Wednesday, May 22, 2013

Simba, Yanga kikaangoni Kagame

Katibu Mkuu wa CECAFA, Nicholas Musonye
Mabingwa watetezi wa mashindano ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati (Kombe la Kagame), Yanga wataanza kutetea taji lao dhidi ya Express ya Uganda katika mechi ya kundi C Juni 20 kwenye Uwanja wa Elfasher saa nane mchana wakati Simba iliyopangwa kundi A la 'kifo' itashuka dimbani siku inayofuata kuivaa El Mereikh.

Kwa mujibu wa ratiba ya mashindano hayo yatakayoanza Juni 18 hadi Julai 2 mwaka huu iliyotolewa jana na Shirikisho la Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA), timu nyingine zinazounda kundi C pamoja na Yanga ni Vital'O ya Burundi na Ports ya Djibouti wakati kundia la kundi A la Simba linahusisha pia timu za APR ya Rwanda na Elman ya Somalia.

Ratiba hiyo inaonyesha kuwa kundi B limezoa timu wenyeji zote tatu za Al Hilal, Al Nasri na Al Ahly Shandy pamoja na Tusker ya Kenya na Super Falcon kutoka Zanzibar.

Yanga ambao ni mabingwa wapya wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara watashuka tena dimbani Juni 22 mwaka huu kuikabili Ports na watakamilisha mechi za hatua ya makundi Juni 25 kwa kuvaana na Vital'O.

SIMBA YAMPANDISHA NGASSA MAHAKAMANI, HIKI NDO SIMBA WALICHOKISEMA

Mrisho Ngassa akikabidhiwa jezi bada ya kujiunga na Yanga.
UONGOZI wa Simba umechukua uamuzi wa kumpandisha kizimbani kiungo mshambuliaji, Mrisho Ngassa kutokana na uamuzi wake wa kusaini mkataba wa miaka miwili kuichezea Yanga.

Ngassa aliyekuwa akiichezea Simba kwa mkopo kutoka Azam FC, amesaini mkataba wa miaka miwili kuichezea Yanga lakini Simba wamesema walishasaini naye mkataba wa mwaka mmoja.
Habari za uhakika kutoka ndani ya Simba zimeeleza kuwa, Msimbazi wameamua kufanya mambo yao kimya na wameamua kutumia mahakama ili iwe fundisho kwa wachezaji wengine.
“Hakika sasa tumeona suala hili si la kufanya kama filamu, maana wenzetu (Yanga) pamoja na Ngassa wameamua kutufanyia uhuni. Wachezaji wanataka kufanya Simba ni kama sehemu ya kuchota fedha na kuondoka.
“Kitu kibaya zaidi tumegundua system (mfumo) ya soka imekuwa ikiwalinda sana kutokana na ushabiki mkubwa uliopo katika kamati zilizo chini ya TFF. Sasa sisi tumeona bora kuchukua hatua zaidi,” kilieleza chanzo cha uhakika.

UWOYA, JOHARI KUZURU SAUZI....!!!

Irene Uwoya.
MASTAA wa sinema za Kibongo, Irene Uwoya na Blandina Chagula ‘Johari’ wametimkia nchini Afrika Kusini ‘Sauzi’ kwenda kurekodi filamu. Akizungumza na paparazi wetu hivi karibuni kwa njia ya simu akiwa nchini humo, Uwoya alisema wamekwenda nchini humo kurekodi sinema ambayo Watanzania wataitambua ikikamilika. Pia wataunganisha na ziara ndefu katika nchi mbalimbali barani Afrika zikiwemo Namibia, Ghana, Lesotho na kwingineko kujifunza soko la filamu.
 
Blandina Chagula ‘Johari’.
“Tupo huku na Johari lakini tutakuwa na ziara ndefu sana ya nchi mbalimbali za Afrika kwa ajili ya kulisogeza soko letu la filamu na kujifunza jinsi wenzetu wanavyofanya katika filamu zao,” alisema Uwoya.

