Wednesday, June 12, 2013

MAGAZETI YA LEO JUMATANO JUNI 12, 2013

1 84bff
2 d40ab
10 ac447

ANGALIA PICHA ZA LWAKATALE ALIVYOPATA DHAMANA JANA

Mkurugenzi wa Usalama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Wilfred Lwakatare akiingia katika chumba cha ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam leo, kabla ya kupata dhamana katika kesi yake inayomkabili ya kula njama ya kutaka kumzuru kwa sumu Mhariri wa gazeti la wananchi.

Wilfred Lwakatare akiwa na furaha pamoja na wakili wake baada kupata dhamana katika mahakama ya hakimu mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni mshtakiwa wa pili katika kesi inayomkali akiwa amerudi rumande baada ya kushindwa kukamilisha masharti ya dhamana.

IGP MWEMA AKUTANA NA MAASKOFU KATOLIKI JIMBO KUU DAR

 
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Said Mwema akiwa na Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki nchini Kardinali Pengo wakiingia katika ukumbi wa mkutano wakati wa kikao cha Mashauriano kati ya Jeshi la Polisi na viongozi wa makanisa ya kikatoliki uliofanyika jijini Dar es Salaam.(Picha na Frank Geofray-Jeshi la Polisi)
Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo kuu la Dar es Salaam Mwadhama Kardinal Pengo amesema viongozi wa dini hawawezi kukwepa jukumu lao la kuhakikisha kuwa uhalifu unapungua hapa nchini kwa kuwa jukumu hilo linaanzia kwao.
Pengo alisema kuongezeka kwa uhalifu ni changamoto kwa viongozi wa dini kwa kuwa wao ndio wenye kazi ya kujenga maadili katika jamii na polisi kusimamia sheria na kuwachukulia hatua wale wanaokaidi
Hayo yalisemwa wakati wa kikao cha mashauriano kati ya Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Said Mwema vongozi wa dhehebu la Romani Katoliki uliofanyika jijini Dar es Salaam .
Naye Askofu Msaidizi wa Kanisa Katoliki Jimbo kuu la Dar Es Salaam, Mhashimu Eusebius Nzigilwa akisoma maazimio yaliyofikiwa katika kikao hicho alisema wamekubaliana kuziimarisha kamati za ulinzi na usalama katika nyumba za ibada zilizopo hivi sasa wakati wakiendelea kupata mafunzo ya ukamataji salama kutoka Jeshi la Polisi.
“Parokia ambazo hazijaunda kamati za ulinzi na usalama zihakikishe zinafanya hivyo ndani ya mwezi huu na zile ambazo zimeundwa lakini hazifanyi kazi mziimarishe ili kwa pamoja tuwe salama katika nyumba zetu za ibada”Alisema Askofu Nzigilwa.

Katika mazungumzo hayo IGP Said Mwqema alisema kwamba Viongozi wa dini wana nafasi kubwa katika jamii ya kupunguza uhalifu kwa kuwa wao wanauwezo wa kuwabadili watu kimatendo na kifikra  kwa kufanya doria ya mwili na roho kwa pamoja hivyo wanaweza kusaidiana na Polisi katika kupunguza
uhalifu.

NIKIFA ASHA BARAKA ASIJE KWENYE MAZISHI YANGU- ALLY CHOKI

ALLY CHOKI ATOA KAULI NZITO: “NIKIFA ASHA BARAKA ASIJE KWENYE MAZISHI YANGU” … “Katika watu nisiowapenda kabisa ni Asha na Baraka Msilwa” 

ASHA BARAKA NAYE AJIBU MAPIGO: “HAYO NI MAMBO YA KIKE” …“Wamanyema peke yake wanatosha kunizika, amtaka Chocky akapime kwanza
MKURUGENZI wa Extra Bongo Ally Chocky ametoa kauli nzito kuhusu waajiri wake wa zamani, Asha Baraka na Baraka Msilwa.
Katika maongezi yake mahususi na Saluti5 Chocky alisema katika watu asiowapenda duniani ni Asha Baraka (Mkurugenzi wa ASET) na Baraka Msilwa (Mwenyekiti wa ASET). Asha Baraka na Baraka Msilwa ni mtu na kaka yake.

