Thursday, July 11, 2013
HII NDO HISTORIA FUPI YA FREEMASON SOMA HAPA....!!!
HISTORIA FUPI YA FREEMASON.
Ni shirika ambalo mambo yake ni siri kuu. Mimi nilifanya utafiki kwenye mitandao, nikafatilia historia yao kama inavyoonyeshwa mara kwa mara kwenye makala za historia katika televisheni za magharibi pamoja na kuongea na watu waliofuatilia kwa karibu mambo yao.
Kwenye maelezo yao kwa nje Free masons wanajitangaza kama shirika zuri tu.
Naomba niorodheshe mambo machache niliyoambiwa kuhusiana na Freemasonry.
1. Ni kweli Freemasonry kama ilivyo maana yake kwanza ilkuwa ni kundi la mafundi waashi (masons) au wajenzi kuwa lugha nyingine. Walikuwa ni wataalamu waliobobea kwenye masuala ya ujenzi wa mahekalu na mabenki ya zama hizo zinazoitwa kwa kizungu (medieval times). Niliambiwa walikuwa ni watunzaji wa pesa za kanisa katoliki. Kwani walikuwa wanajenga mahekalu(cathedrals) za wakatoliki na mabenki/ mahandaki ya kuhifadhia pesa pamoja na kuzikia(catacombs).
Niliambiwa wanaweza kujenga hayo maandaki kwa utaalamu mkubwa kiasi kwamba ukiingia ndani ya hayo mahandaki bila ramani unaweza ukashindwa kutoka hata unaweza kupotelea humo humo ndani usiweze kutoka tena. Hicho ndicho kilichokuwa ni kiwango cha utaalamu wao.
2. Kwa kuwa walikuwa ni waashi ndiyo maana alama zao ni vifaa vya ujenzi, Pima maji n.k
Ni shirika ambalo mambo yake ni siri kuu. Mimi nilifanya utafiki kwenye mitandao, nikafatilia historia yao kama inavyoonyeshwa mara kwa mara kwenye makala za historia katika televisheni za magharibi pamoja na kuongea na watu waliofuatilia kwa karibu mambo yao.
Kwenye maelezo yao kwa nje Free masons wanajitangaza kama shirika zuri tu.
Naomba niorodheshe mambo machache niliyoambiwa kuhusiana na Freemasonry.
1. Ni kweli Freemasonry kama ilivyo maana yake kwanza ilkuwa ni kundi la mafundi waashi (masons) au wajenzi kuwa lugha nyingine. Walikuwa ni wataalamu waliobobea kwenye masuala ya ujenzi wa mahekalu na mabenki ya zama hizo zinazoitwa kwa kizungu (medieval times). Niliambiwa walikuwa ni watunzaji wa pesa za kanisa katoliki. Kwani walikuwa wanajenga mahekalu(cathedrals) za wakatoliki na mabenki/ mahandaki ya kuhifadhia pesa pamoja na kuzikia(catacombs).
Niliambiwa wanaweza kujenga hayo maandaki kwa utaalamu mkubwa kiasi kwamba ukiingia ndani ya hayo mahandaki bila ramani unaweza ukashindwa kutoka hata unaweza kupotelea humo humo ndani usiweze kutoka tena. Hicho ndicho kilichokuwa ni kiwango cha utaalamu wao.
2. Kwa kuwa walikuwa ni waashi ndiyo maana alama zao ni vifaa vya ujenzi, Pima maji n.k
MAMA MZAZI WA PROFESA J AFARIKI DUNIA BAADA YA KUNGONGWA NA GARI HUKO MBEZI JUU, DAR ES SALAAM

Profesa J akiwa na mama yake mzazi Bi Rosemary Majanjara Haule enzi za uhai wake. Picha hii ilipigwa April 4, 2008 katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es salaam wakati wa sherehe ya uzinduzi wa albamu mpya ya Profesa J ya 'Aluta Continua'
HABARI
ZILIZOPOKEWA USIKU NI KWAMBA MAMA YAKE MZAZI MSANII MAARUFU WA
MUZIKI NCHINI, JOSEPH HAULE A.KA. 'PROFESA J' AMEFARIKI DUNIA USIKU HUU
BAADA YA KUGONGWA NA GARI MAENEO YA MBEZI JUU, JIJINI DAR ES SALAAM,
ALIKOKUWA ANAISHI NA MWANAE.
HABARI
ZINASEMA MAREHEMU, BI. ROSEMARY MAJANJARA HAULE, ALIGONGWA NA GARI
AKIWA ANAVUKA BARABARA KUELEKEA DUKANI KIASI CHA SAA MBILI USIKU, NA
KWAMBA BAADA YA KUGONGWA WASAMARIA WEMA WALIMKIBIZA HOSPITALINI TUMBI
KWA KUTUMIA BAJAJI AMBAKO ALIFARIKI DUNIA. TAARIFA ZA AWALI HAZIJATAJA
AINA YA GARI NA KAMA BAADA YA AJALI HIYO LILISIMAMA AU LA.
