Sunday, May 05, 2013

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI MAY 5, 2013

.

.
.

LINA NA BARNABA WAIKACHA SHOW YA MIAKA 13 YA LADY JAY DEE.

Linah na Barnaba wameiambia Bongo5 kuwa hawatakuwepo kwenye show ya miaka 13 ya muziki ya Lady Jaydee itakayofanyika May 31, kwa kile walichodai ni kutoafikiana kwenye malipo.
 
Wamesema licha ya kuendelea kuwepo kwa majina yao kwenye poster ya show hiyo, hawatotumbuiza siku hiyo.
“Dada yetu alituita, akatuambia kwamba ana kazi yake ya kutumiza miaka 13 kwahiyo akawa anasema anahitaji wasanii ambao watamsupport kwaajili ya kufanya show,” amesema Linah. “Sisi tulifuata protocol zote kwasababu kama wasanii tuna viongozi, tukafuata protocol zote kuweza kukubaliana naye mpaka tukafikia hatua kwenye masuala ya biashara, yaani malipo. Kwenye upande huo kidogo tukawa tumepishana, kwenye upande wa masuala ya maslahi. Lakini sasa tunashangaa yeye kuanza kuweka posters.”
Kwa upande wake Barnaba amesema hawajashindwana na Lady Jaydee lakini wao kama wasanii wana menejementi na matakwa ya ofisi zao na hivyo muafaka ulishindwa kufikiwa na pia walikuwa na booking zingine.
Hata hivyo Barnaba amesema hakuna ugomvi wowote baina yao na Lady Jaydee. “Tuko safi tu na dada, mbona tuliafikiana vizuri tu na tuko kwenye maongezi mazuri tu, tulishaongea na hili suala liko vizuri,” amesema Barnaba.
source-zeddylicious

PENZI LA WEMA LAMTESA PREZZO..........!!!


Wema akiwa kwenye pozi la kimahaba na msanii wa Kenya PrezoDar es Salaam, Tanzania

BAADA ya uvumi kwamba msanii wa muziki wa kizazi kipya wa Kenya Prezo kuzama kwenye mahaba mazito na msanii wa filamu nchini Tanzania Wema Sepetu, Msanii huyo ameshikwa na kigugumizi na kushindwa kukanusha tuhuma hizo.


Prezo ambaye alifiwa na mchumba wake ambaye pia alikuwa msanii wa muziki wa kizazi kipya nchini Nigeria marehemu Goldie Harvey, aliyefariki dunia February mwaka huu, juzi alishindwa kudhibitisha tuhuma hizo baada ya kuulizwa swali na kushindwa kulijibu.


Prezo ambaye yuko nchini kwa ziara ya muziki alionekana katika picha za mahaba akiwa na Wema Sepetu, hata hivyo Wema aliwahi kukanusha picha hizo na kudai kwamba walipiga wakati walipokuwa wakirekodi filamu mpya ya Wema na kwamba hana mahusiano yoyote ya mapenzi na msanii huyo.

Akiwa katika mahojiano maalum kwenye kipindi cha mapenzi kilichorushwa usiku na Redio Clouds FM Prezo alishikwa na kwi kwi cha gafla baada ya kutakiwa kudhibitisha juu ya uvumi kwamba amenasa kwenye mahaba mazito na mrembo huyo mwenye skendo za kubadilisha wanaume kila kukicha.

MWANAUME AKIKOSA MTOTO HUPATA HUZUNI ZAIDI KULIKO MWANAMKE


Tofauti na mazoea na mtazamo wa wengi kwamba mwanamke ndiye anayeumia zaidi akikosa mtoto, wataalamu wamegundua kuwa anayeumia zaidi kwa kukosa mtoto ni mwanamume.
Utafiti huo umeonyesha kuwa wanaume wanahitaji mtoto sawa sawa na wanavyohitaji wanawake, lakini wao wanaumia zaidi wanapokosa bahati ya kupata mtoto.
Wataalamu hao wamebaini kuwa sababu kubwa zinazowafanya wanaume wajisikie vibaya zaidi wanapokosa watoto ni tamaduni za toka enzi kuwa wao wanaweza kila kitu na msukumo wa familia.
Tofauti na wanawake, ambao wanahitaji mtoto kwa ajili yao binafsi kwa asili ya kuumbwa kwao, hali ambayo kitaalamu inajulikana kama ‘biological urge’.
Taarifa za utafiti huo ulioongozwa na Robin Hadley, wa Chuo Kikuu cha  Keele, ukishirikisha wanaume 27 na wanawake 81, ambao hawajapata mtoto, uliwasilishwa mbele ya Wanasaikolojia wa Taasisi ya British Sociological Association,  ya Uingereza.