MWENYEKITI WA CCM JAKAYA KIKWETE AONGOZA KIKAO CHA KAMATI KUU YA CCM KUPOKEA RASIMU YA KATIBA MPYA

Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Kikwete, akiongoza kikao cha Maalum ya CCM ‘Kamati Kuu’ kilichokutana jana usiku mjini Dodoma kwa ajili ya kuipokea Rasimu ya Katiba mpya, iliyosomwa hivi karibuni. Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa imekutana jana tarehe 10/06/2013 chini ya
uenyekiti wa Mwenyekiti wa Taifa wa CCM Dr. Jakaya Mrisho Kikwete. Kikao hicho
kilikuwa cha siku moja na maalum kwa ajili ya kupokea rasimu ya katiba mpya.
Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa imekutana jana tareh 10/06/2013 chini ya uenyekiti wa Mwenyekiti wa Taifa wa CCM Dr. Jakaya Mrisho Kikwete. Kikao hicho kilikuwa cha siku moja na maalum kwa ajili ya kupokea rasimu ya katiba mpya.
Kamati Kuu inaipongeza Tume ya Mabadiliko ya Katiba nchini kwa kazi nzuri na kukamilisha kazi kwa wakati.

Tuesday, June 11, 2013

Vodacom, MCL wazindua habari kwa simu

sms f6b99

Mkurugenzi Mtendaji wa Mwananchi Communications Limited, Tido Mhando (kushoto) akimwangalia Mkurugenzi wa Kampuni ya Vodacom, Rene Meza alipokuwa akijisajili katika huduma ya habari zilizotokea hivi punde (Breaking News) kwenye hafla ya uzinduzi wa huduma hiyo Dar es Salaam, jana. Picha na Silvan Kiwale

Kampuni ya Vodacom Tanzania na Mwananchi Communications Limited (MCL), zimezindua mradi wa kufikisha habari za punde (Breaking News) kwa jamii, kuanzia leo.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mradi huo Dar es Salaam jana, Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom, Rene Meza alisema kwa kuanzia, wanatarajia wateja wasiopungua milioni kumi kujiunga na huduma hiyo.

"Mtumiaji mtandao wa Vodacom ataunganishwa na huduma hii kwa kupeleka ujumbe wenye neno Habari kwenda namba 15569, kwa gharama ya Sh150 kwa siku, tunafurahia hatua hii kwani tuna hakika itatuimarisha sokoni," alisema Rene.
Naye Mkurugenzi Mtendaji wa MCL, Tido Mhando alisema mradi huo umegharimu mwaka mmoja na nusu kuuandaa.

MHADHIRI WA CHUO KIKUU ATEMBEZWA UCHI BAADA YA KULIVAMIA KWA PUPA PENZI LA MWANAFUNZI...!!!

Mhadhiri wa chuo kikuu cha Delta State huko nchini Nigeria alijikuta katika aibu kubwa baada ya kuvuliwa nguo na kubaki uchi wa mnyama baada ya mwanafunzi wa kike aliyekuwa akisumbuliwa na Mhadhiri huyo kuamua kumfanyia umafia kwa kumuwekea mtego.

Hatua ya kudharirishwa kwa Mhadhiri huyo ilikuja baada ya mwalimu huyo kumtishia Tega na kumwambia kuwa atamferisha kama hata kubali kufanyanae mapenzi.Kabla ya hapo Mhadhiri huyo aliwahi kumtongoza mwanafunzi huyo lakini mwanafunzi huyo alimkatalia kata kata baada ya kuona hivyo Mhadhiri huyo aliamua kutumia wadhifa alionao kwa kumtishia kuwa kama hato kubali kulala nae basi atamfelisha mtihani.

