Friday, September 13, 2013

IPIGIE KURA BLOG YAKO YA JAMBO TZ ILI IWEZE KUSHINDA KATIKA TANZANIA BLOGS AWARDS

 
Upigaji kura umeanza (7/09/2013), blog hii imeshiriki kipengele cha The Best Newcomer Blog

Jinsi ya kuPiga kura, gonga/bofya/ click hayo maandishi yaliyoandikwa piga kura yako hapa, kisha chagua jambotz8.blogspot.com malizia na vote now.

 PIGA kura yako hapa..........!!! Jambo Tz

Ahsante Kwa Kutupigia Kura.

MAGAZETI YA LEO IJUMAA SEPTEMBA 13, 2013

DSC 0011 60970
DSC 0012 ebf41

RAIS KIKWETE AONGEZA VIONGOZI WANAOTAKIWA KUTANGAZA MALI ZAO

1_0ddb0.png
Waziri Mkuchika akizungumza kwenye katika Semina ya Wahariri wa Vyombo vya Habari semina hiyo.
2_cd971.png
Kamishna wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Jaji Mstaafu Salome Kaganda akizungumza na washiriki wa Semina (hawao pichani).Kushoto kwake ni Waziri Mkuchika na Mwenyekiti wa Baraza la Sekretarieti Balozi Jaji Mstaafu Hamisi Msumi.

JWTZ LAKANUSHA TAARIFA ZILIZOENEA MITANDAONI KUHUSU WANAJESHI WAKE

 
Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) limepata habari kupitia mtandao wa Jamii Forum na Gumzo la Jiji  na mingineyo kuwa likizo zimesitishwa Jeshini  na waliokuwa  likizo wameitwa kurudi kazini.
Taarifa hizo pia zimeeleza kwamba Brigedi za Tembo na Kifaru zimepewa maagizo ya kuwa katika hali ya utayari endapo watahitajika kusonga mbele.

JWTZ  linapenda kuwaeleza wananchi pamoja na watumiaji wa mitandao hiyo kuwa taarifa hizo ni za upotoshaji mtupu na hazina ukweli wowote.  Aidha, taarifa hizo ni zenye nia ya kuzorotesha uhusiano mzuri uliopo kati ya nchi yetu (Tanzania) na majirani zake. 

Sambamba na taarifa hii, pia Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania linapenda kutoa taarifa za kutohusika na viunganishi vya JWTZ kwenye mitandao ya  ‘Facebook‘ – (Facebook/JWTZ) na  ‘Twitter‘  (Twitter/ JWTZ).

Mitandao hiyo yenye viunganishi vya JWTZ imekuwa ikijihusisha na kutoa taarifa ambazo zimekuwa zikichangiwa na watu mbalimbali, ambapo baadhi yao wamekuwa wakitoa taarifa za upotoshaji  na zisizo sahihi.  Tunapenda kutaarifu kwamba akaunti za facebook na twitter zilizotajwa siyo za JWTZ.

Hatua zimechukuliwa za kuwatambua wahusika na kuwachukulia hatua za kisheria.

Aidha inasisitizwa kwamba JWTZ lina taratibu za zake zinazotumika kufanya mawasiliano na Vyombo vya Habari, Taasisi, au mtu binafsi kuhusu utoaji wa taarifa.

Imetolewa na:
Kurugenzi ya habari na Uhusiano
Makao Makuu ya Jeshi
Dar es salaam, Tanzania

Thursday, September 12, 2013

NDOA YA MZEE MAJUTO NA KABINTI KA MIAKA 20 YAVUNJIKA....!!


MWANAMKE anayedaiwa kufunga ndoa ya siri na mchekeshaji mahiri Bongo, Amri Athuman maarufu kama Mzee Majuto au King Majuto, Rahma Abdallah (20), ameibuka na kudai kutelekezwa na mumewe huyo.

Ndoa hiyo ambayo ilifungwa kwa siri jijini Dar Julai 28, mwaka huu na kudumu siku 44, inaonekana imevunjika rasmi baada ya Mzee Majuto kutoa talaka kupitia kwa msanii wa filamu aitwaye Rehema Omary.
 
