Amesema
uamuzi huo unafuatia kaulimbiu ya kutaka kuwajengea wanafunzi maadili
mema katika mazingira ya shule za sekondari tangu wanapoingia kidato cha
kwanza badala ya mfumo wa sasa ambapo wanakuja kupata mafunzo hayo
kidato cha tano na cha sita lakini wanakuwa hawajapata msingi imara
tangu wakiwa wadogo.
Ametoa
kauli hiyo jana jioni (Jumamosi, Septemba 21, 2013) wakati akizungumza
na mamia ya wanajumuiya waliohitimu katika shule hiyo (Alumnae),
wanafunzi waliopo pamoja na wageni mbalimbali waliohudhuria sherehe za
Jubilei ya miaka 50 ya Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Weruweru.
Waziri
Mkuu ambaye alikuwa mgeni rasmi katika sherehe hizo, alikuwa akijibu
maombi yaliyotolewa na Dk. Maria Kamm ambaye aliongoza shule hiyo kwa
miaka 22 kuanzia mwaka 1970 hadi 1992, pamoja na wazungumzaji wengine
katika sherehe hizo.
Alisema
Serikali ilikwishatoa maelekezo kwa Makatibu Tawala wa Mikoa kwa ajili
ya shule tano ambazo ziliondolewa madarasa ya kidato cha kwanza hadi cha
nne na mojawapo ya shule hizo ni Sekondari ya Wasichana ya Weruweru.