Asante
kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, ukitaka kuwa wa kwanza
kupata habari zetu Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya
neno Jambo Tz
Mbunge wa Kigoma Kusini (NCCR-Mageuzi), David Kafulila. PICHA|MAKTABA
KATIKA hali ya kushangaza, Mahakama Kuu, Kitengo cha Biashara
imewazuia waandishi wa habari kuingia mahakamani kusikiliza maombi ya
kampuni ya Pan Africa Power Solutions (PAP) na Kampuni ya Independent
Power Tanzania (IPTL) kwa Bodi ya Rufaa ya Kodi nchini, kutaka Kamishna
Mkuu wa TRA akamatwe na kupelekwa gerezani.
Waandishi wa vyombo mbalimbali vya habari nchini, waliofika
mahakamani hapo jana kusikiliza maombi hayo, walishindwa kusikiliza
kinachoendelea baada ya kuambiwa kuwa waandishi wamezuiwa kusikiliza.
Mmoja wa makarani wa mahakama hiyo, aliwaambia waandishi wa habari
kuwa hawaruhusiwi kusikiliza maombi hayo, lakini hakuwaeleza sababu. Asante
kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, ukitaka kuwa wa kwanza
kupata habari zetu Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya
neno Jambo Tz
Asante
kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, ukitaka kuwa wa kwanza
kupata habari zetu Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya
neno Jambo Tz
MKAZI wa kijiji cha Chibwechangula –Behelo katika wilaya ya Mpwapwa
mkoani Dodoma, Ruth Matonya (26) amejifungua mtoto wa ajabu ambaye nusu
ya sura yake inafanana na binadamu na nusu ikifanana na chura.
Mtoto huyo alizaliwa Desemba 2, mwaka huu katika Kituo cha Afya cha
Mtakatifu Luka kinachomilikiwa na Kanisa la Anglikana, Dayosisi ya
Mpwapwa. Alifariki dunia muda mfupi baada ya kuzaliwa.
Kwa mujibu wa Mganga Mfawidhi wa kituo hicho, Dk Edwin Kihura mara
baada ya mama huyo kufika katika kituo hicho cha afya alikuwa na uchungu
ambao haukuwa na kikomo, lakini alishindwa kujifungua kwa njia ya kawaida licha ya njia ya uzazi kufunguka.
Asante
kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, ukitaka kuwa wa kwanza
kupata habari zetu Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya
neno Jambo Tz
MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Profesa Mussa
Assad (pichani) aliyeapishwa juzi na Rais Jakaya Kikwete amekemea tabia
ya wanasiasa na wafanyabiashara kuingilia kazi za kitaaluma, akisema kwa
upande wake hatapenda kuona watu wa makundi hayo wakifanya hivyo na
kusisitiza kuwa, kufanya hivyo ni kosa.
Aliyasema hayo jana mbele ya waandishi wa habari mara baada ya
ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa kila mwaka wa Wahasibu na Wakaguzi (NBAA)
kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Arusha (AICC), jijini hapa.
Alisema ofisi ya CAG na watendaji wengine watafanya kazi kwa kufuata
maadili ya kazi, huku akiendelea kusisitiza wanasiasa na wafanyabishara
kila mmoja aheshimu taaluma ya ukaguzi wa hesabu za serikali kwa faida
ya nchi.
Alifafanua kuwa iwapo kila mmoja atawajibika katika nafasi yake na
kuaminiana katika shughuli za kila siku, kamwe hakutakuwa na matatizo
yoyote.
‘’Matatizo ya watu binafsi yasichanganywe na shughuli za kila siku za
ofisi ya CAG na wale wenye kufanya siasa na biashara pia wawajibike
katika nafasi zao na ofisi yangu itafanya mambo kwa kufuata Katiba ya
nchi inavyoelekeza, na sio vinginevyo,” alisema Profesa Assad
aliyekabidhiwa mikoba ya Ludovick Utouh aliyestaafu kwa mujibu wa
sheria.
Alitumia fursa hiyo kuwaasa wahasibu na wakaguzi, akisema wanatakiwa
kufanya kazi kwa weledi mkubwa na kiwango cha hali ya juu ili taaluma
yao iweze kuheshimika nchini. Asante
kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, ukitaka kuwa wa kwanza
kupata habari zetu Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya
neno Jambo Tz
Kampuni za Pan Africa Power
Solution Tanzania Limited (PAP) na Independent Power Tanzania Ltd
(IPTL), zimewasilisha maombi ya kutaka Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya
Mapato (TRA) akamatwe kwa kukiuka amri ya Bodi ya Rufaa za Kodi (TRAB)
kwa kufuta Hati za Malipo ya Kodi za Mauzo ya Hisa (Capital Gain
Certificate).
