Thursday, August 15, 2013
BARNABA NA AMINI WALITAMBULISHA KUNDI LAO JIPYA LIITWAYO 'GEMENIH'

Wale wakali toka jumba la vipaji Tzee- THT walioishi kama pacha kwenye jumba hilo (Amini & Barnaba) wameungana na kuunda crew yao mpya kimziki iitwayo “GEMENIH” wakimaanisha wao ni kama mwezi na nyota angani.
“Yap, Tumeungana kufanya kazi pamoja kama kundi nje ya THT tukiwa ni matunda ya THT na tumeamua kujiita hivyo kutokana na kutegemeana kwetu kwenye kazi na umuhimu wa uwepo wa kila mmoja kwenye mziki wa bongo kama umuhimu wa nyota na mwezi angani.” Barnaba alilidokeza BK.
Kundi hilo kwa sasa lina-bang hewani na ngoma yao ya ‘Why me’ huku wakiwa na mipango mingi ya utendaji wao wa kazi kama Gemenih. Pia waliongeza kitu juu ya Gemenih na THT.
“Kikubwa ni kwamba, watu wasidhani tumetoka au tuna ugomvi na THT ila tumehitimu mafunzo pale na kutunukiwa vyeti nasi ni matunda ya THT na bado tunashirikiana nao kwa kuwapa ushauri hata kuwatungia nyimbo. Kwa ufupi tumewaachia wengine nafasibaada ya sisi kufuzu mafunzo pale.” Amini aliongeza.
Gemenih ipo chini ya meneja aitwaye Moses Clemence ambaye ndiye ana-control mambo yote yahusuyo vijana hao.
HATARI!! MAGUNIA 405 YA BANGI YAKAMATWA KATIKA OPARESHENI YA KUSHITUKIZA ARUMERU, ARUSHA....!!!

Katika Operesheni ya Kuzuia Uhalifu na Madawa ya Jeshi la Polisi mkoa wa Arusha liliingia kijijini hapo majira ya saa 2 za asubuhi Agosti 13 mwaka huu.
Ilikuwa ni ziara ya kushtukiza
katika kijiji hicho hali iliyowafanya wanakijiji kutaharuki na kuanza kukimbia
na kutokomea milima wakiziacha nyumba zao zikiwa wazi.
Uongozi wa Kijiji hicho nao
ulitoweka kusikojulikana kwa kuhofia mkono wa Jeshi la Polisi.
Kamishna wa Operesheni hiyo ACP
Ngonyani alisema safari hii waliamua kwenda baada ya mavuno kutokana na ukweli
kwamba zikiwa bado shamabni ni kazi nzito sana ya kufyeka.
POLISI WAMKAMATA ALIYEMUUA BILIONEA ERASTO MSUYA.....!!!

Polisi wamefanikiwa kumtia mbaroni mfanyabiashara tajiri wa madini ya Tanzanite huko Mirerani anayetajwa kuwa ndiye aliyepanga na kukodi watu waliomuua bilionea Erasto Msuya.
Habari za uhakika kutoka ndani ya Jeshi la Polisi zimedai kuwa
mfanyabiashara huyo alikamatwa mwishoni mwa wiki na jana na juzi alikuwa
akihojiwa na makachero.
Kwa mujibu wa vyanzo hivyo, mfanyabiashara huyo ndiye aliyetoa fedha za
kununulia pikipiki mbili zilizotumika katika mpango huo na pia alitoa
fedha kwa ajili ya kununua simu mpya na laini mpya.
“Tumewakamata watu wametupa mwanga mzuri na huyo mfanyabiashara ndiye
aliyetoa fedha za kununua pikipiki na siku moja kabla ya tukio
zilihifadhiwa nyumbani kwake,” alidokeza polisi mmoja.
HAYA NDIO MAPOKEZI YA FEZA KESSY UWANJA WA NDEGE DAR

Mwakilishi
wa Tanzania katika jumba la Big Brother 'The Chase' aliyetolewa
Jumapili Agosti 11 Feza Kessy amewasili leo jioni Tanzania katika
uwanja wa kimataifa wa Mwl J.K Nyerere jijini Dar es Salaam.
Katika mapokezi watu mbalimbali walijitokeza kumpokea Feza Kessy akiwemo Vanessa Mdee,Mama mzazi wa Feza kessy,ndugu jamaa na marafiki pamoja na Meneja wa Uhusiano wa Multichoice Tanzania 'Barbara'.
Katika mapokezi watu mbalimbali walijitokeza kumpokea Feza Kessy akiwemo Vanessa Mdee,Mama mzazi wa Feza kessy,ndugu jamaa na marafiki pamoja na Meneja wa Uhusiano wa Multichoice Tanzania 'Barbara'.

