Tuesday, July 09, 2013
CHELSEA WAANDAA DAU LA JUU ZAIDI KUMSAJILI ROONEY....!!!
WAKATI MZEE MANDELA AKIENDELEA KUPATA MATIBABU FAMILIA YAKE WAZIDI KUTIBUANA

Mandla Mandela aendelea kulikoroga
WAKATI
mgogoro kati ya watoto wa Mandela na wajukuu ukizidi kutokota kuhusu
uhalali wa uchifu wa Mandla Mandela, yeye amejibu mapigo akisema Mfalme
Buyelekhaya Dalindyebo wa kabila la abaThembu ”hana akili timamu”.
Hiyo
inatokana na madai yaliyotolewa na mfalme huyo kwamba Mandla hakuwa
chifu sahihi wa ukoo wa Madiba. Alidai kwamba hakukuwa na cheti chochote
halali kilichotiwa saini wakati mandla alipotawazwa kuwa chifu mwaka
2007 – sherehe ambazo zilisimamiwa na Mandela mwenyewe.
Gazeti
la Mail & Guardian wiki iliyopita liliripoti kuwa uchifu wa Mandla
ulilalamikiwa kabla ya Mandela kulazwa hospitalini, ikielezwa kama kweli
anafaa kuendelea kuwa chofu ikizingatiwa kuwa mama na baba yake
walimzaa bila kuoana.
Mgogoro
unaoendelea hivi sasa kati ya Manla na shangazio yake, Makaziwe
Mandela, na wanafamilia wengine unaonekana kama kichocheo kwa baadhi ya
wanafamilia hiyo ambao wangetaka Mandla avuliwe uchifu.
WEMA SEPETU ANASAKWA NA POLISI BAADA YA KUMTUKANA MENEJA WA HOTELI WAKATI YUKO POMBE...!!!

Msanii
wa filamu za Bongo ambaye pia ni Miss Tanzania 2006, Wema Sepetu
anasakwa na Jeshi la Polisi Kituo cha Kawe, Dar es Salaam kwa tuhuma za
kufanya fujo hotelini, kumtukana matusi ya nguoni na kumpiga makofi
meneja wa hoteli hiyo, Godluck Kuyumbu. Songombingo hilo lilijiri saa
tano usiku wa Jumatano iliyopita kwenye hoteli hiyo iliyopo Kawe Beach,
jijini Dar.
Akizungumza
na mwandishi wetu , meneja huyo alisema siku ya tukio majira ya saa
nane mchana, Wema alifika kwenye mgahawa wa hoteli hiyo akiwa
ameongozana na marafiki zake wapatao kumi.
Meneja
huyo akaendelea kusema, ilipofika saa tano usiku, Wema na marafiki
zake walionekana kuzidiwa na kilevi, wakaanza kufanya fujo kwa kupiga
kelele, kitendo kilichowakera wateja waliokuwa katika mgahawa huo, wengi wakiwa ni Wazungu ambao waliondoka kutokana na fujo hizo.
Aliongeza
kuwa mmoja wa marafiki wa Wema ambaye ilidaiwa ni mpenzi wake,
aliyejulikana kwa jina moja la D, alichukua glasi na kuipasua chini kwa
makusudi huku meneja huyo akishuhudia.
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Akutana na Waandishi Wa Habari Nakutoa maamuzi ya Kamati ya Ushauri (RCC) ya kupeleka Makao makuu ya Mkoa mpya Mkwajuni Wilayani Chunya.
Mwenyekiti wa Kamati ya ulinzi na Usalama Mkoa wa Mbeya, Abbasi Kandoro ambaye pia ndiye Mkuu wa Mkoa Mbeya akiongea na vyombo vya habari ofisini kwake.
Baadhi
ya wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Mbeya
wakimsikiliza mkuu wa mkoa Mbeya akiongea na waandishi wa habari.Picha na Habari na Mdau Joseph Mwaisango
--
Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Mbeya
hatimaye yatoa ufafanuzi na kupigilia Msumari maamuzi ya Kamati ya Ushauri
(RCC) ya kupeleka Makao makuu ya Mkoa mpya Mkwajuni Wilayani Chunya.
"NGUVU YA UMMA" INAVYOGHARIMU UHAI WA WAMISRI...!!!

Miili ya wafuasi wa Rais aliyeondolewa madarakani nchini Misri ikiwa imehifadhiwa
MAAFISA wa Afya Misri wamesema takriban watu 42
wameuawa kwa kupigwa risasi mjini Cairo nje ya kambi ya kijeshi ambapo
wafuasi wa Rais aliyeondolewa madarakani Mohammed Morsi walikua
wamekusanyika na wanaamini anazuiliwa hapo. Watu wengine 300
wamejeruhiwa.
