Wednesday, November 13, 2013

HABARI ZAIDI JUU YA KIFO CHA DR. SENGONDO MVUNGI

Mvungi_01_2d4e9.jpg
Tume ya Mabadiliko ya Katiba nchini Tanzania imepata pigo baada ya mmoja wa wajumbe wake Dr. Sengondo Mvungi kufariki dunia nchini Afrika Kusini, ambako alikuwa akitibiwa.
Dr. Mvungi, alipelekwa Afrika Kusini kwa matibabu zaidi baada ya kuvamiwa na watu wanaoaminika kuwa majambazi nyumbani kwake mjini Dar, es Salaam, wiki iliyopita.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Bw. Assaa Rashid Dkt. Mvungi alifariki majira ya saa 8:30 mchana kwa saa za Afrika ya Kusini akiwa katika Hospitali ya Milpark.
"Kwa masikitiko makubwa, Tume inawafahamisha wananchi kuwa Mjumbe wake, Dkt. Sengondo Mvungi aliyekuwa akipata matibabu katika Hospital ya Milpark iliyopo jijini Johannesburg nchini Afrika Kusini amefariki dunia leo Jumanne, Novemba 12, 2013 saa 8:30 mchana kwa saa za Afrika ya Kusini," amesema Bwana Rashid katika taarifa yake fupi.
Amesema taratibu za kuusafirisha mwili wa marehemu kutoka nchini Afrika Kusini kuja nchini Tanzania kwa mazishi zinaendelea.
Marehemu Dkt. Mvungi alisafirishwa siku ya Alhamisi, Novemba 7, 2013 kwenda nchini Afrika Kusini kwa uchunguzi na matibabu zaidi akitokea Kitengo cha Mifupa Muhimbili (MOI) alipokuwa amelazwa baada ya kuvamiwa nyumbani kwake.
Dkt. Mvungi pamoja na kuwa ni mwanasheria aliyebobea katika fani ya Katiba, pia ni mwanasiasa ambaye aliwahi kugombea urais mwaka 2005 kupitia chama cha NCCR Mageuzi.

MWANAKANDANDA AADHIBIWA NCHINI MISRI KISA KUSHANGILIA ALAMA YA VIDOLE

131111211449_ahmed_abdul_zaher_rabaa_464x261_afp_nocredit_e73c9.jpg
Ahmed Abdul Zaher amejitetea akisema hakunuia kuzua hisia za kisiasa
Mchezaji soka mmoja katika moja ya vilabu maarufu nchini Misri ametupwa nje ya mechi za klabu hiyo baada ya kuonekana kumuunga mkono rais aliyeondolewa mamlakani Mohammed Morsi.
Klabu ya Al Ahly, imesema kuwa Ahmed Abdul Zaher , hatashiriki mchuano wa FIFA wa klabu bingwa duniani baada ya kupiga saluti ya vidole vinne mnamo siku ya Jumapili.
Mchezaji huyo alikuwa anasherehekea bao lake la mchuano wa mabingwa wa Afrika ambapo Al Ahly ilishinda kwa mabao 2-0 dhidi ya Orlando Pirates wa Afrika Kusini.
Ishara hio imekuwa ikitumika kama ishara ya kumuunga mkono bwana Morsi.
Ishara hiyo pia ilitokana na maandamano ya wafuasi wa Morsi waliotawanywa na maafisa wa usalama mnamo mwezi Agosti baada ya kukesha katika eneo walilosema alikuwa amezuiliwa Morsi.
Rais Morsi alikuwa rais wa kwanza wa nchi hiyo kuchaguliwa kidemokrasia, na sasa anakabiliwa na kesi ya kuchochea mauaji ya waandamanaji wakati wa ghasia zilizotokea mjini Cairo mwaka jana.
Yeye mwenyewe aling'olewa kutoka uongozini mwezi Julai.
Abdul Zaher alisherehekea kwa ishara ya vidole vinne baada ya kuingiza bao la Al Ahly la pili ambapo waliibuka washindi dhidi ya Orlando Pirates.
"ndio nilitoa ishara hiyo ya Rabaa," alinukuliwa akisema kwenye mtandao wa FilGoal.
"lakini sikunuia kuzua hisia za kisiasa kwa mtu yeyote, nilichonuia ni kumkumbuka mtu yeyote aliyefariki, awe raia wa kawaida au hata polisi.''
Mnamo siku ya Jumatatu maafisa wa klabu ya Al Ahly, walisema kuwa Ahmed Abdul Zaher hatashirikishwa kwenye mechi itakayochezwa nchini Morocco.

