Sunday, May 19, 2013

HII NDIO MOVIE YA AJABU ILIYOFANYWA NA WASANII WA NIGERIA



Bofya hapa kuangalia movie hiyo au hapa

SIMBA NA YANGA ZAINGIZA MILIONI 500

Mwamuzi Martine Saanya wa mechi ya watani wa jadi Yanga na Simba, akiwa chini baada ya kugongana kwa bahati mbaya na mchezaji Kavumbagu wa Yanga wakati wa alipokwenda kuamulia ugomvi.
Na Boniface Wambura, 
IMEWEKWA MEI 19, 2013 SAA 6:20 MCHANA

MECHI ya watani wa jadi Simba na Yanga la Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, iliyochezwa jana (Mei 18 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kumalizika kwa mabingwa wapya Yanga kushinda mabao 2-0 imeingiza sh. 500,390,000.

Mechi hiyo namba 180 ambayo ilikuwa kati ya saba la kuhitimisha ligi hiyo msimu wa 2012/2013 ilishuhudiwa na watazamaji 57,406 waliokata tiketi kwa viingilio vya sh. 5,000, sh. 7,000, sh. 10,000, sh. 15,000, sh. 20,000 na sh. 30,000.

Kila klabu imepata mgawo wa sh. 123,970,927.45 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 76,330,677.97.
Kiingilio cha sh. 5,000 ndicho kilichovutia watazamaji wengi ambapo waliokata tiketi hizo walikuwa 19,039 na kuingiza sh. 95,195,000 wakati kile cha sh. 7,000 kiliingiza watazamaji 17,647 na kupatikana sh. 123,515,000.

Mgawo mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 63,036,064.81, tiketi sh. 3,818,890, gharama za mechi sh. 37,821,638.88, Kamati ya Ligi sh. 37,821,638.88, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 18,910,819.44 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 14,708,415.12.

"WANAOCHOCHEA VURUGU ZA KIDINI NI WATU WALIOTUMWA NA MATAIFA YA NJE"..... RAIS KIKWETE


Rais Jakaya Kikwete amebainisha kuwa vurugu za kidini na kisiasa zinazotokea nchini, zina uhusiano na watu wa nchi za nje.
div style="line-height: 16.796875px; margin: 0px; text-align: center;"> Kikwete alitoa kauli hiyo jana kwenye ibada maalumu ya kuwekwa wakfu kwa Askofu Mkuu wa Sitta wa Kanisa Anglikana Tanzania, Dk Jacob Chimeledya.
Rais Kikwete alikuwa mgeni rasmi kwenye ibada hiyo iliyofanyika kwenye Kanisa Kuu la Roho Mtakatifu.
“Wanaohamasisha vurugu hizo ni watu wenye uhusiano ya karibu na watu wa nje ambao mambo yakiharibika nchini watakuwa wa kwanza kupanda ndege, ilhali wakiendelea kutoa matamko ya uchochezi wakiwa nje ya nchi wakati wengine wakiendelea kuumia,” alisema Kikwete.
Ibada hiyo ilifanyika chini ya ulinzi wa polisi na askari wa usalama, na ilihudhuriwa na Askofu Mkuu wa Anglikana duniani, Justin Welby.
Rais Kikwete alisema amekuwa akichukizwa na vurugu za kidini zinazofanywa na baadhi ya watu wasioitakia mema Tanzania, huku wakijua kuwa amani ikitoweka ni gharama kubwa kuipata.

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI TAREHE 19.05.2013

DSC 0001 147d5
DSC 0004 f935c

JACQUILINE WOLPER ATAJWA KWENYE LIST YA WASANII AMBAO NI FREEMASONS...!!

Inawezekana kila kitu kina wakati wake, kuna muda watu walikuwa wakisikia neno ‘Freemason’ ama ‘Illuminate’ kama inavyojulikana nchini Kenya wengi walikuwa wanaiona ni habari kubwa, lakini kwa sasa hivi inaweza kuchukuliwa kama sio big deal.