Akizungumza na mwandishi wetu, Septemba 9, mwaka huu, Rahma alidai kuwa alikutana na Mzee Majuto jijini Tanga na kuanzisha uhusiano wa kimapenzi kwa miezi sita kabla ya kufunga ndoa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani uliopita.

“Tulifahamiana Tanga, mimi ni mwenyeji wa huko kama ilivyo kwa Mzee Majuto, wakati tukiwa kwenye uhusiano, ulipofika Mwezi wa Ramadhani akaona bora tufunge ndoa ili tusiendelee kutenda dhambi, akaniambia dhamira yake hiyo nami sikukataa,” alisema Rahma.

MAGAZETI YA LEO ALHAMISI SEPTEMBA 12, 2013

DSC 0016 8abf5
DSC 0017 c9f85

POLISI MKOANI DODOMA YASHINDWA KUMFIKISHA SUGU MAHAKAMANI


JESHI la Polisi mkoani Dodoma limeshindwa kumpandisha kizimbani Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi (CHADEMA), kwa madai kuwa upelelezi bado haujakamilika. Mbilinyi, maarufu kama ‘Sugu’ alifunguliwa jalada na jeshi hilo Ijumaa iliyopita, akidaiwa kumjeruhi jichoni askari wa Bunge, Koplo Nikwisa Nkisu.
Akizungumza na waandishi wa habari jana mjini hapa, Wakili wake, Tundu Lissu, alisema kuwa hawakufikishwa mahakamani kama walivyotegemea kutokana na kuelezwa kuwa upelelzi haujakamilika.
Lissu ambaye ni Mbunge wa Singida Mashariki, alisema kuwa baada ya mteja wake kuripoti kituoni aliambiwa kwamba upelelezi huo ukikamilika wataitwa ili kupewa maelezo ya hatua gani inafuata.
Alisema kitendo hicho cha polisi kuwaita bila kukamilisha upelelezi wao ni kuwapotezea muda.
“Nashangaa ni kwanini tunaitwa, tuliambiwa tufike hapa, lakini tulipokuja hapa hakuna jambo lolote la maana tuliloambiwa, badala yake wanasema tuendelee na shughuli zetu upelelezi haujakamilika na baada ya wiki mbili watatuambia kinachoendelea.

JWTZ WAMPA KICHAPO CHA MBWA MWIZI HAKIMU HUKO KARAGWE KWA KUMDHANIA KUWA NI MNYARWANDA

Matendo Manono (kushoto)
Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Matendo Manono ambaye ni Hakimu Mkazi katika Mahakama ya Wilaya ya Karagwe mkoani Kagera amelalamikia kitendo cha kupigwa na kujeruhiwa vibaya na Askari wa Tanzania, katika zoezi la kuwaswaga wahamiaji haramu wa kinyarwanda wanao ishi nchini Tanzania.
 
 Soma maelezo ya hakimu huyo hapo chini...

" i have a serious contempt of this country...while they know for sure that this country has no National ID stil they want us to show Citizenship ID...
 
Imagine this was travelling to western part of TZ (Karagwe) today i have been arrested by the damned Immigration, police officers and JW people that am a prohibited immigrant simply because am tall with big (long,edged?)nose ..

i have been seriously humiliated and beaten simply because i resemble Rwandese something which is neither sin nor unlawful under The Immigration Act or The Citizenship Act....
I don't know if those people of Human Rights know what is happening in Kagera...total violation of human rights "

KLABU YA SOKA YA SUNDERLAND YA UINGEREZA KUWEKEZA KATIKA SEKTA YA UTALII PAMOJA NA KUINUA MCHEZO WA MPIRA WA MIGUU NCHINI

Mkurugenzi wa Biashara wa klabu ya Sunderland.Bw Gary Hutchinson(wapili kushoto)akiongea na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam kuhusu hatua ya mazungumzo waliyofikia na kujenga kituo cha michezo katika Manispaa ya Ilala ambayo itakuwa chimbuko la kuinua mchezo wa mpira wa miguu(wakwanza kulia)Mkurugenzi wa Michezo Nchini bw.leonard tadeo(wapili kulia)Mkurugenzi wa Mwendeshaji wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) Dk. Aloyce Nzuki(wakwanza kushoto)Mwakilishi wa klabu ya Sunderland Tanzania,Bw Edmund Hazzad.
Mkurugenzi wa Mwendeshaji wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) Dk. Aloyce Nzuki.akifafanua kuhusu sekta ya Utalii inafanikiwa na kuinua uchumi wa nchi kupitia michezo Nchini.
Mkurugenzi wa Biashara wa klabu ya Sunderland.Bw Gary Hutchinson,(kushoto)akimkabidhi mkurugenzi wa wizara ya michezo bw.leonard Tadeo.jezi ambao imesainiwa sahihi na wachezaji wa sunderland.