ANGALIA WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO NA SHULE WALIZOPANGIWA HAPA...!!!
WASICHANA....<<< BOFYA HAPA>>
WAVULANA....<< BOFYA HAPA>>>
>>Ukitaka kuya download bofya hapo chini
WASICHANA: << DOWNLOAD>>
WAVULANA: << DOWNLOAD>>
1. KWA KUANGALIA MATOKEO YA WAVULANA CLICK LINK HII https://docs.google.com/file/d/0B6EsT3rjf-pzamlnNDhZcXJVeUU/edit?usp=sharing
2. KWA KUANGALIA MATOKEO YA WASICHANA CLICK LINK HII https://docs.google.com/file/d/0B6EsT3rjf-pzY0VGVHBfcXdfazQ/edit?usp=sharing
Wednesday, July 10, 2013
MWANAMUZIKI MARIAH CAREY ADONDOSHWA CHINI NA VIATU VIREFU...!!!
Mariah Carey
MUIMBAJI
mwenye sauti yenye mvuto nchini Marekani Mariah Carey ajikuta katika
wakati mgumu na aibu ya aina yake baada ya viatu virefu maarufu kwa jina
la 'high heels' kumdodosha wakati akicheza shoo ya video ya nyimbo
inayojulikana kwa jina la 'Beautiful'
Viatu
virefu ni moja ya vitu ambavyo muimbaji huyo huvipenda lakini huenda
hatotaka tena kuvisikia kutokana na hali iliyompata kudondoshwa na viatu
hivyo na kumsababishia maumivu makali na hatimaye kukimbizwa hospitali .
Mtu
wakaribu wa mwanamuziki huyo aliiambiwa chanzo kimoja cha habari kuwa
ajali hiyo ilitokea wakati wa utengenezaji wa video ya remix ya
'Beautiful' iliyokuwa ikiongozwa na muwewake Nick Canno, ndipo muimbaji
huyo alidondoka na kusababisha maumivu ya bega.
Wakati
huo huo chanzo kingine kiliuambia mtandao wa New York Post kuwa ajali
hiyo ilitokana na viatu virefu alivyokuwa amevaa wakati anacheza video
hiyo.
HII NDIO TWEET YA AGNES MASOGANGE BAADA YA TAARIFA YA KUKAMATWA NA MADAWA YA KULEVYA

Katika
picha agnes masogange anaonekana akihesabu mihela yake na akatweet kuwa
" Anatafuta hela sio umbeya watu wasile bata mnazusha"
KAMATI KUU YA CHADEMA YABARIKI FUJO MIKUTANONI .... WAANDAA "RED BRIGADE"
MUHTASARI
Ili kukabiliana na vitendo vya fujo vinavyofanywa na vijana wa CCM dhidi ya wagombea, Wanachama na viongozi wa CHADEMA, Kamati Kuu imeagiza kwamba kitengo cha ulinzi cha Chama “Red Brigade” kiimarishwe zaidi kwa kuhakikisha kuwa vijana wote wa Red Brigade Nchi nzima wanapewa mafunzo maalum ya UKAKAMAVU yatakayoandaliwa katika Makambi maalum katika mikoa yote.
RIPOTI KAMILI
TAARIFA KWA UMMA
KUHUSU MAAMUZI YA KIKAO CHA KAMATI KUU YA CHAMA KILICHOFANYIKA TAREHE
06-07/07/2013 KATIKA HOTEL YA BLUE PEARL, DAR ES SALAAM.
Kamati kuu ya
Chama cha Demokrasia na Maendeleo ilikutana katika Kikao cha dharura kuanzia
tarehe 06-07/07/2013 katika Hotel ya Blue Pearl Dar es salaam kujadili pamoja na
mambo mengine Rasimu ya Katiba mpya na hali ya Siasa nchini.
Kamati kuu
imejadili na kuyatolea maamuzi mambo mbalimbali kama ifuatavyo:
1:0. Hali
ya Siasa Nchini.
Kamati kuu imepokea taarifa ya hali ya siasa nchini na
kuzingatia mambo yafuatayo:
a) Shambulio la Bomu Arusha.
Kamati
Kuu imesikitishwa na kulaani kwa nguvu zote tukio la Bomu Arusha lililosababisha
watu wanne kuuwawa na zaidi ya watu 70 wengine kujeruhiwa vibaya.
