Friday, June 14, 2013

BAADA YA KUPATA TUZO MBILI ZA KILI DIAMOND AMSUTA ‘MGANGA WAKE’

Nasibu Abdul ‘Diamond’.
STAA anayeng’aa katika Muziki wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ amemsuta mganga aliyejitokeza na kudai kwamba mwaka huu staa huyo hatapata mafanikio yoyote na  atapotea katika fani.
Mganga huyo ambaye alidai utaalamu wake ndiyo uliompandisha chati Diamond alisema  mwaka huu staa huyo hatapata tuzo, atafifia na jina lake litasahaulika kutokana na kukiuka masharti yake.

Akizungumza na Ijumaa hivi karibuni, Diamond alisisitiza kutomtambua mganga huyo na anamshangaa kwa kuwa mwaka huu amepata mafanikio tofauti na alivyosema.
“Hebu angalieni, mganga alidai mwaka huu nitafutika katika fani, mbona nimepata tuzo mbili kwenye Kil na nimechaguliwa kuwa balozi wa Cocacola na shoo zinajaza kinoma?” alihoji Diamond.
Aidha, alisema shoo zake bado zinajaza watu wengi huku akiitolea mfano ya mwisho iliyofanyika Dar Live, Mbagala Zakhem, Dar hivi karibuni iliyojaza nyomi ya watu.
 
NA GPL

WANAFUNZI WA CHUO KIMOJA MKOANI MTWARA WAFANYA PARTY YA KIFUSKA

Pombe  iko  kichwani  hapo....Kila  kitu  kwake  ni  sawa ..

Katika hali isiyokuwa ya kawaida,  wanafunzi wa chuo kimoja maarufu Mkoani Mtwara hivi karibuni walifanya party ya ufuska na kuwaacha watu midomo wazi kwa mambo yaliyokuwa yanatendeka.
Party hiyo ambayo  ilifanyika ndani ya pub moja  mkoani  humo  ilihudhuriwa  kwa  wingi  na  wanafunzi wa chuo  hicho  ambao  wengi  wao  walikuwa  wamevaa  kihasara ...

 Huyu  ni mmoja wa wanafunzi hao aliyefahamika kwa jina la Zaitun ambae anasoma mwaka wa kwanza katika chuo hicho.

KINANA AMBURUZA KORTINI MBUNGE MSIGWA BAADA YA KUMWUITA JANGILI

KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Abdul-rahman Kinana amemfungulia kesi Mbunge wa Iringa Mjini, Peter Msigwa (Chadema), kutokana na kumtuhumu anajihusisha na ujangili na biashara haramu ya pembe za ndovu.
Kinana amefungua kesi hiyo katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam kutokana na kitendo cha Mbunge huyo kutoa tuhuma hizo dhidi yake kwa nyakati tofauti nje na ndani ya Bunge, pia alikataa kuzikanusha na kumuomba radhi.
Inadaiwa kuwa Aprili 21 mwaka huu Msigwa ambaye ni Waziri Kivuli wa Maliasili na Utalii alitoa tuhuma hizo kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika Shule ya Msingi Mbuguni wilayani Nyamagana mkoani Mwanza.
Aidha alizitoa bungeni wakati akiwasilisha hotuba ya Kambi ya Upinzani katika Makadirio ya Bajeti ya Wizara ya Maliasili na Utalii mwaka 2013/2014. Katika hati ya madai, Kinana anadai kuwa kutokana na tuhuma hizo ameharibiwa tabia yake, uaminifu, hadhi yake kitaaluma na weledi na kumfanya achukiwe na kudharauliwa katika jamii.
Anadai jina lake na heshima ambayo ameijenga kwa muda mrefu, vimharibiwa na Msigwa kwa nia mbaya, pia kwa tuhuma hizo anazosisitiza kuwa ni za uwongo, licha ya kumsababishia maumivu ya kisaikolojia, pia zimemsababishia hasara ya fedha.
Anadai kuwa kabla ya tuhuma hizo alikuwa katika hatua za mwisho za mchakato wa mazungumzo ya mradi wa ubia wa kilimo cha mboga na mwekezaji kutoka kampuni ya nje, lakini tuhuma hizo zimesababisha kampuni hiyo kuvunja majadiliano hayo.
Kinana anadai kuwa sababu iliyotolewa na kampuni hiyo kuvunja mazungumzo hayo ni kutajwa kwake na mbunge huyo kuwa ni jangili anayejishughulisha na biashara hiyo.

