Saturday, May 18, 2013

ELIMU YA SHULE ZA MSINGI ITAKUWA NI MIAKA 10 BADALA YA 7...!!

RASIMU ya Sera ya Elimu na Mafunzo nchini inapendekeza kuunganisha elimu ya msingi na sekondari ya kawaida ya sasa ili kuunda elimu-msingi itakayotolewa kwa kipindi cha miaka 10 kuanzia mwaka 2018, imefahamika. 
Rasimu ya kwanza ya Sera hiyo imeshakamilika na sasa wadau mbalimbali wanatoa mapendekezo yao kuiboresha, kabla ya kupelekwa bungeni ili kutungiwa sheria.
Aidha, mikakati hiyo itakayotekelezwa ni kuhuisha muundo na utaratibu mpya wa elimu na mafunzo kwa kuhakikisha kila mtoto mwenye umri wa miaka mitatu na mitano anapitia elimu ya awali kwa kipindi kisichopungua mwaka mmoja kabla ya kujiunga na elimu-msingi.
Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philipo Mulugo alithibitisha kwa gazeti hili wiki hii mjini hapa kuhusu kukamilika kwa rasimu ya kwanza ya Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 2013.
“Ni kweli Sera hiyo imekamilika baada ya kuandaliwa kwa miaka mitatu. Imepita kwa wadau mbalimbali, mashuleni, vyuoni na katika taasisi mbalimbali nchini ambao wametoa maoni yao. “Jumapili (kesho) tunatarajia kuwa waheshimiwa wabunge nao watapata fursa ya kuijadili na kutoa maoni yao katika semina iliyoandaliwa maalumu kwao,” alisema Mulugo katika Viwanja vya Bunge.
Alisema baada ya maoni hao ya wabunge, watapeleka Rasimu hiyo kwa mamlaka husika kwa ajili ya andiko la mwisho kabla ya kupelekwa katika Bunge lijalo ili itungwe sheria kuhusu Sera ya Elimu na Mafunzo.

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI TAREHE 18.05.2013

DSC 0261 1a54f

DSC 0262 5766d

SUGU, PROPESA JAY, ROMA MKATOLIKI WAPIGIWA DEBE KUALIKWA KATIKA SHOW YA LADY JAYDEE KUFUATI, BAADA YA MATONYA NA WENGINE KUMTOSA.


 Joseph Mbilinyi aka "Sugu"
 Joseph Haule aka Proffessor Jay"
 R.O.M.A Mkatoliki

 Lady Jay Dee mwenyewe
 K na D wa Maujanja Saplayaz (Kulwa na Dotto)
WAKATI wapenzi wa muziki wa kizazi kipya nchini wakisubiri kwa hamu kubwa show kali ya Mwanadada Judith Wambura "Lady Jay Dee" ya kuadhimisha kutimiza miaka 13 katika game ya Muziki huo na kutokana na hali ambayo imeendelea kwa baadhi yawasanii mbalimbali waliokuwa wametajwa kushirikiana naye katika show hiyo kujiengua na kutoa sababu kadhaa za kutoshiriki katika Show hiyo (TID, Linah, Barnaba na Matonya)

DIAMOND ATOA SABABU ZA YEYE KUWA KICHECHE......!!!

 KWA mara ya kwanza nyota wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul 'Diamond' ameacha gumzo London, Uingereza baada ya kueleza sababu za kwa nini ni kiwembe?
Akifunguka katika mahojiano maalum wiki iliyopita na Kipindi cha Sporah Show cha runingani alipokuwa kwenye ziara ya kimuziki nchini humo, Diamond alizungumza ishu kibao za kimapenzi hasa juu ya msururu wa wanawake ambao tayari ametoka nao.
ASISITIZA ANASUBIRI MTOTO

Kabla ya yote, staa huyo alisisitiza kuwa muda si mrefu anatarajia kupata mtoto kutoka kwa mpenzi wake wa sasa, Peniel Mungilwa ‘Penny’ akimaanisha kuwa ni mjamzito, kinyume na msichana huyo ambaye hivi karibuni alimshangaa Diamond kueneza habari hizo.
KWA NINI ANAPENDA KUBADILISHA WANAWAKE?