Baada ya kuona hivyo Tega aliamua kumkubalia Mhadhiri huyo na kumshawishi badala kwenda kwenye hoteli kuchukua chumba ni bora waende nyumbani alikopanga mwanafunzi huyo ili wapunguze gharama,kuona hivyo Mhadhiri huyo alikubali haraka na kwenda nyumbani kwa Tega bila kujua kuwa kuna mtego amewekewa kumbe kabla ya hapo Tega alikuwa amesha waambia majirani zake na wanafunzi wenzake kuwa atahakikisha anamrubuni Mhadhiri huyo mpaka akubali kuvua nguo akisha kubali tu anamuaga kuwa anakwenda chooni kisha anawapigia simu waje kumuumbua Mhadhiri huyo kwani milango yote alikuwa ameirudishia tu na alikuwa ameshawaelekeza chumba ambacho atakuwepo Mhadhiri huyo.

Basi baada ya kuwapigia majirani na wanafunzi wenzake walifika eneo hilo la tukio na kufungua milango kimya kimya na kufanikiwa kuingia ndani mpaka chumba alipo Mhadhiri huyo ndipo walipo fanikiwa kumkuta Mhadhiri huyo akiwa uchi wa mnyama kitandani na kisha kumtoa nnje na kumtembeza uraiani ili watu wajionee wenyewe nini baadhi ya wahadhiri hufanya kwa wanafunzi wa kike.

MAGAZETI YA LEO JUMANNE JUNE 11, 2013






Monday, June 10, 2013

TCRA IMEITAKA STAR TV IRUDISHWE KWENYE STAR TIMES KABLA YA SAA KUMI JIONI LEO.

Mkurugenzi Mkuu wa TCRA Prof. John Nkoma akitoa maamuzi kuhusu kujitoa kwa StarTV kwenye Star Times.

TCRA imeagiza Chaneli ya Star Tv irudishwe mara moja kwenye Star Times kabla ya saa kumi jioni leo.

Aidha Star Times na Star TV wameelezwa kuwa wote wamevunja sheria ya Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta ya 2010 na Kanuni zake na kutakuwa kujitetea tarehe 17 Juni 2013.

Agizo la kurudishwa kwa Chaneli ya Star TV linatakiwa kutekelezwa ili kuhakikisha kuwa wananchi hawanyimwi haki ya kupata habari.

Vile vile wote wametakiwa kufuata Sheria inapotokea kutokuafikiana badala ya kutoa maamuzi bila kumshirikisha Mdhibiti (TCRA)

MSANII WA BONGO MOVIE KASH AFARIKI DUNIA LEO

Marehemu Jaji Khamisi (Kashi)

Habari iliyotufikia hivi punde ni kwamba msanii wa filamu nchini Jaji Khamis (Kashi)aliyewahi kutamba na michezo ya ITV enzi zile akiwa na wasanii kama mzee Masinde,Samson na wengine katika mchezo wa Tamu chungu na mingine mingi Amefariki dunia mchana huu katika hosptali ya taifa ya Muhimbili alikokuwa amelazwa,akizungumza na rais wa shirikisho la wasanii amesema kuwa tasnia yake bado inaendelea kukumbwa na majanga  lakini amedai yote ni kazi ya mungu
Nae mzee Masinde ambaye alikuwa nae katika kundi moja akiwa kama kiongozi wake amesema kashi ni msanii ambaye alikuwa mpiganaji na kwa hakika ni pigo kubwa katika tasnia yetu
Mungu ailaze roho ya marehemu Jaji Khamis (Kashi) mahali pema pepponi Amini.

Source:thesuperstarstz

HII NDIO VITA KATI YA STAR TIMES NA STAR TV


 Kampuni ya Sahara Media Group inayomiliki Kituo cha Televisheni cha Star, imeingia katika mgogoro na Kampuni ya Ving’amuzi ya Startimes na kufikia uamuzi wa kuitoa kurusha matangazo ya televisheni ya kituo hicho.

Hatua hiyo ya Kampuni ya Startimes kuondoa Star Tv kwenye orodha ya vituo vinavyopatikana kwenye king’amuzi chake ilianza juzi.