Wednesday, September 11, 2013

KILICHOMUUA MSANII HUYU KINASIKITISHA.....!!!


TASNIA ya filamu Bongo imepata pigo lingine baada ya mwishoni mwa wiki iliyopita kuondokewa na msanii aliyekuwa akichipukia kwa kasi aliyefahamika kwa jina la Zuhura Maftah ‘Malisa’.
Malisa alifariki dunia katika Hospitali ya Hindu Mandal jijini Dar baada ya kusumbuliwa na uvimbe kichwani kwa takriban miezi mitatu.
Wakizungumza na gazeti hili mara baada ya kifo hicho, baadhi ya wasanii wa filamu walielezea masikitiko yao na kusema hakika wamemkosa msanii ambaye siku za baadaye angekuwa moto wa kuotea mbali.
“Kifo chake kimetusikitisha sana, Malisa alikuwa mmoja wa wasanii ambao walikuwa wakija kwa kasi, amefariki dunia wakati ndiyo kwanza nyota yake ilikuwa imeanza kung’ara lakini kazi ya Mungu siku zote haina makosa, akapumzike kwa amani,” alisema mmoja wasanii aliyeomba hifadhi ya jina lake.
Msanii mwingine wa filamu ambaye huenda kifo hicho kimemgusa kuliko wengine ni Yvonne Cheryl ‘Monalisa’ ambaye inadaiwa muda mfupi kabla ya Malisa kufariki waliongea na kumwambia anaendelea vizuri.
Mmoja wa watu waliokuwa wakimhudumia Malisa hospitalini hapo aliyefahamika kwa jina la Vanitha alisema: “Siku ya kifo chake aliniambia nimpigie simu Mona aongee naye kwani hajamuona siku hiyo, ilikuwa saa 12 jioni baada ya kumaliza kumuogesha.
“Waliongea na kumwambia anaendelea vizuri. Baada ya Malisa kumaliza kuongea na Mona niliondoka lakini nilipofika Surender Bridge nikapata taarifa kuwa amefariki dunia,” alisema Vanitha.

NDUNGAI NA MBOWE WALIVUNJA KANUNI ZA BUNGE MAKUSUDI KWA MASLAHI YA VYAMA VYAO


Kumekuwa na mjadala mkali kuhusu iwapo Naibu Spika, Job Ndugai alikiuka Kanuni za Bunge katika kushughulikia vurugu zilizotokea Bungeni Alhamisi iliyopita kwa kuamuru kutolewa nje kwa Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe. 

Ndugai ambaye alikuwa kiongozi wa shughuli za Bunge siku hiyo, aliwaamuru askari kumtoa nje Mbowe baada ya kukaidi amri yake ya kutaka kuketi chini aliposimama kutaka kupewa nafasi ya kuzungumza, hali iliyozua tafrani bungeni. 

Pamoja na mambo mengine Ndugai amekuwa akituhumiwa kwamba anaminya uhuru wa wabunge wa upinzani kutokana na mapenzi aliyonayo kwa chama chake, CCM.
 
Kwa upande mwingine, kumekuwa na lawama kwamba Mbowe alikosea kukaidi amri ya Naibu Spika kwa kuwa kanuni zinamtaka mbunge yeyote (hata akiwa waziri), kuketi pale kiongozi wa Bunge (Spika, Naibu au Mwenyekiti) anaposimama, hivyo kusababisha mtafaruku.

NAPE: CHADEMA WAMEPEWA MABILIONI TOKA NJE KUVURUGA MCHAKATO WA KATIBA.