Diamond: Mimi ni binadamu kama binadamu wengine wa kawaida. Nampenda mwanamke anayenipenda na kuniheshimu. Ikitokea mikwaruzano huwa mimi nakaa pembeni, natafuta sehemu nyingine. Wakati mwingine mimi ndiye huwa naachwa.
KWA NINI MSURURU NDANI YA KIPINDI CHA MIAKA MITATU?

Diamond: Nikiwa na mtu nikiachana naye naonekana nina matatizo kwa sababu wakati mwingine nakuwa na wanawake wenye majina. Siwezi kukaa bila uhusiano na nakuwa wazi kwa sababu lazima itajulikana tu na kuandikwa kwenye magazeti. Kuna kipindi nilikaa miezi sita bila kufanya kitu chochote (mh!). Lakini nikianza (uhusiano), nikihama naonekana msumbufu.

UWT MBEYA WAMJIA JUU MCHUMBA WA DKT SLAA.


Dkt Slaa akiwa na mchumba  wake Bi Bi.Josephine Mushumbusi Kushoto
Na Esther Macha, Mbeya
UMOJA wa wanawake  wa chama cha Mapinduzi Mkoani Mbeya(UWT) umemshukia Bi.Josephine Mushumbusi ambaye ni mchumba Katibu Mkuu wa chama cha
Demokrasia na maendeleo CHADEMA kufuatia kauli za udhalilishaji dhidiya Mke wa Rais Mama Salma Kikwete.
Hatua hiyo inatokana  na kauli za kiudhalilishaji zilizotolewa
mwishoni mwa wiki na mchumba huyo wa Katibu Mkuu wa Chadema kuwa mama Kikwete ameshindwa kumshauri   Rais ambaye ni mume wake  kuiongoza nchi vizuri .
Kauli hiyo imetolewa jana na Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Mkoa wa Mbeya Bi.Priscilla Mbwaga wakati  akitoa Tamko   kwa waandishi wa habari juu ya Matusi ya wazi yaliyotolewa na Bi.Mushumbusi   kwa Mke wa Rais katika mikutano ya hadhara iliyofanyika Wilayani Mbozi Kata ya
Vwawa Mkoani hapa.

Friday, May 17, 2013

WANAFUNZI WA CBE, VETA, UDSM WAJIUZA......!!!

Wanafunzi wa kike wa chuo kikuu cha Dar es salaam [UDSM],Chuo cha elimu ya biashara [CBE]na chuo cha mamlaka ya Elimu na ufundi  stadi [VETA],Dar es salaam ,wamefikishwa katika mahakama ya jiji samora wakidaiwa kufanya biashara ya kuuza mili yao.

Washitakiwa hao waliokamatwa  katika eneo la kona Baa Ambiance Sinza wilayani kinondoni ambao ni miongoni mwa wanawake 35 wanaodaiwa kufanya biashara hiyo na wote walifikishwa mahakamani hapo.

Kesi hiyo ilikuwa chini ya hakimu Willian Mtaki ambapo muendesha mashitaka,bwana John Kijumbe,alisema wasichana hao walikamatwa katika mazingira tofautitofauti.

Wanafunzi hao ni Yasinta Kilimo mwenye miaka 21 CBE mkazi wa upanga,Morin Masatu miaka 19 UDSM,mkazi wa kinondoni na mwanafunzi wa VETA aliyefahamika kwa jina moja la Khadija.

“Nilikwenda pale baa kuchukua simu yangu ambayo ilipotea hivyo waliniita nikaichukue ndipo askari wa jiji wakanikamata,”Alisema Khadija akijitetea.

Kwa mujibu wa bw. Kijumbe washitakiwa  hao wamekosa dhamana baada ya kushindwa kutimiza masharti ya kila mmoja kuwa na wadhamini wawili au kulipa faini ya kulipa sh. 200,000.

