Sunday, September 29, 2013

ANGALIA VIDEO YA AUNTY EZEKIEL NA WEMA SEPETU WAKIPEANA BIRTHDAY LOVE NDANI YA HONG KONG.


ANGALIA VIDEO HAPO CHINI....
 

MTOTO ALIYEFARIKI NA KUZIKWA MIAKA MIWILI ILIYOPITA AONWA NA MAMA YAKE AKIWA HAI‏.

Mtoto Shabani Maulidi akiwa tayari melala kitandani katika hospitali ya wilaya ya Geita.
   Mama mzazi wa mtoto Shabani menye kilemba kichwani akiwa amepigwa bumbuazi  maeneo ya hospitali.




ROSE NDAUKA SASA KUZAA BILA NDOA, MAMA YAKE AGOMA

Staa wa filamu za Bongowood, Rose Ndauka ambaye ni mjamzito anadaiwa kuwa atazaa kabla ndoa mwezi Aprili, mwakani. Akizungumza na mwanahabari wetu, mchumbaa’ke, Malick Bandawe ambaye ni memba wa kundi la muziki la TNG alianika aya za Kurani kuwa katika Dini ya Kiislamu si ruhusa kufunga ndoa na mwanamke ambaye ni mjamzito kwani ni sawa na kufunga ndoa na watu wawili hivyo anamsubiri ajifungue kwanza. 
“Ni kweli mchumbaa’ngu hivi sasa ni mjamzito na anatarajia kujifungua mapema mwezi wanne, mwakani. “Kuhusu kufunga naye ndoa kwa sasa ni ngumu hadi ajifungue kwani kwa dini yetu (Uislam) si ruhusa kufanya hivyo lakini atakapojifungua tu tutafunga ndoa,” alisema Malick. Malick ambaye hivi sasa anatamba na Wimbo wa ‘Crazy Man’ alisema kuwa ana furaha kubwa kuitwa baba mtarajiwa na anamuomba Mwenyezi Mungu Rose ajifungue salama kwani anampenda kupita maelezo. Baada ya kuzungumza na Malick, gazeti hili lilimtafuta mama wa Rose Ndauka, Batuli kufungukia ishu ya mwanaye kubeba ujauzito kabla ya ndoa ambapo aligoma kuzungumza kwani hakubaliani na suala hilo.

WANAWAKE 8000 NCHINI NIGERIA WAANDAMANA KUISHINIKIZA SERIKALI IWASAIDIE WAOLEWE

  Nigeria ina upungufu wa wanaume wa kuoa kiasi kwamba wanawake wanaotamani kupata wenza na kutengeneza familia wameamua kuchukua hatua.  
Zaidi ya wanawake elfu 8 walio single jana wameandamana kutokana na upungufu wa wanaume wa kuwaoa.  
Lengo la maandamano yao ni kuishinikiza serikali kuwasaidia waolewe, kivipi? (Ndio swali hata mimi nimejiuliza!)  
Wanawake waliojikusanya na kuandamana ni mkusanyiko wa 5380 waliopewa talaka, 2200 ni wajane 1200 yatima, na 80 wengine.  
Wanawake hao wamedai kuwa hawana uwezo hata wa kununua chakula cha siku kwa sababu hawana wanaume wa kuwasaidia ndio maana wanahitaji wanaume wa kuwaoa na kuwasaidia mahitaji yao.  
  SOURCE: NAIJA GISTS

MATOKEO YA LIGI KUU YA UINGEREZA LEO JUMAPILI

Stoke-City-Vs-Norwich-City_81e66.png
Stoke City 0 - 1 Norwich City
Timu ya Norwich City imeweza kupata goli hilo katika dk ya 34 na mfungaji alikuwa ni Jonathan Howson. mchezo huo ukiluwa mzuri lakini mpaka mpira unamalizika matokeo yaliendelea  kuwa Stoke City 0 - 1 Norwich City.
Endelea kuifuatilia mjengwablog kwa matokeo ya mchezo baina ya Sunderland na Liverpool ambao mpaka sasa bado hawajafungana na ni kipindi cha kwanza.

KENYA: MAAFISA WALIKUWA NA TAARIFA

westgate 34bc1
Mawaziri wa serikali walipokea taarifa kuhusu tisho la mashambulizi ya kigaidi kabla ya kundi la Al Shabaab kushambulia jengo la Westgate mjini Nairobi.


Kwa mujibu wa taarifa za kijasusi zilizofichuliwa, zilionyesha maelezo ya mipango ya mashambulizi hayo kufanyika Nairobi au mjini Mombasa.
Taarifa zinazohusianaKenya
Mawaziri wanne na mkuu wa majeshi walikuwa wamefahamishwa kuhusu tisho la kufanyika shambulizi la kigaidi.
Watu 67 walifariki na mamia kujeruhiwa katika shambulizi la kigaidi ambalo Al Shabaab walikiri kulifanya Septemba 21 mjini Nairobi.
Kwa mujibu wa taarifa za gazeti la Daily Nation, mawaziri walipokezwa taarifa za kati ta yarehe 13 na 20 kuhusu uwezekano wa kufanyika mashambulizi kadhaa ya kigaidi mjini Mombasa na Nairobi.