MAJANGAAAAAAA... MTU NA MDOGO WAKE WAOANA HUKO BAGAMOYO....POLISI WAINGILIA KATI....!!!
![]() |
Kaka mtu akitiwa mbaroni
|
Baada ya kuanza maisha ya ndoa kama mke na mume, Agosti 6, mwaka huu taarifa zikafika kwenye Kituo cha Polisi cha Ubungo ambapo maafande walisema hiyo haiwezekani.
“Polisi walipopata habari walisema hakuna ndoa hapo, wakajipanga kwenda kuvamia nyumbani kwa wanandoa hao,” kilisema chanzo.

Wednesday, August 14, 2013
SHEIKH PONDA ASOMEWA MASHITAKA AKIWA HOSPITALI

Katibu Mkuu wa Jumuiya na
Taasisi za Kiislamu nchini, Sheikh Ponda Issa Ponda amesomewa mashitaka
ya uchochezi na Mwanasheria wa serikali, akiwa wodini MOI anapoendelea
kupata matibabu. Sheikh Ponda arijeruhiwa Jumamosi iliyopita akiwa
katika mhadhara wa Kiislamu huko mkoani Morogoro. Baada ya kujeruhiwa
Ponda alilazwa katika hospitali ya Taifa Muhimbili kabla ya kuhamishiwa
katika Taasisi ya Mifupa (MOI) aliposomewa mashitaka. Kesi yake
itaendelea pindi atakapopata nafuu.
KAMATI KUU YA CCM KUAMUA HATMA YA MADIWANI BUKOBA

Halmashauri
Kuu ya CCM Mkoa wa Kagera jana tarehe 13/08/2013 katika kikao chake cha
siku moja kilichofanyika mjini Bukoba imetangaza uamuzi wake wa
kuwafutia dhamana ya CCM hivyo kuwavua Udiwani Madiwani wanane wa
Manispaa ya Bukoba waliotokana na CCM.
Kwa
mujibu wa utaratibu wa kutoa adhabu kwa viongozi wa CCM walio kwenye
vyombo vya dola hasa Wabunge na Madiwani uamuzi wa Halmashauri Kuu ya
Mkoa sio wa mwisho. Uamuzi huo unapaswa kupata Baraka za Kamati Kuu ya
Halmashauri Kuu ya Taifa ndipo utekelezwe.
Hivyo
basi, mpaka sasa Madiwani hao wanane waliosimamishwa wanapaswa
kuendelea na kazi zao kama kawaida wakisubiri kikao cha Kamati Kuu ya
Halmashauri Kuu ya Taifa kitakachoketi tarehe 23 Agosti, 2013 mjini
Dodoma ambacho pamoja na mambo mengine kitapitia uamuzi huo wa
Halmashauri Kuu ya Mkoa wa Kagera.
AFANDE FEKI WA KIKOSI CHA USALAMA BARABARANI ABAMBWA LEO HUKO TABATA KINYEREZI
Askari Bandia wa Kikosi cha Usalama Barabarani aliyekamatwa leo mchana maeneo ya Kinyelezi Mnara,Tabata jijini Dar es Salaam akiwa ndani ya sare zake mara baara ya kukamatwa. Askari huyu feki amefikishwa kwenye Kituo cha Polisi Stakishari ili taratibu za kisheria ziweze kuchukuliwa juu yake.
Afande
huyo akiwa chini ya ulinzi wa Polisi mara baada ya kukamatwa mchana wa
leo akila vichwa maeneo ya Kinyelezi Mnara,Tabata jijini Dar es
Salaam.Askari huyu feki amefikishwa kwenye Kituo cha Polisi Stakishari
ili taratibu za kisheria ziweze kuchukuliwa juu yake.
MBOWE AANIKA HADHARANI JINSI ANAVYOKOSWA KOSWA KUUAWA ...!!!
Mwenyekiti wa Chama cha demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) amesema amenusurika kuuawa katika matukio matatu yanayotokana na harakati zake za kisiasa.
Akihutubia umati mkubwa wa wananchi katika mji wa Meatu mkoani Simiu jana, Mbowe alisema hata kama atauawa hatasikitika na kwamba Watanzania wasimlilie.
Mbele ya umati huo akiwemo mbunge wa Maswa, John Shibuda, Mbowe alisema kuna watu ndani na nje ya CHADEMA ambao wamekuwa wakifanya kila mbinu kuwaangamiza viongozi na makada wa chama hicho.
Mbowe alisema viongozi wa CHADEMA akiwemo yeye mwenyewe wamekumbana na misukosuko mingi, ikiwemo yenye kuhatarisha maisha yao kutoka kwa wanasiasa wasioipenda nchi, lakini kwa neema ya Mungu wamenusurika.
“Leo hii hata kama nikiuawa, naomba Watanzania msinililie. Mbele ya jeneza langu, nizikeni huku mkisema Bwana Alitoa na Bwana Ametwaaa, Jina Lake Lihimidiwe.
MWANAFUNZI ATEKWA NA KUFANYISHWA NGONO KWA SIKU NNE....!!!