JK AKATAA ZAWADI YA PANDE LA DHAHABU

jk_taifa_1b3a9.jpg
Rais Jakaya Kikwete jana aligoma kupokea zawadi ya dhahabu kutoka Kampuni ya Nyamigogo Grand Vezir Holdings ya mkoani Geita.
Taarifa iliyotolewa na Ikulu jana ilisema viongozi wa kampuni hiyo walitaka kumkabidhi Rais Kikwete gramu 227 za dhahabu safi wakati alipotembelea mgodi huo.
Rais Kikwete badala yake aliwaelekeza waiuze dhahabu na fedha zitakazopatikana zitumike kuwasaidia watoto yatima.
Alikabidhiwa zawadi hiyo wakati wa sherehe ya kuzindua mgodi wa uchenjuaji dhahabu wa kampuni hiyo nje kidogo ya mji mdogo wa Kharuma ambao ni makao makuu ya wilaya mpya ya Nyang'hwale, Geita.
Gramu hizo 227 zina thamani ya Sh16 milioni kwa bei ya sasa ya soko la dhahabu duniani.
Baada ya kukabidhiwa zawadi hiyo, Rais Kikwete aliuliza: "Sasa nifanye nini na zawadi hii? Nawarudishieni hii dhahabu, iuzeni popote mnakotaka na fedha itakayopatikana tutawapa watoto yatima."
Akizungumza na wananchi katika mgodi huo, Rais Kikwete aliupongeza uongozi wa mgodi huo akisema umeongeza thamani ya dhahabu na maisha ya wananchi katika eneo hilo... "Mmefanya vizuri na mgodi huu, ni mradi wa maana kwa kuongeza thamani ya dhahabu na kuboresha maisha ya wananchi katika eneo hili. Ubunifu huu unastahili pongezi," alisema Rais Kikwete.

WINGI WA SAFARI ZA MESSI WACHANGIA MAUMIVU YA MARA KWA MARA.

Ndani ya siku 64 Lionel Messi ameizunguka dunia kwa kusafiri jumla ya 122,333 KM, alipozitembelea nchi na miji mbali mbali kwa ajili ya shughuli za kibalozi na kutengeneza matangazo,miongoni mwa nchi na miji aliyotembelea ni Senegal, Argentina , Ecuador, Peru, Colombia, Guatemala, Los Angeles, Las Vegas, Chicago, Norway, Germany, Poland, Barcelona, Milan, Israel, Palestine, Thailand and Malaysia.

KAMPENI YA NANI MTANI JEMBE SASA YAHAMIA KANDA YA KASKAZINI. WATALII WAKATA MAUNO BALAA....!!!



Wakazi wa eneo la Maji ya Chai, Arusha wakiangalia burudani iliyokuwa inatolewa na timu ya kampeni ya ‘Nani Mtani Jembe’ inayohusisha mashabiki Simba na Yanga,  ili kuzipigia kura timu zao na kushinda kitita kingi kati ya Tsh.100 milioni zilizotelewa na bia ya Kilimanjaro Premium Lager ambao ndio wadhamini wa timu hizo na timu ya Taifa. 
Timu hiyo ipo kanda ya Kaskazini na Mashariki inayojumuisha mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Singida na Tanga.






