Mhe.Mbowe na Mhe. Lema wakishauriana jambo..
Monday, June 17, 2013
PICHA ZA MH. FREEMAN MBOWE AWATEMBELEA MAJERUHI NA WAFIWA WA BOMU LILILOLIPUKA SOWETO JIJINI ARUSHA
VIONGOZI NA WAZAZI WAASWA KUFICHUA UOVU DHIDI YA WATOTO
(Picha na maktaba)
Na Mwandishi Wetu Steven Kanyeph.Viongozi wa serikali kwa kushilikiana na wazazi wametakiwa kutoa taarifa kwenye vyombo husika wanapoona watoto wanafanyiwa vitendo vya ukatili unyanyasaji wa kijinsia, ukeketaji na kuozeshwa katika umri mdogo.
Hayo yamesemwa na mgeni rasmi kwa niaba ya mkuu wa mkoa ambaye ni mkuu wa wilaya ya kishapu bwana; Willson Mkambaku kwenye maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika yaliyofanyika kimkoa katika viwanja vya shule ya msingi Bubiki kata ya Bubiki wilayani Kishapu mkoani Shinyanga.
Bwana Mkambaku amewataka viongozi na wazazi washilikiane kwa pamoja kuhakikisha watoto wanalindwa dhidi ya unyanyasaji, ubakaji .ulawiti , na kuhakikisha kuwa watoto wanaendelezwa kielimu kushiriki katika maamuzi , ikiwa ni pamoja na kukomesha ajira kwa watoto.
Aidha watoto waameitaka jamii kwa kushirikiana na viongozi kupiga vita imani potofu zenye kuleta madhara kwa watoto kama vile ukeketaji ,ndoa za lazima, uasherati , mauaji ya vikongwe ,albino pamoja na madawa ya kulevya.,
Madhimisho ya siku ya mtoto wa afrika hufanyika kila mwaka tarehe 16 mwezi wa 6 lengo ni kukumbuka mauaji ya kikatili ya mamia ya watoto wa shule yaliyofanyika katika kitongoji cha Soweto afrika ya kusini mwaka 1976 baada ya watoto kufanya maandamano ya kupinga ubaguzi wa rangi.
Kauli mbiu ya madhimisho hayo kwa mwaka huu ni KUONDOA MILA ZENYE KULETA MADHARA KWA WATOTO NI JUKUMU LETU SOTE
WABUNGE WA CHADEMA WAGOMA KUINGIA BUNGENI KUFUATIA BOMU LA ARUSHA...IGP ATOA NAMBA YAKE KWA MTU YEYOTE MWENYE TAARIFA

Wakati
Jeshi la Polisi nchini limesema limepata taarifa za mwonekano wa mtu
aliyetupa bomu katika mkutano wa kampeni wa Chama cha Demokrasia na
Maendeleo (Chadema) Arusha,Mwenyekiti wa chama hicho Freeman Mbowe
amesema wabunge wake leo hawataingia bungeni.
Akizungumza
na waandishi wa habari jana, Mbowe alisema wabunge hao watawasili
Arusha kwa ajili ya kuungana na wananchi pamoja na wanachama kwenye
msiba huo.
Alisisitiza
kwamba kuanzia leo mahema yatawekwa viwanja vya Soweto kwa ajili ya
kuomboleza msiba huo na mara polisi wakimaliza uchunguzi wao na kutoa
majibu juu ya vifo hivyo, marehemu hao watasafirishwa.
Wakati
Mbowe anatoa kauli hiyo Waziri wa Mambo ya Ndani, Dk Emmanuel Nchimbi
akizungumza jana mjini Arusha na waandishi wa habari, alisema taarifa za
awali zinaonesha mlipuko huo ni bomu la kutupwa kwa mkono (grumeti) na
hivi sasa timu ya wataalamu ikiongozwa na Kamishna wa Operesheni
Maalumu wa Jeshi la Polisi, Paul Chagonja inaendelea na uchunguzi wa
tukio hilo.
Naye
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP),
Said Mwema katika taarifa yake kwa vyombo vya habari ameahidi kupambana
na kuhakikisha wahusika wanapatikana.
Sunday, June 16, 2013
BINTI ACHOMWA MOTO HADI KUFA BAADA YA KUOMBA AOLEWE NA NDUGU YAKE...!!!

