Friday, May 03, 2013

MCHUMBA WA MTU ATUPWA JELA KWA KUJIUZA...........!!!


Na Richard Bukos

MREMBO Brandina Barthon (24), Jumatatu iliyopita alihukumiwa kwenda jela miezi 6 baada ya kupatikana na hatia kwenye kesi ya ukahaba iliyokuwa ikimkabili katika Mahakama ya Sokoine Drive (Jiji) jijini Dar.
Brandina alisomewa hukumu hiyo na Hakimu Mfawidhi wa Mahakama hiyo, William Mutaki ambaye alisema kutokana na ushahidi uliothibitika, mahakama hiyo inamhukumu kwenda jela miezi 6, ili liwe fundisho kwa wengine.
Hukumu hiyo ilimfanya mrembo huyo kuchanganyikiwa na kuangua kilio lakini mheshimiwa hakimu aliamua kukazia hukumu yake bila ya kupepesa
macho.
 
Wakati mwanamke huyo akiangua kilio, afande wa Jeshi la Magereza alimfikia na kumchukua  kwa ajili ya kumpeleka kwenye Karandinga kuelekea Gereza la Segerea kuanza maisha ya jela.
Mbali na Brandina, mwanaume aliyedaiwa kuwa ni mpenzi wa mtuhumiwa huyo aliyekuwa akifuatilia kesi hiyo naye alimwaga machozi baada ya kutolewa hukumu hiyo.

HII NDIO LIST KAMILI YA VIONGOZI WA TANZANIA NA WA KIMATAIFA WALIOJIUNGA FREEMASONS


Siri ya List za Viongozi wa Tanzania Yatajwa (Secret Society), Freemason, imedaiwa kuwa na siri nzito na viongozi wakuu wa nchi yetu, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.





MWINYI NA ANDY CHANDE


Madai hayo, yametokana na kile kinachoonekana kwamba Kiongozi Mkuu wa Freemason, Afrika Mashariki, Sir Andy Chande, amekuwa akijiweka karibu na viongozi wakuu wa nchi hii kila awamu, hivyo kuonesha kuwa kuna kitu anakitafuta.
Andy Chande

Andy ChandeKikubwa kinachodaiwa ni kuwa Chande anatumiwa na Freemason kuhakikisha kwamba kila kiongozi wa nchi hii anakuwa karibu na jamii hiyo ya siri.
Inazidi kudaiwa kuwa Freemason inafanya njama za hali ya juu kujiweka karibu na Ikulu, ikiwa na mpango wao wa muda mrefu wa kusimika rais ambaye ni memba wa jamii hiyo katika awamu zinazokuja.
Uchunguzi umeonesha kuwa Chande amekuwa karibu na Ikulu tangu Awamu ya Kwanza chini ya Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Nyerere na amedumu kujiweka karibu na viongozi wa nchi mpaka awamu hii ya nne chini
ya Rais Jakaya Kikwete.

NEEMA YAWASHUKIA WALIOFELI .... MATOKEO YA KIDATO CHA NNE KUPANGWA UPYA


TUME ya kuchunguza sababu za kufeli kwa kiasi kikubwa kwa wanafunzi wa kidato cha nne waliofanya mitihani ya kuhitimu mwaka 2012 imekamilisha kazi yake na taarifa za uhakika zilizolifia gazeti hili zinasema , upangaji alama zao utafanyika upya.

Kama ambavyo gazeti hili lilivyobaini katika uchunguzi wake wa kiuandishi kwamba kulifanyika mabadiliko ya utoaji alama kwa ajili ya mitihani waliyofanya wanafunzi mwaka huo (2012) bila maandalizi kwa wadau, tume hiyo imependekeza alama zipitiwe upya (regrading).Katika alama za awali, alama D anapoyopewa mtahiniwa baada ya mtihani wake kusahihishwa ilikuwa ni kuanzia alama 21 kwenda mbele na F ilikuwa 20 kushuka chini lakini katika mabadiliko yaliyoleta ‘maafa’ ya kufeli kwa watahiniwa wa mwaka jana, alama D ilianzia 35 na kuendelea, wakati ile ya kufeli (F) ilianzia alama 34 kushuka chini.

MAGAZETI YA MAY 3, 2013

.
.

Thursday, May 02, 2013

HUSANA IDD NA NAOMI WA BONGO MOVIE WAGOMBEA PENZI LA JANUARY...!!