WASTARA RUKSA....... KUOLEWA

Wastara Juma.
Habari kutoka kwa chanzo chetu cha kuaminika kilicho karibu na msanii huyo, zinasema kwamba Wastara amemaliza salama eda yake baada ya kufiwa na mumewe Juma Kilowoko ‘Sajuki’ Januari, mwaka huu.
Staa huyo bado yupo Muscat, Oman alikoitwa na ndugu zake kwa ajili ya kukaa eda hiyo na kupumzika baada ya kupata masaibu ya kuondokewa na mumewe kipenzi.
KAMA MWARABU
Chanzo kinaeleza kuwa uamuzi wa Wastara kwenda kukaa eda Uarabuni ni mzuri kwa sababu kwa sasa yupo vizuri kiafya na mawazo ya kuondokewa na mwenzake yamepungua.
“Ni kweli kifo hakizoeleki lakini Wastara amejitahidi sana kutuliza kichwa chake. Ndugu zake wamemsaidia sana, wamekuwa naye katika kipindi hiki kwa upendo wa hali ya juu.


“Yaani ukimuona jinsi alivyopendeza utashangaa, ni kama Mwarabu kabisa. Mungu mkubwa sana jamani, kila mtu anafurahishwa na jambo hilo. Mungu ataendelea kumsimamia,” kilipasha chanzo hicho kilichoomba hifadhi ya jina lake gazetini.


Wastara akiwa Uarabuni.
KUTUA BONGO

KAKA, DADA WANASWA WAKIDUU COCO BEACH, MCHEZO MZIMA ULIKUA HIVI!

UKISTAAJABU ya Musa utayaona ya Firauni. Usemi huu unakamilishwa na tukio la kunaswa kwa vijana wawili wenye undugu wa damu wakifanya mapenzi ‘wakiduu’ kando ya Ufukwe wa Bahari ya Hindi!
Vijana wawili wenye undugu wa damu baada ya kunaswa wakifanya mapenzi.
Imefahamika kwamba vijana  hao, kaka na dada (majina tunayo)  wamenaswa ‘wakiduu’ katika mapango yaliyopo kando ya Ufukwe wa Coco, Oysterbay jijini Dar es Salaam.
TUKIO ZIMA
Tukio zima lilitokea mchana kweupe wa saa 9 na kudhihirisha habari za mara kwa mara zinazoeleza kwamba Ufukwe wa Coco umekuwa ukitumika kwa ufuska usiku na mchana.
Risasi Mchanganyiko lilinasa tukio hilo kwa kutumia mitambo maaalum iliyoelekezwa kando ya bahari.
Wawili hao walinaswa tangu walipokuwa wakiingia katika ufukwe huo na kuwafuatilia nyendo zao, hatua kwa hatua.
...Dada akiwa kaduwaa baada ya kukutwa akivinjali na kaka'ake.
DEMU ALIKUWA AKIZINGUA
Haikufahamika mara moja kama wawili hao walikuwa na makubaliano ya kwenda kuduu katika ufukwe huo au la, lakini kwa mbali ilionekana kama vile dada mtu alikuwa akizingua kwenda kutenda dhambi hiyo.
Picha za video zilizonaswa, zinamuonesha dada huyo akionekana kutoa upinzani pale alipokuwa akishikwashikwa na kaka yake.
Alionekana kama vile hakuwa tayari kwa mchezo huo.
Hata hivyo, kaka mtu anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 23-26 alikuwa akilazimisha kitu fulani ambacho kilionekana dhahiri kupitia kamera zetu.

MAGAZETI YA LEO JUMATANO TAREHE 22.05.2013

DSC 0061 cd132
DSC 0057 39d87
DSC 0059 b2f55

UJIO WA RAIS OBAMA NCHINI TANZANIA KUINEEMESHA SERIKALI...!!

Rais wa Marekani Bw. Baraka Obama na Mkewe wanatarajia kufanya ziara ya nchi tatu barani Afrika itakayojumuisha nchi za Senegal, Afrika ya Kusini na Tanzania, Kuanzia tarehe 26 Juni hadi tarehe 3 Julai. 
 
