Sunday, August 11, 2013

SERIKALI YA RWANDA IMEAPA KUTOWAFUKUZA WATANZANIA...!!!

Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Rwanda amesema kamwe hawatawafukuza Watanzania wanaoingia na kutoka nchini Rwanda kwa shughuli mbalimbali kwani tupo ndani ya shirikisho la Afrika Mashariki na hata kihistoria Rwanda haijawahi kuwa na tatizo na Tanzania.

Akizungumzia sakata la wahamiaji haramu wa Kinyarwanda kufukuzwa na serikali ya Tanzania amesema, kila nchi inayo mamlaka ya kufanya vile inafaa lakini ingekuwa vizuri Tanzania ingewasiliana na Rwanda ili kujua wataondokaje na kupokelewa vipi.

Amesisitiza, "Kwa kuwa wenzetu wameamua kufanya hivyo, tupo tayari kuwapokea wananchi wetu" Lakini pia, Waziri huyo amesema waasi wa FDRL ni kikundi cha wauaji wanaojipanga kuangamiza watu fulani nchini Rwanda hivyo wanatakiwa kupingwa kwa nguvu zote badala ya kuwatambua na kuzungumza nao kama kundi halali na lenye nia njema.

Naye Mtanzania Mohammed, amependekeza Rais Kagame na Kikwete wakutane na kufikia suluhu.Pia baadhi ya Wanyarwanda wamelalamikia kutokutendewa haki kwa kutenganishwa na wake,waume, n.k

TAARIFA RASMI YA JESHI LA POLISI KUHUSU KUPIGWA RISASI SHEKHE PONDA

 Advera Senso- SSP-Msemaji wa Jeshi la Polisi.
--
 JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NDANI

JESHI LA POLISI TANZANIA 
DAR ES SALAAM AGOSTI 10, 2013.
 
1.  MNAMO TAREHE 10, AGOSTI ,2013 MAJIRA YA SAA 8 MCHANA, MAENEO YA SHULE YA MSINGI KIWANJA CHA NDEGE MANISPAA YA MOROGORO, KULIFANYIKA KONGAMANO LA BARAZA LA EID LILILOANDALIWA NA UMOJA WA WAHADHILI MKOANI MOROGORO. DAKIKA KUMI KABLA YA KONGAMANO HILO KUMALIZIKA  ALIFIKA SHEKHE PONDA ISSA PONDA AMBAYE ALIZUNGUMZA KWA MUDA MFUPI.
 
2. KONGAMANO HILO LILIFUNGWA  MAJIRA YA SAA 12:05 JIONI AMBAPO WATU WALIANZA KUTAWANYIKA, BAADHI YAO WAKIWA WAMEZINGIRA GARI DOGO ALILOKUWA AMEPANDA SHEKHE PONDA. BAADA YA KUTOKA KATIKA  ENEO HILO, ASKARI WA JESHI LA POLISI WALIZUIA GARI HILO KWA MBELE KWA NIA YA KUTAKA KUMKAMATA SHEKHE PONDA AMBAYE MPAKA SASA ANATUHUMIWA KWA KOSA LA KUTOA MANENO YA UCHOCHEZI SEHEMU MBALIMBALI HAPA NCHINI YENYE MLENGO WA KUSABABISHA UVUNJIVU WA AMANI.
 
3. BAAADA YA ASKARI KUTAKA KUMKAMATA, WAFUASI WAKE WALIZUIA UKAMATAJI HUO KWA KUWARUSHIA  MAWE ASKARI.  KUFUATIA PURUKUSHANI HIYO, ASKARI WALIPIGA RISASI HEWANI KAMA ONYO LA KUWATAWANYA.
 
4. KATIKA VURUGU HIZO, WAFUASI HAO WALIFANIKIWA KUMTOROSHA MTUHUMIWA.  HIVI SASA IMETHIBITIKA KUWA SHEKHE PONDA YUKO KATIKA HOSPITALI YA TAIFA YA MUHIMBILI AKITIBIWA JERAHA KATIKA BEGA LA MKONO WA KULIA LINALODAIWA ALILIPATA KATIKA PURUKUSHANI HIZO.
 