Sababu ni ile ile kuwa wengi wanaoendelea kwa haraka ama kuwa juu katika kile wanachokifanya basi utasikia huyo ni member wa Freemason, kwa upande wa Marekani wanasema ‘he/she just sold her/his soul to the devil’.  Japo kwa upande wa Marekani wapo wanaokiri kufanya hivyo kweli, ila kwa Africa Mashariki hakuna msanii aliyewahi kukiri.
Lakini yote hayo ni kama yanakanganya na kuonekana kama hayana mantiki hasa pale ambapo vithibitisho vya kinachoongelewa huwa havileti mantiki ya moja kwa moja. Pengine watu wanatafuta pesa kwa bidii na kumuomba Mungu lakini kwa kuwa kwenye mstari wa juu wanajikuta wanahisiwa kuwa member wa secret society (Freemason). Oh..au labda ndo vile kwa upande mwingine lisemalo lipo na kama halipo laja !
Tunathubutu kuziita blaa blaa kwa upande mwingine, lakini tukiweka kwenye mabano kuwa inaweza kuwa na ukweli, who knows!
Mtandao wa malimwengu wa nchini Kenya huenda ukawa na mfano mzuri wa kile nilichokitaja hapo juu, mtandao huo kupitia mwandishi wake imetaja majina ya wasanii wa Tanzania na Kenya wanaosemekana kuwa ni wafuasi wa Freemason, lakini kizuri zaidi ni kwamba mtandao huo umejaribu kuonesha vithibitisho na kushindwa kupata jibu la moja kwa moja kwa nini wasanii hawa wamekumbwa na hili. Inabaki hivyo hivyo kuwa tetesi tu.
Hawa ni wasanii waliotajwa na maelezo yanayowahusu:
TANZANIA:
1.Naseeb Abdul Jumaa (Diamond Platinum)
Picha aliyopiga mwaka jana akiwa na mzungu anaeaminika kuwa ni moja kati ya viongozi wa Freemason wakiwa wameweka pozi na kuonesha ishara inayooaminika kuwa ni ya Freemason, na kwamba alipoulizwa yeye alisema hakufahamu kama alikuwa anaelekezwa kupiga picha kwa pozi la ki-freemason. Kwa mujibu wa mwandishi anaona inaweza kuwa kweli kwa sababu anaonekana kuenjoy!

HAYA NDIO MAJIBU YA HALIMA MDEE KUHUSU STORY ZA YEYE AKUJIHUSISHA NA MAPENZI YA JINSIA MOJA



Kupitia season mpya ya Clouds Fm, ndani ya so so fresh na fetty, Mh Halima Mdee jana amefunguka juu ya swali aliloulizwa kuhusu story zilizosambaa kuwa anashiriki mapenzi ya jinsia moja.
aah unajua huwezi kuzuia watu kusema, na mimi huwa sihangaiki na watu wanasema nini, lakini ukitaka kumjua Halima unaweza ukamchunguza kirahisi sana, kwa kumuangalia alipotoka, historia yake na mahusiano yake, ambayo mengine ni wazi sana watu walikuwa wanayajua, 
watu wanapenda ku speculate pale ambapo wanaona kitu ambacho hawati kuona, sasa hilo swala lilishaandikwa sana, nadhani walioandika baadae wakaja kuomba radhi kwasababu waligundua wameandika kitu kisicho sahihi, probably kutokana na sauti yangu you know, probably kutokana na tembea yangu, kwasababu mimi nimekulia kwenye familia ya wanaume watupu umeona eeh, mimi nimekuwa ni mpambanaji tokea utotoni, kwasababu nimezungukwa na jeshi la kibabe, thats who iam, lakini mtu anaetaka kumjua Halima na ana uhuru tu, hata akitaka niwatajie list ya watu wangu i can do that, lakini sidhani kama is their damn business, cause ma life is personal, na wakitaka kuchunguza wachunguze kwa mpango wao na watapata taarifa, kwa uhuru tu, na wanaweza wakatoa tangazo kwamba jamani watu waliowahi kuwa na uhusiano na huyu if any wajitokeze, watajitokeza kama wapo upande huo, watajitokeza kwasababu sasa hivi si dunia huru bana