Watalii kutoka nchi mbalimbali wakicheza pamoja na washereheshaji wa kampeni ya ‘Nani Mtani Jembe’ inayohusisha mashabiki Simba na Yanga,  ili kuzipigia kura timu zao na kushinda kitita kingi kati ya Tsh.100 milioni zilizotelewa na bia ya Kilimanjaro Premium Lager ambao ndio wadhamini wa timu hizo na timu ya Taifa. 
Timu hiyo ipo kanda ya Kaskazini na Mashariki inayojumuisha mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Singida na Tanga. Watalii hao walikuwa wakitembelea maeneo mbalimbali mkoani Arusha

Tuesday, November 12, 2013

BODI YA LIGI YAFUNGIA VIWANJA SABA


Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPL Board) imefungia viwanja saba vilivyokuwa vikitumiwa na timu za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) na Ligi Daraja la Kwanza (FDL) hadi vitakapofanyiwa marekebisho ili kukidhi mahitaji ya mechi za mpira wa miguu.

Uamuzi huo umefikiwa na TPL Board katika kikao chake cha kwanza kilichofanyika juzi (Novemba 10 mwaka huu) jijini Dar es Salaam ambapo pamoja na mambo mengine kilipitia ripoti za mechi za VPL na FDL katika mzunguko wa kwanza.

Viwanja vilivyofungiwa na marekebisho yanayotakiwa kufanyika kwanza ili viruhusiwe kutumika tena ni Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba (majukwaa yake yamechakaa, hivyo kuhatarisha usalama wa watazamaji), na Uwanja wa CCM Mkwakwani jijini Tanga (vyumba vya wachezaji kubadilishia nguo (dressing rooms) havina hadhi).
Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya (sehemu ya kuchezea- pitch ni mbovu), Uwanja wa Kumbukumbu ya Sheikh Kaluta Amri Abeid jijini Arusha (pitch ni mbovu), Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi (vyumba vya kubadilishia kutumika kwa ajili ya shule ya awali), Uwanja wa Majimaji mjini Songea (pitch ni mbovu) na Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro (pitch ni mbovu). 

BREAKING NEWZZZZZZ...!!! DR. SENGONDO MVUNGI AMEFARIKI DUNIA AFRIKA KUSINI

Sengondo Mvungi 1 
Ni jana tu ambapo Waziri wa mambo ya ndani Dr. Emmanuel Nchimbi alitangaza kushikiliwa kwa watu tisa wanaotuhumiwa kuhusika na ujambazi uliofanywa dhidi ya Dr. Sengondo Mvungi aliekua mjumbe wa Tume ya Marekebisho ya Katiba Mpya na kiongozi wa NCCR-Mageuzi.
Taarifa iliyotumwa inasema Dr Mvungi amefariki dunia akiwa mahututi hospitalini nchini Afrika Kusini muda mfupi uliopita na taarifa kutumwa nyumbani Tanzania ambapo wafanyakazi wenzake ofisi ya tume ya mabadiliko ya katiba wameambiwa wakae karibu na simu zao ili kikitokea chochote kingine wafahamishwe.
Tayari viongozi mbalimbali kama Mh. Warioba, Katibu wa tume, naibu na watumishi wengine wachache wamekwenda nyumbani kwa marehemu.
kifo cha Sengondo Mvungi Nov 12 2013 2

Pichani ni Wafanyakazi wenzake baada ya kupata taarifa za msiba ofisini.



kifo cha Sengondo Mvungi Nov 12 2013

Chanzo: millardayo.com

MSIMU WA SIKUKUU UMEWADIA TANGAZA BIASHARA YAKO NASI KWA BEI NAFUU



MAGAZETI YA LEO JUMANNE NOVEMBA 12, 2013 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.


.
.