Saturday, May 04, 2013

SAKATA LA PADRI ALIYENASWA NA MKE WA MTU..... MAPYA YAIBUKA BAADA YA MUME KULIPONDA KANISA KATOLIKI....!!


 

LILE saga la madai ya fumanizi la Padri Urbanus Ngowi aliyekuwa akihudumu katika Parokia ya Korongoni, Moshi Vijijini kabla ya kuhamishiwa Makomu, Marangu limeibua mtikisiko mkubwa kwa Kanisa Katoliki nchini, .
KWANI ILIKUWAJE?
Katika habari iliyofichuliwa , Aprili 29 hadi Mei 5, mwaka huu, ilidaiwa kuwa Father Ngowi alinaswa chumbani akiwa na mke wa mtu aliyetajwa kwa jina la kijamii la Mama P.

 
Mara baada ya ‘mzigo’ huo kuingia mitaani nchi nzima, mhariri wa gazeti hilo (jina linahifadhiwa) alianza kupokea simu na ujumbe mfupi wa maneno (SMS) kutoka kona mbalimbali kwa watu waliojitambulisha kuwa ni waumini wa kanisa hilo wakidai kushtushwa na tukio hilo.

VIKAO VIZITO
Habari za ndani kutoka Kanisa Katoliki Jimbo la Moshi zilieleza kuwa baada ya ishu kuwa ‘hoti’, viongozi wa jimboni hapo, Jumatatu iliyopita walikaa vikao vizito kulijadili suala hilo na kulitolea uamuzi.
Ilidaiwa kuwa uongozi ulikubaliana kumwita mume wa Mama P ambaye wakati tukio hilo likitokea alikuwa jijini Dar es Salaam kwa shughuli zake binafsi.
Ilisemekana kuwa waliwasiliana na mwanaume huyo ambaye alitakiwa kuondoka Dar, Alhamisi iliyopita kwenda Moshi kukutana na viongozi hao kwa lengo la kuweka mambo sawa.
Ilidaiwa kuwa jamaa huyo ambaye amezaa na Mama P watoto wawili, alikubali kukutana na viongozi hao kwa shingo upande huku akitishia kulipeleka suala hilo mbele zaidi kwa kuwa alishalalamika muda mrefu kwamba Father Ngowi ana ukaribu wenye maswali mengi na mkewe.Tulitonywa kuwa baada ya mwenye mke huyo kulalama sana, Father Ngowi aliitwa na uongozi wa jimbo hilo kisha akaonywa lakini hakuna kilichobadilika.

PENNY...... "SINA MIMBA YA DIAMOND, NAMSHANGA ANAVYOTANGAZA KWA WATU"

HIVI karibuni, staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ aliripotiwa akisema demu wake ambaye ni ‘prizenta’ wa Runinga ya DTV, Peniel Mungilwa ‘Penny’ ana ujauzito wake na kwamba amemnunulia ‘mkoko’ (gari) la mamilioni ya shilingi kwa ajili ya kwenda nalo kliniki, Penny ameifungukia kauli hiyo.
Akizungumza na mapaparazi wetu kwa njia ya simu jijini Dar juzikati, mrembo huyo alionesha hali ya kupaniki huku aking’aka na kushangazwa na habari hizo za ujauzito.
 
 Alisema amekuwa akisoma habari za ‘mimba’ yake kupitia magazeti lakini hajaulizwa na mwandishi yeyote, jambo linalomshangaza sana.
Alipoambiwa kwamba aliyesema habari kwamba yeye ana mimba ni Diamond, Penny alisema: Namshangaa! Ni mimba ipi kwanza?
Alikwenda mbele zaidi kwa kusema mbali na madai ya mimba, lakini pia uhusiano wake na msanii huyo unamnyima raha kutokana na maneno ya watu.
Baada ya waandishi kujitambulisha, mahojiano yalikuwa hivi:

Funguka: Vipi, ujauzito unaendeleaje? Ni kweli una mimba ya Diamond au umeshaitoa?
Penny: Mh! Yaani sijui hata niseme nini, nashangazwa sana na hizi habari, nazisikia tu halafu mimi mwenyewe mhusika sijapewa nafasi ya kuzungumza.
Unajua sijazoea maisha haya ya kila wakati kuzungumza na waandishi. Naomba mniache, nani aliwaambia kuwa mimi nina mimba?
Funguka: Diamond.
Penny: Kama ni Diamond muulizeni yeye mwenyewe! Mbona nakosa raha jamani?
Funguka: Vipi mna mpango wa kuoana na Diamond?
Penny: (kwa hasira) Hizo ni ishu zangu binafsi, kama tutaoana au hatuoani ni mipango yetu, sioni sababu ya kutangaza kwenye media.
Funguka: Unaichukuliaje kauli ya mama mkwe wako, yaani mama Diamond? Inadaiwa alisema hatambui uhusiano wowote wa mtoto wake na mwanamke mwingine hadi atakapofunga ndoa.
Penny: Tafadhali sana, sitaki kuzungumzia habari kuhusu mama Diamond. Kwa hilo ‘no comment.’
Funguka: Vipi lakini, unainjoi kuwa na uhusiano na Diamond?
Penny: (Akakata simu).
Funguka: Haloo… haloo!
Hata hivyo mapaparazi wetu walipojaribu kumpigia simu tena hakupokea licha ya kuita kwa muda mrefu mpaka kukatika yenyewe.

Ruge Mutahaba kumjibu Lady Jay Dee Jumatatu


Kwenye kipindi cha Power Breakfast kitakacho rushwa siku ya jumatatu saa mbili asubuhi Ruge Ataongelea issue ya Jay Dee ,Lady Jay Dee ameingia kwenye vita kali na Clouds Fm huku akimshambulia Joseph Kusaga na Ruge Mutahaba kwa madai kuwa ndio wanaokula jasho la wasanii.

MAGAZETI YA MAY 4 2013 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.

.

WABUNGE:: SERIKALI SASA IWANG'OE VIONGOZI NECTA


Baadhi ya wabunge na wadau wa elimu wametaka Serikali kutoishia kufuta matokeo ya mtihani wa kidato cha nne, bali iwajibishe Baraza la Mtihani Tanzania (Necta) kwa kufelisha wanafunzi.

 
Akizungumza kuhusu kauli ya Serikali kufuta matokeo hayo jana, Mbunge wa Bukoba Vijijini, Jason Rweikiza alisema taarifa ya tume ingekuwa tofauti na ilivyotolewa ilikuwa isababishe vurugu nchini.

“Kauli hii ya Serikali ndiyo iliyotegemewa na wadau wa elimu, tume wangefanya vinginevyo tunge-riot (fanya vurugu), kwa sababu matokeo yaliyotolewa na Necta siyohalisi. Tume imefanya kazi nzuri na kilio cha wanafunzi kimesikika,” alisema Rweikiza na kuongeza:

“Sasa na hili nalisema bila kificho, Necta lazima wawajibishwe kwa sababu wanafunzi wanne wamejiua kwa matokeo hayo yasiyo halali, kule kwangu (Bukoba Vijijini) wanafunzi wamekata tamaa na wanaolewa. Hiyo yote ni hasara ambayo haina wa kuilipa.”

Aliongeza kuwa nchi nyingi duniani ikiwamo Marekani, mtihani wa mwisho hauchukuliwi kama kigezo kwa sababu inategemea mwanafunzi jinsi alivyoamka siku ya mtihani na kwamba, wanatumia mitihani iliyopita kufanya tathmini yao.

IZZO B......... "SINA MAHUSIANO NA WEMA WEMA SEPETU"

Siku chache baada ya kukwenda Arusha kwa mapumziko mafupi kutokana na kudhalilishwa na mpenzi wake wa dhamani Diamond kupitia redio...Beutifully onyinye wa Bongo, sasa hausishwa kutoka kimapenzi na msanii wa hip hop Izzo bizness..
  izzo bizness kupitia xxl ya clous fm chini ya u-heard ya alhamisi ya wiki hii alikanusha kabisa kuwa na mahusiano ya mrembo wema na kuthibitisha kuwa wao ni washikaji na wanakutana mara mojamoja ingawa wenyewe wamezoea kuitana 'darling' kwa mazoea..
KuSikiliza  kauli ya izzo bizness bfya hapo chini !!