KASEJA ANAWINDWA KILA KONA, USIKU NA MCHANA

KLABU
za APR ya Rwanda na Gor Mahia ya Kenya zipo katika harakarti za kumwania
aliyekuwa kipa namba moja wa timu ya Simba, Juma Kaseja,
imefahamika.
Habari
za uhakika ambazo Sports Lady Blog imezinyaka zinasema viongozi wa timu
hizo wameshaanza mazungumzo na Kaseja ili kumsajili kwa msimu ujao katika nchi
hizo.
Mdau
mmoja wa soka ambaye yupo karibu na uongozi wa timu hizo, alidokeza jana kwamba,
kwa nyakati viongozi wa timu hizo mbili, wamekuwa kwenye harakati za kumsaka
Kaseja, wakiamini bado ni kipa mwenye uwezo mkubwa
langoni.
Licha
ya kutemwa kwenye kikosi cha Simba kwa msimu ujao, Kaseja bado kipa namba moja
wa timu ya soka ya Tanzania, Taifa Stars chini ya kocha wake Kim Poulsen, raia
wa Denmark.
Habari
zaidi zinasema, klabu ya APR iliyofika fainali ya Klabu Bingwa Afrika Mashabiki
na Kati-Kagame Cup na kufungwa na Vital’o wiki moja iliyopira nchini Sudan,
inapewa nafasi kubwa ya kumpata kipa huyo.
Hayo
yanatokea huku Kaseja akiwa kwenye kambi ya timu ya Stars inayojiandaa na mechi
ya kuwania tiketi ya Fainali za Afrika kwa Nyota wa Ndani –CHAN dhidi ya Uganda
itakayopigwa Julai 13, Uwanja wa Taifa Dar es
Salaam.
“Ujue
baada ya Simba kutangaza kuachana na Kaseja, kuna timu nyingi hasa za nje
zimeonesha nia ya kutaka kumsajili lakini mpaka sasa ni APR na Gor Mahia ndio
wako makini zaidi na mchakato huo,” kilisema chanzo hicho.
HUYU NDIE MWIGIZAJI WA HOLLYWOOD ALIYEMTUKANA OBAMA NA MKE WAKE
![]() |
Anaitwa
Amanda Bynes ni mwigizaji maarufu HoolyWood. Wiki chache zilizopita
alikua katika vita ya maneno na msanii Rihana kupitia mtandao wa
twitter, sasa vita hiyo kaihamishia kwa Raisi wa nchi yake Obama pamoja
na mke wake.
Katika tweet aliyoandika jana alisema “Barack Obama and Michelle Obama are Ugly” na mda mchache tu baada ya kuandika hivyo watu walianza kumshambulia kwa kumwambia kua alichofanya si kitu kizuri kabisa. Pia katika kuonyesha kua watu hawamungi mkono wengi wa followers wake walimunfollow.
Hii si mara yake ya kwanza kuwaita watu weusi ugly kwani alishawahi kumuita na Drake jina hilo
Katika tweet aliyoandika jana alisema “Barack Obama and Michelle Obama are Ugly” na mda mchache tu baada ya kuandika hivyo watu walianza kumshambulia kwa kumwambia kua alichofanya si kitu kizuri kabisa. Pia katika kuonyesha kua watu hawamungi mkono wengi wa followers wake walimunfollow.
Hii si mara yake ya kwanza kuwaita watu weusi ugly kwani alishawahi kumuita na Drake jina hilo
MWANAMKE APEWA MIMBA NA MAITI, ALIJIFANYISHA MAPENZI WAKATI ANAMUOGESHA.

Mwanamke
mmoja mhudumu wa chumba cha kuhifadhia maiti ameushangaza ulimwengu kwa
kitendo chake cha Kujilazimishia mapenzi kutoka kwa mwanaume ambaye
amekufa hadi kufikia kupata Ujauzito.
Felicity
Marmaduke (38), Mkazi wa Lexington Missouri, alikumbwa na mkasa huo
baada ya kumtamani marehemu huyo wakati wa kumuosha na ndipo alipoamua
kujiweka juu yake na kuanza kufanya naye mapenzi, cha kushangaza ni
kwamba maiti hiyo iliweza kutoa mbegu za kiume.
Baada ya wiki mbili, mwanamke huyo alienda kujipima ujauzito baada ya kujihisi tofauti na ndipo alipogundua ya kwamba ameshika mimba.
Baada ya wiki mbili, mwanamke huyo alienda kujipima ujauzito baada ya kujihisi tofauti na ndipo alipogundua ya kwamba ameshika mimba.
Ilimbidi
atoe taarifa kwa familia husika ambayo ilimfungulia mashataka kwa
kitendo chake hata hivyo naye amefungua mashtaka akidai iuzwe moja ya
nyumba ya marehemu huyo ili alipwe gharama za matunzo.