MWANAFUNZI wa kidato cha kwanza katika shule ya sekondari Marangu inayomilikiwa na kanisa Katoliki jimbo la Moshi, (jina limehifadhiwa) alitekwa na kukufungiwa kwenye hoteli moja ya kitalii mjini hapa na kufanyiwa vitendo vya ngono kwa muda wa siku nne mfululizo.
Mwanafunzi huyo anadaiwa kutekwa Agosti 6 mwaka huu na kijana mmoja
(jina linahifadhiwa) mfanyakazi wa kampuni ya simu za mikononi (Airtel)
mjini Dodoma.
Akizungumza jana na Tanzania Daima Jumatano, kaka wa mwanafunzi huyo,
Joseph Temba, alidai mdogo wake alitekwa na mtu huyo na tayari mtuhumiwa
ameshakamatwa.
Alisema walifanikiwa kumkamata mtuhumiwa huyo Agosti 10, mwaka huu,
katika baa moja akiwa na mdogo wake baada ya raia wema kutoa taarifa za
kuonekana kwake.
JAY Z NOMA-AWAPA WAFANYAKAZI WAKE BONAS YA MILION 70 KILA MMOJA-MPAKA MFANYAKAZI WA NDANI

Hip hop mogul na mfanyabiashara mwenye
‘kisu’ cha maana (pesa) Shawn Carter a.k.a Jay Z licha ya kuwa baba
mzuri kwa Blue Ivy, mume mzuri wa mkewe Beyonce lakini pia ni boss mzuri
(tena sana) kwa wafanyakazi wake baada ya kuamua kuwapa ‘bonus’ ya
kutisha (kwa ukubwa) ya mshahara.
Hivi karibuni Jay Z na Beyonce waliamua kurudisha fadhila kwa wafanyakazi hao wapatao 80 kwa kuamua kuwapa bonus ya zaidi ya $46,000 sawa na zaidi ya shilingi milioni 70 kila mmoja kutokana na kazi nzuri wanayoifanya.
Wafanyakazi waliodondokewa na zali hilo ambalo hawakulitegemea ni wale wa kampuni zake zote, club yake ya 40/40 hadi wale wafanyakazi wao wa nyumba zao 3 za Marekani.
Hivi karibuni Jay Z na Beyonce waliamua kurudisha fadhila kwa wafanyakazi hao wapatao 80 kwa kuamua kuwapa bonus ya zaidi ya $46,000 sawa na zaidi ya shilingi milioni 70 kila mmoja kutokana na kazi nzuri wanayoifanya.
Wafanyakazi waliodondokewa na zali hilo ambalo hawakulitegemea ni wale wa kampuni zake zote, club yake ya 40/40 hadi wale wafanyakazi wao wa nyumba zao 3 za Marekani.
CHELSEA YADUWAZWA, DAVID LUIZ AMCHANA MOURINHO KUWA ANATAKA KUONDOKA KUJIUNGA NA BARCELONA


Raha kwa Barca: David Luiz amewaambia Chelsea kuwa anataka kutimkia Barcelona
Taarifa hizi ni kwa mujibu wa gazeti la Mundo Deportivo
Luiz
amekuwa katika harakati za kujiunga na Barcelona baada ya dili la
Thiago Silva, aliyekuwa akitajwa kujiunga Camp Nou kubuma. Kocha
Jose Mourinho hakufurahishwa na kiwango cha Luiz mechi za nyuma, lakini
alisema nyota huyo mwenye umri wa miaka 26 hatauzwa majira haya ya
kiangazi.
Subscribe to:
Comments (Atom)








