Wednesday, December 13, 2017

VIGOGO WENGINE WA ACT WAHAMIA CCM

 Mwenyekiti na katibu wa Chama cha ACT Wazalendo mkoani Singida, wamejivua uanachana na vyeo vyao na kuhamia CCM.

Viongozi hao ni aliyekuwa mwenyeketi Wilfred Noel Kitundu na katibu wa mkoa wa chama hicho, Loth Robert Thomas.
Viongozi hao wamechukua uamuzi huo mbele ya mkutano mkuu wa uchaguzi CCM mkoa wa Singida uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Chuo cha Uhazili mjini hapa juzi.

Kwa nyakati tofauti walisema changamoto ambazo upinzani walikuwa wakizipigia kelele, Rais John Magufuli ameendelea kuzitatua kwa ufanisi.

Tuesday, December 05, 2017

MBWA WA POLISI WAMUUMBUA ALIEDANGANYA KUWA KAPOLWA MIL. 20 ZA KAMPUNI

Mfanyakazi  wa kampuni ya saruji ya Simba Cement, Edward Ngassa amekamatwa na Jeshi la Polisi mkoani Dodoma kwa tuhuma za kutengeneza tukio la uongo la kuporwa Sh. milioni 20.4 na majambazi jana.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi mkoa wa Dodoma, Gilles Muroto, mbwa wa polisi mwenye mafunzo ndiye aliyegundua udanganyifu huo wa Ngassa nyumbani kwake.

Kamanda Muroto alisema mtuhumiwa huyo alitengeneza tukio la uongo kwamba ameporwa fedha na majambazi katika eneo la Uhindini karibu na mgahawa wa Sunja.

Saturday, December 02, 2017

MKULIMA AFARIKI KWA KUPIGWA NA RADI AKIWA SHAMBANI USIKU

Mkazi mmoja wa kijiji cha Senga Kata ya Kamsamba wilaya ya Momba aliyetambuliwa kwa jina la Cleo Saini (23/25)amefariki baada ya kupigwa na radi alipokuwa analima kwa jembe la kukokotwa na ng'ombe mapema saa tisa usiku.

Pamoja na marehemu kufariki pia ng'ombe wawili waliokuwa wakikokota jembe wamekufa. Mtendaji wa kijiji cha Kamsamba Venance Athanas ametoa taarifa Polisi Kituo cha Kamsamba.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Songwe Mathias Nyange amekiri kutokea kwa tukio ambapo Polisi wamekwenda eneo la tukio kwa uchunguzi zaidi wa tukio hilo.

SOMA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI DECEMBER 02, 2017 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

https://jambotz8.blogspot.com/

 
Subscribe katika YouTube channel ya Jambo Tz upate kuona habari na matukio mbalimbali toka duniani kote.

MBUNGE NASSARI AVAMIWA NA MAJAMBAZI USIKU WA LEO

Katika ukurasa twitter wa Mh. Joshua Nassari ameandika kuwa amevamiwa na watu waliokuwa na silaha za moto, na mara baada ya yeye pamoja na mkewe kuwagundua waliamua kukimbilia kituo cha polisi yeye ili kuokoa maisha yao.

Sunday, November 26, 2017

RAIS MAGUFULI ATOA SIKU SABA KWA VYOMBO VYA UCHUNGUZI KUBAINI MMILIKI WA MAGARI YALIYOTELEKEZWA BANDARINI

Haya ndio maagizo ya Rais John Pombe Magufuli Bandarini leo baada ya kugundua uwepo wa magari zaidi ya 50 yaliyoingizwa nchini kwa kutumia jina la Ofisi ya Rais.

Saturday, November 25, 2017

TAZAMA VIDEO YA WAZIMBABWE WAKIIGIZA JINSI MUGABE ALIVYOLAZIMISHWA KIJIUZULU

Subscriber to our channel on YouTube @jambotz upate video nyingine zaidi.

PROF. LIPUMBA "SIKUTEGEMEA KAMA DR. SLAA ATATEULIWA"

Mwenyekiti wa Chama cha CUF, Profesa Ibrahim Lipumba amezungumzia uteuzi wa Dk. Wilbroad Slaa kuwa balozi akisema hakutarajia.

Rais John Magufuli juzi alimteua Dk. Slaa aliyewahi kuwa katibu mkuu wa Chadema kabla ya kukihama chama hicho wakati wa kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015.

Wakati wa mchakato wa uchaguzi huo, Profesa Lipumba na Dk. Slaa ambao vyama vyao vilikuwa katika umoja uliojulikana Ukawa, walijiondoa baada ya Chadema kumpitisha Waziri Mkuu wa zamani Edward Lowassa kuwa mgombea wake wa urais.

Akizungumza na Mwananchi jana, Profesa Lipumba alisema, “Imekuwa kama surprise, sikutegemea kama Dk. Slaa atateuliwa kwa sababu muda mwingi yupo Canada”.

Hata hivyo, Profesa Lipumba alisema hana shaka na uteuzi huo “Narudia, sikutegemea. Ila popote atakapopangiwa kazi Dk. Slaa atafanya kwa sababu najua ni mchapakazi,” alisema.
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe alisema Rais Magufuli ana mamlaka kisheria ya kumteua mtu atakayemuona anafaa katika nafasi fulani.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...