TAARIFA KAMILI KUHUSU KIFO CHA LANGA NA RATIBA YA MAZISHI...!!


Wakati ambapo mashabiki wa muziki wa Hip Hop nchini wakianza kusahau majonzi ya kumpoteza Albert Mangweha aka Ngwair mwezi uliopita, leo wametoneshwa tena kwa kifo cha mwana hip hop mwingine, Langa Kileo aka Lyrically And Naturally Gifted African.
971547_562592510448211_1469657651_n
Kwa mujibu wa Afisa Uhusiano wa hospitali ya taifa ya Muhimbili, Aminiel Aligaesha aliyezungumza na Clouds FM, Langa amefariki leo June 13, saa 11 jioni baada ya kufikishwa hospitalini hapo tangia juzi mida ya jioni. Hata hivyo amesema kutokana na maadili na taratibu za hospitali asingeweza kutoa chanzo cha kifo cha Langa na jukumu hilo ni la ndugu zake.
Hata hivyo taarifa za awali zilidai kuwa Langa alikuwa anaumwa Malaria kali iliyopelekea kukimbizwa Muhimbili jana jioni.
Baba wa marehemu Mzee Kileo amesema taarifa kamili na mipango ya mazishi zitatolewa pale vikao vya familia vitakapofanywa.Pia baba yake alisema msiba huu umetokea wakati mama yake Langa hayupo Tanzania,alisema kwa sasa mama yake Langa yupo Marekani lakini baada ya kupewa taarifa hizo tayari ameshakata tiketi ya kurudi Tanzania na ataanza safari kesho.Msiba uko nyumbani kwao maeneo ya Mikocheni(Anna Peter).

MAJINA YA WANAFUNZI WA KIDATO CHA SITA 2013 NA KAMBI ZA JESHI WALIKOPANGIWA...TAREHE YA KURIPOTI NI 24 MWEZI HUU

TANGAZO
MKUU WA JKT MEJA JENERALI RAPHAEL MUHUGA ANAWAITA VIJANA 10,849 WALIOHITIMU KIDATO CHA SITA MWAKA 2013 KUJIUNGA NA JKT KWA MUJIBU WA SHERIA KAMA IFUATAVYO:-

1. VIJANA WOTE WALIOHITIMU KIDATO CHA SITA WALIOPATA DIVISION I NA DIVISION II.

2. VIJANA WOTE WALIOHITIMU KIDATO CHA SITA WALIOSOMA MASOMO YA MCHEPUO WA SAYANSI NA KUPATA DIVISION III.

3. VIJANA HAO WANATAKIWA KURIPOTI KATIKA MAKAMBI YA JKT TAREHE 24 JUNI 2013 BILA KUKOSA. AMBAYE HATARIPOTI ATACHUKULIWA HATUA ZA KISHERIA.

4. TANGAZO HILI HALIWAHUSU VIJANA WOTE WALIOHITIMU KIDATO CHA SITA 2013 KATIKA SHULE ZA SEKONDARI ZA UNGUJA NA PEMBA. AIDHA, SHULE 27 AMBAZO VIJANA WAKE WAMEHITIMU MAFUNZO YA JKT AWAMU YA KWANZA HAZIHUSIKI.

5. VIJANA HAO WATUNZE TIKETI ZAO KWA AJILI YA KUREJESHEWA NAULI WATAKAZOTUMIA MARA TU WATAKAPORIPOTI VIKOSINI.

6. TAARIFA ZAIDI ZITATOLEWA KWENYE MAGAZETI MBALIMBALI YA HAPA NCHINI.


Zifuatazo  ni  selection  za  kambi  walikopangiwa
 Attached Files

MAGAZETI YA LEO IJUMAA JUNI 14, 2013 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.

.
.
.
.

