Wapiganaji wa IS wakibeba mabaki ya ndege waliodai kuidungua huko Syria
Wapiganaji
wa kundi la Islamic State wamesema kuwa waliidungua ndege ya jeshi la
muungano ,lakini Marekani inasema kuwa ushahidi uliopo unaonyesha kuwa
hilo si kweli.
Jordan ni miongoni mwa mataifa manne ya kiarabu
yaliopo katika muungano wa majeshi yanayoungwa mkono na Marekani ambayo
yameanzisha mashambulizi dhidi ya wanamgambo wa IS.Ndege hiyo aina ya F-16 ni ndege ya kwanza ya jeshi hilo la muungano kupotea katika maeneo yanayodhibitiwa na IS tangu mashambulizi yaanze mnamo mwezi Septemba.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.