Msanii anayechipukia kwenye soko la filamu na muziki, Naomi Mbaga ameibuka na kumuonya Husna Idd ‘Sajent’ amuachie bwana wake, January.
 Akizungumza na mwandishi wetu, Naomi aliweka bayana kuwa January ambaye ni Mwanamuziki wa Bendi ya Victoria ni mpenzi wake wa muda mrefu hivyo alishangazwa kuona habari mitandaoni kuwa Sajent amejituliza kwa mpenzi wake huyo baada ya kumwagana na mzazi mwenzake, Charles Gabriel ‘Chaz Baba’.

“Aniachie bwana wangu, kama ameachika kwa huyo Chaz Baba atafute bwana mwingine na siyo wa kwangu. Ole wake nimkute naye siku, atanitambua,” alisema Naomi.

Sendeka, Shelukindo wamtetea Kinana

Tuhuma dhidi ya Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Abdulrahman  Kinana, (pichani) kuhusika katika usafirishaji wa pembe za ndovu, zimewalazimisha wabunge kadhaa wa  CCM kumsafisha.

Hali hiyo ilijitokeza juzi jioni wakati wakichangia hotuba hiyo ya Wizara ya Maliasili na Utalii.

Tuhuma hizo zilitolewa na Msemaji wa Kambi ya Upinzani, Mchungaji Peter Msingwa (Chadema), kuituhumu kampuni ya Sharaf Shipping Agency inayomilikiwa na Kinana kukamatwa na pembe za ndovu nchini China.

Mbunge wa Simanjaro , Christopher  Ole Sendeka (CCM), alimtetea Kinana kuwa kampuni yake haihusiki katika sakata la pembe za ndovu.

Chadema yachelea kujitoa mchakato wa Katiba

Sina mpango wa kujitoa kwenye Tume kwa kuwa nimekula kiapo kwa ajili ya Watanzania, hadi sasa sijaona sababu ya kutaka kujitoa, alisema Profesa Baregu.
Dar es Salaam. Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimeshindwa kutoa kauli kuhusu kujitoa kwake kwenye mchakato wa Katiba Mpya baada ya muda kilioutoa kwa Serikali kutaka kurekebishwa kwa baadhi ya mambo katika mchakato huo kumalizika juzi.
Mwenyekiti wa Chadema na Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe alisema bungeni Aprili 11, mwaka huu kuwa chama chake kitajitoa katika mchakato huo endapo mambo muhimu mawili hayatapatiwa ufumbuzi hadi kufikia Aprili 30, mwaka huu.
Mambo hayo ni kufutwa kwa uchaguzi wa wajumbe wa mabaraza ya wilaya ya katiba uliofanywa na Kamati za Maendeleo za Kata (WDC), badala yake wachaguliwe moja kwa moja na wananchi wa kata husika bila kuchujwa na kamati hizo.

YULE MHINDI ALIYEDAIWA KUMUUA MWALIMU WA SHULE YA MSINGI NAYE AJIUA.......!!!

MHINDI mwenye uraia wa India, Srinivasa Rao Talluri, 36 anayedaiwa kumuua Mwalimu Elizabeth Mmbaga wa Shule ya Msingi Atlas, jijini Dar es Salaam amejiua Aprili 17 mwaka huu katika Hoteli ya Transit iliyopo Karakata.

Talluri ambaye alikuwa akifanya kazi katika kampuni ya vinywaji vikali ijulikanayo kwa jina la Moan’s Drinks Ltd iliyopo Oysterbay, Dar maiti yake ilikutwa chumbani saa mbili asubuhi na inadaiwa alijiua kwa kunywa sumu ambayo mabaki yake yamepelekwa Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali kwa uchunguzi.
Habari za kipolisi zimesema kuwa baada ya wafanyakazi wa Hoteli ya Transit jijini Dar kugundua kuwa Mhindi huyo amekufa, walitoa taarifa polisi ambao walifika na walipochunguza chumbani, walikuta kuna pombe aina ya Pushkin chupa tatu, chupa yenye sumu ya kuulia wadudu, chips na maziwa glasi moja.
Marehemu Elizabeth Mmbaga enzi za uhai wake.
Inadaiwa kwamba Mhindi huyo aliachishwa kazi katika kampuni hiyo Aprili 2, mwaka huu baada ya kugundulika kuwa alitumia vibaya zaidi ya shilingi 400,000 ambapo Aprili 3, mwaka huu alifikishwa polisi Kituo cha Oysterbay, jijini Dar.
Mwandishi wetu alifika katika ofisi za Moan’s Drinks Ltd alikokuwa akifanyia kazi Mhindi huyo na kuonana na mmoja wa viongozi wa kampuni hiyo aliyejitambulisha kwa jina moja la Raju na akakiri kutokea kwa kifo cha Talluri.
Habari zinasema mwili wake ulifanyiwa uchunguzi katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili Jumatatu iliyopita na ukasafirishwa kupelekwa India Jumatano ya wiki iliyopita  kwa ajili ya mazishi.
Kitanda walichokuwa wakilala wapenzi hao.
Mhindi huyo anadaiwa kuwa alikuwa mpenzi wa Mwalimu Elizabeth ambaye siku moja kabla ya kifo chake imeelezwa kuwa alikuwa naye kwenye baa moja karibu na nyumba ya Eliza, hata hivyo, alikutwa amekufa katika chumba chake Kimara Baruti, Dar Aprili 15 mwaka huu huku shingoni kukiwa na michubuko iliyoashiria kuwa alinyongwa.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Ilala, ACP Marietha Minangi amethibitisha kutokea kwa kifo hicho katika hoteli hiyo.
“Ni kweli alikutwa amekufa katika Hoteli ya Transit na chumbani tulikuta sumu ambayo tumepeleka kwa Mkemia Mkuu wa Serikali kwa uchunguzi,” alisema.

