Saturday, December 21, 2013

YANGA YAKUBALI KICHAPO CHA MAGOLI 3 KWA 1 KUTOKA KWA SIMBA KATIKA MCHEZO WA KUMTAFUTA NANI MTANI JEMBE

Wachezaji wa Timu ya Simba na baadhi ya viongozi wao wakipozi na kombe lao baada ya kukabidhiwa kwa kuifunga Timu ya Yanga Mabao 3-1 katika mchezo wa Nani Mtani Jembe, uliochezwa kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam jioni ya leo.Mabao ya Simba yalifungwa na Hamis Tambwe mawili na Ramadhan Singano huku la kufutia machozi la Yanga likifungwa na Emmanuel Okwi.Picha zote na Othman Michuzi.
Meneja wa Yanga, Afidh Ally akipokea mfano wa hundi ya zaidi sh. 98 milioni Kwa kuibuka washindi katika shindano la Nani Mtani Jembe kwa kupata kura nyingi katika unywaji wa bia ya Kilimanjaro.
Hundi ya Simba ilisomeka hivi pamoja na Ushindi Mkubwa walioupata dhidi ya wapinzani wao.
Mgeni Rasmi katika Mchezo huo,Waziri wa Sheria na Katiba,Mh. Mathias Chikawe akikabidhi Kombe la Ushindi wa Nani Mtani Jembe kwa Nahodha wa Timu ya Simba mara baada ya kumalizika kwa mchezo huo jioni hii kwenye Uwanja wa Taifa,Jijini Dar es Salaam.
Mshambuliaji wa Timu ya Yanga,Mrisho Ngassa (17),akiwa mpiga chenga ya Mwili Beki wa Timu ya Simba,Donald Mtosi wakati mchezo wao wa Nani Mtani Jembe unaoendelea hivi sasa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.Hadi hivi sasa Simba wanaongoza kwa Bao 1-0 na tayari dakika 35 za mchezo zishakatika.Picha zote na Othman Michuzi.
Simba wakiandika Bao la Kwanza mnamo dakika ya 19 ya mchezo.
 Mashabiki wa Simba.
Nahodha wa Timu ya Simba,Henry Joseph Shindika akikabiliana na Mpinzani wake wakati wa Mtanange wa Nani Mtani Jembe uliopigwa Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam,jioni ya leo.
Kelvin Yondani wa Yanga akitoa pasi nzuri.
 Sehemu ya mashabiki wa Yanga, waliokwisha keti katika siti zao wakisubiri kuishangilia timu yao.
Sehemu ya mashabiki wa Simba, waliokwisha keti katika siti zao wakisubiri kuishangilia timu yao.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...