Thursday, June 13, 2013

KAULI YA BALOZI WA TANZANIA KUHUSU MSICHANA ANAYEDAIWA KUTAKA KUNYONGWA BAADA YA KUKAMATWA NA MADAWA YA KULEVYA EGYPT

.
Baada ya watu wengi kuzipata habari na bila kujua imekuaje kwa Mtanzania anaedaiwa kukamatwa na dawa za kulevya nchini Egypt na kwamba alikua anakaribia kunyongwa, balozi Mohamed Haji wa Tanzania nchini Egypt ameongea Exclusive na millardayo.com na kueleza yote anayoyafahamu kuhusu hii ishu. Namkariri akizungumza 1. Ni kweli kuna raia wawili Watanzania wamekamatwa na dawa za kulevya ambao ni Mbarak Abdallah Salim (28) na Sharifa Mahmud (27) wakazi wa Magomeni Kagera Dar es salaam, wanaundugu wa mtoto wa shangazi na mjomba. 2. Walikamatwa tarehe 16 May 2013 wakati wakiingia Misri, kwa mujibu wa maelezo safari yao ilianzia Dar es salaam kwenda Mombasa, Nairobi mpaka Misri.
.
3. Dawa za kulevya walizokamatwa nazo zimetajwa kwamba ni Heroine kilo saba. 4. May 18 2013 ndio tuliitwa kwenda kutazama Raia wetu, nikatuma maafisa wawili wazuri kwenda kutazama ili raia wetu wasimbambikiwe kesi. 5. Baada ya hapo waliwekwa rumande na tukapata nafasi ya kuwaunganisha na nyumbani huku Tanzania wakaongea kwenye simu kilichowapata. . 6. 26 May 2013 ndio walipelekwa Mahakamani kwa mara ya kwanza na kurudishwa rumande wote wawili. 7. Hawa ndio Watanzania wa kwanza kukamatwa na kesi kama hii na ikithibitishwa wamefanya kweli, hili kosa ndilo litakua doa la kwanza kwa Tanzania hapa Misri. 8. Ishu ya kunyongwa, tunajaribu kufanyia kazi lakini hakuna kumbukumbu za mgeni yeyote kwa sisi tunavyojua ambae amewahi kunyongwa kuhusu ishu ya dawa za kulevya. 9. Tunajitahidi kuwasiliana na mamlaka zinazohusika ili kujua siku gani watapelekwa tena Mahakamani alafu tutawafahamisha nyumbani. Kwa ushahidi unaweza kumsikiliza balozi hapa chini na pia kutazama video hapo chini ya ushahidi wa kukamatwa na dawa za kulevya…

PICHA ZA KALA JEREMIAH AKIAMKABIDHI MAMA MZAZI WA MANGWAIR TUZO YAKE

Mama mzazi wa marehemu Albert Mangweha akiwa ameshikilia tuzo aliyopewa kwa niaba ya mwanae, tuzo hii aliipata msanii Kala Jeremiah kwenye tuzo za Kilimanjaro ikiwa kama tuzo ya msanii bora ya Hip Hop 2013-14


 
 
 
 

MH: ZITO KESHO KUWA MGENI RASMI SHOW YA MWANA FA, HUKU SUGU AKIWA KWA JIDE

 
Ile the Big Square 1, show za magwiji wa muziki Tanzania mwana FA ‘The Finest’ na Lady Jay Dee ‘Miaka 13 ya Lady Jay Dee’ zitapigwa kesho June 14, huku presha ikiwa inaongezeka hasa kwa fans wanaotamani kuhudhuria show walioichagua na kuona ukubwa wa show kama walivyotarajia.

Show hizi kubwa zina nguvu sana kutokana na ukubwa wa majina ya wasanii husika. Kwa mujibu wa lady Jay Dee timu anaconda kesho itaungwa mkono na mheshimiwa Joseph Mbilinyi a.k.a Sugu.

Jide ambae hivi karibuni ameachia wimbo mpya unaopatikana kwenye album yake ‘Nothing but the truth’ inayoitwa Yahaya, amepost kupitia kupitia ukurasa wake wa facebook na pia katika akaunti yake ya Twitter kuonesha list ya wasanii watakaopanda jukwaani, na pia uwepo wa Sugu.

” Miaka 13 ya Lady JayDee, Ijumaa ya kesho shughuli inaanza rasmi saa 3:00 usiku...Ukiskia paaaa ujue show imeisha

1. Prof Jay 2. Juma Nature 3. Grace Matata 4. Hamza Kalala 5. Wakazi na ugeni wa Mh. Joseph Mbilinyi a.k.a SUGU

Nyimbo zote unazozipenda zitalia tar 14 June, pale Nyumbani Lounge sababu yaaaaa sababu yaaaaaa ?????????”


Kwa upande wa Mwana FA ambae atapiga show yake na Live band akiwa na kundi kubwa na maarufu kwa upigaji wa Live Band ‘Wananjenje’, yeye amepewa full sapoti na mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto kabwe.
Zitto ameweka wazi kupitia akaunti yake ya twitter kuwa anamsapoti sana msanii huyo.

