Tuesday, October 01, 2013

WAKAZI DODOMA WAANDAMANA KUPINGA BOMOABOMOA YA CDA




 Maelfu ya Wananchi wa Kata ya kikuyu kusini wakiandamana katika mitaa ya mji wa Dodoma kwa ajili ya kupinga kubomolewa na mamraka ya ustawishaji makao makuu  [CDA] wanaotarajia kubomoa nyumba, mapagale na misingi ya wakazi hao.

  Maelfu ya Wananchi wa Kata ya kikuyu kusini wakiandamana katika mitaa ya mji wa Dodoma kwa ajili ya kupinga kubomolewa na mamraka ya ustawishaji makao makuu  [CDA] wanaotarajia kubomoa nyumba, mapagale na misingi ya wakazi hao.

JAMAA APEWA ADHABU YA KUOSHA GARI LA ZIMA MOTO MARA BAADA YA KUWADANGANYA KWA KUWAPIGIA SIMU

Mmoja wa wakazi wa Rugelele kata Rujewa wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya  DUKA MKWILA[20]ni miongoni mwa wananchi waliopiga simu za uongo katika kikosi cha zimamoto mkoa wa mbeya akiwa amepewa adahabu ya kuosha gari la zimomoto
Hata hivyo DUKA alikiri kutenda kosa na kuomba msamaha kwa jeshi hilo ambapo aliachiwa huru na kisha kurejea kwao huku akijutia kosa alilolifanya na kuahidi kutorudia tena.

VIWANGO VYA NAULI KUTOKA UBUNGO HADI MIKOA MINGINE

MAGAZETI YA LEO JUMANNE OKTOBA 1, 2013

DSC 0051 4272d
DSC 0052 dc9bc

MKENYA ALIYEDAIWA KUMTEKA DK. ULIMBOKWA ATOZWA FAINI 1,000/-

fain_269e9.jpg
Mkenya Joshua Mulundi aliachiwa huru baada ya kulipa faini ya Sh1,000 kwa kupatikana na hatia ya kuidanganya polisi kuwa alihusika kumteka na kumjeruhi Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari Tanzania, Dk Steven Ulimboka.
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ilimhukumu kifungo cha miezi sita jela au kulipa faini hiyo. Mulundi alilipiwa faini hiyo na Mwandishi wa Habari wa Redio Times, Chipangula Nandule.
Hukumu hiyo imetolewa leo na Hakimu Mkazi, Aloyce Katemana baada ya Wakili wa Serikali Mwandamizi, Tumaini Kweka kusoma maelezo ya awali na mshtakiwa huyo kukiri alitoa taarifa ya uongo kwa polisi kuhusu tukio hilo.
Kabla ya hukumu hiyo, Mulundi aliomba Mahakama impunguzie adhabu kwa kuwa hilo lilikuwa kosa lake la kwanza. Pia alijitetea kuwa Juni 27, 2012 akiwa Arusha alitekwa na kupelekwa Dar es Salaam ambako alikuwa hana mwenyeji wala hakuwahi kufika.
Alisema kutokana na kutekwa huko alichanginyikiwa hivyo kukubali chochote alichoambiwa afanye kwa kuwa aliyemteka alikuwa na silaha na alimwelekeza mambo ya kuzungumza.
"Mheshimiwa kwa ajili ya vitisho hivyo, nilikwenda Kawe katika Kanisa la Ufufuo na Uzima lililoko kwenye eneo la Tanganyika Packers, mbele ya Mchungaji Joseph Malwa Kiliba na kuungama kuwa ni miongoni mwa watu waliomtesa Dk Ulimboka katika Msitu wa Pande," alisema Mulundi na kuongeza:
"Siwalaumu Serikali, upande wa mashtaka wala polisi kwa kitendo cha kuniweka gerezani kwa muda mrefu, najilaumu mimi mwenyewe."
Kabla ya kutolewa kwa hukumu hiyo, Kweka aliiambia Mahakama kuwa hana kumbukumbu za uhalifu za mshtakiwa lakini aliomba apewe adhabu kali kutokana na mazingira ya tukio hilo.
Akitoa hukumu, Hakimu Katema alisema alifikia uamuzi huo kwa kuzingatia maombi ya mshtakiwa ya kupunguziwa adhabu.