MCHUNGAJI AKAMATWA KWA KOSA LA KUUPINGA USHOGA NA USAGAJI.

Tonny
Miano ni Mchungaji kutoka nchini mMarekani ambaye alikwenda Nchini
Uingereza katika Kufanya Mahubiri Huko. Kilichomkuta kilisababishwa na
yeye kusema ya kwamba tabia za kishoga na kisagaji ni Dhambi na
hazimvutii Mungu,.
Polisi
walipigiwa simu na mwanamke mmoja aliyekuwa eneo la tukio akilalamika
ya kwamba hajafurahishwa na maneno anayoongea Tonny, ambaye ni askari
mstaafu wa jeshi la polisi nchini Marekani.
Tuesday, July 09, 2013
MBONA MAJANGAAA....!!! AGNESS MASOGANGE AKAMATWA NA MADAWA YA KULEVYA AFRIKA KUSINI
HATIMAYE wale Wanawake wawili walionaswa na madawa ya kulevya Afrika kusini wametambuliwa kuwa ni mabinti wa KITANZANIA ..
Mabinti
hao wanadaiwa kuingiza shehena ya dawa za kulevya zenye thamani ya
zaidi ya Sh. bilioni 6.8 nchini Afrika Kusini wakitokea Tanzania.
Akizungumza
na mwandishi wetu jana, Kamanda wa Polisi Kitengo cha Kuzuia na
Kupambana na Dawa za Kulevya, Geofrey Nzoa, alisema haijafahamika
wanawake hao wanatoka mikoa gani.
Kamanda
Nzoa aliwataja wanawake hao kuwa ni Agnes Jerald (MASOGANGE) ambaye
alisema hajapiga hesabu ya umri wao, ila alizaliwa mwaka 1988 kwa maana
hiyo ana umri wa miaka 25 na Melisa Edward ambaye alisema amezaliwa
mwaka 1989 kwa maana hiyo atakuwa na umri wa miaka 24. Wawili hao bado
wanaendelea kuhojiwa na polisi wa Afrika Kusini.
CHELSEA WAANDAA DAU LA JUU ZAIDI KUMSAJILI ROONEY....!!!
WAKATI MZEE MANDELA AKIENDELEA KUPATA MATIBABU FAMILIA YAKE WAZIDI KUTIBUANA

Mandla Mandela aendelea kulikoroga
WAKATI
mgogoro kati ya watoto wa Mandela na wajukuu ukizidi kutokota kuhusu
uhalali wa uchifu wa Mandla Mandela, yeye amejibu mapigo akisema Mfalme
Buyelekhaya Dalindyebo wa kabila la abaThembu ”hana akili timamu”.
Hiyo
inatokana na madai yaliyotolewa na mfalme huyo kwamba Mandla hakuwa
chifu sahihi wa ukoo wa Madiba. Alidai kwamba hakukuwa na cheti chochote
halali kilichotiwa saini wakati mandla alipotawazwa kuwa chifu mwaka
2007 – sherehe ambazo zilisimamiwa na Mandela mwenyewe.
Gazeti
la Mail & Guardian wiki iliyopita liliripoti kuwa uchifu wa Mandla
ulilalamikiwa kabla ya Mandela kulazwa hospitalini, ikielezwa kama kweli
anafaa kuendelea kuwa chofu ikizingatiwa kuwa mama na baba yake
walimzaa bila kuoana.
Mgogoro
unaoendelea hivi sasa kati ya Manla na shangazio yake, Makaziwe
Mandela, na wanafamilia wengine unaonekana kama kichocheo kwa baadhi ya
wanafamilia hiyo ambao wangetaka Mandla avuliwe uchifu.
WEMA SEPETU ANASAKWA NA POLISI BAADA YA KUMTUKANA MENEJA WA HOTELI WAKATI YUKO POMBE...!!!

Msanii
wa filamu za Bongo ambaye pia ni Miss Tanzania 2006, Wema Sepetu
anasakwa na Jeshi la Polisi Kituo cha Kawe, Dar es Salaam kwa tuhuma za
kufanya fujo hotelini, kumtukana matusi ya nguoni na kumpiga makofi
meneja wa hoteli hiyo, Godluck Kuyumbu. Songombingo hilo lilijiri saa
tano usiku wa Jumatano iliyopita kwenye hoteli hiyo iliyopo Kawe Beach,
jijini Dar.
Akizungumza
na mwandishi wetu , meneja huyo alisema siku ya tukio majira ya saa
nane mchana, Wema alifika kwenye mgahawa wa hoteli hiyo akiwa
ameongozana na marafiki zake wapatao kumi.