“You have my full support “@MwanaFA”

"BABY MADAHA ASITAKE KUPATA UMAARUFU KUPITIA JINA LANGU TENA ANIKOME" ...... JACK WOLPER

MWANADADA anayefanya vizuri katika tasnia ya filamu Jaqueline Massawe ‘Wolper Gambe’ amesema anamshangaa sana msanii wa muziki ambaye pia ni mwigizaji Baby Madaha kutumia vyombo vya habari kutengeneza ugomvi wakati hana mawasiliano naye yoyote na wala si rafiki yake au mtu aliyekaribu naye na hana mazoea naye.


“Nimelizika na umaarufu nilio nao sihitaji kujipeleka katika magazeti na kuongelea vitu ambavyo havina faida katika jamii, mimi sina urafiki na Baby Madaha, namshanga anavyotapatapa kuniandika vibaya kwa jambo lisilo nihusu, mambo hayo niliyafanya nikiwa Chipukizi”

“Nakumbuka mimi nilipigiwa simu na rafiki yake akiniomba namba mwenye nyumba lakini ghafla nikapiwa simu na mwandishi wa habari mara Polisi nikashangaa huyo mtu hata namba ya mwenye nyumba sijamtumia nasumbuliwa na watu utafikiri mimi ndio mtuhumiwa, lakini jambo ninalomshangaa mimi ni dalali?,” alihoji Wolper.
Hivi karibuni yalizuka maneno yakiwahusisha wasanii hawa wawili ikisemekana walikuwa wakigombea nyumba ya kupanga, huku Baby Madaha kuigizwa mjini na mwenye nyumba kwa kupangishwa nyumba hewa, Wolper amedai kuwa kwa sasa yeye amekuwa makini halipii nyumba kienyeji bali ulipia kwa mwanasheria wake tena kwa kufuata taratibu kwa kukwepa utapeli.

MUME WA MTU ANASWA GEST AKIWA NA SHOGA WAKIFANYA UCHAFU WAO


Tukio hilo lililoshuhudiwa na watu kibao, lilijiri Juni 10, mwaka huu katika nyumba moja ya kulala wageni iliyopo Kinondoni jijini Dar.
Kunaswa kwa wanaume hao ambao ilidaiwa walikuwa kwenye harakati za kufanya Usodoma na Ugomora, kulifuatia mke wa mmoja wao kunasa meseji za kimapenzi walizokuwa wakitumiana wawili hao.
Mama huyo alipobaini meseji hizo chafu, wawili hao wakisisitiziana kukutana kwenye gesti hiyo usiku wa siku hiyo, alimpigia simu mmoja wa waandishi na  kumpa  mkasa  mzima ambapo  walikubaliana  saa  moja  zoezi  la  kuwanasa  litaanza.. 
Ilipofika saa 1:30 usiku, timu yetu, mama huyo, wapambe wake na polisi walikuwa wanafanya doria nje ya gesti hiyo.

Saa 5:30 usiku, mume wa mwanamke huyo akiwa na mwanaume anayedaiwa kuwa shoga walifika gesti hiyo bila kujua kama waliwekewa mtego wa kunaswa na kwenda kuchukua chumba namba 2.


 Wakiwa ndani, mke alimpigia simu mumewe na kuhoji alipokuwa akajibiwa alikuwa mitaa ya nyumbani kwao Manseze, Dar akipiga stori na rafiki zake.

Wawili hao wakiwa wanajiandaa na mchezo wao usiofaa, polisi aligonga mlango akijifanya mhudumu aliyetaka kumpatia taulo, jamaa bila kujua alifungua ndipo walipofumaniwa na kuibua varangati zito.
 
Kufuatia timbwili hilo, waliwekwa chini ya ulinzi na kutolewa pale gesti tayari kupelekwa kituoni ndipo mwanaume anayedaiwa kuwa shoga akatimua mbio mithili ya mwanariadha wa kimataifa, Usain Bolt wa Jamaika na wanandoa hao waliendelea kuzozana huku mke akimlalamikia mumewe na kumwambia wakifika nyumbani ampe talaka yake.

Hata hivyo, mwanamke huyo aliomba sakata hilo lisipelekwe polisi kwa madai alichotaka ni kumfumania mumewe na kwamba alikuwa na ushahidi wote.