Kampuni hizo mbili, ambazo ziko kwenye mgogoro wa
umiliki, ndizo zinahusika kwenye sakata la uchotwaji wa Sh306 bilioni
kutoka Akaunti ya Tegeta Escrow iliyofunguliwa kuhifadhi fedha za malipo
ya tozo ya kuuza umeme unaofuliwa na IPTL, kwa Shirika la Umeme
(Tanesco), wakati wa kusubiri uamuzi wa mahakama katika kesi ya kupinga
tozo hilo.
PAP, ambayo inadai imenunua hisa zote za IPTL,
ndiyo iliyolipwa fedha zote zilizokuwa kwenye akaunti hiyo na kuamsha
mjadala mkubwa bungeni ulioisha kwa Bunge kufikia uamuzi wa
kuwawajibisha kisheria wote waliohusika, wakiwemo mawaziri. Asante
kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, ukitaka kuwa wa kwanza
kupata habari zetu Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya
neno Jambo Tz
Katibu
Mtendaji wa Baraza la Ushauri la Watumiaji Huduma za Usafi wa nchi kavu
na Majini, Dk Oscar Kikoyo akizungumza na waandishi wa habari ofisini
kwake Dar es salaam jana juu ya hali ya usafiri kipindi cha siku kuu za Krismas na mwaka mpya ambapo ametahadharishja abiria kuto kukubali
kutozwa nauri za juu na pindi ikitokea hivyo Sumatra ipewe taarifa
haraka.
Asante
kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, ukitaka kuwa wa kwanza
kupata habari zetu Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya
neno Jambo Tz
Asante
kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, ukitaka kuwa wa kwanza
kupata habari zetu Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya
neno Jambo Tz
MAHAKAMA
inaangalia uwezekano wa kuruhusu vyombo vya habari kurekodi picha na
sauti kuwezesha vituo vya radio na televisheni kuripoti habari za
mahakama wakati kesi zinaendelea.
Jaji
Mkuu, Mohamed Chande Othman alisema jana mahakama inajifunza kutoka kwa
nchi zinazoruhusu vituo vya redio na televisheni kurekodi na kuripoti
habari wakati kesi zinaendelea.
Alisema
hayo alipozungumza na waandishi wa habari jana wakati wa mkutano baina
ya Baraza la Vyombo vya Habari na Mahakama uliofanyika jijini Dar es
Salaam. Asante
kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, ukitaka kuwa wa kwanza
kupata habari zetu Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya
neno Jambo Tz
Rais Robert Mugabe awalaumu baadhi ya wapinzani
wake ndani ya chama cha ZANU PF kwa kupanga kumuondoa mamlakani.
Rais
wa Zimbabwe Robert Mugabe amelaumu baadhi ya watu ndani ya chama chake
tawala cha ZANU-PF kwamba wanapanga kumng'oa madarakani.
Akizungumza
katika kongamano la chama hicho, Mugabe amesema amebaini kuwepo
majaribio ya kuwahonga wajumbe kumpinga kama kiongozi, lakini
akasisitiza wajumbe hawawezi kupokea hongo. Mugabe ameahidi
kupambana na rushwa ndani ya chama na kukabiliana na maafisa wa chama
hicho ambao kazi yao ni kutoa hongo na kupokea rushwa.
Wanachama wengi wa chama hicho wangali ni wafuasi sugu wa Rais Mugabe
Hasira ya Mugabe ilionekana
kufuatia madai ya njama ya kutaka kumuua yanayodaiwa kuandaliwa na
naibu wake Joyce Mujuru. Hata hivyo Mujuru alikanusha madai hayo ambayo
yamekuwa yakimuandamana.Mugabe alisema kutokuwepo kwa Bi Mujuru kwenye mkutano huo wa chama kunaonyesha kuwa anaogopa. Asante
kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, ukitaka kuwa wa kwanza
kupata habari zetu Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya
neno Jambo Tz
Luke Somers raia wa Marekani mwandishi wa habari anayeshikiliwa mateka na al-Qaeda huko Yemen
Marekani
imeeleza kuwa ilijaribu kumwokoa raia wake mzaliwa wa Uingereza Luke
Somers, anayeshikiliwa mateka na al-Qaeda nchini Yemen.