Katika ziara yake hiyo, Rais atawekea mkazo umuhimu ambao Marekani inauweka katika ushirikiano wetu wa kina na unaoendelea kuimarika na nchi za Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara kupitia mipango mbalimbali ikiwemo ile ya kuimarisha ukuaji wa uchumi, uwekezaji na biashara, uimarishaji wa taasisi za kidemokrasia na uwekezaji katika kizazi kipya cha viongozi wa Kiafrika.
Rais atakutana na viongozi mbalimbali wa kiserikali, sekta binafsi na jumuiya huru ya kiraia ikiwemo vijana ili kujadili ubia wetu wa kimkakati katika ushirikano wetu rasmi na masuala mengine ya kimataifa.
 
Ziara hii itadhihirisha dhamira ya dhati ya Rais ya kupanua na kuimarisha ushirikiano kati ya Marekani na watu wa nchi za Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara katika kuimarisha amani na ustawi katika kanda hii na duniani kote kwa ujumla

Tuesday, May 21, 2013

GODBLESS LEMA AUMBUKA....VODACOM WADAI KWAMBA ULE UJUMBE WA VITISHO HAUKUTOKA KWA MKUU WA MKOA


BARUA  TOKA  VODACOM

KAMANDA wa Polisi wa Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas, amedai kuwa uchunguzi wa awali kuhusu ujumbe unaodaiwa kutumwa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo, umetumwa na mtandao wa simu wa nje ya nchi.
Kamanda alisema katika ujumbe huo ambao Lema anadai uliandikwa na Mkuu wa Mkoa Mulongo na kutumwa kwenye simu yake Aprili mwaka huu, uchunguzi wa polisi umeonyesha kwamba haukutumwa kupitia kampuni moja wapo ya simu za mikononi ya hapa nchini.

BABA YAKE DULLY SYKES ANASWA AKIVUTA BANGI....!!

   Baba mzazi wa mwanamuziki wa bongo flava nchini Dully Sykes, Mzee Sykes pichani kama inavyoonekana akiwa na madawa haram ya kulevya aina ya bangi mkononi huku mbegu mbegu zikiwa zimedondoka chini.-----  

Baba mzazi wa mwanamuziki nyota wa bongo flava nchini Dully Sykes , Mzee Sykes hivi karibuni alinaswa  akichambua bangi mikononi mwake kwa ajili ya kuivuta.

Tukio hilo la aina yake lilitokea  nyumbani kwa msanii aliyefahamika kwa jina la Shebo, na kushuhudiwa na mwandishii wetu ambae alifanikiwa kumpiga picha mzee huyo akiwa na bangi mkononi mwake.

Mzee huyo akiwa hana shaka yoyote alionekana  akichambua bangi hiyo huku mbegu zake zikidondoka chini kama mchele ( picha ya juu)

Hata hivyo mzee huyo alishindwa kuendelea na zoezi la kuitayarisha bangi hiyo kutokana na kumtilia wasi wasi mwandishi akidhani ni afande.

Prof. Jay ajiunga CHADEMA Angalia PICHA


 


Msanii mkongwe wa muziki wa kizazi kipya maarufu kama Bongo Fleva, Joseph Haule (Prof. Jay) amejiunga rasmi leo na chama cha CHADEMA.

KUTOKA JAMII FORUM, SIRI YA KIFO CHA KAMANDA BARLOW ZAVUJA. KAMANDA MUNA ATAJWA.....!!!

Sasa ni wazi kwamba aliyekuwa kamanda wa Jeshi la Polisi mkoa wa Mwanza ameuawa na genge ndani ya Polisi akiwemo Kamanda Polisi anayejulikana kwa jina la Muna, gazeti la Jamhuri limeripoti katika ukurasa wa Mbele kabisa (Nimesoma kwenye website yao Deo Balile akilalamika gazeti kununuliwa kwa jumla na watu wasiojulikana)

Kuvuja kwa siri hiyo kumetokana na mmoja wa jambazi sugu ajulikanaye kwa jina la
Edward Malele kujisalimisha ktk vyombo vya ulinzi na kutoa siri zote.