Kundi la Muslima Brotherhood limewataka raia wa Misri kuwapinga wale linawaita wanaopokonya raia uhuru na demokrasia.
Brotherhood imelaumu jeshi kwa kuwaua raia wake.
Katika kikao na waandishi wa habari, wafuasi hao walimlaani vikali mkuu wa jeshi Abdel Fattah Al-Sisi na kumtaja kama muuaji aliyewashambulia raia wenzake.
Haya yanajiri huku ghasia zikiendelea baada ya kuondolewa mamlakani kwa aliyekuwa rais Mohammed Morsi.
NDEGE YA RAIS WA SOMALIA 'YASHIKA MOTO'
Rais wa Somalia, Hassan Sheikh Mahamud
*******
NDEGE iliyokuwa inambeba rais wa
Somalia, imelazimika kutua kwa dharura mjini Mogadishu baada ya moja ya
mabawa yake kushika moto. (HM)Rais Hassan Sheikh Mohamud, alielezea kuwa rais hakujeruhiwa lakini wazima moto walifanya kila hali kuzima moto huo.
Bwana Mohamud alichaguliwa kama rais wa Somalia mwaka jana katika mpango ulioungwa mkono na Umoja wa Mataifa, katika hatua za kumaliza vita vya miaka mingi.
Mwandishi wa BBC Mohamed Mwalimu, alisema kuwa magurugumu ya ndege yaliharibiwa vibaya baada ya tukio hilo.
Rais alikuwa anaelekea katika mji mkuu wa Sudan Kusini, Juba, wakati ndege hiyo ilipolazimika kurejea Mogadishu.
Moja ya ripoti zilizotolewa za mwanzo kuhusu tukio hilo, ilitoka kwa akaunti ya Twitter ya kundi la al-Shabab lakini haikusema kama imeshambulia ndege hiyo.
Wanajeshi wa Muungano wa Afrika pamoja na wale wa Somalia, wanaounga mkono bwana Mohamud wamewaondoa wapiganaji wa al-Shabab kutoka mji mkuu Mogadishu, mwaka jana ingawa kundi hilo bado hufanya mashambulizi ya mara kwa mara ya kuvizia.
Serikali mpya ni ya kwanza kwa zaidi ya miaka 10 kutambuliwa na serikali ya Marekani na shirika la fedha duniani (IMF).
Chanzo: bbcswahili
Monday, July 08, 2013
RAIS WA ZANZIBAR DK. ALI MOHAMED SHEIN AWAASA WAISLAMU NCHINI
Rais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein amewataka Waislamu wote nchini kuishi na Watanzania wenzao katika misingi ya kuheshimiana, kuvumiliana na kupendana, kama Uislamu ulivyofundisha.
Dk
Shein aliyasema hayo jana katika ufunguzi wa msikiti wa Masjid Taqwa,
uliopo Ilala Bungoni, jijini Dar es Salaam, katika hotuba ilyosomwa kwa
niaba yake na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi, Dk Mwinyihaji MakameKatika hotuba hiyo ya ufunguzi wa msikiti
huo, Dk Shein alisema kuwa ni wajibu kwa Waislamu kufanya kila jitihada
katika kuilinda amani na utulivu alioubariki Mwenyezi Mungu hapa
Tanzania.
Alisema kuwa kuna kila sababu kwa Waislamu kumshukuru Mwenyezi Mungu kwamba wanaweza kufanya ibada zao katika mkusanyiko mkubwa kama huo wa ufunguzi wa msikiti bila ya hofu, woga wala bughudha ya namna yoyote.Dk Shein alipongeza jitihada zinazochukuliwa na wasimamizi wa msikiti huo katika kuimarisha na kuitunza historia yake tangu ulipoanzishwa mnamo mwaka 1927, ambapo historia hiyo inadhihirisha kuwa msikiti huo ni miongoni mwa misikiti mikongwe katika Jiji la Dar es Salaam.
Alisema kuwa kuna kila sababu kwa Waislamu kumshukuru Mwenyezi Mungu kwamba wanaweza kufanya ibada zao katika mkusanyiko mkubwa kama huo wa ufunguzi wa msikiti bila ya hofu, woga wala bughudha ya namna yoyote.Dk Shein alipongeza jitihada zinazochukuliwa na wasimamizi wa msikiti huo katika kuimarisha na kuitunza historia yake tangu ulipoanzishwa mnamo mwaka 1927, ambapo historia hiyo inadhihirisha kuwa msikiti huo ni miongoni mwa misikiti mikongwe katika Jiji la Dar es Salaam.
MKE WA RAIS MSTAAFU BENJAMIN MKAPA, MAMA ANNA MKAPA AMETENGWA...!!!

MAMA ANNA MKAPA.