Ufaransa yakubali ndoa ya jinsia moja



Rais wa Ufaransa, Francois Hollande, ametia saini sheria yenye utatanishi, inayohalalisha ndoa kati ya watu wa jinsia moja.
Ufaransa sasa imekuwa nchi ya 14 duniani kuruhusu ndoa kama hizo.
Makundi ya watu wanaofanya mapenzi ya jinsia moja nchini Ufaransa yamefurahi kuwa hatimaye sheria hiyo imepitishwa.
Wanasema kuna marafiki kadha wanaosubiri kufunga ndoa na maelfu ya watoto wanaolelewa na watu wa jinsia moja 
ambao sasa watapata hifadhi kisheria.
Wanaopinga sheria hiyo wamehamaki.
Wanaona kuwa Rais Hollande ameshughulika mno na ndoa kati ya jinsia moja kwa sababu ameshindwa katika maswala muhimu zaidi - kama swala la uchumi wa nchi.
Maandamano mengine ya kupinga ndoa kati ya jinsia moja yanapangwa kufanywa tarehe 26 May. 
Yanaweza kuwa makubwa na ya fujo kama yaliyopita.
Sababu ni upinzani dhidi ya ndoa za jinsia moja umechanganyika na malalamiko mengine ya mrengo wa kulia dhidi ya serikali.
Na hali nchini sasa ni tete.
Lakini kwa kweli vita vimemalizika.
Watu wa jinsia moja sasa wataanza kufunga ndoa nchini Ufaransa.
Baadhi ya wanasiasa wa mrengo wa kulia wataahidi kuwa watabatilisha sheria hiyo wakipata madaraka, lakini historia inaonesha kuwa kufuta mabadiliko kama haya katika jamii ni shida sana.

Saturday, May 18, 2013

SIMBA YACHAPWA MAGOLI 2 KWA 0


_MG_0384Mchezaji wa timu ya Yanga Didier Kavumbagu akikokota mpira mbele ya mchezaji wa timu ya Simba Abdallah Seseme katika mchezo wa ligi kuu ya Vodacom unaofanyika jioni hii kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam , hivi sasi ni kipindi cha pili na Yanga wanaongoza magoli 2 -0 dhidi ya Simba ambayo imekosa penati katika kipindi cha kwanza wakati mchezaji wake Mussa Mude akipiga vibaya mpira huo baada ya Mrisho Ngassa wa Simba kuangushwa kenye eneo la hatari _MG_0386Wachezaji wa timu ya Simba na Yanga wakiwania mpira wakati wa mchezo wao unaofanyika kwenye uwanja wa Taifa jioni hii. _MG_0398Baada ya golikipa wa Simba Juma K. Juma kuteswa hali ilikuwa hivi. _MG_0401Wachezaji wa Yanga wakishangilia baada ya kupata goli la kwanza dhidi ya Simba.

KANYE WEST NI "SHOGA" ANA BWANA PARIS-"MPENZI WAKE KIM KARDASHIAN AFUNGUKA"


Jarida la In Touch limeandika, muigizaji nyota ambaye kwa sasa ni mjamzito Kim Kardashian, anahofia boyfriend wake Kanye West huenda akawa ni shoga na ana boyfriend jijini Paris.
Kwa mujibu wa jarida hilo, Kardashian anapata wasi huo sababu watangazaji wengi wa kwenye mitandao wanamuhisi kwamba boyfriend wake huenda akawa yupo kwenye mahusiano ya kimapenzi na mwanaume ambaye aliwahi kumtengenezea nguo aitwaye Riccardo Tisci.”

