Thursday, May 18, 2017

SHILOLE AWATAJA DIAMOND, ZALI KWENYE KESI YAKE

 
MSANII wa Bongo Fleva, Zuwena Mohamed ‘Shilole’, ameieleza mahakama jinsi mwanafunzi wa Chuo cha Bandari, Thomas Lukas, alivyokuwa akitumia mtandao wa kijamii wa Instagram kutuma meseji za matusi ya nguoni kwa watu mbalimbali.

Shilole alitoa ushahidi huo jana katika Mahakama ya Wilaya Kinondoni mbele ya Hakimu, Boniface Lihamwike.

Akiongozwa na wakili wa Serikali, Tumaini Mfikwa, Shilole alidai shughuli zake ni muziki na anatambulika kwa jina la Shilole ama Shishi baby.

Shilole: Mheshimiwa mimi nafanya kazi sehemu nyingi hasa kwenye Instagram, WhatsApp, Facebook na Twitter…, nipo kwenye mitandao hiyo tangu nilipokuwa superstar miaka mitano iliyopita.

Alieleza Shilole huku akidai kwamba mwaka jana alipokea simu za watu tofauti wakiwemo wasanii wenzake na mashabiki wake wakimlalamikia kuhusu meseji za matusi anazowatumia kupitia ukurasa wake wa Instagram.

Shilole: Yaani mimi kama mwanamke nilidhalilishwa sana na hayo matusi, mheshimiwa Hakimu ukitaka nayataja hapa.
Hakimu: Subiri…
Shilole: Ndipo nikaamua kwenda kituo cha Polisi Osterbay kuonyesha jinsi mtuhumiwa alivyotumia jina langu vibaya.

Hata hivyo, alipotakiwa na Wakili wa utetezi, Julias Kamote na Christina Roman ataje baadhi ya majina ya wasanii waliomlalamikia, aliwataja kwamba ni Queen Darlin, Diamond, Zali, Ant Ezekiel na Harmonize mwingine ni mtangazaji, Efrahim Kibonde.

Mahakama iliahirisha kesi hiyo hadi Juni 6, mwaka huu na mtuhumiwa yupo nje kwa dhamana.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...