Saturday, May 14, 2016

HII NDIO YANGAAA.... WAKABIDHIWA RASMI KOMBE LA UBINGWA WA VPL

Waziri wa Kilimo na Mifugo Mh. Mwigulu Nchemba (kushoto) ambaye alikuwa mgeni rasmi wa mchezo huo akikabidhi kombe hilo kwa nahodha Nadir Haroub ‘Cannavaro’ baada ya kumalizika kwa mchezo kati ya Ndanda FC Yanga dhidi ya Yanga uliomalizika kwa timu hizo kutoka sare ya kufungana magoli 2-2.
Kikosi cha Yanga wakishangilia baada ya kukabidhiwa kombe lao.
Donald Ngoma (kushoto) na Simon Msuva wakipongezana wakati wa mchezo wa leo.
Yanga imekabidhiwa taji lao la ubingwa wa VPL msimu wa 2015-16 baada ya kufanikiwa kulitetea taji hilo ambalo walilitwaa msimu uliopita. Yanga imepewa kombe hilo ikiwa na pointi 74 huku ikiwa na mchezo mmoja mkononi baada ya kuifunga Ndanda FC kwenye uwanja wa taifa.

Ndanda walianza kupata goli kwa mkwaju wa penati Omary Mponda lakini bao hilo lilisawazishwa na Simon Msuva dakika chache baadaye. Donald Ngoma akaifungia Yanga bao la pili na kuiweka mbele klabu yake lakini Salum Minely akachomoa bao hilo na kuilazimisha Yanga kwenda sare kwenye uwanja wa taifa ambao Ndanda ndiyo walikuwa wenyeji katika mchezo huo. 
Waziri wa Kilimo na Mifugo Mh. Mwigulu Nchemba ambaye alikuwa mgeni rasmi wa mchezo huo alilikabidhi kombe hilo kwa nahodha Nadir Haroub ‘Cannavaro’ baada ya kumalizika kwa mchezo kati ya Ndanda FC Yanga dhidi ya Yanga uliomalizika kwa timu hizo kutoka sare ya kufungana magoli 2-2. 

Ubingwa huo unawafanya Azam FC kulikosa taji hilo ndani ya misimu miwili mfululizon wakati Simba wao wameendelea kulikosa taji hilo ndani ya misimu minne mfululizo.

KAGAME AKANA KUWASAIDIA WAASI WA BURUNDI


Rais wa Rwanda Paul Kagame

Rais wa Rwanda Paul Kagame amekana madai yaliotolewa na Umoja wa Mataifa kwamba taifa lake linaendelea kuwasaidia waasi katika nchi jirani ya Burundi.

Kagame amesema kuwa tatizo la Burundi linatoka ndani ya nchi hiyo, na sio nje. Burundi imekabiliwa na mgogoro mbaya wa kisiasa tangu rais Pierre Nkurunziza kuamua kupigania muhula mwengine mwaka uliopita.

Ni mwaka mmoja kamili tangu rais Nkurunziza kuepekua jaribio la mapinduzi. Rwanda ilikana madai kama hayo kuhusu kuwaunga mkono waasi katika ripoti ya awali ya Umoja wa Mataifa mnamo mwezi Februari.

Pia Kagame amekosoa wachapishaji wa ripoti hiyo ambayo inatarajiwa kuwasilishwa katika baraza la usalama la Umoja wa Mataifa baadaye,ikisema mda wake ungetumika vyema kuangazia matatizo yanayokumba mataifa badala ya kuyazidisha. 

Ripoti hiyo iliopatikana na chombo cha habari cha Reuters imeishtumu Rwanda kwa kutoa mafunzo pamoja na usaidizi wa kifedha kipindi chote cha mwaka 2016 kwa waasi wanaolenga kumuondoa madarakani rais Pierre Nkurunziza.

UN "UHUSIANO WA IS NA BOKO HARAM NI TISHIO"


Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa limeelezea wasiwasi wake kuhusu kasi ya kuimarika kwa ushirikiano kati ya kundi la wapiganaji la Boko Haram nchini Nigeria na lile la Islamic State, wakati Nigeria inaandaa kongamano la kupambana na kundi hilo la kigaidi.

Katika taarifa kwa vyombo vya habari, baraza hilo la wanachama 15 limesema kuwa Boko Haram linaendelea kuwa tishio kwa amani na usalama wa mataifa ya Afrika Magharibi na Afrika ya kati.

Boko Haram lilitangaza utiifu wake kwa Islamic State mwaka jana, na inaripoitiwa kuwa liliwatuma wapiganaji wake kuungana na Islamic State nchini Libya. 

Baraza hilo pia limekaribisha kongamano lililoandaliwa na rais wa Nigeria Mohamadu Buhari siku ya Jumamosi, kuangazia upya jitihada za kupambana na wapiganaji hao. Kongamano hilo litahudhuriwa na viongozi wa kikanda pamoja na rais wa ufaransa Francois Hollande.