Japo yeye anamuita "rafiki" alilieleza kwenye jarida hilo, “Kim alifunguka zaidi na kusema. Kama kweli ikitokea kwamba Kanye yupo na Riccardo kimapenzi, itamumiza sana - zaidi ya nilivyowahi kuumizwa kwenye maisha yake yote.”
Jarida la In Touch limeandika, “Kuna vielelezo ambavyo Kim hawezi kuvipinga,” huku vikiorodheshwa, “Katika kipindi chote ambacho Kim ni mjamzito Kanye amekuwa akitumia muda wake mwingi akiwa karibu na Riccardo kwenye jiji hilo lililopo nchini Ufaransa… Na hivi karibuni Riccardo amenunua nyumba New York umbali wa nusu ya maili toka sehemu ambayo Kanye anaishi.”

DADA WA DIAMOND "ESMA" AZUNGUMZIA JUU YA HARUSI YA DIAMOND NA PENNY


https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhqauc854yv2PrYw-bH3bOCkwEGbb-8ERY5V3dCosbi_ICE5-UpO4U43B3LeqSrSiO4NSVr80ZZySDQv2QX2Vik0kITUUu3Bw8CBMmq31Snt4dIClzxcu912csTxh2z5C9Bx-EzdUQw-I0/s1600/diamond.jpg
Esma Abdul ambae ni dada yake staa wa Tanzania, Diamond Platnums, amesema wamejiandaa vizuri kwa ajili ya harusi ya Diamond ambae anatarajiwa kumuoa mtangazaji wa TV aitwae Penny.

Esma ambae anaishi nyumba moja na kaka yake amesema, "Tumemkubali sana wifi yetu na tunampenda kwa sababu mtu yeyote mimi nitakaetambulishwa siwezi nikamkataa, manake nikimuingilia kwenye mapenzi yake na yeye ataniingilia kwenye mapenzi yangu."
Huu ni mwezi wa tano toka Esma amjue wifi yake ambae ni Penny, anasema nyumbani amekubalika na mipango ya harusi inaandaliwa japo hajui ni lini itafanyika, manake hiyo ni siri kwa sasa. 

Zaidi ya wiki tano zilizopita, Diamond aliongea na kusema ndoa yake imekaribia kufungwa na huyo mkewe mtarajiwa ambae ni mjamzito lakini pia akathibitisha kumnunulia gari la kutembelea aliloliagiza nchini Japan - Hyundai IX 35.

Mpaka sasa Diamond Platnums ambae aliongoza kwa kuwa msanii wa Tanzania alieandikwa sana kwenye internet 2012, ameshaingia kwenye headlines za kuwa mapenzini na mastaa wa kike Tanzania kipindi cha nyuma kama Jokate, Wema Sepetu na wengine. 

KATI YA HAWA MMOJA ATATANGAZWA KWENDA BBA.


Jacqueline Pentzel ‘Jack wa Chuz’, Jacqueline Patrick ‘Jack Patrick’ (pichani) , Wema Sepetu ‘Beautiful Onyinye’ na Baby Joseph Madaha ‘Baby Madaha’  mmoja wapo ataungana na mwanaume kuiwakilisha Bongo kwenye Shindano la Big Brother Africa 2013 linalokwenda na kikolombwezo cha The Chase. 

 
Jack Pentezel
Kwa mujibu wa chanzo chetu (tunaficha jina lake), mastaa hao wa kike, mmoja ndiye ataibuka mshiriki kwa mwaka huu ambapo atakaa ndani ya mjengo kuanzia Mei 26, 2013 ambapo shindano litaanza rasmi. 
 
Jack Patrick
“Mimi nawamegea tu kwamba kati ya Wema, Baby Madaha, Jack wa Chuz na Jack Patrick  mmoja wao anakwenda Big Brother mwaka huu.
 