ZAIDI YA WATU 10,000 WAHOFIWA KUFARIKI UFILIPINO


017217323_35400_2f32e.jpg
Wanajeshi na polisi wa Ufilipino wamepelekwa katika miji ilioathirika na kimbunga kikali kuwahi kuipiga nchi hiyo ili kudhibiti wizi wa mali unaohatarisha juhudi za kutoa misaada ya kibinaadamu kwa waathirika.
Zaidi ya watu 10,000 wanahofiwa kufariki kutokana na kimbunga hicho kwa jina Haiyan kilichopiga kwa mawimbi mazito na upepo mkali na kusababisha athari kubwa nchini Ufilipino siku ya Ijumaa, huku mji wa Tacloban ukiwa moja ya miji ilioathirika pakubwa.
Waokoaji kwa sasa wanajaribu kupeleka misaada ya chakula na malazi kwa waathirika wa kimbunga hicho katika mji huo ulio na idadi ya watu 220,000.
Hata hivyo hatua hiyo iliendeshwa kwa changamoto kubwa kutokana na wizi uliokuwa ukiendelea. Waporaji walivunja maduka pamoja na kuvamia gari la misaada la msalaba mwekundu na kuchukua vile vilivyokuwemo ndani.
Baadhi ya waathiriwa ambao ni wafanyabiashara wadogo pia wameripoti kuibiwa kwa televisheni, na mashini za kufulia nguo. 
Kulingana na msemaji wa wizara ya ulinzi wa raia nchini humo, Reynaldo Balido, kurejesha usalama na hai ya utulivu katika mji huo wa Tacloban, ni moja ya mambo wanayoyapa kipaumbele.

KIONGOZI WA MSAFARA WA RAIS AKUTWA NA ZAIDI YA KILO 297 ZA DAWA ZA KULEVYA

558644_610253689038629_153892185_n_a1d1b.jpg
KASHFA NZITO LIBERIA: Msafara wa Rais Ellen Johnson Sirleaf wakutwa na zaidi ya kilo 297 za bangi. Watu 4 akiwemo kiongozi wa msafara washikiliwa kwa mahojiano.
== Liberia's Drug Enforcement Agency has arrested the head of the presidential motorcade for allegedly using an official vehicle to smuggle 297 kilograms (654 pounds) of marijuana into Liberia from neighboring Sierra Leone, officials said Monday.
The motorcade commander, Perry Dolo, was arrested over the weekend along with three other men after crossing from Sierra Leone via the town of Bo Waterside, said DEA Director Anthony Souh. The other three men were a Liberian official, a Guinean and a Sierra Leonean believed to be a member of the armed forces, Souh said. He did not provide further details about the men.
The vehicle used in the operation is known as "Escort 1," the jeep that normally leads the president's convoy, Souh said.
"He took the car during his day off to go do this thing. He was not on duty, but he used the official car," Souh said of Dolo.
Journalists were denied access to the suspects because they were still being interrogated at the DEA after their arrest by a joint force that included members of the Emergency Response Unit.
"They are still with me going through the process," Souh said. "We want to speedily send them to court as soon as possible because the case is too high. Using a presidential car? It's too big."
Liberia's DEA has in recent years tried to combat marijuana farming in Liberia's interior counties, which is primarily done for local sale and consumption. However, weak drug laws have made the practice difficult to curtail.
According to the 2012 World Drug Report from the United Nations Office on Drugs and Crime, 9 percent of Liberian high school students use cannabis.
———
abc News

Monday, November 11, 2013

MAGAZETI YA LEO JUMATATU NOVEMBER 11, 2013 YA UDAKU, MICHEZO NA HARDNEWS

.
.