5. KUFUATIA TUKIO HILO, TIMU INAYOSHIRIKISHA WAJUMBE KUTOKA JUKWAA LA HAKI JINAI IKIONGOZWA NA KAMISHINA WA JESHI LA POLISI  CP ISSAYA MNGULU IMEANZA KUFANYA UCHUNGUZI WA TUKIO HILO.
 
6. AIDHA, JESHI LA POLISI LINATOA  WITO KWA  WANANCHI KUWA WATULIVU WAKATI SUALA HILI LINASHUGHULIKIWA KISHERIA.
 
Imetolewa na:-
Advera Senso- SSP
Msemaji wa Jeshi la Polisi.

HIVI NDIVYO SHEIKH ISSA PONDA ALIVYOJERUHIWA....!!!



SERIKALI YADAIWA KUMGEUKA DR ULIMBOKA YADAI AMEFICHA USHAHIDI WA KUTEKWA KWAKE


SIKU chache baada ya Mahakama ya Kisutu kumwachia mtu aliyedaiwa kumteka na kumtesa kiongozi wa Jumuiya ya Madaktari nchini, Dk. Steven Ulimboka, serikali imemshukia daktari huyo na kudai ndiye chanzo cha kukwama kwa dola kukamata watu waliomteka.

Jana Mwendesha Mashitaka Mkuu wa Serikali (DPP), Eliazer Feleshi, alidai kuwa vyombo vya dola vimeshindwa hadi sasa kuwakamata waliohusika katika shambulio hilo kutokana na Dk. Ulimboka kukwepa kutoa ushirikiano kwa Jeshi la Polisi.

Feleshi ambaye jana aliambatana na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, Said Mwema, katika mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, alidai lawama zinazosukumwa kwa Jeshi la Polisi kwa madai ya kushindwa kuwakamata waliomtendea unyama daktari huyo hazina msingi, kwa kuwa mhusika mwenyewe hajafika polisi, licha ya kuitwa mara nyingi kutoa maelezo.

Alisema kama Dk. Ulimboka angetoa ushirikiano kwa Jeshi la Polisi kungekuwa na mafanikio makubwa katika kuwasaka na hata kuwatia mbaroni waliohusika katika unyama huo.

“Kila mara mmekuwa mkilaumu polisi wanashindwa kukamata wahalifu lakini tutakamataje kama wenye ushahidi hawataki kutoa ushirikiano?

Kwa mfano mdogo tu ni ‘ishu’ (suala) ya Dk. Ulimboka, hadi leo hajatoa taarifa lakini polisi wanaendelea kusakamwa na kutukanwa tu,” alisema.

Hata hivyo, wakati Feleshi akitoa kauli hiyo, Dk. Ulimboka katika andiko lake alilolitoa mara tu baada ya kurejea nchini kutoka Afrika Kusini alikopelekwa kwa ajili ya matibabu, alimtaja mtu anayeaminika kuwa mfanyakazi wa Idara ya Usalama wa Taifa, Ramadhani Ighondu, kuwa ndiye aliyemteka na kumtesa.

Ulimboka akimtumia Wakili Nyaronyo Kicheere alisema Ighondu na wenzake ni mhusika mkuu katika unyama aliofanyiwa, kauli ambayo imekanushwa mara kadhaa na serikali.

Mapema wiki hii, raia wa Kenya, Joshua Mulundi, aliyekuwa akikabiliwa na tuhuma za kumteka na kumtesa Dk. Ulimboka aliachiwa na Mahakama ya Kisutu baada ya DPP Feleshi kumfutia shitaka. Hata hivyo Mulundi alikamatwa tena na sasa amefunguliwa mashitaka ya kutoa maelezo ya uongo kwa polisi.

KUTOKA KWENYE MTANDAO WA DAILYMAIL UINGEREZA:SHEIK PONDA AHUSISHWA NA KESI YA MABINTI WA UINGEREZA WALIOMWAGIWA TINDIKALI

Sheikh Ponda Issa who is suspected of inciting the attack on Kirstie Trup and Katie Gee was shot by police in Tanzania's capital last night

Sheikh Ponda Issa who is suspected of inciting the attack on Kirstie Trup and Katie Gee was shot by police in Tanzania's capital last night 


A radical Muslim preacher wanted in connection with an acid attack on two British teenagers in Zanzibar has been shot by police, it was reported.

