DAR ES SALAAM. KWA mara ya kwanza Rais Jakaya Kikwete amemtolea uvivu Rais wa Rwanda, Paul Kagame kutokana na kitendo chake cha kumtolea lugha za matusi baada ya kumshauri kukaa meza moja na vikundi vya waasi wa nchi yake (FDLR), huku akimtaka kuacha kukuza mgogoro usiokuwepo.
Rais Kikwete alitoa ushauri huo kwa Rwanda
takribani miezi miwili iliyopita wakati akizungumza katika kikao cha
Mkutano wa Umoja wa Afrika (AU) uliofanyika mapema mwaka huu, mjini
Addis Ababa, Ethiopia, ambao ulikuwa ukij
adili suala la amani ya Jamhuri
ya Kidemokrasi ya Congo (DRC) pamoja na Ukanda wa Maziwa Makuu.
Ushauri huo pia uliwagusa Rais Yoweri Museveni wa
Uganda na Joseph Kabila (DRC), ambao aliwataka kufanya mazungumzo na
waasi wanaopingana na Serikali zao.