CCM WAMVAA MKUU WA MKOA WA ARUSHA.....WANADAI AMEMUONGEZEA UMAARUFU GODBLESS LEMA...!!

VIGOGO wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wakiwemo wabunge, wamemjia juu Mkuu wa Mkoa (RC) wa Arusha, Magessa Mulongo kwa jinsi alivyoshughulikia kesi ya Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema (CHADEMA).

Wabunge hao waliliambia gazeti hili mjini Dodoma kuwa kesi ya uchochezi iliyofunguliwa na serikali dhidi ya Lema kwa shinikizo la mkuu huyo, itaiathiri kwa kiasi kikubwa CCM.

Mbunge wa Mwibara, Kangi Lugola alisema kuwa amefuatilia kwa makini chanzo cha kesi ya Lema na hatimaye kukamatwa na polisi mithili ya gaidi, na kubaini kuwa hulka 

za utendaji kazi wa baadhi ya viongozi wa serikali zinawapa sifa na umaarufu zaidi CHADEMA.
“Mimi sitaki kuingilia kesi, lakini ukiangalia kuanzia ile inayoitwa video ya vurugu za Chuo cha Uhasibu Arusha na jinsi Mkuu wa Mkoa alivyofika eneo la tukio na kuondoka, utabaini udhaifu mkubwa wa kiongozi huyo ambao leo unamfanya Lema aonekane shujaa.
“Leo tunaingia kwenye uchaguzi mdogo wa madiwani pale Arusha, tunaweza tukashinda, lakini tutafanya kazi ya ziada kwa sababu tu ya udhaifu wa Mkuu wa Mkoa wa Arusha,” alisema Lugola.

LIL WAYNE AZIDIWA TENA, AKIMBIZWA HOSPITALI.


According to TMZ, rapper Lil Wayne was rushed to Cedars-Sinai Hospital in L.A on Tuesday night after suffering another seizure. He was treated and released yesterday morning.
Wayne then did a radio interview yesterday afternoon and explained he's an epileptic, and has been suffering from seizures since he was a kid.

MWAKA MMOJA KABURINI... KANUMBA THE GREAT FILM INAPUMULIA MASHINE

Mojawapo ya ofisi za Kampuni ya Kanumba The Great Films illiyopo Sinza Mori.
MIPANGO endelevu inapaswa kufuatwa na kila mwanadamu, katika familia zetu za Kiafrika mara nyingi tunaanguka katika suala la mipango mikakati ya muda mrefu. Mwanadamu akifariki, mara nyingi wanaoachwa kuendeleza kazi za marehemu wanaishia kusuasua na kutofikia malengo.

Yapata mwaka mmoja tangu, aliyekuwa legend wa simema za Kibongo, Steven Kanumba ‘The Great’ afariki dunia na kuiacha Kampuni yake ya Kanumba The Great Film ikiendeleza shughuli zake za kuzalisha filamu kama kawaida.
Kampuni aliyoiacha pale Sinza-Mori, jijini Dar ilibaki chini ya mikono ya wafanyakazi wake  wakiongozwa na mdogo wa marehemu, Seth Bosco, mpiga picha za video, Zakayo Magulu pamoja na Mayasa Mrisho ‘Maya’ ambaye alikuwa akifanya kazi kama msimamizi wa ‘location’ (location manager) na masuala ya makeup.
Kadiri siku zilivyozidi kusonga, umoja kati yao ulianza kupungua. Kila mmoja anaonekana kuhangaika kivyake licha ya kwamba kampuni bado ipo. Mikakati ya jumla ikawa haijadiliwi, kila mmoja akawa anaangalia namna ya kujikwamua kivyake.
Mara kadhaa nimekuwa nikizungumza na baadhi ya wasanii waliokuwa tegemezi katika kampuni hiyo, wamekuwa wakiniambia wapo bize kufanya kazi zao binafsi nje ya Kanumba The Great Film. Hiyo inaonesha dalili kwamba kazi za umoja zimeanza kulegalega.

