Tuesday, July 16, 2013

MAGAZETI YA LEO JUMANNE JULAI 16, 2013

ALICHOKIANDIKA RAY KUHUSU MAREHEMU KANUMBA....!!!


Steven Kanumba, Vincent Kigosi

Maswahiba wawili wakitoka safari marehemu Kanumba na Ray

MWIGIZAJI, mtayarishaji na muongozaji mahiri wa filamu Swahiliwood Vincent Kigosi ‘Ray the Greatest’ hivi karibuni aliangusha bonge la sherehe ya siku yake ya kuzaliwa na kuwakaribishwa rafiki zake na wadau wa filamu katika moja ya Hotel, siku hiyo pia aliweza kumkumbuka swahiba yake marehemu Kanumba na kuhisi uenda angekuwepo siku hiyo.



“Ni siku ambayo nimesheherekea siku yangu ya kuzaliwa na ndugu zangu wa karibu na wasanii wenzangu, ni siku ambayo nimekumbuka mambo mengi sana katika maisha yangu, mara nyingi swahiba wangu marehemu Kanumba siku kama ya leo ningekuwa naye katika sherehe kama hii, lakin ndio mambo ya Mungu huwezi kulaumu kilichobaki ni kumuombea Mwenyezi Mungu ampumzishe kwa amani Amen,” alisema The Greatest. 

Katika sherehe hiyo iliyopambwa na vinywaji na malaji kibao ilijumuisha wasanii nguli katika tasnia ya filamu kama Bonge la bwana, JB, Maya, Odama, Chikoka na wasanii wengine kibao huku kukiwa na michezo kadha wa kadhaa ni jambo jema kwa marafiki kukumbuka katika matukio kama hayo.

CHANZO FILAMU CENTRAL

MUGABE ATOA KALI YA MWAKA, ATAKA MASHOGA NA WASAGAJI WAPEANE MIMBA LA SIVYO JELAAAA...!!!

Rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe

 RAIS wa Zimbabwe, Robert Mugabe ametoa kali ya mwaka kwa kuwachimba mkwara Mashoga na Wasagaji kwamba wasipotiana mimba ni lazima atawafunga jela.

Mubabe ametoa kali hiyo Ijumaa  wakati akizindua kampeni za chama chake cha kwa ajili ya uchaguzi utakaofanyika mwezi. 

Isome taarifa nzima ya rais huyo mwenye umri mkubwa aliye madarakani duniani na ambaye wazungu wanambloo kwa misimamo yake isiyoyumba.

DIAMOND AMBANA PREZZO PATAMU BAADA YA PREZZO KUMPIGIA SIMU NA KUOMBA MSAMAHA


Diamond Platnumz amesema Rapcellency Prezzo alimpigia simu hivi karibuni kumuomba msamaha kufuatia tweet za kumdiss alizoziandika wiki iliyopita, lakini hitmaker huyo wa Kesho amesema kama Prez ana nia ya kumuomba msamaha basi afanye hivyo hadharani kwenye mtandao wa Twitter.
Diamond alikuwa akihojiwa mchana wa leo kwenye kipindi cha Mambo Mseto cha Radio Citizen ya nchini Kenya kinachoendeshwa na mtangazaji William Tuva.

Msanii huyo anayeongoza kwa kulipwa zaidi kwenye show nchini, amesema alishangazwa na kitendo hicho cha Prezzo kumdis kutokana na majigambo aliyoyatoa kabla ya show yao kwenye Tamasha la Matumaini mwanzoni mwa mwezi huu.

VAN PERSIE AJIUNGA NA UNITED ZIARANI, ROONEY ABAKI NJIA PANDA BAADA YA MOYES KUSISITIZA KUMSAJILI FABREGAS

Straight into the action: Robin van Persie warms up alongside United coach Phil Neville in Sydney, hours after arriving for the second leg of the club's pre-season tour
Karudi kazini: Robin van Persie amerudi na kujiunga na Manchester United katika ziara yao Sydney
Robin van Persie in training with Manchester United in Sydney
Robin van Persie (right) trains with Phil Neville during Manchester United's pre-season tour to Australia
Doubts: Yet again, question marks over Rooney's future have risen again
Maisha ya Rooney ya baadaye katika klabu yake ya United bado haijulikani
David Moyes at United's match against Singha All-Stars 

WALIOSAJILIWA NA WALIOTEMWA KWENYE LIGI KUU


 
Mabeki wa Toto African, Evarist Maganga (kushoto) na Peter Mutabuzi wakimkaba mshambuliaji wa Azam Brian Umony. Beki Mutabuzi amejiunga na Kagera Sugar kwa ajili ya msimu ujao wa ligi. Picha na Michael Matemanga.
 
*********
 
Mosses Oloya wa Uganda anayecheza soka la kulipwa nchini Vietnam anaweza akawa ndiye mchezaji anayetikisa zaidi kwenye usajili wa soka la Bongo kwa timu 14 zinazojiandaa kushiriki Ligi Kuu Bara msimu ujao.
Oloya anamudu vyema kucheza nafasi ya winga wa kushoto pamoja na kulia kama ilivyokuwa kwa mfungaji hatari wa Simba, Emmanuel Okwi aliyetua klabu ya Etoile du Sahel ya Tunisia Januari mwaka huu, baada ya kupata mafanikio makubwa akiwa na Simba.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...