MKUTANO
wa wake za marais uliofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam na
kuhudhuriwa na viongozi wazito, akiwemo Rais wa zamani wa Marekani,
George W. Bush na Mkewe, Laura, umeacha kitendawili kizito kuhusu mke wa
Rais wa zamani, Benjamin Mkapa, Mama Anna Mkapa. Imebainika kuwa katika
mkutano huo, ambao mke wa Rais Jakaya Kikwete, Salma alikuwa ni
mwenyeji wao, Mama Anna Mkapa hakuhudhuria, lakini pia imeonyesha wazi
kwamba hakupewa fursa kulingana na hadhi yake.
Mkutano
huo wa Kimataifa ulifanyika katika Hoteli ya Serena, jijini Dar es
Salaam, Juni 2-3 mwaka huu, uliozungumzia nafasi ya wanawake kuinuka
kimaendeleo, ukizihusisha taasisi zinazoendeshwa na wake wa marais,
wakiwemo wale wastaafu.
HAKEEM NA FATIMA WAAGA SHINDANO LA BBA USIKU WA LEO; MWANAMZIKI WA KIBONGO ATUMBUIZA

Ikiwa
leo ni siku ya 42 ndani ya jumba la BBA,kama inavyokuwaga siku zote
kila jumapili huwa ni eviction day yaan lazma mshirik hata mmoja aage
mashindano
Mwanadada
Fatima kutoka Malawi ndiye aliyekuwa wa kwanza kuaga mashindano ya BBA
kwa usiku wa leo.Mshiriki mwenzake kutoka Malawi Natasha hakuamini
kilichotea na kuanza kulia huku Fatima akimwambia Natasha "No drama, no
drama. It's not about you, chill out "kasha akaagana na wenziwe na
kutoka nje ya jumba la BBA.
.Usiku wa leo ndania ya BBA ulipambwa na msanii mahiri kutoka TANZANIA aitwaye WAKAZI aliyeimba nyimbo zake WEEKEND na TOUCH.
HIZI NDIYO SABABU ZA MH ZITTO KABWE KUTOSHIRIKI TAMASHA LA MATUMAINI
Kupitia account yake ya facebook Mh. Zitto Kabwe amepost hotuba hii akielezea kushindwa kwake kufika katika tamasha la siku ya matumaini.
POST YAKE AMEANZA KWA KUANDIKA HIVI.
Global Publishers leo 7.7.2013 waliandaa Tamasha la Matumaini. Bahati mbaya sana sikuweza kuwahi kutokana na safari nilizonazo. Hii ni hotuba niliyopanga kuitoa na kuwatumia waandaaji.
TAMASHA LA MATUMAINI
Leo nilikuwa niwe nanyi kwa ajili ya siku hii muhimu sana kwa nchi yetu, siku ya matumaini kama inavyoandaliwa na Kampuni ya Global Publishers. Napenda kutoa shukrani zangu za dhati kabisa kwa ndugu yangu Erick Shigongo kwa kuandaa tamasha hili kila mwaka. Nasikitika kuwa sitaweza kufanya pambano la ngumi na ndugu Ray na pia kuchezea timu yangu ya Wabunge wa Simba dhidi ya watani zetu Yanga. Hata hivyo naamini kuwa tamasha litakuwa na mafanikio makubwa na nipo nanyi japo sipo Dar es Salaam.
Ilikuwa niwepo Dar es Salaam leo, lakini nimeshindwa kuondoka Marekani kwa sababu Spika wa Bunge Mama Anna Makinda ameniagiza kwenye safari nyingine ndefu kwenda visiwa vya Cayman na baadaye Namibia kwa shughuli za Umoja wa Wabunge wa Jumuiya ya Madola. Sikuweza kukwepa jukumu hili la kitaifa maana limekuja ghafla na mimi nipo huku jirani na maeneo hayo. Naomba radhi sana kwamba sipo nanyi leo.
Sunday, July 07, 2013
BABU CHA MIAKA 92 AFUNGA NDOA NA BINTI ALIYEMZIDI MIAKA 70...!!!
Musali Mohammed al-Mujamaie (kulia) akiwa na mkewe, Muna Mukhlif al-Juburi. |
Mkulima
mmoja nchini Irak mwenye miaka 92 amemuoa mwanamke waliyetofautiana
miaka 70 katika ndoa tatu kwa mpigo sambamba na wajukuu zake wa kiume
wawili.
Musali
Mohammed al-Mujamaie alimuoa mke mwenye umri wa miaka 22, Muna Mukhlif
al-Juburi katika sherehe iliyodumu kwa masaa manne.
Wajukuu
zake wa kiume, wenye umri wa miaka 16 na 17, nao walifunga ndoa kwenye
sherehe hiyo iliyofanyika kaskazini mwa Baghdad Alhamisi iliyopita, kwa
mujibu wa ripoti.