Startimes ilianza kutoa taarifa kuwa kutokana na matakwa ya Star Tv, wameamua kuitoa kwenye orodha ya chaneli zao bila ya ufafanuzi wa kina kuhusu uamuzi huo.
Waziri wa Sayansi, Mawasiliano na Teknolojia, Profesa Makame Mbarawa, alipotafutwa kutolea ufafanuzi wa kitendo hicho, alisema hafahamu lolote.
“Sifahamu kwani niko Pemba lakini labda watafute Mamlaka ya Mawasilino Tanzania (TCRA), Profesa John Nkoma (Mkurugenzi wa TCRA) watakuwa wanajua,” alisema Profesa Mbarawa.

Taifa Stars yawasili leo ikitokea Morocco, Poulsen asema Refa aliuharibu mchezo wetu.

IMG_5878
 Wachezaji wa Taifa Stars wakiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Julius Nyerere Jumatatu alfajiri wakitokea Morocco.
IMG_5874
IMG_5825
-Asema adhabu ya kadi nyekundu haikuwa na ulazima
-Asema wangecheza 11 ushindi ulikuwa wazi
Kocha wa Timu bali matokeo ya Taifa (Taifa Stars), Kim Poulsen amesema refa wa mechi ya Taifa Stars na Morocco iliyopigwa Marrakech Jumamosi kusaka tiketi ya kucheza fainali za Kombe la  Dunia Brazil mwakani aliuwa mchezo kwa kutoa kadi nyekundu kwa mchezaji Aggrey Morris.

MJUE MSANII WA BONGO MOVIE ALIEANZA KUCHEZA FILAMU ULAYA


Lucy Francis Komba (amezaliwa tar. 24 Oktoba, 1980) ni mwigizaji wa filamu, mwongozaji na mtayarishaji kutoka nchini Tanzania. Huenda akawa anafahamika zaidi kwa kutayarisha filamu ya Yolanda 1-2 na Utata. Lucy pia ni mmoja kati ya waliokuwa waigizaji wa kundi la sanaa la Kaole Sanaa Group.

Maisha ya awali


Lucy Francis Komba alizaliwa mnamo tarehe 24 Oktoba ya mwaka wa 1980, katika Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam, Tanzania.
Alipata elimu yake ya awali (chekechea) katika shule ya St. Peters Nusery School na msingi alisoma katika shule ya Oysterbay Primary School. Elimu ya sekondari alisoma Moshi katika mkoa wa Kilimanjaro, kwa kidato cha 1 - 4 na 5 - 6 alisoma katika shule ya Kibosho Secondary School.
Kwa elimu ya vyuo, alisoma katika Chuo cha Utumishi wa Serikali na alisomea maswala ya IT (Information Technology) na alipata Diploma katika elimu hiyo.
Sanaa ya awali
Lucy Komba alianza maswala ya sanaa katika kundi la sanaa la Fukuto Arts Professional. Akiwa huko alishiriki katika baadhi ya mifululizo ya vipindi vya televisheni kama vile "Valentine Day" na "Rangi ya Chungwa".
Baada ya hapo akaelekea zake katika kikundi cha Dar Talent, akiwa huko alipata kushiriki katika filamu moja ya vichekesho. Baada ya hapo alilekea zake katika kikundi cha sanaa cha Kaole Sanaa Group, akiwa huko alipata kushiriki katika mifululizo minne ya vipindi vya televisheni (tamthilia).
[hariri]Kazi binafsi

JK kuteta na Wabunge, Mawaziri Dodoma.

Rais Jakaya Kikwete anatarajiwa kuwasili mjini Dodoma, ambapo pamoja na mambo mengine atakutana na Kamati ya Bunge ya Bajeti ikiwa siku chache kabla ya kuwasilishwa kwa Bajeti Kuu ya Serikali itakayoainisha Mapato na Matumizi yake kwa mwaka wa fedha 2013/14, Juni 13.


