******
DAR ES SALAAM.
MTANGAZAJI wa Kituo cha Televisheni cha ITV, Ufoo Saro ambaye alijeruhiwa kwa kupigwa risasi na mzazi mwenzake, Anthery Mushi, amefanya ibada na kusema: “Namshukuru Mungu kwa kumponya.”
Ni mara ya kwanza Saro kuzungumza tukio hilo tangu
aliporuhusiwa kutoka Taasisi ya Mifupa na Mishipa ya Fahamu, MOI ya
Hospitali ya Taifa Muhimbili alikokuwa amelazwa.
Katika ibada hiyo iliyofanyika katika Kanisa la
Kilutheli Tanzania (KKKT) Usharika wa Kibamba, Jimbo la Magharibi, Ufoo
huku akitokwa na machozi na wakati mwingine kushindwa kuzungumza
alisema: “Ni miujiza tu ya Mungu yeye kunifanya mimi kuwa hai leo.”
Mtangazaji huyo ambaye alilazwa kwa zaidi ya wiki
mbili, aliwashukuru watu wote waliomtia moyo, kumsaidia kipindi chote
alichokuwa mgonjwa.