Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe
Mwenyekiti
wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema, Freeman Mbowe amesema
uchovu ndiyo sababu iliyomfanya kuugua ghafla jana na kulazwa katika
Hospitali ya Taifa, Muhimbili, jijini Dar es Salaam.
Akiwa katika maandamano ya kumsindikiza mgombea urais kwa tiketi ya Chadema, Edward Lowassa, kuchukua fomu jana, Mbowe aliugua ghafla eneo la Manyanya, Kinondoni na kulazimika kukimbizwa Muhimbili ambako amelazwa hadi leo.
Akiwa katika maandamano ya kumsindikiza mgombea urais kwa tiketi ya Chadema, Edward Lowassa, kuchukua fomu jana, Mbowe aliugua ghafla eneo la Manyanya, Kinondoni na kulazimika kukimbizwa Muhimbili ambako amelazwa hadi leo.
Hata hivyo, mwanasiasa huyo
ambaye anawania ubunge katika jimbo la Hai kupitia Chadema
amewahakikisha wanachama na wafuasi wa Ukawa kuwa afya yake ni njema na
huenda akaruhusiwa kutoka hospitalini ndani ya saa 48.
Akizungumza
na Mwananchi jana, Ofisa Uhusiano wa Muhimbili Aminieli Aligaesha
pamoja na kukiri kulazwa kwa mwanasiasa huyo, hakutaka kuweka hadharani
kilichokuwa kinamsumbua Mbowe. Asante kwa kutembelea blog hii, endelea kuwa nasi, like page yetu ya facebook bofya neno Jambo Tz.
No comments:
Post a Comment