VIJANA WANAVYOSAJILIWA KUPIGANIA AL SHABAAB

alshabaab-soldiers-in-training_495033_e5a43.png
Uchunguzi wa BBC umefichua ambavyo vijana husajiliwa kujiunga na kundi la kigaidi la Al Shabaab katika pwani ya Kenya.
Al Shabaab limekiri kufanya shambulizi la kigaidi dhidi ya jengo la Westgate ambapo zaidi ya watu sitini waliuawa na mamia kujeruhiwa.
Uchunguzi wa BBC, unatizama ambavyo vijana wanafunzwa itikadi kali za dini katika kuwaandaa, kujiunga na kundi la Al Shabaab.
Vikao vya kuwasajili Vijana hao huanza na viongozi wa dini kutoa hotuba kwa vijana waisilamu wengi ambao wamesilimu.
Uchunguzi huo umebaini kuwa vijana hao ambao wanakuwa wamejitolea kupigania kile wanachosema ni dini, hupelekwa katika maeneo ya vijijini katika fuo za bahari kama sehemu ya kwanza ya safari yao kwenda Somalia.
Mmoja wa wahubiri hao kwa jina Makaburi, ametetea shambulizi lililofanywa dhidi ya Jumba la Westgate na kuwaua watu zaidi ya sitini akisema kwamba ilikuwa hatua sahihi.
Kulingana naye, ilikuwa sawa kwa sababu majeshi ya kigeni yanapigana nchini Somalia.
Jeshi la Kenya lilipeleka wanajeshi wake nchini Somalia,miaka miwili iliopita kupambana na kundi la Al Shabaab.
Wakati huohuo, maombi yanafanyika katika sehemu mbali mbali mjini Naiobi kuwaombea waathiriwa wa shambulizi hilo

Monday, September 30, 2013

MSAJILI WA VYAMA VYA SIASA JAJI MUTUNGI USO KWA USO NA VYAMA VYA UPINZANI VILIVYOUNGANA


MUUNGANO wa vyama vya siasa vya upinzani nchini, jana ulitinga ofisi za Msajili wa Vyama, Jaji Godfrey Mutungi, kwa nia ya kueleza dhamira yao ya kupinga Rais Jakaya Kikwete kuusaini Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba.
Vyama hivyo vya CHADEMA, CUF na NCCR-Mageuzi, vinavyounda ushirikiano wa kisiasa wa kupinga Rais kusaini muswada huo, vilimfafanulia Msajili huyo kilichotokea bungeni hivi karibuni, kwa wabunge wa upinzani nje ya ukumbi wa Bunge, wakati wale wa CCM wakipitisha muswada huo pamoja na marekebisho yake.

Akizungumza na waandishi wa habari katika viunga vya viwanja vya Ofisi ya Msajili, jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa ushirikiano huo, Profesa Ibrahim Lipumba, alisema moja ya mapendekezo waliyompatia Msajili ni kutaka maridhiano ya kikatiba, hivyo Rais Jakaya Kikwete asisaini sheria hiyo.

“Tumefanya mazungumzo na Msajili, tulifika kumsabahi na kumweleza yaliyojiri bungeni kuhusu Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, mchakato ulianzia tume mpaka kura ya maoni ya katiba… Zanzibar haikushirikishwa, Serikali ilipeleka vipengele 6,” alisema Profesa Lipumba.

Profesa Lipumba alisema Oktoba 10 mwaka huu, ni siku ya kitaifa ya kupinga kusainiwa kwa Sheria hiyo na kwamba maandamano yatakayofanyika yatakuwa ya amani.

IJUE SABABU YA MKUU WA WILAYA YA MBULU KUWAPIGIA WANANCHI MAGOTI....!!!


Mkuu wa Wilaya ya Mbulu, mkoani Manyara, Anatory Choya akiwa amewapigia wananchi magoti kwa maana ya kuonyesha unyenyekevu
Mbulu. Mkuu wa Wilaya ya Mbulu, mkoani Manyara, Anatory Choya, amesema kuwa aliwapigia magoti wananchi wa Kijiji cha Hydom, ili kuonyesha unyenyekevu kwa wananchi hao aliodai walionekana kujazwa maneno ya uchochezi na wanasiasa ili wavuruge amani .

Alisema kutokana fujo zilizofanywa na baadhi ya wananchi hao katika mkutano wa hadhara uliofanyika majuzi, kwa nafasi yake angeweza kuagiza hata Jeshi la Polisi kuwadhibiti watu, lakini misingi ya dini yake haimruhusu kumdhuru mtu zaidi ya kumwonyesha unyenyekevu.
 
 
Alisema hali hiyo ndiyo iliyomfanya kuamua kupiga magoti na kumshtakia Mungu.