GPL

RAIS JACOB ZUMA ASEMA KUWA AFYA YA NELSON MANDELA YAANZA KUIMARIKA

Rais wa zamani wa Afrika Kusini Nelson Mandela kulia na rais wa sasa Jacob Zuma
Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma amesema kuwa afya ya rais wa zamani wa taifa hilo Nelson Mandela imeanza kuimarika kidogo kutokana na matibabu anayopewa na Madaktari wake jijini Pretoria.
Zuma amewaambia wabunge kuwa Mandela anayefahamika kwa jina maarufu kama Madiba ameanza kuimarika na ni habari njema kwa raia wa nchi hiyo ambao wamekuwa wakikumbwa na wasiwasi kutokana na afya yake kuendelea kudorora.
Rais huyo ameongeza kuwa kila mmoja anakumbuka mchango wa Mandela ambaye alifungwa jela miaka 27 akiwa katika harakati za kupinga ubaguzi wa rangi nchini humo na baadaye kufanikiwa kuwa kiongozi wa kwanza mweusi nchini humo mwaka 1994.
Kiongozi huyo wa Afrika Kusini amewataka raia wa nchi hiyo na dunia nzima kuendelea kumwombea Mandela ili apate nafuu haraka na kuruhisiwa kurudi nyumbani.

Familia ya Mandela imesema kuwa imeguswa mno na salamu za heri njema zinazotumwa na watu mbalimbali duniani kumtakia kiongozi huyo wa zamani nafuu ya haraka.

Mandela mwenye umri wa miaka 94 alilazwa hospitalini Jumamosi iliyopita baada ya kuanza kusumbuliwa na mapafu tatizo ambalo limemsumbua kwa muda mrefu.

MAGAZETI YA LEO JUNI 13, 2013


.
 .

MWANA FA AFUNGUKA KUHUSU BIFU LAKE NA LADY JAYDEE

Baada ya kutibuana na Lady Jaydee, Mwana FA ameamua kuvunja ukimya na kuwataka mashabiki wachukulie poa maana ni hali ya kawaida tu katika maisha ya kibinadamu.....

Ugomvi wa wasanii hawa ulianza baada ya Mwana FA ku re -tweet post moja ya shabiki wake ambayo ilikuwa ikiiponda show ya Lady Jaydee...

Lady jaydee alijaribu kumuonya mara kadhaa lakini FA hakusikia na badala yake aliretweet post ya shabiki mwingine ikimponda Lady Jaydee....

Uvumilivu ulimshinda Lady Jaydee na kuamua kujibu mashambulizi kwa kumuita Mwana Fatuma na na mengine mengi.....

Wasikilize hapo chini wakifunguka

RAIS KAGAME AMGOMEA JK



RAIS wa Rwanda, Paul Kagame, amemshambulia kwa maneno makali Rais Jakaya Kikwete, akijibu ushauri alioutoa kwa serikali yake wa kukaa katika meza ya mazungumzo na waasi wa kikundi cha Democratic Force for the Liberation of Rwanda (FDLR), ili kumaliza mapigano. Shirika la Habari la Rwanda, linalojulikana kwa jina la News of Rwanda, jana lilimkariri Rais Kagame akitoa maneno ya kejeli na yenye mwelekeo wa kupuuza ushauri wa Rais Kikwete.

Kauli hiyo ya Rais Kagame, ambayo pia imesambazwa katika mitandao mbalimbali ya habari, inaonyesha kukerwa na ushauri wa Rais Kikwete ambao ameuita upumbavu uliojazwa ujinga.

Hii ni mara ya kwanza kwa Rais Kagame kutoa kauli hiyo tangu Rais Kikwete alipotoa ushauri huo, wakati akizungumza katika kikao cha Mkutano wa Umoja wa Afrika uliofanyika mapema mwaka huu, mjini Addis Ababa, Ethiopia.

Waasi wa FDLR ambao jamii yao ni Watutsi, walikimbilia nchini Kongo baada ya mapigano ya kimbari ya mwaka 1994, yaliyosababisha maelfu ya watu kupoteza maisha na wamekuwa wakiendesha chokochoko dhidi ya Serikali ya Rais Kagame.

Akizungumza katika sherehe ya kuhitimu mafunzo ya kijeshi maofisa 45 wa jeshi lake, Rais Kagame alisema ushauri wa kufanya mazungumzo na waasi wa FDLR ni ujinga na haupo katika historia ya Wanyarwanda.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...