Msichana
wa miaka 19 amechomwa moto hadi kufa na mama yake kupigwa baada ya
kuwaomba wazee wa kijiji kuruhusiwa kuolewa na mvulana mmoja kutoka
kijijini hapo na ukoo mmoja, polisi wa India wamethibitisha.
Anju
Yadav, kutoka kijiji cha Karahkol, wilayani Deoria katika jimbo la
Uttar Pradesh, alichomwa moto nyumbani kwake wakati mama yake, Gyanwati
Devi, mwenye miaka 48, alipokuwa upande mwingine wa kijiji hicho
akiiomba halmashauri ya kijiji kumruhusu Anju aolewe na rafiki yake wa
kiume aliyekuwa na mahusiano naye kwa miaka miwili, Ranjit Yadav, mwenye
miaka 21.
Lakini
halmashauri ya kijiji hicho, sambamba na baba wa mvulana huyo, Jai Hind
Yadav, mwenye miaka 52, walitupilia mbali maombi hayo wakisisitiza
ilikuwa kinyume cha utamaduni.
Badala yake, baba wa mvulana huyo alikimbilia kwenye nyumba ya familia na kumchoma moto msichana huyo, ilidaiwa.
Jamii
ya India inafahamika mno kwa mfumo wake wa ukoo ulioingiliana, ambao
unaweza kuzuia watu kutoka jamii tofauti kuoana na katika baadhi ya
matukio kuafikiana na jambo kama hilo.
OMMY DIMPOZ AANZA SAFARI YA KWENDA NYUMBANI KWA AKINA MANGWEA KUOMBA MSAMAHA

Kutokana
na kauli aliyotoa msanii Ommy Dimpoz ya SITAKUFA KIJINGA NA KIMASIKI
KAMA KAMA ALIVYOKUFA NGWAIR, hii ndio kauli aliyotoa baada ya mashabiki
na Wanamuziki wenzake kumaind kwa kile alichokisema

NANUKUHU:
"Samahani
tena sana sitawacha kuomba msamaha, nimekubali makosa na hivi sasa
naelekea nyumbani kwao kuomba msamaha kwa familia na nitue kwa vituo vya
radio kuomba msamaha kwa wabongo na wote niliowaudhi. Samahani sana na
nakubali mimi si mtu bila nyinyi na sikuongea kuhusu legend Ngwair kwa
ila mbaya. One love". mwisho wa kunukuu
KIM KARDASHIAN AJIFUNGUA MTOTO WA KIKE...!!!