Thursday, May 05, 2016

SNURA AWAOMBA RADHI WATANZANIA, AWASILISHA VIDEO SAFI YA CHURA BASATA

Snura amewaomba radhi watanzania kwa video ya wimbo wake ‘Chura’ inayowadhalilisha wanawake na iliyo kinyume na maadili. Muimbaji huyo amekutana na waandishi wa habari Alhamis hii kwenye ukumbi wa Habari Maelezo jijini Dar es Salaam.
 
Jana video na wimbo huo vilifungiwa na wizara ya habari, utamaduni, sanaa na michezo kwa madai kuwa inakiuka maadili ya Kitanzania. Pia alizuiwa kufanya maenesho ya hadhara kwakuwa hajajisajili kwenye baraza la sanaa la taifa, BASATA.
 
Kwenye mkutano huo na waandishi wa habari, Snura amedai kuwa tayari amekamilisha mchakato wa usajili na BASATA imempa kibali. Pia amedai kuwa amewasilisha video mpya ya wimbo huo kwa bodi ya filamu ya Tanzania ambayo itaikagua. Tangaza biashara yako hapa. Pia like page yetu ya facebook Jambo Tz. tu-follow instagram @jambotz.

HUKUMU KESI YA KAFULILA MEI 17

Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Tabora inayosikiliza kesi ya kupinga matokeo ya uchaguzi wa Jimbo la Kigoma Kusini iliyofunguliwa na aliyekuwa mgombea kupitia Chama cha NCCR-Mageuzi, David Kafulila inatarajia kutoa hukumu Mei 17, mwaka huu.

Jaji wa mahakama hiyo anayesikiliza kesi hiyo mjini Kigoma, Ferdinand Wambali, alisema kuwa amepanga kutoa hukumu tarehe hiyo baada ya pande zote mbili kuwasilisha ushahidi na maelezo yao.

Baada ya kukamilika kwa ushahidi huo, Jaji Wambari aliomba kupatiwa muda wa kutosha kupitia ushahidi na vielelezo vilivyowasilishwa mahakamani hapo ili aweze kutoa hukumu ya haki.

Aliyekuwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Uvinza, Ruben Mfune ambaye alikuwa msimamizi wa uchaguzi wa jimbo hilo ni mshtakiwa wa tatu katika kesi hiyo. Katika kesi hiyo namba 2 ya mwaka 2015, Kafulila anaishawishi mahakama itengue matokeo yaliyompa ushindi aliyekuwa mgombea wa CCM, Hasna Mwilima badala yake imtangaze yeye kama mshindi halali wa jimbo hilo.

Walalamikiwa katika kesi hiyo ni pamoja na Mbunge wa jimbo hilo Hasna, aliyekuwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Uvinza, Ruben Mfune ambaye alikuwa msimamizi wa uchaguzi wa jimbo hilo na Mwanasheria wa Serikali ambaye anaiwakilisha Tume ya Taifa ya Uchaguzi. Katika kesi hiyo, Wakili Kenedy Fungamtama anamtetea Husna huku Kafulila akitetewa na mawakili watatu, Profesa Abdallah Safari, Tundu Lissu na Daniel Rumenyela.

MAGAZETI YA LEO ALHAMIS MEI 05, 2016 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

20160505_074606 20160505_074619 20160505_074634 20160505_074644


Tangaza biashara yako hapa. Pia like page yetu ya facebook Jambo Tz. tu-follow instagram @jambotz.

VYUO VIKUU BORA DUNIA

Orodha mpya ya vyuo vikuu bora zaidi duniani ya Times Higher Education, kwa kuangazia sifa za chuo kikuu husika, imetolewa, huku vyuo vikuu kutoka bara Asia vikiimarika sana. Mwaka huu, kuna vyuo vikuu 17 kutoka Asia vilivyomo kwenye orodha ya vyuo 100 bora, likiwa ongezeko kutoka vyuo 10 mwaka jana.

Kwa mara ya kwanza, kuna chuo kikuu kutoka Uchina katika 20 bora, Chuo Kikuu cha Tsinghua University kutoka Beijing ambacho kimo nambari 18. Vyuo vikuu vya Marekani bado vinatawala orodha hiyo, chuo kikuu cha Harvard kikiwa ndicho kinachoongoza. Vifuatavyo ni vyuo vikuu bora 100.

1 . Harvard University

Marekani

2 . Massachusetts Institute of Technology

Marekani

3. Stanford University

Marekani


4. University of Cambridge

Uingereza

WAPENZI WA JINSIA MOJA WAPINGA UKAGUZI WA 'TUPU ZA NYUMA'

wapenzi wa jinsia moja
 
Wanaume wawili wanaosema kuwa maafisa wa polisi wa Kenya waliwalazimisha kufanyiwa ukaguzi wa tupu ya nyuma ili kubaini kwamba walishiriki katika ngono ya mapenzi ya jinsia moja wameanzisha kesi mahakamani wakitaka ukaguzi huo kuwa ukiukaji wa katiba.

