Monday, November 10, 2014

RAIS OBAMA AIZUNGUMZIA IRAQ

Rais wa Marekani Barack Obama
Rais Obama amesema awamu ya kwanza ilikuwa ni kwa ajili ya kuandaa serikali ya pamoja na yenye kuaminika nchini Iraq. Kitu ambacho amesema kimefanyika, na kuongeza kwamba muungano huo wa kijeshi unaopambana dhidi ya kundi hilo la wapiganaji unajiandaa kwa mashambulizi.
Tulichojua ni kwamba awamu ya kwanza iulikuwa ni kupata serikali ya umoja wa Kitaifa na ya uhakika Iraq. Na tumefanya hicho. ''..Na sasa tulichofanya ni zaidi ya kulimaliza nguvu kundi hilo la ISIL.
Kwa sasa tupo katika nafasi ya kuanza tena mashambulio kama ya awali. Mashambulizi ya anga yaliyofanywa yalifanikiwa katika kushusha uwezo wa kundi hilo la ISIL na kupunguza nguvu hatua waliyopiga.
Sasa tunachohitaji ni jeshi la ardhini, Jeshi la ardhini la Iraq, litakaloweza kuwarudisha nyuma..'' Nchini Iraq kwenyewe maafisa wanasema jeshi limekuwa likipiga hatua katika jihada za kuwaondoa wapiganaji hao wa kiislamu katika mji wa Baiji. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...