Marehemu Steven Kanumba akiwa na tuzo za filamu enzi za uhai wake.

MAGAZETI YA LEO ALHAMIS MEI 2, 2013

DSC 0001 bc82f


DSC 0003 2124b


DSC 0005 0924a

Mh. Rais Ang'atwa na Chui............!!!

 
Rais wa Botswana, Ian Khama ameshonwa baada ya kung'atwa na Duma, kwa mujibu wa maafisa wakuu nchini humo.

Mnyama huyo alikuwa analishwa alikokuwa anahifadhiwa katika kambi ya kijeshi wakati alipomrukia rais Khama na kumgwara

Tukio hilo ilikuwa ajali tu wala sio shambulio kali, kwa mujibu wa msemaji wa serikali Jeff Ramsay aliyezungumza na waandishi wa habari.

Majeraha ya Bwana Khama, yalikuwa madogo wala haikujitokeza kama ajali kubwa.
Inaarifiwa ajali ilitokea ghafla na kumgutukia Rais Khama na walinzi wake.

"Duma alimgwara tu lakini sio kumshambulia, kama wanavyodahani watu wengi,'' alisema bwana Ramsay.

Bwana Khama alionekana akiwa amevalia plaster kwenye mkutano ulioandaliwa baada ya tukio hilo.

Duma, ambao ndio wanyama wenye kasi kubwa zaidi ardhini, ni moja ya wanyama wanaokabiliwa na tisho kubwa la kuangamia.

Ni wanyama 12,400 pekee wanaosemekana kusalia mbugani katika baadhi ya nchi za Afrika ikiwemo Botswana.

WASTARA AKATAA KUWA MKE WA PILI

http://api.ning.com/files/rCNzRKkcZYaRl8rT2Ghdp11G9XsjfHgOhCzL8GUhxCcWXmVRrcxNgzbihjqVgYMmwttiYFQiMBFUCChccEmDHRHxexbh7OqI/Wastara.jpg 
                                                          Wastara Juma.
MSANII wa filamu za Kibongo, Wastara Juma hivi karibuni alikataa kuolewa na kuwa mke wa pili baada ya kupigiwa simu na mwanamke mmoja jijini Dar akimtaka awe mke mwenzake.
Wastara ambaye hivi sasa yuko Uarabuni kwa ajili ya mapumziko baada ya kufiwa na mumewe, Sadick Juma Kilowoko ‘Sajuki’, Januari mwaka huu, alikataa ofa hiyo na kusema kwamba kwa sasa hafikirii kabisa kuolewa.
Kwa mujibu wa chanzo chetu makini, mwanamke huyo aliamua kufanya hivyo baada ya kushauriana na mumewe kuhusu Wastara kuingia katika familia yao.
“Mwenyewe alisema alishauriana na mumewe na haoni tatizo Wastara kuwa mke mwenzake kwa sababu imani ya dini yao inaruhusu,” kilieleza chanzo hicho.

MHASHAMU TITUS ASIMIKWA KUWA ASKOFU MSAIDIZI DAR

IMG_0286  
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na MwadahamaPolycarp Kaldianali Pengo (kushoto) wakishuhudia wakati Mhashamu Titus Mdoe, Askofu Msaidi wa Jimbo Kuu la Dar es salaam katika Misa ya kumsimika Askofu huyo zilizofanyika kwenye viwanja vya Msimbazi Centre jijini Dar es salaam Me 1, 2013. (Picha na  Ofisi ya Waziri Mkuu)
IMG_0326 
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akimkabidhi zawadi ya picha Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu la Dar es slaam, Mhashamu Titus Mdoe katika ibada ya kumsimika askofu huyo iliyofanyika kwenye viwanja vya Msimabazi Centre jijini Dar es salaam, Mei 1, 2013 . kulia ni Mke wa Waziri Mkuu, Mama Tunu Pinda. (picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)IMG_0330 
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na  Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu la Dar es slaam, Mhashamu Titus Mdoe katika ibada ya kumsimika askofu huyo iliyofanyika kwenye viwanja vya Msimabazi Centre jijini Dar es salaam, Mei 1, 2013 . kulia ni Mke wa Waziri Mkuu, Mama Tunu Pinda. (picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...