Tuesday, January 03, 2017

PLUIJM AKARIBIA KUPEWA MIKOBA YA UKOCHA AZAM FC

Mabingwa watetezi wa Kombe la Kagame, Azam FC wamebakiza hatua chache kukamilisha mpango wa kumkabidhi timu hiyo aliyekuwa kocha wa zamani wa Yanga, Hans Pluijm.

Habari za kuaminika kutoka vyanzo makini ndani ya Azam zilithibitisha kuwa tayari Azam imekuwa na mazungumzo ya kina na kocha huyo Mdachi ambaye kwa sasa ni mkurugenzi wa ufundi Yanga.
Awali, Azam ilipanga kumpa timu hiyo kocha wa Majimaji, Kally Ongala ambaye amewahi kuitumikia klabu hiyo kama kocha msadizi, lakini wakabadilisha mawazo kutokana na kocha huyo kuwa na uzoefu mdogo na michezo ya kimataifa.

Mwenyekiti wa Azam, Nassoro Idrissa ‘Father’ amesema Pluijm ni kocha wa kiwango cha juu na amethibitisha hilo nchini kwa kuipa Yanga mataji manne tofauti, hivyo watafurahi kama atafanya nao kazi. Tangaza biashara yako hapa. Pia like page yetu ya facebook Jambo Tz. tu-follow instagram @jambotz.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...