NI
siku ya furaha kwa Kanye West! Kim Kardashian amejifungua mtoto wa kike
Jumamosi asubuhi katika hospitali ya Cedars-Sinai Medical Center, Los
Angeles, mtandao wa OMG umethibitisha.
Inasemekana Kardashian, 32, alikuwa na West pembeni mwake wakati wa kujifungua, kumkaribisha duniani binti yao mwezi mmoja kabla ya muda uliotarajiwa. Tarehe halisi ya kujifungua ilitazamiwa kuwa Julai 11.
"Kim aliugua Ijumaa usiku na hatimaye kupata mtoto mapema," chanzo cha hospitali kimeileza Us Weekly. “Inafurahisha, wote katika hali nzuri!"
Kanye West, 36, na Kim - wote wawili wakiwa ndo mara ya kwanza kuwa wazazi, wamekuwa wapenzi tangu Aprili 2012. Desemba 30, 2012, West alitangaza kwamba mpenzi wake alikuwa na mimba wakati wa tamasha lake Atlantic City.
"Simamisha muziki na wote mpige kelele kwa mama kijacho," alisema West jukwaani akionyesha kidole kwa Kim ambaye alikuwa mmoja wa watazamaji.
Inasemekana Kardashian, 32, alikuwa na West pembeni mwake wakati wa kujifungua, kumkaribisha duniani binti yao mwezi mmoja kabla ya muda uliotarajiwa. Tarehe halisi ya kujifungua ilitazamiwa kuwa Julai 11.
"Kim aliugua Ijumaa usiku na hatimaye kupata mtoto mapema," chanzo cha hospitali kimeileza Us Weekly. “Inafurahisha, wote katika hali nzuri!"
Kanye West, 36, na Kim - wote wawili wakiwa ndo mara ya kwanza kuwa wazazi, wamekuwa wapenzi tangu Aprili 2012. Desemba 30, 2012, West alitangaza kwamba mpenzi wake alikuwa na mimba wakati wa tamasha lake Atlantic City.
"Simamisha muziki na wote mpige kelele kwa mama kijacho," alisema West jukwaani akionyesha kidole kwa Kim ambaye alikuwa mmoja wa watazamaji.
HABARI YA KINA KUHUSU MLIPUKO WA BOMU ARUSHA
Mkutano wa Chadema wa kumaliza kampeni za uchaguzi mdogo wa udiwani
mjini Arusha, jana ulivunjika baada ya bomu kulipuka na kuua watu wanne
na wengine kujeruhiwa.Bomu hilo
lililipuka jana saa 11:50 dakika chache kabla ya Mwenyekiti wa chama
hicho Taifa, Freeman Mbowe kumaliza kuhutubia mkutano huo uliofanyika
katika Viwanja vya Soweto mjini Arusha na kuhudhuriwa na mamia ya
wananchi.Hilo ni tukio la pili la
bomu kulipuka katika mkusanyiko wa watu, Mei 5 mwaka huu bomu
lililipuka katika Kanisa Katoliki la Mtakatifu Joseph Mfanyakazi,
Parokia ya Olasit mjini Arusha na kuua watu watatu na wengine
kujeruhiwa.
Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mount Meru Frida Mokiti alisema katika hospitali yake kuna maiti moja ya mtoto na majeruhi 11.Habari zingine zilisema katika hospitali ya Misheni ya Selian kuna maiti za watu wawili, waliokufa kutokana na shambulio hilo na majeruhi ambao idadi yao haijafahamika.Akizungumzia tukio hilo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas alisema katika tukio hilo watu wawili wamepoteza maisha, mwanamke na mwanamume na kwamba idadi ya majeruhi bado haijafahamika kwa kuwa wametawanywa katika hospitali mbalimbali mkoani humo.
Mama akikimbizwa hospitali kupata matibabu.
Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mount Meru Frida Mokiti alisema katika hospitali yake kuna maiti moja ya mtoto na majeruhi 11.Habari zingine zilisema katika hospitali ya Misheni ya Selian kuna maiti za watu wawili, waliokufa kutokana na shambulio hilo na majeruhi ambao idadi yao haijafahamika.Akizungumzia tukio hilo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas alisema katika tukio hilo watu wawili wamepoteza maisha, mwanamke na mwanamume na kwamba idadi ya majeruhi bado haijafahamika kwa kuwa wametawanywa katika hospitali mbalimbali mkoani humo.
HILI NDILO CHIMBUKO LA JINA LA ANACONDA ANALOTUMIA JAYDEE
Huyu naye alikuwepo ili kuonyesha uhalisia wa jina la Anaconda ambalo sasa anatumia msanii mkongwe wa muziki wa kizazi kipya nchini Jay Dee, ambapo jina hilo limetokana na vuguvugu ambalo linaendelea hivi sasa ambalo hilo vuguvugu ndilo limechangia shoo ya mwanamuziki huyo kujaa huku mashabiki wakionyesha hali ya kumshinda mtu anyemkandamiza msanii huyo |
CHADEMA YAKANA TUHUMA ZA KUUA WATU.
![]() |
Singo Kigaila. |
Huku
kukiwa na madai kuwa Chadema inahusika na matukio ya kula njama za
utekaji na kuteka, kupiga na kuua watu, chama hicho kimekuja juu na
kukanusha madai hayo.
Pamoja
na kukanusha, kimemwomba Rais Jakaya Kikwete aunde tume huru ya
kimahakama kuchunguza matukio yaliyotokea ili hatua za kisheria
zichukuliwe dhidi ya wote watakaobainika kuhusika.
Akizungumza
na Waandishi wa Habari Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Mafunzo na
Oganaizesheni wa chama hicho, Singo Kigaila, alisema walishamwomba Rais
aunde Tume lakini akadai ombi hilo halijatekelezwa hadi sasa.
Saturday, June 15, 2013
JOH MAKINI ALAZWA SINZA PALESTINA, HII NDIO MESEJI YAKE
POLISI WAMTIA MBARONI MAMA ALIYEMTUPA MTOTO BAADA YA BABA WA MTOTO KUMKANA KISA ANA NYWELE ZA KIARABU