Wema sepetu
“Halafu ninachojua mimi, mshiriki ameshatumiwa taarifa kutoka Multi Choice, ila tatizo wale jamaa wanataka mtu msiri sana, mshiriki hatakiwi kumwambia mtu mpaka siku atakapoondoka,” kilisema chanzo chetu.
Risasi Jumamosi lilipiga kiguu hadi Ofisi za Multi Choice jijini Dar na kuulizia Mbongo anayekwenda, likakumbana na majibu haya:

Baby Madaha
“Sisi pia hatujui. Unajua ilivyo ni kwamba huwa tunatuma majina, sifa na anuani za watu kama watano kule Sauzi, halafu wao wanaangalia vigezo vyao, anayeshinda anataarifiwa kutoka kulekule bila sisi kujua,” alisema mtumishi mmoja ambaye aliomba jina lake lihifadhiwe.
Risasi Jumamosi juzi Alhamisi liliongea na Jack wa Chuz ambaye alisema aliwahi kuombwa kushiriki shindano hilo kwa sababu ya ushombe wake lakini hakuweka wazi kama alijaza fomu za maombi au la!
Aidha, Baby Madaha alipoulizwa alikiri kujaza fomu za kukusudia kushiriki siku za nyuma akiwa sambamba na Wema lakini akasema hajui nani kashinda ingawa lazima mshiriki ameshapatikana kati yao.
“Nasikia mshiriki anatakiwa kujijua wiki tatu au mbili kabla. Kwa hiyo atakuwa tayari anajijua, inakuwa siri ya mtu, hakuna anayeweza kujitaja kwa watu,” alisema Baby Madaha.
Simu ya Jack Patrick haikuwa hewani siku hiyo huku watu wake wa karibu wakisema yupo nje ya Bongo kibiashara zaidi. Simu ya Wema muda mwingi iliita bila kupokelewa hadi mpigaji akachoka.
Kwa upande wa wanaume, wanaotajwa kushiriki shindano hilo mwaka huu ni staa wa sinema za Bongo, Hemed Suleiman ‘PHD’, nyota wa Bongo Fleva, Khaleed Mohamed ‘TID’ na aliyewahi kuwa Mtangazaji wa Clouds TV, Rommy Jones ambaye ni ndugu na Mbongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’. 

MAMA SHARO... AAMBULIA PATUPU KWENYE AKAUNTI YA MWANAYE.


Maskini! Mama mzazi wa aliyekuwa msanii maarufu wa vichekesho na muziki Bongo, Marehemu Hussein Mkieti ‘Sharo Milionea’, amejikuta katika wakati mgumu baada ya kufunga safari kutoka Tanga hadi Dar kwa ajili ya kushughulikia fedha zilizokuwa kwenye akaunti ya mwanaye na kuambulia patupu.


Akizungumza na Risasi Jumamosi juzi kwa njia ya simu, mama huyo alisema kwa kuwa tayari ameshafungua mirathi, ilibidi aanze kushughulikia suala la benki ambapo alianzia kwenye akaunti za marehemu lakini alipofuatilia hakukuta hata senti tano.

“Namshukuru Mungu kwa yote maana nimerudi Tanga kama nilivyotoka na nauli yangu kwani sikukuta fedha yoyote kwenye akaunti zote za Sharo ila inawezekana alichukua fedha zote kwa ajili ya manunuzi yake kabla ya kifo.
“Huwezi jua kwani alikufa kwa ajali hivyo ni lazima vitu vyake vingi vibaki gizani,” alisema mama Sharo na kuongeza:
“Sioni haja ya kumlaumu mtu zaidi ya kumuachia Mungu ambaye ndiye muweza wa yote, hapa duniani sote tunapita.”
Sharo Milionea alipatwa na umauti Novemba mwaka jana kwa ajali ya gari katika eneo la Songa- Maguzoni wilaya ya Muheza mkoani Tanga wakati akiwa safarini akitokea Dar es Salaam kuelekea nyumbani kwao, Kijiji cha Lusanga, Muheza mkoani Tanga.

NEY WA MITEGO KUITWA BABA SOON, HUYU NDO MAMA KIJACHO WAKE.