Sheikh Issa Ponda Issa was hit in the shoulder with a tear gas canister as he tried to escape from officers after being cornered near Tanzania's capital Dar es Salaam, The Sunday Mirror said.

JAPAN KUJENGA KIWANDA CHA PIKIPIKI TANZANIA

070 6d3e9 
Serikali ya Japan imesema ina mpango kabambe wa kukuza uchumi wa Tanzania, ikiwa ni pamoja na kampuni kubwa duniani za Honda na Panasonic kujenga viwanda vitakavyokuwa matawi yake hapa nchini. (HM)

Uamuzi na msimamo wa Japan umetangazwa jana jijini Dar es Salaam na Waziri wa Uchumi, Biashara na Viwanda wa nchi hiyo, Toshimistu Motegi alipokutana na kufanya mazungumzo na Rais Jakaya Kikwete, Ikulu.

Taarifa ya Ikulu iliyosambazwa na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, ilimnukuu Motegi akisema: "Kwa kuanzia kampuni mbili za Honda na Panasonic zimekubali kujenga viwanda nchini, kimoja kwa ajili ya kutengeneza pikipiki za Honda na kingine kwa ajili ya kutengeneza vifaa vya umeme."

Akaweka msisitizo: "Huu ni mwanzo tu Mheshimiwa Rais (Kikwete) kwa sababu kama nilivyosema kuwa tunataka Tanzania kuwa nchi ya mfano ya uwekezaji wa Japan katika eneo hili la dunia, na namna hiyo kwa pamoja tutakuwa tumeshirikiana katika kuongeza ajira kwa wananchi wa Tanzania."

WAINGEREZA WALIOMWAGIWA TINDIKALI WAITESA SERIKALI

071 c44b8

Siku tano baada ya raia wawili wa Uingereza kumwagiwa tindikali visiwani Zanzibar, Serikali kupitia vyombo vyake vya uchunguzi imeibuka na kueleza kuwa bila wananchi kutoa taarifa za ushahidi wa uhalifu wa aina mbalimbali, ni vigumu kuwabaini wahusika. (HM)

Kauli hiyo ilitolewa kwa pamoja jana na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Said Mwema, Mkemia Mkuu wa Serikali, Profesa Samwel Manyele na Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali (DPP) Eliezer Feleshi, katika mkutano wao na waandishi wa habari, uliolenga kueleza mikakati ya kupambana na matumizi yasiyo sahihi ya tindikali nchini.

Katika ufafanuzi wao walisema, "Kutoa taarifa ya uhalifu wa jambo lolote siyo hiari, ni jukumu la kisheria na kikatiba," huku Feleshi akitolea mfano jinsi Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari nchini, Dk Steven Ulimboka alivyoshindwa kutoa ushahidi wa tukio lililomkuta la kutekwa, kupigwa na kisha kutupwa katika Msitu wa Mabwepande, hivyo kufanya uchunguzi kuwa mgumu.

Saturday, August 10, 2013

NDEGE YA KIJESHI YALIPUKA NA KUTEKETEA KWA MOTO WAKATI IKITUA KWA DHARURA.

Ndege hiyo ilikuwa ya jeshi la Ethiopia.MOJA YA NDEGE ZA NCHI YA SOMALIA.Ndege ya kivita MaliPICHA YA NDEGE ZA JESHI YA MAKTABA SIO YA SOMALIA.
NDEGE ya kijeshi imelipuka na kuteketea nchini Somalia baada ya kutua kwa dharura katika uwanja wa kimataifa wa ndege mjini Mogadishu.
Kikosi cha muungano wa Afrika nchini Somalia ambacho kina kambi yake katika uwanja huo wa ndege kimesema kuwa wanajeshi wake kadhaa wameuawa na wengine wawili kujeruhiwa.

Inasemekana kuwa ndege hiyo ilikuwa ya jeshi la Ethiopia.
Kuna ripoti kuwa ndege ilikuwa imebeba zana za kivita.
Wafanyakazi katika uwanja huo wa ndege waliel
ezea kusikia milipuko kadhaa huku moto ukienea kwa ndege hiyo.