Kamati hiyo inayoongozwa na Mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge imekuwa na vikao karibu kila siku, wakati mwingine vikimalizika usiku ili ikijiweka sawa kabla ya


 Rais Jakaya Kikwete akizungumza na vyombo vya habari siku za hivi karibuni
kuwasilishwa kwa Bajeti Kuu ya Serikali.
Habari zilizopatikana zinaeleza kuwa Rais Kikwete akiwa mjini Dodoma atakutana na baraza lake la mawaziri na Kamati ya Bajeti ili kupata picha ya mwelekeo wa bajeti, ambayo sehemu kubwa imeelezwa kubanwa na upatikanaji wa fedha za kutosha kwa ajili ya kuziwezesha wizara na taasisi zake kwa shughuli za kawaida na maendeleo.
Hata hivyo, habari zinadai kuwa ugumu uliopo ni namna ya kupata fedha kwa asilimia 100 kwa ajili ya kutekeleza shughuli mbalimbali za maendeleo na matumizi ya kawaida kwa wizara na Idara za Serikali.

Chanzo chetu kilieleza kuwa pamoja na 'kukuna kichwa' jinsi ya kupata fedha hizo, hata utekelezaji wa bajeti ya 2011/12 na 2012/13, ulikuwa mgumu kwa kuwa baadhi ya wizara na
taasisi zake zilipata nusu ya bajeti iliyopitishwa au asilimia 30 ya bajeti nzima.

Upatikanaji wa fedha hizo chini ya asilimia unatarajiwa kwa wizara na taasisi zake huku ikielezwa kuwa ni kutokana na kumegwa kwa asilimia za mafungu kulikosababishwa na kuongezeka kwa matumizi ya Serikali zikiwemo dharura.

KATIBU MKUU WA CCM NDUGU ABDULRAHMAN KINANA AANZA KUTEKELEZA AHADI ZAKE KWA VITENDO

1
Na Gladness Muushi wa Fullshangwe-Meru
Chama cha mapinduzi Wilaya ya Meru kimefanikiwa kutoa   Kiasi cha
Shilingi Milioni sita  pamoja na ahadi ya Milioni nane ikiwa ni ahadi
ya Katibu mkuu wa chama hicho Abdulrahman  Kinana aliyotoa mwaka jana
kwa ajili ya maendeleo ya vijana na wanawake wa Wilaya hiyo ingawaje
inatawaliwa na wapinzani
 Akikabidhi fedha hizo  mapema jana  katika uzinduzi  wa mashina ya
wakereketwa wa ccm   mjumbe wa kamati ya siasa mkoa wa arusha John
Pallangyo alisema kuwa fedha hizo ni moja ya ahadi zilizotolewa na
katibu mkuu wa ccm taifa Abdulrhaman Kinana mara alipofanya ziara ya
kujitambulisha mwaka  jana
Alisema kuwa mara baada ya katibu huyo kufanya ziara wilayani humo
aliamua kuwaunga mkono  vijana wa bodaboda  na wanawake wajasiramali
wa wilaya hiyo mkono ili waweze kujiendeleza kiuchumi ili waweze
kujikwamua katika hali ngumu ya kimaisha.
Aliongeza kuwa kwa kuwa ajira ni sehemu ya ilani ya chama cha
mapinduzi wameamua kutekeleza ahadi hiyo ili kuhakikisha kuwa vikundi
hivyo vinajiendeleza na kuachana na hali ya kuwa tegemezi  kwa kuwa
kupitia fedha hizo wataweza kujipatia mitaji ya kujienedeleza.
“Katika kutekeleza ilani ya chama chetu cha mapinduzi ni lazima
kuhakikiasha kuwa ajira inakuwepo hasa kwa vijana hivyo naombeni fedha
hizi mzitumie kwa uangalifu ili ziweze kuwasaidia kujiajiri wenyewe na
pia zitawasaidia kuachana na makundi ya upotoshaji”alisema Pallangyo

Kwa upande wake katibu wa chama hicho wilaya ya meru Langaeli Akyoo
alitoa wito kwa vijana wote na wanawake wa uwt wilayani humo kutumia
vizuri mitaji waliyopewa na chama hicho na kuhakikisha kuwa fedha hizo
zinawabadilishia hali zao za maisha pamoja na familia zao.
Aidha akyoo akielezea kuhusiana na uzinduzi wa mashina ya wakereketwa
alisema kuwa ni mkakati wa wa chama hicho wa kuhamasisha wananchi wote
katika harakati zake za kurudisha jimbo lililoko chadema na
kulirudisha mikononi mwao
Hata hivyo katika uzinduzi huo  mashina   yaliyozinduliwa ni pamoja na
kilala,usa madukani,sabato,imbaseny madukani,mji mpya,njia ng’ombe
,kimandafu pamoja na Arudeco.