Rais Barack Obama aliidhinisha kikosi cha kumwokoa Luke, mwezi uliopita. "Kwa
masikito, Luke hakuwepo, japokuwa mateka kutoka mataifa mengine
walikuwepo na waliokolewa," Baraza la Usalama la Taifa, limesema. Mtu
anayejitambulisha kama Luke Somers, ambaye alitekwa mwaka 2013,
ameonekana katika video, akisema maisha yake yako hatarini na anaomba
msaada. Video hiyo pia inamwonyesha mfuasi wa al-Qaeda huko Yemen
akitishia kumuua Bwana Somers hadi madai yao ambayo hayajatajwa,
yatakapotimizwa. Bwana Somers, mwenye umri wa miaka 33,
alifanyakazi kama mwandishi wa habari na mpiga picha wa mashirika ya
huko na kazi zake zikaonekana katika vyombo vya habari vya kimataifa,
ukiwemo mtandao wa BBC. Asante
kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, ukitaka kuwa wa kwanza
kupata habari zetu Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya
neno Jambo Tz
Asante
kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, ukitaka kuwa wa kwanza
kupata habari zetu Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya
neno Jambo Tz
Viwanda vikitoa moshi angani na kuchafua mazingira
Mwaka
huu unaoishia unasemekana kuwa na kiwango cha juu zaidi cha joto
duniani na kwa Uingereza tangu kumbukumbu zianze kutunzwa.
Makadirio
ya awali yanaonyesha kuwa katika miezi kumi ya kwanza ya mwaka 2014,
wastani wa kiwango cha hali ya joto duniani kilikuwa 0.57C juu ya
wastani uliokuwepo muda mrefu.
Dhoruba nchini Uingereza iliyosababishwa na mabadiliko ya tabia nchi
Na miezi kumi na mmoja ya
kwanza nchini Uingereza imezalisha wastani wa joto la 1.6C likiwa juu ya
wastani uliokuwepo kwa muda mrefu.Utafiti mwingine uliofanywa na
Ofisi ya Hali ya Hewa ya Uingereza umeonyesha kuwa ongezeko la viwango
vya joto vilivyoshuhudiwa, visingetokea bila ya ongezeko la gesi
zinazoharibu mazingira kutokana na shughuli za binadamu. Asante
kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, ukitaka kuwa wa kwanza
kupata habari zetu Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya
neno Jambo Tz
Wapiganaji wa Islamic State katika jimbo la Anbar,Syria Marchi 2014
Wapiganaji wa kundi la Islamic State wafungua kambi za mafunzo Libya
Wapiganaji
wa kundi la Islamic State wameanzisha kambi za mafunzo mashariki mwa
Libya, amesema mkuu wa kamandi ya Marekani ya masuala ya Afrika.
Wapiganaji wa Kikurd wakiwa katika mafunzo ya
kijeshi kukabiliana na wapiganaji wa Islamic State Septemba 2014 nchini
Iraq.Asante
kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, ukitaka kuwa wa kwanza
kupata habari zetu Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya
neno Jambo Tz
Upangaji
wa makundi ya timu kumi na sita zilizofuzu kucheza fainali za
mashindano ya 30 ya kuwania Kombe la Mataifa ya Afrika kwa mwaka 2015
yamefanyika katika mji mkuu wa Equatorial Guinea, Malabo.
Mashindano hayo yataanza Januari 17, 2015.
Upangaji
wa makundi ulirudishwa wiki moja nyuma ili kuiwezesha Equatorial
Guinea, kujiandaa baada ya kuchukua nafasi ya Morocco, iliyokuwa iandae
mashindano hayo, lakini ilishindwa kufanya hivyo baada ya kutaka
mashindano hayo yasogezwe mbele kuhofia ugonjwa wa Ebola ambao
umeyakumba baadhi ya mataifa ya Afrika Magharibi, ambako zinatoka timu
nyingi zinazoshiriki michuano hiyo.
Mabingwa watetezi Nigeria ni
moja ya timu kubwa zilizoshindwa kufuzu kucheza fainali za mwakani,
pamoja na Misri na Angola ambazo zote kwa mshangao hazitaweza kushiriki.
Haya hapa makundi manne ya AFCON 2015:
Kundi A Equatorial Guinea, Burkina Faso, Gabon, Congo Kundi B Zambia, Tunisia, Cape Verde, DR Congo Kundi C Ghana, Algeria, South Africa, Senegal Kundi D Ivory Coast, Mali, Cameroon, Guinea
Wenyeji
Equatorial Guinea na Congo zitacheza mechi ya ufunguzi wa michuano
hiyo. Kundi D ndilo linaloonekana kuwa gumu zaidi kutokana na timu
zilizopangwa kundi hilo. Asante
kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, ukitaka kuwa wa kwanza
kupata habari zetu Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya
neno Jambo Tz