Binti mmoja aliyefahamika kwa jina la Khadija Idd anashikiliwa na jeshi la polisi mkoani Morogoro akidaiwa kumtupa barabarani mtoto wake mwenye umri wa miezi 6 baada ya mwanaume aliyezaa naye kumkataa.
Shuhuda wetu ambaye ni dereva wa bodaboda aliyefahamika kwa jina la Shabani, alisema tukio hilo lilitokea Juni 11, mwaka huu maeneo ya Mafiga karibu na Msikiti wa Mahita ambapo Khadija alichukua uamuzi huo baada ya mwanaume aliyezaa naye kumgomea mtoto kwa madai ana nywele za Kiarabu hivyo si wake.
“Huyu dada alifika kwenye kijiwe chetu akiwa amembeba mtoto mgongoni na kukodi pikipiki ili nimpeleke mjini.
“Tulipofika kwenye msitu uliopo karibu na mashamba ya SUA, aliniambia niendeshe spidi kuna mtu anamuwahi.
Nilitii amri lakini tulipofika mbele kidogo nikashangaa anamtupa yule mtoto.
RAIS OBAMA AHAIRISHA ZIARA YAKE YA KUZITEMBELEA NCHI ZA AFRICA IKIWEMO TANZANIA...!!!

WAKATI Serikali ya Tanzania ikiendelea na maandalizi ya kupokea msafara wa watu 700 waliotarajia kuingia nchini kwa ziara ya Rais wa Marekani Barack Obama, Rais huyo amesitisha safari yake.
Ikulu ya Marekani imetangaza kwamba msafara wa Rais Obama kuja kutembelea Bara la Afrika haitakuwepo tena,baada ya serikali ya nchi hiyo kukosa fedha itakayoweza kugaramia safari ya Rais huyo.
Taarifa
iliyonaswa na kutoka katika mitandao mbalimnali nchini Uingereza na
Marekani zinaeleza kwamba mbali na suala la bajeti ya Rais huyo kuja
nchini Tanzania kuwa kubwa pia kamati ya sheria ,ulinzi na usalama wa
Marekani imeshindwa kuthibitisha juu ya suala la ulinzi na Usalama wa
Rais Obama katika kipindi chote atakachokuwa nchini Tanzania pamoja na
baadhi ya nchi Barani Afrika.
Taarifa
hiyo pia ilieleza kwamba msafara wa Rais Obama unahitaji maandalizi ya
kutosha kwa sababu ni msafara unaohusisha watu wengi pamoja na vyombo
mbalimbali vya ulinzi ikiwemo wanyama.
Msemaji
wa Ikulu ya Marekani alisema kwamba serikali ilijaribu kuangalia
uwezekano wa Rais Obama kuja Tanzania na baadaye kutembelea Senegel
pamoja na Afrika Kusini ambapo alitakiwa kukaa Tanzania kwa saa mbili
tu lakini gharama za ulinzi imekuwa kubwa sana.

Katika
msafara wa Obama inatakiwa kuwe na ndege mbili za mwendo kasi, kwa
ajili ya kulinda ndege ya Rais,iwepo ndege za askari wa majini
zinazotembea kwenye meli habarini, iwepo pea maalum za magari zitakazo
sushwa katika nchi zote tatu mapema kwa kutumia ndege za jeshi kwa ajili
kuimarisha ulinzi kabla ya Rais kutua katika nchi hizo" alisema Mseaji
wa Ikulu ya marekani Josh Earnest.
Nakala
ya taarifa hiyo pia ilimkariri msemaji huyo wa Ikulu ya Marekani
akisema kwamba pia katika msafari huo ni lazima iwe na vifaa maalum vya
kutolea matibabu katika kipindi chote cha ziara ya Rais, lazima pia
iwe na chombo maalum kwa ajili ya waandishi mbalimbali wa habari pamoja
na vyombo vingine vya usalama kwa ajili ya kutoa taarifa ya safari ya
Rais ,pamoja ndege zitakazokuwa zikizunguka kuangalia hali ya usalama
katika hoteli zote atakapo kuwa ana alala Rais Obama na msafara wake.
Taarifa
hiyo ilifafanua kwamba safari hiyo ndiyo safari kubwa kuliko aliyowahi
kuifanya Barani Afrika ambapo alifika nchini Ghana, tangu
alipochaguliwa kuwa Rais wa Marekani mwaka 2009 ambapo inakadiriwa kuwa
itachukua kati ya dola za marekani 60 million sawa na tsh bilioni
96,000,000,000 na dola 100 milion sawa tsh bilioni 160,000,000,000.
Subscribe to:
Posts (Atom)