MAGAZETI YA LEO JUMATATU JUNI 10, 2013 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


1 8a11b

2 bd675

Sunday, June 09, 2013

AKAMATWA KWA KUIBA STULI YA MWENGE WA UHURU...!!!

 

JIJI la Arusha limeendelea kujijengea sifa ya kuwa moja ya maeneo yenye vituko, kufuatia kijana mmoja mkazi wa eneo la Phillips, kata ya Sekei jijini humo, Hamad Rashid (32) kukamatwa leo akiiba kiti (stuli) kinachotumika kuwekea mwenge wa Uhuru wakati mwenge ukiwa katika mbio zake mkoani Arusha.
Tukio la kuiba na kisha kukamatwa limetokea jana saa 11 jioni katika eneo la Sanawari Mataa eneo lililopangwa kwaajili ya mkesha wa mwenge huo baada ya kukamilisha mbio zake na kazi ya kuweka mawe ya msingi na uzinduzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo.

Kamanda wa polisi mkoa wa  Arusha Liberatus Sabas ameithibitishia Nkoromo Blog kutokea tukio hilo na kwamba mtuhumiwa huyo alikamatwa na polisi waliokuwa wakiulinda mwenge pamoja na kiti hicho.

SALAMA JABIR ATAMANI KUOLEWA NA A.Y.....!!!

  

Mtangazaji mahili wa show za TV/Radio aliyeisimamisha wima show mpya na kali inayorushwa kupitia channel 5 ‘Mkasi’ namzungumzia Salama Jabir ametupia ‘neno’ kupitia kipindi hicho kuwa huenda siku moja akaolewa na AY!

Kama uliiangalia show ya Mkasi jumatatu ama marudio yake leo (jumamosi) ambapo crew nzima ya kipindi cha mkasi chini ya C.E.O na Producer wa show Ambwene Yesaya ‘AY’ walikuwa wakieleza changamoto na mambo mbalimbali waliyokutana nayo wakati wanaanza kufanya kipindi hicho, mwishoni Salama ambae alikuwa akimuelezea AY kuwa ni msanii ambae anajivunia kufanya nae kazi kutokana na jinsi alivyomchapakazi na mtu wa kuaminika alimaliza kwa kusema “huenda ipo siku moja tutaona..!”.

Wote tunajua Salama  alivyo mtu wa utani sana, kitu kinachoongeza burudani ya ziada katika show zake, alitamka hivyo na kumgeukia AY akimuuliza, na AY mwenyewe akajikuta anacheka na kukubali.
Pengine ulikuwa ni utani tu, lakini hakuna aijuae kesho ukizingatia wote wako single!

"MNAOWANIA URAIS MSIKUBALI KUPOKEA PESA ZA HUYU MFANYABIASHARA FISADI AMBAYE NI KINARA WA MADAWA YA KULEVYA".... REGINALD MENGI


Mwenyekiti wa makampuni ya IPP Reginald Mengi ametoa ya moyoni kwa wote wenye mpango wa kugombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania miaka miwili ijayo.

Bwana Mengi ameyatoa maombi yake ya moyoni na kuyaweka hadharani kupitia akaunti yake ya twitter June 7, na hiki ndicho alichokiandika.

“Nawaombea Mungu wanaotaka Urais wasipokee mshiko wa mfanyabiashara fisadi mkubwa ambaye pia ni kinara wa madawa ya kulevya.”

