Thursday, February 18, 2016
Saturday, February 13, 2016
MWANAMKE ALIYEWAPORA SILAHA MAJAMBAZI APEWA ZAWADI NA JESHI LA POLISI
Sophia Manguye akisaini mara baada ya kukabidhiwa zawadi yake.
Mwanamke aliyepambana na jambazi na kufanikiwa kumnyang’anya bunduki aina ya SMG, Sophia Manguye (46), amepewa zawadi ya Sh 500,000 na Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu Tarime/Rorya, Gemini Mushy.
Mwanamke huyo ambaye aliomba Serikali kumpa silaha ili kujilinda, alisema kuwa hajaridhika na zawadi hiyo kwa kuwa kama asingemmudu jambazi huyo watu wengi wangepoteza maisha.
Hata hivyo, Mushy alimwomba Manguye kupokea kiasi hicho japokuwa ni kidogo kwa kuwa ni zawadi kutoka ofisi yake. Like page yetu ya facebook Jambo Tz
UTAFITI: UMAARUFU WA MAGUFULI WAONGEZEKA LOWASSA WASHUKA...!!!
Matokeo ya utafiti mpya uliofanywa mapema mwezi huu yanaonyesha kuwa umaarufu wa Rais John Magufuli umeongezeka kufikia asilimia 74.5, akimuacha mbali mpinzani wake wa karibu kwenye Uchaguzi Mkuu, Edward Lowassa.
Magufuli alishinda mbio za urais kwenye Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25, akipata asilimia chache kuliko wagombea wengine kutoka CCM, lakini amejiongezea umaarufu kutokana na hatua ambazo amekuwa akichukua tangu alipoapishwa Novemba 5, 2015.
Katika uchaguzi huo, Dk Magufuli alipata kura milioni 8.8 sawa na asilimia 58.47, akifuatiwa na Lowassa aliyepata kura milioni 6.07, sawa na asilimia 39.97. Like page yetu ya facebook Jambo Tz
PICHA YA DEREVA WA BASI LA SIMBA MTOTO ENZI ZA UHAI WAKE
Fred Venance enzi za uhai wake.
Huyu ndiye aliyekuwa dereva wa bus la Simba Mtoto lililopata ajali juzi . Taarifa zinasema ametoka kufunga ndoa Jumapili iliyopita tu. Baba
wa kijana huyu ni dereva wa bus la Tashriff.
Like page yetu ya facebook Jambo Tz
Watu 11 akiwamo mama, mwanawe na mjukuu wake wamekufa papohapo na wengine 34 kujeruhiwa katika ajali ya basi la kampuni ya Simba Mtoto lililogongana uso kwa uso na lori. Familia iliyopatwa na janga hilo ni ya mwandishi wa habari mwandamizi wa Redio ya Mlimani, Hamis Dambaya aliyefiwa na mkewe, Raya Said, mtoto wake Nargis Hamis na mama mkwe wake ambaye jina lake halikutambuliwa mara moja. Like page yetu ya facebook Jambo Tz
Watu 11 akiwamo mama, mwanawe na mjukuu wake wamekufa papohapo na wengine 34 kujeruhiwa katika ajali ya basi la kampuni ya Simba Mtoto lililogongana uso kwa uso na lori. Familia iliyopatwa na janga hilo ni ya mwandishi wa habari mwandamizi wa Redio ya Mlimani, Hamis Dambaya aliyefiwa na mkewe, Raya Said, mtoto wake Nargis Hamis na mama mkwe wake ambaye jina lake halikutambuliwa mara moja
UFISADI WA SHILINGI MILIONI 20 WAZUA TAFRANI MSIKITINI JIJINI DAR ES SALAAM
Waumini
wa dini ya Kiislam wakizozana nje ya Msikiti wa Masjidi Pelapela uliopo
eneo la Mtakuja Vingunguti jijini Dar es Salaam katika swala ya Ijumaa
leo mchana, baada ya kutokea tafrani ya waumini hao dhidi ya viongozi
wao ambao wanatuhumiwa kutafuna fedha zaidi ya sh.milioni 20
walizochanga kwa ajili ya ujenzi wa msikiti mpya.
Muumini
wa Msikiti huo, Mbarouk Mohamed Makame (kushoto), akizungumza kuhusu
fedha hizo zinazodaiwa kutumiwa vibaya na viongozi wao. Kulia ni mmoja
wa wazee wa msikiti huo, Mzee Selasela.
Mzee
Selasela akionesha dari la msikiti huo lililochakaa ambapo fedha hizo
zinazodaiwa kutumiwa vibaya na viongozi wao zingesaidia kuufanyia
ukarabati. Like page yetu ya facebook Jambo Tz
Wednesday, February 10, 2016
Subscribe to:
Posts (Atom)