Wanasema kuwa walilazimishwa kufanyiwa ukaguzi wa magonjwa ya virusi vya ukimwi na Hepatitis kufuatia kukamatwa kwao mnamo mwezi Februari 2015 baada ya kushukiwa kwamba wanashiriki katika ngono ya mapenzi ya jinsia moja.

Vitendo vya wapenzi wa jinsia moja kushiriki ngono ni kinyume na sheria nchini Kenya na adhabu ya makosa hayo ni miaka 14 jela. Mahakama ya Mombasa imewapatia mawakili wa serikali wiki moja kutoa jibu. Chini ya sheria ya kimataifa, ukaguzi wa lazima katika tupu ya nyuma ni kitendo cha kikatili,unyama na ni sawa na mateso kulingana na kundi la haki za kibinaadamu Human Wrights Watch

KATUMBI ATANGAZA KUWANIA URAIS CONGO

 Mwanasiasa mashuhuri nchini Jamhuri ya Demokrasi ya Congo Moise Katumbi amethibitisha kuwa atagombea urais kwenye uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwezi Novemba.

Mfanyabiashara huyo na gavana wa zamani wa jimbo la Katanga alitoa tangazo hilo kupitia kwa mitandao ya kijamii. Muungano wa vyama kadha vya upinzani uliamua kumuidhinisha Bw Katumbi kuwa mgombea mwezi Machi.
Bw Katumbi, akitangaza kuwania kwake, amepuuzilia mbali madai kwamba alipokuwa waziri wa hati alitumia mamluki kutoka nje akisema habari hizo ni za uongo. Kwa mujibu wa katiba ya nchi hiyo Rais Joseph Kabila anatakiwa kuondoka madarakani mwaka huu lakini wapinzani wake wana hofu kuwa huenda ana mipango ya kusalia madarakani.

CHURA AMPONZA 'SNURA MAJANGA' AFUNGIWA KUFANYA KAZI ZA SANAA



Serikali imesitisha wimbo na video ya ‘Chura’ wa msanii, Snura Mushi ‘Snura Majanga’, kuchezwa kwenye vyombo mbalimbali vya habari hadi itakapofanyiwa marekebisho. Wimbo na video hiyo umetokana na maudhui ya utengenezwaji wake ambayo hayaendani na maadili ya Mtanzania. Tangaza biashara yako hapa. Pia like page yetu ya facebook Jambo Tz. tu-follow instagram @jambotz.

Pia Serikali imesitisha maonyesho yote ya hadhara ya msanii huyo, mpaka atakapokamilisha taratibu za usajili wa kazi zake za sanaa katika Baraza la Sanaa la Taifa (Basata). Licha ya hivyo, Serikali imewataka wasanii wajiulize kabla ya kubuni kazi zao za sanaa kwa kufikiria wazazi, ndugu, jamaa na marafiki zao namna watakavyozipokea.


Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano serikalini, Zawadi Msalla, aliwaambia waandishi wa habari kwamba wasanii wanapotunga nyimbo zao wavae nafasi za wanaowadhalilisha na waelewe kwamba sanaa si uwanja wa kudhalilisha watu. Tangaza biashara yako hapa. Pia like page yetu ya facebook Jambo Tz. tu-follow instagram @jambotz.

MAN CITY WACHAPWA 1-0 NA REAL MADRID

 
Manchester City wameshindwa kufika katika fainali za kwanza za klabu bingwa barani Ulaya (UEFA) baada ya kutolewa na mabingwa mara 10 wa michuano hiyo Real Madrid katika mchezo uliokua wa kuvutia tena wa aina yake. Walichapwa 1-0.

Baada ya kutokuwa na ushindi wowote katika mzunguko wa kwanza, Real Madrid walianza kuongoza kipindi cha kwanza kufuatia mpira wa krosi uliopigwa na Gareth Bale kumbabatiza kiungo wa City Fernando na kuingia nyavuni.
Real waliutawala mchezo huku mpira wa kichwa uliopigwa na Bale ukigonga mwamba na baadaye mlinda mlango wa City Joe Hart akiondoa mikwaju ya Luka Modric na Cristiano Ronaldo. 

Klabu hiyo ya Uingereza ilikuwa ikihitaji bao moja muhimu la ugenini hususan katika dakika za lala salama kuelekea fainali,lakini hilo halikuweza kufanikiwa licha ya kushangiliwa na mashabiki wake wapatao 4,500.

Madrid walipata wakati mgumu kidogo pale mkwaju mkali wa Sergio Aguero ulipogonga nyavu za juu za lango la Madrid. Real sasa watakutana na Atletico katika uwanja wa San Siro tar 28 Mei, hii ikiwa ni kama marudio ya fainali za mwaka 2014 ambapo Real walishinda kwa mabao 4-1 baada ya muda wa nyongeza.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...