Swali ni mfanyabiashara gani, hilo linaweza kuwa ni jiwe gizani kama yupo kweli aliyetajwa litakuwa limemfikia. 
Na  kama  kuna  msomaji  wetu  anayemjua, ANARUHUSIWA  KUMTAJA  kwenye  COMMENTS  hapo  chini

WASHINDI WA TUZO ZA MUZIKI ZA KILI ( KILIMANJARO ) 2013


KALA JEREMIAH, OMMY DIMPOZ  WATISHA KWA KUZOA TUZO TATU 

* CHALZ BABA,  , OMMY DIMPOZ  WAZOA TUZO MBILI MBILI

NEY WA MITEGO ABEBA TUZO NDANI YA SIKU YAKE YA KUZALIWA

*OMMY DIMPOZ AMSHUKURU ZITTO KABWE KWA KUFANIKISHA UTENGENEZAJI WA VIDEO YAKE YA BAADAE

* ZEMBELA ATISHA KWA USHEHERESHAJI

* SALEHE ABDALLAH YAZIPU NA KILIMANJARO BAND WABEBA TUZO ZA HESHIMA
* LADY JAY DEE ABEBA TUZO YA MSANII BORA WA KIKE


MBUNGE WA MTWARA MJINI AKAMATWA NA POLISI KWA TUHUMA ZA KUCHOCHEA VURUGU ZA MTWARA

Jeshi la Polisi mkoani Mtwara limemkamata mbunge wa Mtwara Mjini (CCM), Hasnain Murji likimtuhumu kuchochea vurugu za kupinga mradi wa bomba la gesi kutoka mkoani humo kwenda jijini Dar es Salaam.

Habari zilizopatikana na kuthibitishwa na Msemaji wa Jeshi la polisi nchini, Advera Senso zinaeleza kuwa Murji alikamatwa jana jioni nyumbani kwake maeneo ya Shangani mjini Mtwara.

Kukamatwa kwa mbunge huyo kunakuja ikiwa zimepita siku tano tangu viongozi wanne wa vyama vya upinzani mkoani Mtwara, kufikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Mtwara, Juni 4, mwaka huu wakikabiliwa na mashtaka matatu ikiwamo kula njama, kufanya uchochezi na kuamsha hisia mbaya kwa wakazi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Washtakiwa hao ni Katani Ahmed Katani (33) na Saidi Kulaga (45) wa CUF, Hassan Uledi (35) wa NCCR Mageuzi na Hamza Licheta (51) wa TLP, wote wakazi wa Mtwara.

Taarifa zaidi zilieleza kuwa baada ya polisi kumkamata mbunge huyo, walifanya upekuzi katika nyumba yake kwa saa kadhaa na baada ya kujiridhisha walikwenda kupekua na ofisi yake.


“Amekamatwa kwenye saa 11:00 jioni, hata hati ya kukamatwa kwake imeeleza kuwa anatuhumiwa kuchochea vurugu za kupinga gesi inayopatikana mkoani Mtwara kwenda Dar es Salaam,” alisema Katibu wa Mbunge huyo, Meckland Millanzi.

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI JUNI 9, 2013

2 b911e

3 21fb8

Saturday, June 08, 2013

WENGI WANACHANGANYA MAMBO, ILA HUU NDIO UHUSIKA WA BIG BROTHER NA FREEMASON

WATU WANASEMA MANENO UUMBA, INAWEZA KUA KWELI AU SI KWELI. JIONI HII WAKATI NIKIZUNGUKA ZUNGUKA NIMEKUTANA NA PICHA HAPO JUU IKIICHAMBUA LOGO MPYA YA BIG BROTHE. KAMA UNAVYOONA HAPO JUU KATIKA PICHA UTAONA KUA LOGO HIYO INAHUSISHWA NA MAMBO YA FREEMASON. UKIANZA NA HILO JICHO PAMOJA NA VITU VINGINE.

 SO KAZI KWAKO KUCHAMBUA PUMBA ZIPI NA MCHELE UPI.

HII NDO NYUMBA YA MASANJA MKANDAMIZAJI ALIYO JENGA KIJIJINI KWAO

Aliyekuwa na Ngwair "M 2 The P" Aongea na Kusema Haya...!!!