TAMKO LA SERIKALI LA KUYAFUNGIA MAGAZETI YA MWANANCHI NA MTANZANIA

DSC_0068_b4d0a_d830f.png
DSC_0066_048af_a3496.png
Serikali imeyafungia kutochapishwa Magazeti ya MWANANCHI na MTANZANIA kuanzia 27 Septemba, 2013 kutokana na mwenendo wa magazeti hayo kuandika habari na makala za uchochezi na uhasama kwa nia ya kusababisha wananchi wakose imani kwa vyombo vya dola hivyo kuhatarisha amani na mshikamano ulipo nchini.
Gazeti la MWANANCHI limefungiwa kutochapishwa kwa siku kumi na nne (14) kuanzia 27 Septemba, 2013. Adhabu hii imetangazwa kwa Tangazo la Serikali (Government Notice) Namba 333 la tarehe 27 Septemba, 2013.


Gazeti la MWANANCHI limepewa adhabu hiyo kutokana na hivi karibuni kuchapisha habari zenye mwelekeo wa
uchochezi na uvunjifu wa amani, mfano tarehe 17 Julai, 2013 katika toleo Namba 4774 ilichapisha habari isemayo "MISHAHARA MIPYA SERIKALINI 2013" kwa kuchapisha waraka uliozuiliwa kwa matumizi ya vyombo vya habari waraka huo ulikuwa wa Siri haukupaswa kuchapishwa Magazetini.
Aidha, katika toleo la Jumamosi, tarehe 17 Agosti, 2013 lilichapisha habari yenye kichwa kisemacho "WAISLAM WASALI CHINI YA ULINZI MKALI" habari hiyo ilikolezwe na picha ya mbwa mkali mwenye hasira.

Saturday, September 28, 2013

ANGALIA MAJINA YA WALIOPATA MIKOPO VYUO VIKUU 2013/2014

NOTICE TO SUCCESSFUL LOAN APPLICANTS FOR 2013/2014 ACADEMIC YEAR
The Higher Education Students’ Loans Board is hereby announcing names of successful first time loan applicants for 2013/2014 Academic Year who applied and were eligible for student loans.

The list includes the Institution to which the student is admitted to and the amounts of loans allocated to a particular student in all or part of the loanable items as per Guidelines and Criteria for Issuance of Loans and Grants for 2013/2014 Academic Year.

Loan applicants can access their loan status by keying in their Form Four Index Numbers to view the results. Loan applicants are reminded that the loan money will be sent to their respective institutions where they will be required to sign to acknowledge receipt of the loans, after registration processes.


Issued by:
The Executive Director
Higher Education Students’ Loans Board
P. O. Box 76068

RATIBA YA LIGI KUU YA UINGEREZA LEO JUMAMOSI

Barclays-Premier-League-fixtures-May-_05dde.jpg
14:45 Tottenham Hotspur na Chelsea
17:00 Aston Villa na Manchester City
17:00 Fulham na Cardiff City
17:00 Hull City na West Ham United
17:00 Manchester United na West Bromwich Albion
17:00 Southampton na Crystal Palace
19:30 Swansea City na Arsenal
Endelea kuifuatilia Mjengwablog ili kupata matokeo ya mechi hizi.

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI SEPTEMBA 28, 2013

DSC 0066 048af
DSC 0067 182bf

"SINA MIKOSI KAMA WATU WANAVYOENEZA MANENO MITAANI" AUNTY EZEKIEL

Stori: Mayasa Mariwata
STAA wa filamu Bongo, Aunt Ezekiel amesema hana mkosi kama watu wasiomtakia mema wanavyoeneza maneno mitaani.
Akipiga stori na paparazi wa Ijumaa juzikati, Aunt alisema kuna baadhi ya watu wasioitakia mema ndoa yake wamekuwa wakieneza maneno kwamba ana mkosi ndiyo maana kila mwanaume anayekuwa naye hupatwa na balaa.
Staa huyo aliongeza kuwa haumizwi kichwa na maneno hayo kwa kuwa anaamini kila kinachotokea katika maisha yake ni mipango ya Mungu.
“Maneno yao ni imani potofu na siwezi kumfikiria mwanaume niliyewahi kuwa naye huko nyuma kabla ya kuolewa na mume wangu Demonte kwani hakuna baya lililomfika tangu tulipooana,” alisema Aunt.
-GPL