POLISI YAWATIA MBARONI KANGAMOKO ..... RIPOTI KAMILI HII HAPA

JESHI la Polisi Mkoa wa Kinondoni, linalishikilia baadhi ya wanenguaji wa kundi maarufu kwa kucheza maungo yakiwa wazi ‘Kanga Moko na Laki si Pesa’, gazeti la Tanzania Daima la leo lina hatimiliki ya hii habari.
Watuhumiwa hao wamekamatwa sambamba na watu wengi wanaofanya biashara ya kuuza miili yao, kufanya mapenzi hadharani na vitendo vya kishoga.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kinondoni, Charles Kenyela, alisema kuwa kundi hilo sambamba na watu hao walikamatwa katika maeneo ya Hoteli ya Travertine, Ambiance Club, Kinondoni Makaburini, Coco Beach na Barabara ya Tunisia.“Tumewakamata hao wanaofanya mchezo maarufu wa Kangamoko na Laki si Pesa na tayari wanafikishwa mahakamani muda wowote na msako bado unaendelea ili kudhibiti vitendo hivyo na michezo hiyo ya kangamoko au baikoko ambayo watu wengi wameilalamikia kutokana na mtindo wanaoutumia,” alisema.
Kundi la kangamoko limekuwa likilalamikiwa mara kwa mara kutokana na kucheza wakionesha maungo ya miili yao wazi na kuvaa nguo nyepesi wanazozimwagia maji.
Kukamatwa wasanii wa kundi hilo kumekuja siku chache tu tangu walalamikiwe katika Bunge la Jamhuri ya Muungano kwamba wamekuwa wakipotosha jamnii.

UN YAWASHAURI WATU KULA WADUDU



Umoja wa Mataifa (UN) umeshauri kula wadudu wengi ili kukabiliana na janga la njaa. Kwa mujibu wa ripoti ya Shirika la Chakula na Kilimo la UN, kula wadudu wengi kunasaidia kuongeza virutubisho mwilini na pia kupunguza uharibifu wa mazingira.

Tayari watu zaidi ya bilioni mbili duniani wanakula wadudu kama sehemu ya mlo wao. Hata hivyo, UN imekubali kuwa bado kuna watu wengi hasa kutoka nchi zilizoendelea ambao wanaona kinyaa kula wadudu.

UN imesema kuwa kwa sasa wadudu kama manyigu na kombamwiko wanatumika kwa uchache sana kama sehemu ya mlo. Ripoti hiyo imesema kuwa wadudu wapo kila sehemu na wanazaliana kwa wingi sana lakini hawatumiki kama chakula.

Waandishi wa ripoti hiyo wanadai kuwa wadudu wana virutubisho, hasa protini, mafuta na madini. Wanadai wadudu ni muhimu sana kama chakula hasa kwa watoto ambao hawapati lishe ya kutosha.

Ripoti hiyo imeshauri kuwa sekta ya chakula inaweza kusaidia kwenye kampeni ya kula wadudu kwa kujumuisha recipes mpya za wadudu katika vyakula vyao na kuongeza wadudu kama menu kwenye mahoteli. 

Uko tayari kula wadudu kama kombamwiko (mdudu wa jamii ya memde) kama sehemu ya mlo wako?

CD ZA UAMSHO NA ZILE ZA SHEIKH ILUNGA ZAPIGWA MARUFUKU....!!



Serikali ya Umoja wa Kitaifa ya Zanzibar inayoongozwa na Dr Shein na Makamu  wake Maalim Seif kupitia Jeshi la Polisi wamepiga marufuku rasmi CD  zote za mawaidha ya Kiislam za UAMSHO,MUJAHID ABOUD ROGO na SHEIKH ILUNGA.
 

Agizo hilo lilitolewa na OCD  wa  zamani Murtad MKADAM ambae kwa  sasa yupo ofisi kuu ya polisi kitengo cha madawa ya kulevya Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Maalim Seif. 

Alisema cd hizo za kiislam ni chanzo cha uvunifu wa amani hapa nchini na ndio zinazosababisha uchochezi baina ya dini ya ukiristo na uislam.
 

OCD alibainisha kuwa mpaka sasa wameshawakamata watu kadhaa wanaojihusisha  na  kuuza cd hizo na kuwaonya wale wote ambao huweka kuzisikiliza maana watachukuliwa hatua kwani serikali ina mkono mrefu.
 ...

Akijibu baadhi ya maswali aliyoulizwa kwamba waliowakamata hawawaoni kuwa wamewadhulumu kwa kufanya biashara halali ya uzaji cd, Ocd alijibu cd zile za mawaidha ni Haram wala sio riziki ya halali kwa upande wa serekali kwani zinapelekea uvunjifu wa Amani katika nchi.