Meneja
huyo akaendelea kusema, ilipofika saa tano usiku, Wema na marafiki
zake walionekana kuzidiwa na kilevi, wakaanza kufanya fujo kwa kupiga
kelele, kitendo kilichowakera wateja waliokuwa katika mgahawa huo, wengi wakiwa ni Wazungu ambao waliondoka kutokana na fujo hizo.
Aliongeza
kuwa mmoja wa marafiki wa Wema ambaye ilidaiwa ni mpenzi wake,
aliyejulikana kwa jina moja la D, alichukua glasi na kuipasua chini kwa
makusudi huku meneja huyo akishuhudia.
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Akutana na Waandishi Wa Habari Nakutoa maamuzi ya Kamati ya Ushauri (RCC) ya kupeleka Makao makuu ya Mkoa mpya Mkwajuni Wilayani Chunya.
Mwenyekiti wa Kamati ya ulinzi na Usalama Mkoa wa Mbeya, Abbasi Kandoro ambaye pia ndiye Mkuu wa Mkoa Mbeya akiongea na vyombo vya habari ofisini kwake.
Baadhi
ya wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Mbeya
wakimsikiliza mkuu wa mkoa Mbeya akiongea na waandishi wa habari.Picha na Habari na Mdau Joseph Mwaisango
--
Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Mbeya
hatimaye yatoa ufafanuzi na kupigilia Msumari maamuzi ya Kamati ya Ushauri
(RCC) ya kupeleka Makao makuu ya Mkoa mpya Mkwajuni Wilayani Chunya.
"NGUVU YA UMMA" INAVYOGHARIMU UHAI WA WAMISRI...!!!

Miili ya wafuasi wa Rais aliyeondolewa madarakani nchini Misri ikiwa imehifadhiwa
MAAFISA wa Afya Misri wamesema takriban watu 42
wameuawa kwa kupigwa risasi mjini Cairo nje ya kambi ya kijeshi ambapo
wafuasi wa Rais aliyeondolewa madarakani Mohammed Morsi walikua
wamekusanyika na wanaamini anazuiliwa hapo. Watu wengine 300
wamejeruhiwa.
Kundi la Muslima Brotherhood limewataka raia wa Misri kuwapinga wale linawaita wanaopokonya raia uhuru na demokrasia.
Brotherhood imelaumu jeshi kwa kuwaua raia wake.
Katika kikao na waandishi wa habari, wafuasi hao walimlaani vikali mkuu wa jeshi Abdel Fattah Al-Sisi na kumtaja kama muuaji aliyewashambulia raia wenzake.
Haya yanajiri huku ghasia zikiendelea baada ya kuondolewa mamlakani kwa aliyekuwa rais Mohammed Morsi.
NDEGE YA RAIS WA SOMALIA 'YASHIKA MOTO'
Rais wa Somalia, Hassan Sheikh Mahamud
*******
NDEGE iliyokuwa inambeba rais wa
Somalia, imelazimika kutua kwa dharura mjini Mogadishu baada ya moja ya
mabawa yake kushika moto. (HM)Rais Hassan Sheikh Mohamud, alielezea kuwa rais hakujeruhiwa lakini wazima moto walifanya kila hali kuzima moto huo.
Bwana Mohamud alichaguliwa kama rais wa Somalia mwaka jana katika mpango ulioungwa mkono na Umoja wa Mataifa, katika hatua za kumaliza vita vya miaka mingi.
Mwandishi wa BBC Mohamed Mwalimu, alisema kuwa magurugumu ya ndege yaliharibiwa vibaya baada ya tukio hilo.
Rais alikuwa anaelekea katika mji mkuu wa Sudan Kusini, Juba, wakati ndege hiyo ilipolazimika kurejea Mogadishu.
Moja ya ripoti zilizotolewa za mwanzo kuhusu tukio hilo, ilitoka kwa akaunti ya Twitter ya kundi la al-Shabab lakini haikusema kama imeshambulia ndege hiyo.
Wanajeshi wa Muungano wa Afrika pamoja na wale wa Somalia, wanaounga mkono bwana Mohamud wamewaondoa wapiganaji wa al-Shabab kutoka mji mkuu Mogadishu, mwaka jana ingawa kundi hilo bado hufanya mashambulizi ya mara kwa mara ya kuvizia.
Serikali mpya ni ya kwanza kwa zaidi ya miaka 10 kutambuliwa na serikali ya Marekani na shirika la fedha duniani (IMF).
Chanzo: bbcswahili
Monday, July 08, 2013
RAIS WA ZANZIBAR DK. ALI MOHAMED SHEIN AWAASA WAISLAMU NCHINI
Rais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein amewataka Waislamu wote nchini kuishi na Watanzania wenzao katika misingi ya kuheshimiana, kuvumiliana na kupendana, kama Uislamu ulivyofundisha.
