Monday, March 03, 2014

ZITAMBUE CHANGAMOTO SITA (6) KWA KILA UCHUMBA/ NDOA...!!!


jambotz8.blogspot.com/
Ukweli ni kuwa watu wawili wanapoamua kwa dhati kuwa katika mahusiano ni kwamba wanakuwa tayari katika akili zao wamejenga matarajio au matumaini ya kunufaika na uhusiano husika, hata kama hawawezi ambiana moja kwa moja kuwa “ aisee, mie kuwa na wewe nataraji moja , mbili, tatu….”.
Kunapokuwepo na upendo, basi pia kunaleta majukumu, ambapo bila ya kutimizwa kwa majukumu yanayotarajiwa kutimizwa, maana halisi ya mahusiano bora inapotea.
Hii si tuu kwa mahusiano ya kimapenzi, bali hata dini zinatufundisha kuwa Mungu anatupenda, na katika hilo, tunajukumu la kutii amri zake, na kwamba tusipotii amri zake, tunakuwa tumeharibu maana nzima ya upendo wake, kwani tutajikuta tumeingia motoni/jehanamu (Kinyume cha upendo).
Hata katika familia, tumesikia mzazi pamoja na upendo alioonyesha kwa mtoto wake toka yupo tumboni mpaka mtoto ameweza kujitegemea, endapo mtoto husika akashindwa kumjali ( hili ndio jukumu linalokuja na upendo wa mzazi), basi unaweza sikia mzazi huyo akitoa ‘laana’ au ‘akamwachia radhi’ mtoto wake mwenyewe wa kumzaa.
jambotz8.blogspot.com/
Ni wazi kuwa mara nyingi majukumu yanayoletwa na upendo huwa hayaelezwi wazi wazi, hata hivyo katika mahusiano, mambo yafuatayo yanaweza kuwa sehemu ya matarajio ambayo  wapenzi wanaweza kuwa makini ili waweze kuwapendeza wenzao. Kwa maana nyingine ni kuwa yafuatayo, ndio maeneo ambayo mtu aliye kwenye mahusiano ni muhimu ‘acheze’ vema ili kulinda mahusiano/penzi:-

Fedha:  Katika swala la fedha, jambo kubwa linalojitokeza ni namna ya kufanya maamuzi kuhusu matumizi ya fedha.  Ni muhimu kuweka mikakati ya pamoja kwa mambo ya msingi kimaisha , na kila mmoja kutilia maanani mipango hiyo, kabla ya kuamua kutumia kipato chake kwa mambo ambayo pengine hayapo nje ya mipango ya kifedha ya wawili nyie kama wapenzi.  Bila shaka, kuendana na aina yenu ya kipato, aina yenu ya maisha, kama wapenzi mtakuwa na kiwango fulani cha fedha ambacho si busara mmoja wenu kuamua kutumia bila kumtaarifu mwenzake , hata kama matumizi husika ni muhimu sana, na haijalishi nani kazitafuta fedha husika.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz 

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...