MSIKILIZE MUIGIZAJI MAHIRI WA FILAMU NCHINI, LULU ALIVYOFUNGUKA KWENYE SEMINA YA FURSA KWA VIJANA JIJINI MWANZA

Angalia video hapo chini

ANGALIA NJIA RAHISI NA ZA KISASA ZA KUWAFUNDISHA WATOTO KUJUA KUSOMA NA KUANDIKA

 
Angalia video hapo chini

MAGAZETI YA LEO JUMATATU SEPTEMBA 30, 2013


DSC 0067 139a0
DSC 0068 4c367

ICC INAHARIBU MAHUSIANO YAKE NA AFRIKA - RAIS KIKWETE

zzzzzzzzzzzjk_f1554.jpg
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amesema kuwa mwenendo wa Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya Jinai (ICC) kuhusu Bara la Afrika na viongozi wake, unainyima Mahakama hiyo nafasi kubwa ya kuungwa mkono na Bara la Afrika.
Rais Kikwete pia amelaani vikali mashambulizi yanayoongezeka dhidi ya vikosi vya kimataifa vya kulinda amani katika nchi mbali mbali duniani wakiwamo walinda amani wa Tanzania.

Rais Kikwete alitoa msimamo huo wa Tanzania mwishoni mwa wiki wakati alipohutubia Kikao cha Baraza Kuu la Umoja wa
Mataifa (UNGA) mwaka huu, kwenye Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa mjini New York, Marekani.
Katika hotuba yake fupi na iliyowavutia wasikilizaji, Rais Kikwete alisema kuwa ni dhahiri kuanzishwa kwa ICC kutokana na Mkataba wa Rome kulikuwa ni hatua muhimu sana katika mfumo wa kimataifa wa kupambana na makosa ya jinai.
"Kwa hakika kuundwa kwa Mahakama hiyo kuliweka mfumo mzuri wa kuondokana na watu kutenda vitendo vya jinai na kuweza kuepukana na kuwajibika kwa vitendo hivyo na Mahakama hiyo ilianzishwa kwa kuungwa mkono kwa kiasi kikubwa na Afrika.
"Hata hivyo, muongo mmoja tu baada ya kuanzishwa kwa Mahakama hiyo, ni dhahiri kuwa mvutano umezuka kati ya ICC na Bara la Afrika. Sasa Mahakama hiyo inaonekana kama taasisi isiyojali maoni na msimamo wa Afrika, kwa mambo ambayo kwa maoni yangu, ni hofu halali ya Waafrika," amesema Rais Kikwete na kuongeza:
"Bado Mahakama hiyo inaendelea kupuuza maombi ya mara kwa mara ya Umoja wa Afrika. Ni jambo la kutia huzuni kuwa maombi ya kubadilisha muda wa kuanza kusikilizwa kwa kesi dhidi ya Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya na Naibu Rais William Ruto yalipuuzwa na hata hayakujibiwa kabisa."

Sunday, September 29, 2013

TAARIFA YA ZITTO KABWE KUHUSIANA NA KUFUNGIWA MAGAZETI YA MWANANCHI NA MTANZANIA

KUFUNGIWA MAGAZETI - WAHAFIDHINA SASA WANAONGOZA
Zitto Kabwe, Mb
Kwa mshtuko na masikitiko makubwa kuanzia jana jioni tumepokea taarifa za kufungiwa kwa magazeti mawili ya kila siku hapa nchini ya Mwananchi na Mtanzania. Serikali imechukua uamuzi huo kwa kutumia sheria ya kidikteta ya magazeti ya mwaka 1976 ambayo Tume ya Jaji Francis Nyalali iliiorodhesha kama sheria kandamizi. Sababu zilizotolewa kuhalalisha uamuzi huu ni sababu zisizo na maana na ambazo Serikali ingeweza kufungua mashtaka ya kawaida kabisa mahakamani kushtaki magazeti hayo iwapo haikupendezwa na habari walizochapisha.

Moja ya sababu ya kufungiwa kwa gazeti la Mwananchi ni kuchapisha taarifa kuhusu mishahara ya Serikali. Serikali inasema habari hii ni siri. Serikali hii hii ambayo imesaini makubaliano ya kuendesha serikali kwa uwazi (Open Government Initiative) na kumwagiwa sifa na Rais Barack Obama wa Marekani inalifungia gazeti kwa kuandika habari za mishahara ya watumishi wa Serikali. Mishahara kuanzia mshahara wa Rais mpaka wa mtendaji wa Kijiji haipaswi kuwa jambo la siri.

ANGALIA VIDEO YA AUNTY EZEKIEL NA WEMA SEPETU WAKIPEANA BIRTHDAY LOVE NDANI YA HONG KONG.


ANGALIA VIDEO HAPO CHINI....
 

MTOTO ALIYEFARIKI NA KUZIKWA MIAKA MIWILI ILIYOPITA AONWA NA MAMA YAKE AKIWA HAI‏.

Mtoto Shabani Maulidi akiwa tayari melala kitandani katika hospitali ya wilaya ya Geita.
   Mama mzazi wa mtoto Shabani menye kilemba kichwani akiwa amepigwa bumbuazi  maeneo ya hospitali.




Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...