,
,

VAN PERSIE AIZAMISHA ARSENAL, MAN UNITED WAFUFUA MATUMAINI YA UBINGWA

article-2497133-1954DA9800000578-907_634x446_f36bf.jpg
MHOLANZI Robin van Persie amezamisha klabu yake ya zamani, Arsenal akiifungia bao pekee la ushindi Manchester United na kuirejeshea matumaini ya kutetea ubingwa wa Ligi Kuu England.
Van Persie alifunga bao tamu kwa kichwa akiunganisha kona iliyochongwa kitaalamu na Wayne Rooney dakika ya 27 Uwanja wa Old Trafford.
Kikosi cha United kilikuwa; De Gea, Smalling, Vidic/Cleverley dk45, Evans, Evra, Valencia, Jones, Carrick, Kagawa/Giggs dk78, Rooney na Van Persie/Fellaini dk85.
Arsenal; Szczesny, Sagna, Koscielny, Vermaelen, Gibbs, Arteta/Gnabry dk82, Flamini/Wilshere dk61, Ramsey, Ozil, Cazorla/Bendtner dk78 na Giroud.

TAARIFA RASMI YA ZITTO KABWE KUHUSU KINACHOITWA “TAARIFA YA SIRI YA CHADEMA”

Zitto-Kabwe_c2a4f.jpg
Tamko rasmi la Ndugu Zitto Z. KABWE (MB) kuhusiana na kinachoitwa "Taarifa ya Siri ya CHADEMA"
Ndugu Wanahabari,
NILIPOKUWA katika ziara ya bara la Ulaya kati ya Oktoba 21 mpaka Novemba 2 mwaka huu (2013), nilipokea kwa njia ya barua pepe ripoti inayoitwa "Taarifa ya Siri ya Chadema" ambayo pia ilikuwa imesambazwa katika mitandao mbalimbali ya kijamii.
"Taarifa ya Chadema inasema kwamba chama hicho (chama changu) kilikuwa kimechunguza mwenendo wangu tangu
mwaka 2008 hadi 2010 na kubaini kuwa mimi napokea fedha kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM) ili kuivuruga Chadema.
Ripoti hiyo ilinihusisha pia na mwananchi raia wa Ujerumani, Andrea Cordes ambaye, kwa mujibu wa ripoti hiyo, alinisaidia kupokea na kuhifadhi kiasi cha dola 250,000 za Marekani kupitia kwenye akaunti yake binafsi.
Taarifa hii ya kutunga na iliyojaa uongo wa kiwango cha kutisha, imenifadhaisha, kunisikitisha na kunikasirisha.

KENYA YAIUNGA MKONO TZ A.MASHARIKI

131110120158_amina_mohamed_304x171_bbc_nocredit_860b3.jpg
Amina Mohamed,waziri wa mambo ya nje wa Kenya
Kenya imekuwa nchi ya kwanza kutoka Jumuia ya Afrika Mashariki kuipongeza Tanzania kwa hatua yake ya kutangaza bayana kwamba haiko tayari kutoka katika jumuiya hiyo kama ilivyodhaniwa.
Wasiwasi kuwa Tanzania ingejitoa kutoka jumuia ya Afrika Mashariki ulitokana na hali iliyojitokeza kwa baadhi ya nchi za jumuia hiyo kuendesha mikutano yao bila kuishirikisha Tanzania na Burundi.
Baadhi ya wanasiasa na wananchi nchini Tanzania walitaka nchi yao iachane na jumuia hiyo wakizishutumu Kenya, Rwanda na Uganda kuitenga Tanzania hata katika mikutano ya masuala yaliyohitaji maamuzi ya jumuia.
Kufuatia mfarakano huo, ulionekana kutishia uhai wa Jumuia ya Afrika Mashariki, Rais Jakaya Kikwete wa Tanzania, wiki hii alilihutubia bunge la Muungano wa Tanzania mjini Dodoma, katikati ya nchi na kutangaza bayana kuwa Tanzania haitatoka katika jumuiya ya Afrika Mashariki, kwani imefanya kazi kubwa kuifufua na kuiunda upya baada ya kusambaratika mwaka 1977.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...