Rais Jakaya Kikwete amebainisha kuwa vurugu za kidini na kisiasa zinazotokea nchini, zina uhusiano na watu wa nchi za nje.
Rais Kikwete alikuwa mgeni rasmi kwenye ibada hiyo iliyofanyika kwenye Kanisa Kuu la Roho Mtakatifu.
“Wanaohamasisha vurugu hizo ni watu wenye uhusiano ya karibu na watu wa nje ambao mambo yakiharibika nchini watakuwa wa kwanza kupanda ndege, ilhali wakiendelea kutoa matamko ya uchochezi wakiwa nje ya nchi wakati wengine wakiendelea kuumia,” alisema Kikwete.
Ibada hiyo ilifanyika chini ya ulinzi wa polisi na askari wa usalama, na ilihudhuriwa na Askofu Mkuu wa Anglikana duniani, Justin Welby.
Rais Kikwete alisema amekuwa akichukizwa na vurugu za kidini zinazofanywa na baadhi ya watu wasioitakia mema Tanzania, huku wakijua kuwa amani ikitoweka ni gharama kubwa kuipata.






Mchezaji wa timu ya Yanga Didier Kavumbagu akikokota mpira mbele ya mchezaji wa timu ya Simba Abdallah Seseme katika mchezo wa ligi kuu ya Vodacom unaofanyika jioni hii kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam , hivi sasi ni kipindi cha pili na Yanga wanaongoza magoli 2 -0 dhidi ya Simba ambayo imekosa penati katika kipindi cha kwanza wakati mchezaji wake Mussa Mude akipiga vibaya mpira huo baada ya Mrisho Ngassa wa Simba kuangushwa kenye eneo la hatari
Wachezaji wa timu ya Simba na Yanga wakiwania mpira wakati wa mchezo wao unaofanyika kwenye uwanja wa Taifa jioni hii.
Baada ya golikipa wa Simba Juma K. Juma kuteswa hali ilikuwa hivi.
Wachezaji wa Yanga wakishangilia baada ya kupata goli la kwanza dhidi ya Simba.