Mzee Mujamaie alisema kwenye
siku hiyo maalum alikuwa akisubiria kwa muda mrefu kutokana na harusi za
wajukuu zake kuwa zinaahirishwa mara kadhaa ili aweze kuunganisha na
sherehe yake.
TBS YAPIGA MARUFUKU UUZWAJI WA MAFUTA YA KUPIKIA YA 'OKI'.....WADAI YANA MADHARA KIAFYA.
Shirika la Viwango Tanzania (TBS), limebaini kuwa mafuta ya kula aina ya Oki na Viking yaliyoenea sokoni nchini, yamebainika kuwa hayafai kwa matumizi ya binadamu.
Kwa
mujibu wa TBS, vipimo vyote vitatu vilivyotumika kuyapima kuonyesha
ubora, vimefeli na vimeonyesha mafuta hayo kuharibika kwa haraka tangu
yalipotengenezwa na mpaka leo.
Pamoja
na Oki, mafuta mengine yenye walakini ni Asma, Vikingi, Partiner na
Premier Gold ambayo huuzwa kwa dumu lenye ujazo wa lita 20 kwa bei ya
kuanzia Sh 38,000 hadi 45,000, wakati bei ya mafuta ya kula
yanayotengenezwa nchini kwa ujazo huo huuzwa kati ya Sh. 52,000 na
Sh.55,000.
Baada
ya kupimwa, Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Udhibiti Ubora TBS, Lazaro
Msasalaga, anasema ilithibitika kuwa mafuta ya Oki yanayozalishwa
Malaysia na kupakiwa Singapore hayana ubora.
Alisema
mafuta hayo yametengenezwa 2011 na kuonyesha mwisho wa kutumika ni
Oktoba mwaka huu. Msasalaga alisema walipoyachunguza wamebaini hayana
namba ya ufuatiliaji wakati suala hilo ni la muhimu kuwekwa.
Isitoshe,
wawalipoyapima kutoka kipimo kimoja kwenda kingine, majibu yake
yalishindwa na kuzidi kuonyesha mafuta hayo kuharibika kila
walipoyapima.
Alisema kuna vipimo vya maabara ukipima vinaeleza mafuta kama yanafaa kutumika lakini kipimo hicho hakikufanikiwa.NA TALK BONGO
LUCY KOMBA NA IRENE UWOYA NDANI YA BIFU ZITO, KISA NDIKUMANA...!!!
MWANAFUNZI na mwalimu wake katika
sanaa, Irene Uwoya na Lucy Komba wameingia katika bifu zito chanzo
kikidaiwa kuwa ni mwalimu huyo kumzunguka mwanafunzi wake kwa mumewe,
Hamad Ndikumana ‘Katauti’. Lucy ambaye ndiye mwalimu wa Uwoya kisanaa,
imedaiwa kuwa amemzunguka Uwoya kwa mumewe, Ndiku kwa kisingizio cha
kucheza naye filamu iliyofahamika kwa jina la Kwa nini Nisimuoe?
“Kimenuka! Lucy Komba amemhadaa Ndiku, akazuga kuigiza naye filamu moja ndipo walipozama kwenye ukaribu kwelikweli.
“Mbaya zaidi filamu yenyewe wameigiza
wahusika wawili tu (Lucy na Ndiku) mwanzo mwisho kule Tegeta. Sasa wewe
unafikiri kuna nini hapo kama siyo mapenzi?’’ kilihoji chanzo hicho
makini.
Baada ya paparazi wetu kuyanasa madai
hayo, Jumatano iliyopita alimtafuta Uwoya kwa njia ya simu ambapo
alipopewa taarifa hizo, alionesha kushtuka na kuchanganyikiwa mumewe
kuigiza filamu moja na Lucy, alikata simu kisha baadaye akampigia
paparazi yeye.
“Kuna wakati nilikuwa namtafuta Ndiku
sijui alipo kumbe alikuwa na Lucy, sawa lakini kama Lucy ameamua
kunifundisha mimi na sasa amemfundisha mume wangu sawa, tupo hapa!”
Paparazi wetu alihamishia majeshi kwa kumtwangia ‘mtuhumiwa’, Lucy ambaye alitiririka kama ifuatavyo:
“Nilijua Uwoya akisikia itakuwa ni
balaa maana siku za nyuma niliwahi kumshutumu kutoka na mzazi mwenzangu
(Patrick Mbasha) lakini mimi nipo tayari kwa lolote!”
Lucy Komba ndiye aliyemuingiza Uwoya
kwenye sanaa baada ya kumchezesha Filamu ya Yolanda ambayo ndiyo
iliyomtambulisha vyema staa huyo kisha kuliteka soko la sinema Bongo.
Subscribe to:
Comments (Atom)