Dk
Shein aliyasema hayo jana katika ufunguzi wa msikiti wa Masjid Taqwa,
uliopo Ilala Bungoni, jijini Dar es Salaam, katika hotuba ilyosomwa kwa
niaba yake na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi, Dk Mwinyihaji MakameKatika hotuba hiyo ya ufunguzi wa msikiti
huo, Dk Shein alisema kuwa ni wajibu kwa Waislamu kufanya kila jitihada
katika kuilinda amani na utulivu alioubariki Mwenyezi Mungu hapa
Tanzania.
Alisema kuwa kuna kila sababu kwa Waislamu kumshukuru Mwenyezi Mungu kwamba wanaweza kufanya ibada zao katika mkusanyiko mkubwa kama huo wa ufunguzi wa msikiti bila ya hofu, woga wala bughudha ya namna yoyote.Dk Shein alipongeza jitihada zinazochukuliwa na wasimamizi wa msikiti huo katika kuimarisha na kuitunza historia yake tangu ulipoanzishwa mnamo mwaka 1927, ambapo historia hiyo inadhihirisha kuwa msikiti huo ni miongoni mwa misikiti mikongwe katika Jiji la Dar es Salaam.
Alisema kuwa kuna kila sababu kwa Waislamu kumshukuru Mwenyezi Mungu kwamba wanaweza kufanya ibada zao katika mkusanyiko mkubwa kama huo wa ufunguzi wa msikiti bila ya hofu, woga wala bughudha ya namna yoyote.Dk Shein alipongeza jitihada zinazochukuliwa na wasimamizi wa msikiti huo katika kuimarisha na kuitunza historia yake tangu ulipoanzishwa mnamo mwaka 1927, ambapo historia hiyo inadhihirisha kuwa msikiti huo ni miongoni mwa misikiti mikongwe katika Jiji la Dar es Salaam.
MKE WA RAIS MSTAAFU BENJAMIN MKAPA, MAMA ANNA MKAPA AMETENGWA...!!!

MAMA ANNA MKAPA.
MKUTANO
wa wake za marais uliofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam na
kuhudhuriwa na viongozi wazito, akiwemo Rais wa zamani wa Marekani,
George W. Bush na Mkewe, Laura, umeacha kitendawili kizito kuhusu mke wa
Rais wa zamani, Benjamin Mkapa, Mama Anna Mkapa. Imebainika kuwa katika
mkutano huo, ambao mke wa Rais Jakaya Kikwete, Salma alikuwa ni
mwenyeji wao, Mama Anna Mkapa hakuhudhuria, lakini pia imeonyesha wazi
kwamba hakupewa fursa kulingana na hadhi yake.
Mkutano
huo wa Kimataifa ulifanyika katika Hoteli ya Serena, jijini Dar es
Salaam, Juni 2-3 mwaka huu, uliozungumzia nafasi ya wanawake kuinuka
kimaendeleo, ukizihusisha taasisi zinazoendeshwa na wake wa marais,
wakiwemo wale wastaafu.
HAKEEM NA FATIMA WAAGA SHINDANO LA BBA USIKU WA LEO; MWANAMZIKI WA KIBONGO ATUMBUIZA

Ikiwa
leo ni siku ya 42 ndani ya jumba la BBA,kama inavyokuwaga siku zote
kila jumapili huwa ni eviction day yaan lazma mshirik hata mmoja aage
mashindano
Mwanadada
Fatima kutoka Malawi ndiye aliyekuwa wa kwanza kuaga mashindano ya BBA
kwa usiku wa leo.Mshiriki mwenzake kutoka Malawi Natasha hakuamini
kilichotea na kuanza kulia huku Fatima akimwambia Natasha "No drama, no
drama. It's not about you, chill out "kasha akaagana na wenziwe na
kutoka nje ya jumba la BBA.
.Usiku wa leo ndania ya BBA ulipambwa na msanii mahiri kutoka TANZANIA aitwaye WAKAZI aliyeimba nyimbo zake WEEKEND na TOUCH.
HIZI NDIYO SABABU ZA MH ZITTO KABWE KUTOSHIRIKI TAMASHA LA MATUMAINI
Kupitia account yake ya facebook Mh. Zitto Kabwe amepost hotuba hii akielezea kushindwa kwake kufika katika tamasha la siku ya matumaini.
POST YAKE AMEANZA KWA KUANDIKA HIVI.
Global Publishers leo 7.7.2013 waliandaa Tamasha la Matumaini. Bahati mbaya sana sikuweza kuwahi kutokana na safari nilizonazo. Hii ni hotuba niliyopanga kuitoa na kuwatumia waandaaji.