So much is happening in the Bongo Flava scene!! TID anataka kuoa, Nurah anatarajia kufunga ndoa June 8 na sasa Nay wa Mitego naye anategemea kuitwa baba, basi raha tupu!!

b89c11b6b7ab11e286be22000a9f139c_7

0bb7758abce711e2935222000a1fb825_7
Kupitia Instagram Nay aka True Boy ambaye hivi karibuni amekuwa dhahabu kwenye show za promotion za makampuni ya simu, amekuwa akishare picha za msichana ambaye kwa mujibu wake ni ‘Mama Kijacho Wake’. “Mic u mama kijacho wanguuuuuuuu…” aliandika hivi karibuni kwenye picha ya msichana huyo.

NISHA AMKIMBIZA WEMA KWA KUMILIKI NYUMBA YA KIFAHARI, HII NDO NYUMBA YA NISHA YENYE THAMANI YA MILIONI 95.

Unakumbuka zile habari za Wema Isaac Sepetu kununuliwa jumba la kifahari na bilionea mmoja Kijitonyama, Dar? Sasa zimegeukia kwa staa wa sinema za Kibongo, Salma Jabu ‘Nisha’ ambaye naye kuna madai mazito ya kuhongwa nyumba.
Ilikuwa mwishoni mwa wiki iliyopita ambapo gazeti hili lilipokea ujumbe mfupi wa simu ya mkononi ‘sms’ kutoka kwa chanzo chake.
HABARI ILIVYOANZA
Chanzo: Hivi ninyi mna habari?
Risasi Jumamosi: Nyingi tu lakini kama una ya kwako itatufaa sana.
Chanzo: Kwa taarifa yenu Nisha kanunuliwa bonge la mjengo hapa Kijitonyama karibu kabisa na Kituo cha Polisi cha Kijitonyama ‘Mabatini’.
Risasi Jumamosi: Nani kamnunulia?
Chanzo: Nasikia ni bilionea mmoja mwenye fedha zake hapa Dar es Salaam, kainunua kisha kamhonga Nisha kwa sababu ni mpenzi wake.
Risasi Jumamosi: Tunashukuru kwa taarifa, kaa mkao wa kula itaruka hewani mara moja baada ya upelelezi wetu.

RISASI LATUA KIJITONYAMA
Baada ya kuzinyaka habari hizo, gazeti hili lilisaga soli hadi maeneo hayo na kuanza kugonga geti moja baada ya lingine hadi lilipofanikiwa kuinasa nyumba hiyo huku Nisha akiwa ndani kapumzika.
Msichana aliyejitambulisha kuwa ni dada wa kazi au hausigeli kwa lugha laini ndiye aliyetoboa siri kuwa ni kweli staa huyo yupo ndani na amehamia mahali hapo muda si mrefu.

NAY WA MITEGO AMTUPIA KIJEMBE CHA NGUVU DIAMOND PLATNUMZ

Katika hali ya Amani kimuziki Msanii Nay wa Mitego amemrushia
vijembe Msanii mwenzake
Diamond Platnumz Jionii ya Leo......''
Niliamua kumwendea hewani Nay wa Mitego Kujua kajianda vipi
kuhusiana na Show ya kesho
Usiku Darlive......Na Mnukuu Nay wa Mitego akifunguka
 baada ya swali aliloulizwa,
Nay''Napenda kumwambia bwana mdogo Diamond kuwa kesho
akae tayari kwa kuwa naenda kuandika
Historia Mpya Darlive,Nataka watanzania wote wajitokeze waje
 kuona navyomkalisha mbana pua
na wavaa nguo za dada zao wanaojidai kwenda sawa na utandawazi......''
Nay alizidi kufunguka kuwa kesho ndo utakuwa mwisho wa
Diamond na kumthibiishia
kuwa Hip Hop ndo muziki unaolipa na wenye maana zaidi......!!

Hayo ndo maneno aliyoyatoa Nay dakika chache zilizopita
alivyopigiwa na Mwandishi wa This Is Diamond
Kuhusiana na Show kubwa kesho Darlive......

Stay Tuned Nitamuenda Hewani The Kid From Kigoma baada ya
kumfikishia ujumbe huu wa Nay...
Je maneno hayo kakubaliana nayo....?
 Stay here kusubiria jibu la Diamond Juu ya ujumbe huu.....!!

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...