYA 2014. Nakutakia furaha, Baraka, Mafanikio, Afya tele, Amani na Upendo. Kwa namna ya kipekee kabisa. Pia endelea kuwa nasi mwaka 2014 kwani tumejipanga vilivyo kukuletea habari.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

HAYA NDIO MAGAZETI YA KWANZA KABISA KUTOKA MWAKA 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS .... HERI YA MWAKA MPYA

.
.
.
 Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

AJALI MBAYA IMETOKEA ENEO LA CCM MBEYA USIKU WA MWAKA MPYA NA KUUA MTU MMOJA

 
 Boda boda Mbili zikiwa zimegongana
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz 


Tuesday, December 31, 2013

JAMAA APANDA JUU YA MNARA WA SIMU UBUNGO JIJINI DAR LEO NA KUGOMA KUSHUKA MPAKA AONANE NA RAISI KIKWETE

 Askari wa Kikosi cha Zima moto na Uokoaji Wakiwa wamepanda juu ya Mnara wa Simu Uliopo Ubungo Jijini Dar Es Salaam Muda mfupi uliopita kwaajili ya kumuokoa kijana mmoja aliyefahamika kwa jina moja la Hassan Ambaye alipanda juu ya mnara huo kwa lengo la kufikisha Ujumbe wa kutaka kuonana na Raisi Kikwete ili aweze kumwelezea kwa kile anachodai kuwa jeshi la polisi lilimbambikia kesi na hatimaye kuhukumiwa kifungo cha Miaka 6 kwenda jela.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...