TAMASHA LA MATUMAINI
Leo nilikuwa niwe nanyi kwa ajili ya siku hii muhimu sana kwa nchi yetu, siku ya matumaini kama inavyoandaliwa na Kampuni ya Global Publishers. Napenda kutoa shukrani zangu za dhati kabisa kwa ndugu yangu Erick Shigongo kwa kuandaa tamasha hili kila mwaka. Nasikitika kuwa sitaweza kufanya pambano la ngumi na ndugu Ray na pia kuchezea timu yangu ya Wabunge wa Simba dhidi ya watani zetu Yanga. Hata hivyo naamini kuwa tamasha litakuwa na mafanikio makubwa na nipo nanyi japo sipo Dar es Salaam.
Ilikuwa niwepo Dar es Salaam leo, lakini nimeshindwa kuondoka Marekani kwa sababu Spika wa Bunge Mama Anna Makinda ameniagiza kwenye safari nyingine ndefu kwenda visiwa vya Cayman na baadaye Namibia kwa shughuli za Umoja wa Wabunge wa Jumuiya ya Madola. Sikuweza kukwepa jukumu hili la kitaifa maana limekuja ghafla na mimi nipo huku jirani na maeneo hayo. Naomba radhi sana kwamba sipo nanyi leo.
Sunday, July 07, 2013
BABU CHA MIAKA 92 AFUNGA NDOA NA BINTI ALIYEMZIDI MIAKA 70...!!!
Musali Mohammed al-Mujamaie (kulia) akiwa na mkewe, Muna Mukhlif al-Juburi. |
Mkulima
mmoja nchini Irak mwenye miaka 92 amemuoa mwanamke waliyetofautiana
miaka 70 katika ndoa tatu kwa mpigo sambamba na wajukuu zake wa kiume
wawili.
Musali
Mohammed al-Mujamaie alimuoa mke mwenye umri wa miaka 22, Muna Mukhlif
al-Juburi katika sherehe iliyodumu kwa masaa manne.
Wajukuu
zake wa kiume, wenye umri wa miaka 16 na 17, nao walifunga ndoa kwenye
sherehe hiyo iliyofanyika kaskazini mwa Baghdad Alhamisi iliyopita, kwa
mujibu wa ripoti.
Mzee Mujamaie alisema kwenye
siku hiyo maalum alikuwa akisubiria kwa muda mrefu kutokana na harusi za
wajukuu zake kuwa zinaahirishwa mara kadhaa ili aweze kuunganisha na
sherehe yake.
TBS YAPIGA MARUFUKU UUZWAJI WA MAFUTA YA KUPIKIA YA 'OKI'.....WADAI YANA MADHARA KIAFYA.
Shirika la Viwango Tanzania (TBS), limebaini kuwa mafuta ya kula aina ya Oki na Viking yaliyoenea sokoni nchini, yamebainika kuwa hayafai kwa matumizi ya binadamu.
Kwa
mujibu wa TBS, vipimo vyote vitatu vilivyotumika kuyapima kuonyesha
ubora, vimefeli na vimeonyesha mafuta hayo kuharibika kwa haraka tangu
yalipotengenezwa na mpaka leo.
Pamoja
na Oki, mafuta mengine yenye walakini ni Asma, Vikingi, Partiner na
Premier Gold ambayo huuzwa kwa dumu lenye ujazo wa lita 20 kwa bei ya
kuanzia Sh 38,000 hadi 45,000, wakati bei ya mafuta ya kula
yanayotengenezwa nchini kwa ujazo huo huuzwa kati ya Sh. 52,000 na
Sh.55,000.
Baada
ya kupimwa, Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Udhibiti Ubora TBS, Lazaro
Msasalaga, anasema ilithibitika kuwa mafuta ya Oki yanayozalishwa
Malaysia na kupakiwa Singapore hayana ubora.
Alisema
mafuta hayo yametengenezwa 2011 na kuonyesha mwisho wa kutumika ni
Oktoba mwaka huu. Msasalaga alisema walipoyachunguza wamebaini hayana
namba ya ufuatiliaji wakati suala hilo ni la muhimu kuwekwa.
Isitoshe,
wawalipoyapima kutoka kipimo kimoja kwenda kingine, majibu yake
yalishindwa na kuzidi kuonyesha mafuta hayo kuharibika kila
walipoyapima.
Alisema kuna vipimo vya maabara ukipima vinaeleza mafuta kama yanafaa kutumika lakini kipimo hicho hakikufanikiwa.NA TALK BONGO
LUCY KOMBA NA IRENE UWOYA NDANI YA BIFU ZITO, KISA NDIKUMANA...!!!