JESHI LA POLISI LATANGAZA DAU LA MILIONI 10 KWA MTU ATAKAYEWATAJA WATU WALIOWAMWAGIA TINDIKALI WAZUNGU

Zanzibar, Tanzania — Kamanda wa Polisi, Kamishna Musa Ali Musa amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imeahidi kutoa Shilingi milioni 10/= kwa mtu yeyote atakayetoa taarifa zitakazofanikisha kukamatwa kwa watu waliowashambulia mabinti wawili kutoka Londona, Uingereza, Kirstie Trup na Katie Gee.

Mabinti hao walishambuliwa kwa tindikali usoni, kifuani na mikononi siku ya Jumatano walipokuwa njiani kuelekea kwenye chakula cha jioni.

Friday, August 09, 2013

JAJI MUTUNGI AANZA KUTUMA SALAMU ZA UTENDAJI KAZI WAKE ....!!!



Jaji Mkuu, Mohamed Chande Othman akimpongeza Francis Mutungi baada ya kuapishwa na Rais Jakaya Kikwete kuwa Jaji wa Mahakama Kuu katika hafla iliyofanyika Ikulu, Juni 19,2012. Jaji Mutungi jana aliteuliwa kuwa Msajili wa Vyama vya Siasa. Picha na Maktaba. 
********
Dodoma. Msajili mteule wa Vyama vya Siasa nchini,  Jaji Francis Mutungi amewataka Watanzania kutulia na kusubiri utendaji wake atakapokabidhiwa rasmi jukumu hilo jipya alilopewa na Rais Jakaya Kikwete.
Mutungi aliteuliwa kushika wadhifa wa msajili wa vyama vya siasa kuchukua nafasi ya John Tendwa ambaye amestaafu. Tendwa aliiongoza taasisi hiyo kwa miaka 13.
Mutungi alisema: “Ninafahamu nina majukumu mazito mbele yangu, lakini siwezi kusema chochote kwa kuwa sijakabidhiwa rasmi ofisi. Ninachotaka kusema ni kwamba nitakuwa mtumishi wa kila mmoja.”

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL ASHIRIKI SWALA YA SIKUKUU YA IDDI KITAIFA MKOANI TABORA


 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akitoa salamu maalum za Sikukuu ya Iddi baada ya Swala iliyofanyika Kitaifa Mkoani Tabora katika Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi leo.

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal (wa sita kutoka kulia), akishiriki na waumini wa dini ya Kiislamu katika Swala ya Sikukuu ya Iddi, iliyoswaliwa Kitaifa kwenye Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi Mkoani Tabora leo.

SIMBA KUADHIMISHA SIMBA DAY KESHO TEREHE 10.

KESHO, Jumamosi tarehe 10 Agosti mwaka 2013, klabu ya soka ya Simba itaadhimisha kile kinachoitwa Siku ya Simba (SIMBA DAY) katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
 
Utaratibu wa kuwa na Simba Day ulianzishwa na klabu kwa lengo la kuwa na siku ambapo wapenzi, wanachama, viongozi, wachezaji wa zamani na wa sasa pamoja na watu wengine mashuhuri, hukutana kwa pamoja na kusherehekea klabu ambayo imewafanya wawe wamoja pamoja na tofauti nyingi walizonazo.
 
Mwaka huu, shughuli hiyo itafanyika katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Pamoja na mambo mengine, Simba SC inatarajiwa kucheza mechi ya kirafiki na klabu ya soka ya Sports Club Villa kutoka nchini Uganda.
Katika kusherehesha tukio hilo, wasanii maarufu kama vile Juma Nature, Tunda Man na Snura maarufu kwa jina la ‘Mama Majanga’ watatumbuiza uwanjani hapo.