Jambazi huyu aliombwa wa genge ndani ya polisi kushiriki katika mpango wa kumwua kamanda Barlow. Akakataa kwa kuwa aliwahi kumfahamu kwa karibu kamanda Barlow.

Baada ya kukataa kutekeleza agizo hilo baada ya siku chache alishtakiwa kwa kosa la ujambazi na kuswekwa Rumande.

" MATOKEO YA KIDATO CHA SITA".....SIFURI KIBAO ZAFUTWA KIMYA KIMYA


MPANGILIO wa alama mpya za kufaulu kwa wahitimu wa kidato cha sita waliohitimu mwaka jana, ambao matokeo ya mitihani yao yanaweza kutangazwa wakati wowote kuanzia sasa, unadaiwa kuzua aibu na kama si uamuzi uliotajwa bungeni wa matumizi ya alama za ufaulu za zamani, matokeo hayo yangeibua aibu kama ilivyojitokeza kwa kidato cha nne, 2012.

Kwa mujibu wa vyanzo vyetu vya habari kutoka Baraza la Taifa la Mitihani (NECTA) ambalo linaendelea kupanga matokeo hayo ya kidato cha sita kwa kuzingatia alama za zamani kama ambavyo taarifa ya awali ya Tume iliyoundwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, ilivyosomwa bungeni hivi karibuni, hali ingekuwa mbaya zaidi katika ufaulu kwa wanafunzi wa kidato cha sita kiasi cha kuweza kutishia uhai wa vyuo vikuu nchini kukosa wanafunzi wa kutosha.


“Hali ilikuwa mbaya sana kama alama za kufaulu zingeachwa zitumike zile mpya na si za zamani. Vyuo vikuu nchini visingeweza kupata wanafunzi wa kutosha.


 "Tatizo hapa si uwezo wa wanafunzi moja kwa moja katika kumudu mitihani bali ni kufanywa kwa mabadiliko ya alama bila kuwaandaa.

HII NDIO PRIVATE JET ATAKAYOKUWA AKIITUMIA MAKAMU WA RAISI WA KENYA RUTO


Full size bed ndani ya ndege hiyo
Huu ni mlango wakuingilia kwenye ndege hiyo
Breakfast and diner on board 

BIASHARA YA NGONO YASHAMIRI DODOMA..... MACHANGU WA DAR WAKIMBILIA HUKO



BIASHARA ya ngono katika mji wa Dodoma imeshika kasi kubwa ambapo imebainika kuwa wateja wakubwa ni watumishi wa serikali, wanasiasa na madereva.

Uchunguzi wetu  umebaini kuwa katika biashara hiyo kuna makundi mbalimbali yanayotofautiana kwa malipo ya biashara hiyo.
Wapo wanafunzi wa vyuo vikuu na wanawake ambao wamedai kuwa wanalazimika kufanya biashara hiyo kutokana na kubanwa na maisha, hususani katika marejesho ya mikopo wanaichukua kutoka katika taasisi mbalimbali ya kifedha.

Mmoja wa wafanyabiashara ya ngono (jina tunalo) bila kujua anaongea na nani, alieleza kuwa kwa sasa katika mji wa Dodoma kuna ushindani mkubwa wa biashara ya ngono kwani wanafunzi wa vyuo vikuu vya mjini hapa vimeteka soko hilo.

Alisema kutokana na ushindani huo kwa sasa kima cha chini ni sh 7,000 kwa mchepuo mmoja na sh 30,000 hadi 40,000 kwa kulala.

Mfanyabiashara huyo alieleza kuwa wateja wakubwa wa ngono ni wafanyakazi wa serikali, wanasiasa (wabunge), madereva pamoja na wafanyakazi wa benki.

MAGAZETI YA LEO JUMANNE TAREHE 21.03.2013

DSC 0043 f478a

DSC 0047 b993f

DSC 0045 6ff67

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...