MWANAFUNZI na mwalimu wake katika
sanaa, Irene Uwoya na Lucy Komba wameingia katika bifu zito chanzo
kikidaiwa kuwa ni mwalimu huyo kumzunguka mwanafunzi wake kwa mumewe,
Hamad Ndikumana ‘Katauti’. Lucy ambaye ndiye mwalimu wa Uwoya kisanaa,
imedaiwa kuwa amemzunguka Uwoya kwa mumewe, Ndiku kwa kisingizio cha
kucheza naye filamu iliyofahamika kwa jina la Kwa nini Nisimuoe?
“Kimenuka! Lucy Komba amemhadaa Ndiku, akazuga kuigiza naye filamu moja ndipo walipozama kwenye ukaribu kwelikweli.
“Mbaya zaidi filamu yenyewe wameigiza
wahusika wawili tu (Lucy na Ndiku) mwanzo mwisho kule Tegeta. Sasa wewe
unafikiri kuna nini hapo kama siyo mapenzi?’’ kilihoji chanzo hicho
makini.
Baada ya paparazi wetu kuyanasa madai
hayo, Jumatano iliyopita alimtafuta Uwoya kwa njia ya simu ambapo
alipopewa taarifa hizo, alionesha kushtuka na kuchanganyikiwa mumewe
kuigiza filamu moja na Lucy, alikata simu kisha baadaye akampigia
paparazi yeye.
“Kuna wakati nilikuwa namtafuta Ndiku
sijui alipo kumbe alikuwa na Lucy, sawa lakini kama Lucy ameamua
kunifundisha mimi na sasa amemfundisha mume wangu sawa, tupo hapa!”
Paparazi wetu alihamishia majeshi kwa kumtwangia ‘mtuhumiwa’, Lucy ambaye alitiririka kama ifuatavyo:
“Nilijua Uwoya akisikia itakuwa ni
balaa maana siku za nyuma niliwahi kumshutumu kutoka na mzazi mwenzangu
(Patrick Mbasha) lakini mimi nipo tayari kwa lolote!”
Lucy Komba ndiye aliyemuingiza Uwoya
kwenye sanaa baada ya kumchezesha Filamu ya Yolanda ambayo ndiyo
iliyomtambulisha vyema staa huyo kisha kuliteka soko la sinema Bongo.
SERIKALI YA AFRIKA YA KUSINI YAKANA MZEE NELSON MANDELA KUWA HANA FAHAMU
SERIKALI ya Afrika Kusini imekanusha taarifa kuwa rais wa zamani wa nchi
hiyo, Nelson Mandela, hana fahamu zake tena kama inavyoelezwa katika
nyaraka za mahakama zilizowasilishwa mnamo 26.06.2013.
Zuma alisema jana mchana baada ya kumtembelea hospitalini kuwa Madiba anapewa matibabu ya hali ya juu na timu ya madaktari bingwa waliobobea katika taaluma ya utabibu, ambao wako kando ya kitanda chake hospitalini kila wakati.
Nyaraka za mahakama zilizopatikana na shirika la habari la AFP zinaonyesha madaktari wanaomtibu Mandela walisema hana fahamu na kuishauri familia wiki moja iliyopita iruhusu mashine zinazomsaidia kuishi zizimwe ili apumzike.
MFANYABIASHARA MWENYE ASILI YA KIARABU MBARONI KWA KUMBAKA TAHIRA
Na Cresensia Kapinga,Songea.
JESHI la polisi mkoani Ruvuma linamshikiria mfanyabiashara mmoja Jamali Nassoro (67) mwenye asili ya kiarabu mkazi wa eneo la Making'inda katika manispaa ya Songea kwa tuhuma za kumbaka na kumsababishia ujauzito wa mimba ya miezi 5 msichana mwenye umri wa miaka 27 ambaye anadaiwa kuwa na ugonjwa wa utindio wa ubongo(TAILA) ambaye jina lake tunalo limehifadhiwa.
Akizungumza
na waandishi wa habari jana Kaimu kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma
George Chiposi alisema kuwa tukio hilo la kukamatwa kwa mfanyabiashara
huyo mwenye asili ya kiarabu limetokea hivi karibuni baada ya wazazi wa
msichana kubaini kuwa mtoto wao yupo tofauti kimaumbile na kuchukuwa
jukumu la kwenda kumpima ambako vipimo vilionesha kuwa ni mjamzito wa
miezi 5.
Chiposi
alisema kuwa wazazi wa msichana huyo baada ya kubaini mtoto wao ni
mjamzito walimuhoji ili kujuwa ni nani aliyemfanyia unyama huo ambapo
licha ya kuwa msichana huyo ni tahira alieleza kwa shida kuwa alikamatwa
kwa nguvu na kulazimishwa kutoa nguo yake ya ndani na Nassoro ambaye
alimtaka ampelekee maji ya kuoga chumbani kwake.
Subscribe to:
Comments (Atom)