MMILIKI ARSENAL ASEMA WENGER ANABAKI ARSENAL

wenger 24bf5
CHIFU wa Arsenal, Stan Kroenke anataka kocha Arsene Wenger abaki katika klabu hiyo kwa muda mrefu na kuleta taji la Ligi Kuu ya Enland Emirates.
Mfaransa huyo amekuwa katika klabu hiyo kwa miaka 17 na The Gunners ikiwa inakabiliwa na ukame wa mataji kwa msimu wa tisa sasa, amekuwa akipigwa zengwe aondoke, hususan kutokana na Mkataba wake kumalizika mwishoni mwa msimu.
Lakini mtu mwenye hisa nyingi za klabu, Kroenke hana shaka anataka Wenger abaki.
Mmarekani huyo amesema kwamba hafikiri kama kuna mwingine bora kuliko yeye na anaamini Wenger anafanya kazi nzuri.
Alipoulizwa kama mwalimu huyo mwenye umri wa miaka 63 yumo kwenye mipango ya muda mrefu ya klabu hiyo, Kroenke alisema: "Hiyo ni sahihi kabisa. Arsene anafahamu ambavyo tunahisi, falsafa zetu ni nini, nini tunataka kufanya na ninahisi tuko pamoja sana,".
Kufuatia klabu kuvuna rekodi yake ya usajili kwa kumsaini Mesut Ozil kutoka Real Madrid.
Kroenke alisema: "Kwa kweli namfurahia Arsene - safi sana, mweledi. Ana upeo mkubwa wa uongoza timu na klabu. Yuko sahihi katika hilio.
Kroenke pia amesema Wenger hastahili lawama kwa klabu hiyo la Kaskazin mwa London kumkosa mshambuliaji Luis Suarez, kwani ni Liverpool ndio hawakuwa tayari kumuuza nyota huyo kutoka Uruguay. Chanzo: binzubeiry

WAKUU WA USALAMA KUHOJIWA KENYA

wakuu_wa_usalama_ce362.jpg
Maafisa wakuu wa ujasusi wametakiwa kufika mbele ya kamati ya ulinzi ya bunge ili kuhojiwa kuhusu mashambulizi ya kigaidi dhidi ya jumba la Westgate mjini Nairobi.
Taarifa kwenye vyombo vya habari nchini humo zinaonyesha kuwa hali ya kulaumiana imeanza kuibuka huku mashirika ya usalama yakinyosheana kidole.
Watu 67 waliuawa kwenye shambulizi hilo huku zaidi ya miamoja sabini na tano wakipata majeraha mabaya. Shirika la Red Cross nalo linasema kuwa watu 61 wangali hawajulikani waliko.
Wataalamu wa uchunguzi wa mauaji wangali wanafanya uchunguzi wao wakitafuta miili na dalili za kilichosababisha shambulizi hilo.
Kamati ya bunge inataka maafisa wanaohusika na maswala ya usalama waweze kuwajibishwa.
Kundi la kigaidi la nchini Somalia, al-Shabab limedai kufanya mashambulizi hayo yaliyodumu siku nne kama hatua ya kulipiza kisasi kwa Kenya kujihusisha nchini Somalia kijeshi.
Hii leo ni siku ya tatu ya maombolezi kwa wathiriwa wa shambulizi hilo wakiwemo raia na wanajeshi.
Rais Uhuru Kenyatta amehudhuria mazishi ya mpwa wake na mchumba wake mjini Nairobi ambapo aliwahutubia waumini.
Walipuuza onyo?
Hatua ya kuwataka maafisa hao wa usalama kufika mbele ya tume ya bunge siku ya Jumatatu, inakuja kutokana na wasiwasi miongoni mwa wakenya kuhusu kiwango cha maafisa hao kujiandaa kwa tukio lolote la kigaidi sawa na lililotokea Westgate.
Kwa mujibu wa vyombo vya habari mmoja wa maafisa waliotakiwa kufika mbele ya kamati hiyo ni mkuu wa shirika la ujasusi Michael Gichangi, anayesema alitoa taarifa za ujasusi kuhusu shambulizi hilo kwa polisi.
Lakini, afisaa mmoja mkuu katika idara ya polisi alikana kuwa taarifa hiyo ilitolewa kwa polisi.

BAADAYA KUTOSWA NA DIAMOND, MDOGO WAKE AIMBA NYIMBO YA KUMPONDA

HUU wimbo hatari tupu. Inaelezea maisha ya Diamond kabla hajatoka kimuziki. Dogo aloimba anadai Diamond ni ndugu yake wa damu na hakumbuki alipotoka. Duuh kaongea mambo mengi sana. Sina mbavu kwa kweli. Isikilize hapa Chini. Ni balaa tupu. Ni bonge moja la Ngoma.

ANGALIA VIDEO YA NDOA YA WATOTO WADOGO HUKO MJINI DODOMA



Vitendo vya ukatili wa kijinsia bado vipo katika jamii yetu, huko mkoani Dodoma ilishuhudiwa ndoa ya watoto wadogo kabisa, kiukweli ni ya kushangaza na hata huwezi kuamini, ila ndio mambo ya walimwengu hawa.


  ANGALIA VIDEO HAPO CHINI...

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...