Monday, December 29, 2014

MTIBWA SUGAR CHUPU CHUPU KWA STAND

TIMU ya soka ya Mtibwa Sugar ambao ni vinara wa Ligi Kuu Tanzania bara jana ililazimishwa sare ya bao 1-1 na Stand United ya Shinyanga katika mechi iliyochezwa kwenye Uwanja wa Manungu, Turiani Morogoro jana asubuhi.
Mchezo huo ilikuwa uchezwe juzi lakini ulivunjika katika dakika ya sita baada ya mvua kubwa iliyosababisha maji kujaa kwenye uwanja wa Manungu na kuamuliwa uchezwe jana saa mbili asubuhi.
Katika mchezo huo wa jana wachezaji wa Stand United walionesha mpira wa kuvutia hasa kipindi cha kwanza na kuwawezesha kupata bao la kuongoza katika dakika ya 22 ya mchezo.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.
 
Bao hilo lilipachikwa na mshambuliaji wa timu hiyo, Shaaban Kondo baada ya kuunganisha krosi ya Haruna Chanogo. Baada ya kuingia bao hilo Mtibwa Sugar ilikianza kipindi cha pili kwa mashambulizi makali langoni mwa Stand United, lakini kikwazo kikubwa alikuwa kipa Mohamed Makaka kwa kuokoa mikwaju mingi ya hatari ya washambuliaji wa timu ya Mtibwa Sugar.
Juhudi za Mtibwa kusaka bao la kusawazisha zilizaa matunda katika dakika ya 86 baada ya Said Mkopi kufunga kwa kichwa. Mkopi aliliokoa jahazi la timu yake lisizame baada ya kutumia vyema mpira wa kona na iliyochongwa na Jamal Mnyate .
Wakati huo huo, katika mechi iliyochezwa kwenye uwanja wa Jamhuri Morogoro jana jioni Polisi ya mjini hapa iliibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Mgambo JKT ya Tanga.
Polisi ilianza kuandika bao la kuongoza katika dakika ya 22 mfungaji akiwa Nicolas Kabipe aliyefunga kwa shuti kali baada ya kuunganisha pasi ya Said Bahanuzi kabla ya kumbabatiza kipa wa Mgambo, Said Lubawa.
Imani Mapunda aliifungia Polisi bao la pili kwa kichwa baada ya kuunganisha mpira wa kona iliyopigwa na Kabipe.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...