TUHUMA: MAWAZIRI KUUZA DAWA ZA KULEVYA

Mbunge wa Mwibara (CCM), Kangi Lugola
  Mbunge sasa 'asakwa' kiana
  Pinda akwepa, awasafisha
Serikali imembana Mbunge wa Mwibara (CCM), Kangi Lugola, kwa kumtaka awasilishe ushahidi kuthibitisha kuwa baadhi ya mawaziri wanajihusisha na biashara ya dawa za kulevya.

Hatua hiyo imechukuliwa baada ya mbunge mmoja kuitaka serikali itoe kauli kutokana na madai kwamba mawaziri wake wanajihusisha na biashara hiyo haramu.

Mbunge wa Tumbe (CUF), Rashid Ally Abdallah, alitaka kauli ya serikali jana alipouliza swali la papo kwa papo kwa Waziri Mkuu.

Akijibu swali hilo, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, alisema kuwa mbunge aliyetoa tuhuma hizo apeleke ushahidi, ili upelekwe kwa Rais.

Katika swali lake Abdallah, alisema kuwa Lugola alitoa kauli akisema wapo baadhi ya mawaziri wanaojishughulisha na biashara haramu ya dawa za kulevya, licha ya wabunge hao kulindwa na ibara ya 100 ya katiba.

HUU NDIO WARAKA WA MASHITAKA YANAYO MKABILI MSANII LADY JAYDEE MASHTAKA YALIYOFUNGULIWA NA JOSEHP KUSAGA NA RUGE MTAHABA


Mwanamuziki Judith Wambura, amepigwa stop na Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Kinondoni kuongelea lolote kuhusiana na ugomvi wake na viongozi wa Clouds Media Group, nje ya mahakama mpaka hapo kesi yake ya msingi dhidi ya viongozi hao ambao ni wadau wa burudani itakapomalizika.

Katika status yake aliyoiandika muda mfupi tu kupitia ukurasa wake wa Facebook, Lady Jaydee ambaye siku za karibuni amekuwa maarufu kwa jina la Anaconda amesema:

"Nadhani baada ya hii, maswali yatapungua kama sio kuisha kabisa...Nafahamu kila mtu anasoma kwa wakati wake pengine hamkuona sababu nilizoelezea kwanini sijatoa waraka mwingine Tar 15 kama nilivyo ahidi.

Sababu ni kuwa mahakama imesema nisizungumzie hilo swala kwasasa, ambapo kesi bado iko mahakamani...Mpaka nitakapopewa ruhusa ya kuzungumza au kutozungumza tena".
-
Mdimuz

MOVIE ALIYOFANYA MAMA KANUMBA KUTOKA KESHO MITAANI, HAWA NDO WAHUSIKA WAKUU

fffffffffffffffffffffffffffffff
Movie titled “Without Daddy” ambayo imepata kick kutokana na Mama Kanumba kuwa ndani yake, kesho itakuwa mitaani. Watu wengi wana hamu kubwa ya kuona jinsi gani mama Kanumba anauwezo kiasi gani kwenye ishu za kuigiza. Basi usikose kuikamata copy yako kesho na uangalie jinsi gani mama Kanumba kafanya mambo humu ndani. Kweli alimpa kipaji mwanae au ni vingine?

HUU NDIO WARAKA WA 'ANTIVIRUS' KWENDA KWA RUGE NA KUSAGA!! USOME HAPA

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg5XHEZ5q85-oyxw_UcRunmglJKxUKAuUy-5b4mEa-6uNsPv06vU8iPGScZjMT2LvGytaQjZa33m5EEesulepmqHh2kcbWXXTtQc9hLq1KCfyiG4wBvq7hmj9A4A9AyS_vrJbtnwvM8u2k2/s1600/Anti+virus.jpgANTiVIRUS DAWA YA Virus WA Hiphop in Tanzania

WARAKA NAMBA 1(ZIPO 88) KILA WIKI UTAPATA WARAKA MMOJA

Ni wazi na dhahiri kabisa kesi iliofunguliwa mahakamani dhidi ya Lady JayDee haina maana yoyote isipokuwa ni hofu ya mafisadi wa muziki nchini (Kusaga na Ruge) kwa kuwa waraka wa pili ulikuwa utoke tar 15 may na mwingine tar 17 may mwaka huu wa 2013.