 'M 2 the P' ambaye awali naye aliripotiwa kuwa amefariki kabla ya taarifa hizo kukanushwa, alisema jana kuwa hadi sasa hajui nini kiliwatokea.
Msanii huyo alisema kwamba hakumbuki kilichotokea hadi wakazidiwa na kukimbizwa hospitali wakiwa hawajitambui.

Alisema pia bado anajisikia anaumwa hadi sasa licha ya kuruhusiwa kutoka katika hospitali ya St. Hellen Joseph ya Afrika Kusini alikokuwa amelazwa.
chanzo:Nipashe
Msanii 'M 2 the P' ambaye alikuwa na marehemu Albert Mangweha nchini Afrika Kusini wakati rapa huyo anafariki na yeye pia kuzidiwa hadi kulazwa katika chumba cha wagonjwa mahututi, alihudhuria mazishi mjini Morogoro juzi.

MAGARI MATANO YALIYOWAHI KUTUMIWA NA HAYATI BABA WA TAIFA ENZI ZA UHAI WAKE

Leo tupo katika utalii wa ndani kwa kutazama baadhi ya  magari aliyotumia Baba wa Taifa na Rais wa kwanza wa Tanzania Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere wakati wa harakati za Uhuru na baada ya Uhuru mpaka alipofariki Oktoba 14,1999. Maelezo ya makala haya ni kwa mujibu wa nyaraka zilizopo Makumbusho ya Taifa, Dar es Salaam hasa kuhusiana na magari na miaka ya magari yalipotumika. Fuatana nasi.
1.AUSTIN MORRIS A-40

AUSTIN MORRIS A-40

 Gari aina ya  Austin Morris A-40 lilitengenezwa nchini Uingereza kati ya mwaka 1940 – 1950. Ni gari la kwanza kutumiwa na Baba wa Taifa na Rais wa kwanza Tanzania hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI JUNI 8, 2013 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.
.
.
.

SHOW YA SNURA YAACHA WANAUME MIDOMO WAZI, KWELI MAJANGA


 

Naamini kwapicha hizi uwezi kosa show yake jumapili hii NEW MAISHA CLUB atazindua video yake ya majanga kuwa mjanja kuwa wa kwanza kuiona, atasindikizwa na WEMA SEPETU atakata utepe wa video ya majanga,MIRROR,SAMIR,ALI NIPISHE,TIMBULO,BAUCHA,MENINAH, na MADEE kiingilio 10,000 tu hii show sio yakukosa kabisa.
 

MWIGIZAJI WA KIKE WA BOLLYWOOD “JIAH KHAN” AJIUA IKSA MAPENZI


Muigizaji maurufu ambae ni mmoja kati ya wanadada warembo nchini India anaejulikana kama “Jiah Khan” amekutwa amekufa juzi kwa kujiua baada ya kujua Boyfriend wake ana mwanamke mwingine….

Mama yake na Khan amesema kua alirudi na kukuta mwili wa mtoto wake akiwa ameshakufa huku Police wakiwa bado wanachunguza chanzo cha kifo cha mrembo huyo ila baadhi ya majirani walizungumza na Mtandao wa BBC na kusema kua wanachujua mwanadada Khan alikua na mkwaruzano na BF wake…..

Jiah Khan amefariki wakiwa na Miaka 25 na alijipatia umaarufu mkubwa Inchin india baada ya kuigiza na mkongwe wa tasnia ya movie anaijulikana kama Amitah Bachchan na pia aliweza kuigiza na Aamir Khan na Akshay Kumar kwa wale mnaofatilia Bollywood Movies hakika mnawatambua hawa.

mwili wa Jiah Khan ulipelekwa Hospital kwa uchunguzi zaidi…..


Khan alizaliwa New York na akakulia London kabla ya kwenda Mumbai India na kujiingiza kwenye mambo ya sanaa ya uigizaji wa filamu…

Filamu yake ya Mwisho kuigiza inaitwa Housefull ambayo ilitoka mwaka 2010..

TAZAMA VIDEO YA MAZISHI YAKE HAPA

Popout

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...