ZNape_7c07c.png
Adai ndio chanzo cha kupigana bungeni Asema ndizo walizotumia kuzunguka na helkopta nchini. Aeleza yaliyotokea bungeni sio bahati mbaya, Chadema waliyapanga Ashukuru bunge kuendelea kuonyeshwa"live" ili wananchi waone ujinga wao.
 Awatuhumu kuweka masilahi yao mbele badala ya nchi. Asisitiza CCM kuendelea kuheshimu uamuzi wa wananchi juu ya katiba. Aonyesha madai ya Chadema kitakwimu yasivyojali wakulima na wafanyakazi.



Katibu wa NEC ya CCM itikadi na Uenezi amesema kinachowasumbua Chadema mpaka wanafanya yote waliyoyafanya hasa ngumi na vurugu bungeni ni namna watakavyoeleza kwa waliowapa pesa za kuvuruga mchakato wa katiba nchini kwani wanatakiwa kupeleka mrejesho jinsi walivyofanikiwa na jinsi walivyotumia mabilioni hayo.

Nape ameyasema hayo kwenye mkutano mkubwa wa hadhara mjini Kahama kwenye ziara ya karibu siku ishirini kanda ya ziwa kwa mikoa mitatu yaani Shinyanga,Simiyu na Mara ya Katibu Mkuu wa CCM Taifa Ndg. Abralhaman Kinana.

MAGAZETI YA LEO JUMATANO SEPTEMBA 11, 2013

DSC 0525 d5eb2
DSC 0526 0ce62

MASHITAKA MATATU ALIYOSOMEWA MAKAMU WA RAIS WA KENYA MBELE YA MAHAKAMA YA ICC


William Ruto amekana mashtaka yote yanayomkabili kwenye Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC).

Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Mahakama hiyo, Fatou Bensouda anayesimamia kesi hiyo, alisema watuhumiwa wawili waliofikishwa mahakamani hapo jana, Ruto na mtangazaji wa Redio, Joshua arap Sang wanakabiliwa na mashtaka matatu kila mmoja, ambayo ni kuwalazimisha watu kukimbia makazi yao, mauaji na kuchochea ghasia.


Kesi hiyo imeanza kusikilizwa siku chache baada ya Bunge la Kenya kupiga kura kutaka nchi hiyo ijitoe uanachama wa ICC, wakieleza kwamba imekuwa haina tija na inatumiwa kuwakandamiza Waafrika.


Ruto ambaye alionekana kujiamini alifika kwenye jengo la Mahakama akiwa ameambatana na baadhi ya wabunge waliosafiri kutoka Kenya hadi The Hague kwa ajili ya kumuunga mkono.

MFANYABIASHARA MAARUFU ALEX MASSAWE AFIKISHWA MAHAKAMANI HUKO DUBAI


Mfanyabiashara maarufu nchini, Alex Massawe amefikishwa mahakamani Dubai, Falme za Kiarabu (UAE), kwa tuhuma za mauaji baada ya Serikali ya Tanzania kupitia Shirika la Polisi la Kimataifa (Interpol), kuiomba Serikali ya nchi hiyo kumkamata.

Massawe anayetarajiwa kuletwa nchini wakati wowote kuanzia sasa, alikuwa anatafutwa na Polisi wa Tanzania kwa muda mrefu na alikamatwa Dubai, mapema Julai na maofisa wa usalama wa UAE baada ya alama zake za vidole kuonyesha kuwa alikuwamo kwenye orodha ya watu waliokuwa wanasakwa na Interpol.

Baada ya kukamatwa, Mkuu wa Interpol, Tawi la Tanzania, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP), Gustav Babile alisema Massawe alikamatwa kati ya Juni 20 na 25, mwaka huu kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dubai akitokea Afrika Kusini.

Massawe ambaye anafanya biashara zake katika Miji ya Arusha, Dar es Salaam na Moshi, inadaiwa kwamba akiwa Dubai, alikutwa na pasi tatu bandia za kusafiria zilizokuwa na majina tofauti wakati alama zake za vidole zilionyesha anaitwa Alex Massawe. “Ombi la kuleta mhalifu nchini kutoka nje ya nchi (extradition request), lina hatua ndefu.
Unajua kuna mlolongo wa taratibu za kutekeleza. Kwanza lazima Polisi wa Tanzania watoe tangazo kwa Interpol kuhusu kumsaka mtu huyo ili aletwe,” alisema Babile.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...