MUME WA JOYCE KIRIA, HENRY KILEWO AWALIZA WATU KWENYE MKUTANO MABIBO SAHARA

Leo akiwa anawahutubia wakazi wa mabibo-Sahara kwa mara ya kwanza toka atoke jela huko gereza la uyui- Tabora ktk mkutano ambao mgeni rasmi alikua John Mnyika, aliwaliza baadhi ya wananchi waliofika katika mkutano huo. Hii kutokana na kuguswa na hotuba ya kamanda Kilewo ambayo ilikua inaudhunisha kutokana na simulizi ya namna alivyokamatwa na huko jela namna ya watu waliofungwa pasipo na hatia.

kiukweli inasikitisha, lakini bado alisisitiza kwa kusema 'hakuna dhambi kubwa hapa duniani kama uoga' na ' watatupiga kwa mabomu na watatu ua kwa risasi lakini na wao watakufa kwa presha ya dhambi

WANYARWANDA 520 WATII AGIZO LA RAIS KIKWETE LA KUONDOKA NCHINI

044 2423a 
Zikiwa zimesalia saa 48 kabla ya kumalizika kwa muda uliotolewa na Rais Jakaya Kikwete kwa wahamiaji haramu kuondoka nchini au kuhalalisha ukaazi wao na wenye silaha kuzisalimisha, makundi ya wahamiaji hao, yameanza kuondoka kwa hiari.
Wastani wa wahamiaji haramu 150 wanaendelea kujiandikisha kuvuka mpaka katika Kituo cha Rusumo, Ngara mkoani Kagera kutekeleza agizo hilo.

Ofisa Uhamiaji wa Kituo cha Rusumo, Samweli Mahirane alisema mpaka sasa Wanyarwanda 520 wameshaondoka katika maeneo mbalimbali ndani na nje ya Ngara na kurejea makwao huku Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Fabian Massawe akisema silaha 17 za aina mbalimbali zimesalimishwa.
Mahirane alisema wahamiaji hao wanatokea katika vijiji vya Wilaya za Ngara, Karagwe, Kyerwa, Biharamulo na Geita pamoja na Runzewe na wamekuwa wakiishi katika maeneo hayo bila vibali halali. (HM)

"Kuondoka kwa hiari kwa wahamiaji haramu, kutahitimishwa Jumatatu Agosti 12 na baada ya tarehe hiyo, vyombo vya dola vitaanza kufanya kazi kama agizo la Rais Kikwete lilivyoelekeza katika Mikoa ya Kagera na Kigoma," alisema.
Aliwahakikishia wahamiaji hao usalama katika mataifa yao kwani hivi karibuni Serikali ya Rwanda ilikubali kuwapokea hata walio na mifugo kwa masharti kuwa ndani ya kipindi kifupi wataipunguza kwa kuiuza na kuboresha maisha yao.

"Rwanda wanahitaji mifugo michache, hivyo walio na mingi wanatakiwa kuipunguza kwa kuuza na kujenga makazi bora ikiwa ni pamoja na kuhifadhi ama kulinda mazingira ya nchi hiyo," alisema Mahirane. Chanzo: mwananchi

MOURINHO: HATUTAKATA TAMAA MPANGO WA KUMSAJILI ROONEY...!!!

jose 13f47
Jose Mourinho amesisitiza kwamba atapigana mpaka siku ya mwisho katika jaribio lake la kumsaini Wayne Rooney. (HM)

Chelsea tayari walishatuma ofa mbili ambazo zimekataliwa na Manchester United, ofa ya mwisho inayotajwa kuwa ni zaidi ya paundi million 25 ilitumwa jumapili. Lakini Mourinho alisema: "Hatuna kizuizi cha muda kwenye suala hili.

'Tumemuona Rooney kama ni mchezaji ambaye tungependa kuwa nae. Tumefanya kila kitu katika utaratibu unaopaswa na tutafanya hivyo mpaka siku ya mwisho ya usajili. Tunafnya kila kitu tukizingatia sheria, kutoa ofa rasmi kwa klabu moja kwa moja.
 

'Hakujawahi kuwepo kwa mawasiliano na mchezaji, hakijatokea kitu kama hicho. Tusubiri tuone kama mambo yatabadilika.'

Rooney inaaminika kwamba amemwambia kocha wake David Moyes kwamba anataka kuondoka, lakini United imekuwa ikisisitiza kwamba hauzwi. Chanzo: shaffihdauda

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...