GADNER....... "KAMA ASINGEKUWEPO LADY JAYDEE BASI NINGEKUWA NA VANESSA MDEE"

MUME wa Legend wa Bongo Fleva, Judith Wambura ‘Lady Jadee’, Gardner G Habash ‘Kapteini’ aliwaacha watu midomo wazi baada ya kusema kama angekuwa hajaoa, basi angemuoa msanii anayekuja kwa kasi kwenye gemu, Vanessa Mdee.
Kapteini alitamka hayo juzi katika kinyang’anyiro cha kumtafuta Redds Miss Dar Indian Ocean 2013 kilichochukua nafasi katika Ukumbi wa Makumbusho ya Taifa, Posta jijini Dar ambapo mume huyo wa Lady Jaydee alikuwa MC wa shughuli hiyo hivyo kutumia kipaza sauti kumnadi Vanesa.
Gardner G Habash ‘Kapteini’.
“Kiukweli Vanesa ni msanii mzuri, ana uwezo mkubwa wa kufanya muziki wa Hip Hop na kulitawala jukwaa. Ningekuwa sijaoa kwa kweli ningemuoa Vanesa Mdee,” alisema Gardner.
Mbali na Vanesa, wasanii wengine wanaounda familia ya B Heatz walipata nafasi ya kutumbuiza katika hafla hiyo akiwemo mkongwe, Ally Baucha

Friday, May 03, 2013

AGNES MASOGANGE HAISHI KUPIGA PICHA ZA KIMITEGO

SHILOLE......... "BILA CONDOM HUWEZI KULIFAIDI PENZI LANGU HATA UKINIHONGA MABILIONI"

Mwigizaji na mwanamuziki wa muziki wa kizazi kipya Zena Mohamed, maarufu kwa  jina  la   shilole amedai kuwa anaweza kufanya ujinga wowote humu duniani lakini linapokuja suala la mapenzi kamwe hawezi kwenda pekupeku ( bila  condom )  ....

Akiongea kwa  kujiamini ,Shilole  alisema kuwa hata mtu awe vipi, au awe wa dini gani au awe na pesa kiasi gani kamwe hawezi kumvulia nguo kama  hana  kondom  mkononi.....
Msanii  huyo  alienda  mbali  zaidi  na  kuzilaani   kauli   za  baadhi  ya  watu zinazosema eti ukitumia "CONDOM"  ladha ya mapenzi inapungua.Yeye  anadai  kuwa  ni  mdau  wa  "GEMU"  hilo  na  huwa  anatumia  NDOM  kama  kawa  na  hufurahia  kama  kawaida...

" Hata niwe nimelewa kiasi gani huwa nipo makini sana maana najua vijana wengi wa mjini wananimezea  mate....Waje  tu , lakini  bila  KINGA wataambulia  PATUPU!!” Alisisitiza Shilole

WOLPER "NAJUTA KUJIINGIZA KWENYE MAPENZI"...!!

DIVA wa kiwango cha juu cha filamu hapa Bongo, Jacqueline Wolper, ameonekana kujutia historia yake ya kimapenzi baada ya kufungukia kitendo cha yeye kumuanika kila aliyekuwa akimpenda kwamba kimemtibulia na sasa amejifunza kutokana na makosa.
Jacqueline Wolper.
Akizungumza na Ijumaa hivi karibuni, Wolper alisema kuwa, kwenye maisha yake ya huko nyuma ameshajianika akiwa na wapenzi tofauti lakini sasa atakayempa nafasi kwenye moyo wake hatamuanika ila hilo litakuja baadaye sana kwani sasa hivi kaweka pembeni kwanza mambo ya mapenzi.
“Sitaki yajirudie yaliyotokea katika maisha yangu ya huko nyuma, hata hivyo sasa hivi niko bize sana na kazi, mambo ya wanaume nimeamua kuyaweka pembeni kwanza,” alisema Wolper na kuongeza:
“Sitaki itokee kama ilivyokuwa kwa Dallas ambapo kila mtu alijua alikuwa ni mtu wangu, kwa sasa nimeamua kutulia kwanza na hata nikimpata mwingine watu hawatamjua hadi wakati wa ndoa.”

BREAKING NEWZZZZZZZZZZZZZ!!!! : MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2012 KUSAHISHWA UPYA,

wpid-Prime-Minister-Mizengo-PindaTAARIFA  KUTOKA BUNGENI MUDA HUU AMBAPO WAZIRI LUKUVI  AMETANGAZA KURUDIWA UPYA KUSAHISHWA KWA MITIHANI YA KIDATO CHA NNE KWA MWAKA 2012,HII IMETOKANA NA MAPENDEKEZO YALIYO TOLEWA NA TUME ILIYO UNDWA KUCHUNGUZA TATIZO LA WANAFUNZI WENGI KUFELI KATIKA HUO MTIHANI,PIA AMESITISHA KUANZA KUTUMIKA KWA VIWANGO VIPYA VYA UFAULU.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...