Hapa la kujiuliza ni juu ya interview ya Rugen a kinachoendelea sasa,eti suala limefika mahakamani,kweli Kusaga na Ruge mmeweza kuthibitisha nyie ni mafisadi na mnamuaibisha Rais Kikwete ambaye nina uhakika anajua kuwa nyie ndio kikwazo kikubwa na hata Bungeni alishawahi kuzungumza kuwa alitoa studio na pango kumbe tatizo sio hilo,tujiulize wote kuna nini wanachoficha hadi kumtafutia kesi raia mwema asie na hatia?

Tena anaejitafutia rizki ambayo wao wanapigana nayo kwa kumkandamiza?
Huku wakitumia mabavu wakilindwa na baadhi ya viongozi wa serikali na waandishi ambao majina yao mtayapata kupitia nyaraka zinazokuja (zipo 88) na huu ndio wa kwanza.
Nimesikitika sana na njia pekee ya kuufahamisha umma juu ya ufisadi huu wa Ruge Mutahaba na Joseph Kusaga ni kuyaanika yote ambayo jamii na Viongozi wa Serikali kama mlikuwa hamjui sasa ndio wakati muafaka wa kuwajua watu hawa ambao kila kukicha ni kuimarisha ufisadi wao na kujipendekeza kwa Viongozi sambamba na watoto wao (mtajua mpaka majina yao)

Tukio la bomu latua UN


Tukio la kutupwa bomu katika Kanisa Katoliki la Joseph Mfanyakazi, Arusha limetua katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa (UN) baada ya kuwasilishwa na Balozi wa Vatican UN, Askofu Mkuu Frances Chullikatt.
Askofu Chullikatt anakuwa kiongozi wa kwanza wa Vatican kutoa tamko kuhusiana na shambulizi hilo ambalo mmoja wa viongozi wake alikuwapo.
Bomu hilo lilirushwa katika kanisa hilo wakati likizinduliwa na Balozi wa Vatican nchini, Askofu Mkuu Francisco Padilla Mei 5, mwaka huu na kusababisha vifo vya watu watatu na
kujeruhi zaidi ya 50.

Wakati wa shambulizi hilo, Askofu Padilla na Askofu Mkuu wa Jimbo la Arusha, Josephat Lebulu walionusurika.

LINAH, BARNABA KUTUPIWA VILAGO THT?

Msanii Linah 
Barnaba
Na  Andrew Chale
KUELEKEA shoo maalumu ya Miaka 13, ya mwanamuziki nguli wa bongo fleva nchini na kiongozi wa bendi yenye msisimko mkubwa ya ‘Machozi Band’, Judith Wambura ‘Lady Jay Dee’ au Jide’  huenda kwa upande wa wasanii wa Nyumba ya Vipaji ya THT, Linah Sanga na Barnaba  mwaka huu ukawa mchungu kwao kufuatia kuwepo taarifa za kutimuliwa na uongozi wa juu. 
Kwa mujibu wa vyanzo kutoka kwa mtu wa karibu wa Linah kilieleza kuwa mpaka sasa msanii huyo hana raha na wala hajui ataanza vipi katika harakati zake za kimuziki hasa kufuatia hivi karibuni kukacha shoo ya nguli Lady Jay Dee kwa shinikizo kutoka kwa wakubwa zake. 
Hata hivyo, Linah inadaiwa uongozi wa juu umekaa kikao na hatua iliyofuatia kwenye kikao hicho ni kuwaondoa kabisa kwani huenda wakatia doa wasanii wenzao ndani ya kundi hilo.
“Juzi Lina,haikuwa kawaida yake maana hata alipopigiwa simu na ** kwa ajili ya hatua zingine alionekana kuw na hofu, na wala hakutaka kusikia ushauri wangu ambao nilikuwa nikimhusia kuwa aachane na mawazo hayo kwani jambo analoliwaza huenda likaisha na hata maamuzi yatakayotoka yatakuwa ni kawaida” kilieleza chanzo kutoka kwa mtu wakaribu wa Lina, amabaye hata hivyo alisema kuwa huenda ukweli wa jambo ukawa hadharani.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...